unamkumbuka Mwl yupi shuleni/chuoni kwako ayekuwa na tabia ya 'ajabu'??

Nyakageni

JF-Expert Member
Feb 1, 2011
15,045
5,092
Binafsi namkumbuka mwl wangu wa Literature miaka hiyo pale Shinyanga sec aliitwa mwl Mipawa almaarufu kama Okonkwo. Alikuwa akija na mtoto wake darasani na huku yeye anakula kiazi na kufundisha. Parade alikuwa anamkosoa headmaster tense na grammar. Alikuwa akimfunga mtoto mgongoni kwa kitenge na kuja naye kazini au kutoka naye! We unakumbuka lipi, tuendelee wadau . . . . . .
 
Binafsi namkumbuka mwl wangu wa Literature miaka hiyo pale Shinyanga sec aliitwa mwl Mipawa almaarufu kama Okonkwo. Alikuwa akija na mtoto wake darasani na huku yeye anakula kiazi na kufundisha. Parade alikuwa anamkosoa headmaster tense na grammar. Alikuwa akimfunga mtoto mgongoni kwa kitenge na kuja naye kazini au kutoka naye! We unakumbuka lipi, tuendelee wadau . . . . . .

Huyo kiboko!
Mimi nakumbuka miaka hiyo nilikuwa shule moja huko mbeya. Kuna ticha mmoja alikuwa discipline master alikuwa mkorofi sana. Ukijichanganya ukaingia line zake ni LAZIMA akudunde! no matter utatoa utetezi gani uwe wa ukweli au wa uwongo. Ni lazima mwisho wa huo utetezi atakulamba bakora za kutosha. Kutokana na style yake hiyo allikuwa anachukiwa na karibu wanafunzi wa shule nzima.

Siku moja akiwa assembly akamwona jamaa wa form six kafuga ndevu, akamaind. Akamwita aende mbele, na kuanza kumsemea mbovu! Weeeeee! Kumbe yule jamaa naye alishajichokea, ndani ya sekunde yule jamaa alishusha kipondo kikali kwa ticha palepale mbele ya assembly. Kuona hivyo wanafunzi wote wakaungana na jamaa kwa kumvamia yule ticha kwa makofi, viboko, mawe n.k.

Ticha aliumizwa vibaya ila alifanikiwa kutoka salama. Kwa tukio lile naamini yule ticha hatakuja asahau kamwe ktk maisha yake.
 
ebwana mimi namkumbuka mwal mmoja anaitwa lisapita kwa waliosomea old moshi yule alikua more than fun na ukichaa juu anaweza akakula makofi ghafla na kukutoa nduki mbaya mpaka nje ya shule
 
ebwana mimi namkumbuka mwal mmoja anaitwa lisapita kwa waliosomea old moshi yule alikua more than fun na ukichaa juu anaweza akakula makofi ghafla na kukutoa nduki mbaya mpaka nje ya shule

Mwl wa nidhamu, shule moja huko kanda ya Kasikazini. Huyu yeye alikuwa anawaamusha wanafunzi saa kumi usiku kwa ajili ya machakamchaka. Na alikuwa ngumi mkononi. Alikuwa anakuja kimya kimya bwenini, na kuwasha taa huku akitoa sauti kali ya kutoka nje. Basi madogo walikuwa wanatoka nje na chupi tu kwa hofu.
Bweni moja waliamua kumtega kwenye swichi ya umeme. Jamaa kama kawaida alipofika mlangoni, kutaka kuwasha taa akakutana na waya wa umeme na kupigwa shock. Jamaa aliruka sana na kuanza kusema 'hamniwezi, hamniwezi huku akiondoka'. Nisikilizie tibwili lake asubuhi, bweni shughuli ilikuwepo. Lakini huyo ticha alikuwa noma kwa kuamsha mchakamchaka utafikiri alikuwa hajaoa, kumbe alikuwa na mke na watoto kadhaaaaa.
 
