Unataka kunichezea tu!

Jamani umewapa za uso! Mdada hata kuzoeana bado anataka utangaze ndoa lol! Maisha menyewe haya.....mmmhhhh

Nakubaliana nawe kwa asilimia nyingi tu..
Ikiwa hata kuzoeana bado wakaka mwawezaje kumtaka kimwili mdada?

Kama kigezo ni kuzoeana ni vema basi mkazoeana kama kaka na dada kwanza kabla ya kuazisha hayo mahusiano.

Angalizo: Huu ni mtazamo wangu tu kuwa huenda hiyo ni gia yenu (wakaka) tu ya kupenda kumega mega ovyo....Mshindwe kabisa
 
Rev au mwanaume yeyote humu, ulishawahi kutendwa na mpenzi wako uliyempenda?
Ulijisikiaje? ulichukia kwa kupoteza muda wqako right?
 
Umwambie msichana wa kitanzania lets have funny and enjoy each other huyo huwezi mpata hata siku moja! Labda um-bake ......!

Wapo wanaopatikana mkuu. Fikiria wale wanaowakubali waume za watu. Fikiria wake za watu wanaokubali kumegwa. Lakini hata hapa JF wapo waliowahi kushuhudia kuwa waliamua kumegwa na rafiki za wachumba wao just fo utamu au kulipiza kisasi.
 
Rev au mwanaume yeyote humu, ulishawahi kutendwa na mpenzi wako uliyempenda?
Ulijisikiaje? ulichukia kwa kupoteza muda wqako right?

Nimeisha tendwa mara nyingi mno! Kuanzia mashuleni, vyuoni, makazini na mitaani...ila nasonga mbele....sijalalamika nimetumika wala kuchezewa.
 
Huwa inapendeza sana ikiwa mkaka atakuwa wazi hasa kuhusu nia yake kwa mdada. Siyo lazima useme kuwa unamchezea tu waweza tumia neno tofauti lenye maana sawa na hiyo. Wapo wadada wengi tu ambao wao huwa hawahitaji mtu wa future...Hivo ni vema kuwatafuta hao kuliko wampotezea mda mtu mwenye malengo yake ya kuwa nawe maishani.

Ntawatambuaje?
 
wanawake wanapenda kudanganywa, ukimwambia ni part time anagoma,
 
Unapokuwa kijana unakutana na kijana mwenzio iwe safarini, sehemu za kazi ama mtaani. Uzalendo unakushinda na kuanza kurusha ndoana zako kwa mdada. Chemistry inaanza kuwapanda wote. Unaanza kujiweka karibu na binti mnaenda dinner na movie kadhaa. Kabla ya kulala mwapigiana simu ....etc etc missing you kwa sana. Hapo mkaka unatafuta kasi umwombe tunda. Siku ya siku unameza mfupa na kumwambia mdada inakuwaje sasa? Jibu bwana mimi nakupenda pia ila naogopa utanichezea tu na kuniumiza moyo wangu, niliwahi umizwa na mkaka mmoja nilimpenda kuliko wewe!!!!!!! Hapa hujiuliza kuchezewa kupi huko? Nadhani labda wadada mbadili kauli iwe tunachezeana its makes more sense kwangu.

Haya wadada mpo?

...Mtani nakuunga mkono kwenye hili, ila ungeweka "censored" hapa;

.......unatafuta kasi umwombe tunda.

Wasomaji wa mstari kwa mstari hawatakuelewa bana, au unaonaje?
'wanafundishwa' ...."mwanaume akishaonja, humuoni tena...!"
 
Ni bora kama mnajua hamko tayari kwa big thing muambiane mapema kwamba huu uhusiano wa kuchezeana tu. naona wote machezeana hakuna wa kumchezea mwenzake. Sema kwa kuwa wakakandio mnaazisha game ndio maana lawama zote zinawaangukia
 
Ntawatambuaje?

Utawafahamu tu mara utakapokutanana nao....
Wengine huwa wanasema wazi wazi tu na wengine huwa after zawadi au pesa kabisa na siyo love.
Tatizo wadada wa aina hiyo huwa na wakaka wengi pia kitu ambacho wakaka hawapendi.

Mara nyingi wakaka wamekuwa wakihitaji wadada ambao wana tabia njema kwa malengo yasiyokuwa na future.
 
Back
Top Bottom