The Inquisitive
Senior Member
- Oct 27, 2010
- 177
- 29
Nilienda duka moja hapa DSM (jina nalihifadhi). Nikachagua nilivyotaka, nikauliza bei. Nikaambiwa bei inategemea kama nataka risiti ya TRA au risiti "ya kawaida". Nikauliza tofauti ya bei ya risiti ya TRA na hiyo nyingine. Muuzaji akapiga hesabu ktk calculator akanionyesha jumla ya risiti ya TRA (ambayo ndio bei halisi) na "ya kawaida" - amepunguza kama 10% hv. Lakini hapo hapo akasema kuwa kwenye ile risiti "ya kawaida" ataandika figure XXX ambayo ilikuwa kama 1/3 ya bei halisi!!! Sikuelewa mchezo uliokuwa unachezwa hapo, nikamwambia anipe risiti ya TRA.
Kwa mnaojua haya mambo, hii ni dili ya namna gani?
Kwa mnaojua haya mambo, hii ni dili ya namna gani?