Elections 2010 Unataka Prof. Baregu kugombea URAIS mwaka 2010? Jiandikishe hapa.

Marafiki mnachanganya sana elimu na uongozi! shauri lenu.

wakati nwingine napata shida sana na jinsi tunavyo dhani kuhusu kiongozi bora, hii habari ya fulani anafaa mara filani. urais si mchezo inataka utashi wa mtu mwenyewe binafsi wala si elimu tu au makongamano yake
Ni sawa tusichanganye uongozi na elimu na si kweli kwamba kuwa elimu kubwa lazima utakuwa kiongozi mzuri, tutambue vile vile kuwa na elimu kubwa kama u-prof. haukuzuii wewe kuwa kiongozi mzuri.

Elimu katika uongozi inategemea na field ya elimu uliyonayo mfano si kila aliye na degree anaweza kuwa mwalimu. Prof. Sarungi na Prof. Baregu wote ni wanasiasa lakini tofauti iko kwenye fields zao Sarungi ni Medical doctor wa mifupa wakati Baregu ni Dr. wa Political Science, kwa hiyo unaweza kuona wazi ni yupi ambaye siasa inaweza isimpige chenga kwa mbali.

paulss amezungumzia utashi, mchukulie Dr. Shein na prof. Baregu, wote ni wanasiasa na niseme ni wasomi kwa elimu zao lakini wenye utashi tofauti. Unaweza kuona wazi kabisa ni yupi kati ya hao wawili aliye na utashi binafsi wa siasa na yule anayelazimisha siasa. Kwa hiyo naweza kusema kuwa Prof. Baregu ana vitu vyote mlivyovitaja yaani Elimu, field ya elimu yake na utashi, achilia mbali utashi wa yeye kutangaza nia hata historia yake shuleni/chuoni.
 
Kama ndio tumekosa wagombea uraisi kihivi,basi sintashangaa tena Kikwete akipata above 85%.
 
Basi acha tumchague CCM na Kikwete wake na tutegemee kutokea MABADILIKO.

Nilishasoma maneno ya Mwanakijiji kuwa "huwawezi kuwa unafanya jambo lilelile kwa namna ileile na utehemee mabadiliko".

HONGERA Kikwete, HONGERA CCM.

Nilitegema walau Baregu anaweza kuleta mabadiliko bila kujali ni Mabaya au Mazuri.

Anyway, niliandika Baregu kwa kufikiria kuwa wakati mwingine inabidi mtu usitumie "common sense" ili mambo yabadilike (maneno ya Mtanzania). Ngoja tubaki na Kikwete na tutumie Common Sense.
 
Sioni kama maprofesa wanafaa sana kuwa rais. They are more intellectuals than politicians. Baregu hajulikani sana kwa watu wa kawaida ambao ndio wapiga kura
 
Inawezekana akawa kichwa kwa Wasomi na wanafunzi wake LAKINI shangazi zangu, mama zangu, wajomba zangu na baba zangu kule kijijini ni nini wanachofahamu kumuhusu Baregu ili wampe kura? Wanaomwona kwenye TV ni wachache na ambao tarehe 31 October 2010 sidhani kama tuko kwenye orodha ya watakaochafuliwa vidole na wino!!!!
 
Back
Top Bottom