Huyo kiboko!
Mimi nakumbuka miaka hiyo nilikuwa shule moja huko mbeya. Kuna ticha mmoja alikuwa discipline master alikuwa mkorofi sana. Ukijichanganya ukaingia line zake ni LAZIMA akudunde! no matter utatoa utetezi gani uwe wa ukweli au wa uwongo. Ni lazima mwisho wa huo utetezi atakulamba bakora za kutosha. Kutokana na style yake hiyo allikuwa anachukiwa na karibu wanafunzi wa shule nzima.

Siku moja akiwa assembly akamwona jamaa wa form six kafuga ndevu, akamaind. Akamwita aende mbele, na kuanza kumsemea mbovu! Weeeeee! Kumbe yule jamaa naye alishajichokea, ndani ya sekunde yule jamaa alishusha kipondo kikali kwa ticha palepale mbele ya assembly. Kuona hivyo wanafunzi wote wakaungana na jamaa kwa kumvamia yule ticha kwa makofi, viboko, mawe n.k.

Ticha aliumizwa vibaya ila alifanikiwa kutoka salama. Kwa tukio lile naamini yule ticha hatakuja asahau kamwe ktk maisha yake.

eeh! Hiyo ilikuwa kali sana. Nadhani alipewa uhamisho baada ya hapo! Duh
 
ebwana mimi namkumbuka mwal mmoja anaitwa lisapita kwa waliosomea old moshi yule alikua more than fun na ukichaa juu anaweza akakula makofi ghafla na kukutoa nduki mbaya mpaka nje ya shule

yaani anakukimbiza! Your not serious mkuu!
 
Mwl wa nidhamu, shule moja huko kanda ya Kasikazini. Huyu yeye alikuwa anawaamusha wanafunzi saa kumi usiku kwa ajili ya machakamchaka. Na alikuwa ngumi mkononi. Alikuwa anakuja kimya kimya bwenini, na kuwasha taa huku akitoa sauti kali ya kutoka nje. Basi madogo walikuwa wanatoka nje na chupi tu kwa hofu.
Bweni moja waliamua kumtega kwenye swichi ya umeme. Jamaa kama kawaida alipofika mlangoni, kutaka kuwasha taa akakutana na waya wa umeme na kupigwa shock. Jamaa aliruka sana na kuanza kusema 'hamniwezi, hamniwezi huku akiondoka'. Nisikilizie tibwili lake asubuhi, bweni shughuli ilikuwepo. Lakini huyo ticha alikuwa noma kwa kuamsha mchakamchaka utafikiri alikuwa hajaoa, kumbe alikuwa na mke na watoto kadhaaaaa.

hee! Hawa walimu! Siku hizi vituko vimepungua nadhani, sababu ya njia shirikishi
 
Nilikutana na kichwa kinaitwa Lawrence Kibatara. Kweli hiki kichwa, alikuwa ni Dr( PHD holder) halafu headmaster. Kwanza alioa mwanafunzi wake mara alipomaliza form four tu. U can imagine yeye alikuwa na miaka kama 60 hivi by that time.

Alikuwa anakusanya ada na michango anatokomea nayo bagamoyo ambapo alikuwepo bi mkubwa, akishaishiwa anarudi tena kudai. Alifanya mbinu ya kuiba generator la shule halafu akatuchangisha tukanunua jipya
 
Kulikuwa na Ticha moja second master huko Mara sekondari anaitwa Bachubira nickname (luba) ana nata kinoma ngumi mkononi shule haikuwa na fensi wanafunzi wa bweni walitoroka kwenda Musoma town kudadadadeki anakariri huyo hadi kisogo hata akikuona mbali atakuatambua, umesimama paredi anapita kila mstari unashangaa anakudaka NILIKUONA MJINI unatoka uwanja wa karume kucheki mechi taja na wenzako na kweli hasingizii mtu,adhabu ya hapo uchague kuingia mgodini(kutapisha choo/karo) au suspension.Kulikuwa na jamaa mmoja mfupi sana ukienda nae town lazima mkamatwe watu walimkimbia eti nuksi!

Akiwa anakuja mabwenini utasikia mtu anatoa muruzi kisha anaita machaleeee! utasikia vishindo watu wanatimuka au bila hata sababu bora wasikutane nae uso kwa uso maana atakubambikia kesi hapo hapo mfano ni denti alinyoa kipara akapigwa suspension ya wiki mbili mpaka nywele ziote.

Kuna jamaa mtundu alikuwa mcheza serekasi alimweza siku moja, ukaguzi usafi ni kila thursday anakagua ndefu,kucha,mikanda mipana n.k akamkuta jamaa kwa makusudi kavaa laba za kike ticha kamvua kakatiza huku jamaa akimfuata akisema nipe viatu vya mama! sitosahau hiyo vunja mbavu
ni hadith nyingi ntantoa nyingine naogopa kujaza ukurasa.
 
Kulikuwa na Ticha moja second master huko Mara sekondari anaitwa Bachubira nickname (luba) ana nata kinoma ngumi mkononi shule haikuwa na fensi wanafunzi wa bweni walitoroka kwenda Musoma town kudadadadeki anakariri huyo hadi kisogo hata akikuona mbali atakuatambua, umesimama paredi anapita kila mstari unashangaa anakudaka NILIKUONA MJINI unatoka uwanja wa karume kucheki mechi taja na wenzako na kweli hasingizii mtu,adhabu ya hapo uchague kuingia mgodini(kutapisha choo/karo) au suspension.Kulikuwa na jamaa mmoja mfupi sana ukienda nae town lazima mkamatwe watu walimkimbia eti nuksi!

Akiwa anakuja mabwenini utasikia mtu anatoa muruzi kisha anaita machaleeee! utasikia vishindo watu wanatimuka au bila hata sababu bora wasikutane nae uso kwa uso maana atakubambikia kesi hapo hapo mfano ni denti alinyoa kipara akapigwa suspension ya wiki mbili mpaka nywele ziote.

Kuna jamaa mtundu alikuwa mcheza serekasi alimweza siku moja, ukaguzi usafi ni kila thursday anakagua ndefu,kucha,mikanda mipana n.k akamkuta jamaa kwa makusudi kavaa laba za kike ticha kamvua kakatiza huku jamaa akimfuata akisema nipe viatu vya mama! sitosahau hiyo vunja mbavu
ni hadith nyingi ntantoa nyingine naogopa kujaza ukurasa.


Mkuu
Hii inakuwa miaka ya 97 na 98wakati wa Igosha
 
Mimi kwa upande wangu simzungumzii Mwalimu wangu, but kuna Afande mmoja alikuwa Makongo Sekondari, sijui kama alikuwa ni Mwalimu kabisa au vipi, ni marehemu now, Afande Miraji, nilikuwa napewa stori zake za vituko, alikuwa ni noma, yaani wanakuambia akikupa adhabu, hutomsahau, akiwa anakutafuta, akikukamata utakiona cha moto, anaweza kukutia aibu mbele hata ya demu wako, wanaJf waliosoma Makongo, hapana shaka watakuwa wanamjua, cause alikuwa ni maarufu sana sana Makongo, alikuwa ana vituko vingi sana, alishawahi kuwalazimiza wanafunzi wakiume mahardcore, waimbe na kucheza taarabu mbele ya wenzao, nasikia pia alipokuwa akipigisha kwata utajuta kuwa mwanafunzi wa Makongo, kina Babu Ayubu, hawawezi kumsahau kabisa, cause mpaka sauti yake alikuwa anaiigiza vizuri kabisa
 
Kulikuwa na Ticha moja second master huko Mara sekondari anaitwa Bachubira nickname (luba) ana nata kinoma ngumi mkononi shule haikuwa na fensi wanafunzi wa bweni walitoroka kwenda Musoma town kudadadadeki anakariri huyo hadi kisogo hata akikuona mbali atakuatambua, umesimama paredi anapita kila mstari unashangaa anakudaka NILIKUONA MJINI unatoka uwanja wa karume kucheki mechi taja na wenzako na kweli hasingizii mtu,adhabu ya hapo uchague kuingia mgodini(kutapisha choo/karo) au suspension.Kulikuwa na jamaa mmoja mfupi sana ukienda nae town lazima mkamatwe watu walimkimbia eti nuksi!

Akiwa anakuja mabwenini utasikia mtu anatoa muruzi kisha anaita machaleeee! utasikia vishindo watu wanatimuka au bila hata sababu bora wasikutane nae uso kwa uso maana atakubambikia kesi hapo hapo mfano ni denti alinyoa kipara akapigwa suspension ya wiki mbili mpaka nywele ziote.

Kuna jamaa mtundu alikuwa mcheza serekasi alimweza siku moja, ukaguzi usafi ni kila thursday anakagua ndefu,kucha,mikanda mipana n.k akamkuta jamaa kwa makusudi kavaa laba za kike ticha kamvua kakatiza huku jamaa akimfuata akisema nipe viatu vya mama! sitosahau hiyo vunja mbavu
ni hadith nyingi ntantoa nyingine naogopa kujaza ukurasa.


teh teh teh teh......mkuuu nimeugua kikohozi kwa mastori yako...... Watoto wa Mara walikuwa wakorofi aisee stori zao naziskia sanaaa, ukiweka na wale wa ihungo, tarime, tabora boys, geita sec na Musoma tec ni full vituko aiseee! mzee Bachuuuuuu.................
 
Kuna huyo madamme alikuwa kiherehere kweli yani anaingia dom la boys ka ladies room kuja kuamsha watu asubuhi,ikapangwa mbinu jamaa akachukua shuka na kujifunika usoni baada ya kumsikia anakuja huku chini akiwa uchi antenna juu,madame kuja jamaa akawa anamfwata straight we! Madame alisepa na akakoma kale katabia
 
Nilikutana na kichwa kinaitwa Lawrence Kibatara. Kweli hiki kichwa, alikuwa ni Dr( PHD holder) halafu headmaster. Kwanza alioa mwanafunzi wake mara alipomaliza form four tu. U can imagine yeye alikuwa na miaka kama 60 hivi by that time.

Alikuwa anakusanya ada na michango anatokomea nayo bagamoyo ambapo alikuwepo bi mkubwa, akishaishiwa anarudi tena kudai. Alifanya mbinu ya kuiba generator la shule halafu akatuchangisha tukanunua jipya

eeh hii mbona kali. Bado yuko hai? Kabadilika?
 
Kulikuwa na Ticha moja second master huko Mara sekondari anaitwa Bachubira nickname (luba) ana nata kinoma ngumi mkononi shule haikuwa na fensi wanafunzi wa bweni walitoroka kwenda Musoma town kudadadadeki anakariri huyo hadi kisogo hata akikuona mbali atakuatambua, umesimama paredi anapita kila mstari unashangaa anakudaka NILIKUONA MJINI unatoka uwanja wa karume kucheki mechi taja na wenzako na kweli hasingizii mtu,adhabu ya hapo uchague kuingia mgodini(kutapisha choo/karo) au suspension.Kulikuwa na jamaa mmoja mfupi sana ukienda nae town lazima mkamatwe watu walimkimbia eti nuksi!

Akiwa anakuja mabwenini utasikia mtu anatoa muruzi kisha anaita machaleeee! utasikia vishindo watu wanatimuka au bila hata sababu bora wasikutane nae uso kwa uso maana atakubambikia kesi hapo hapo mfano ni denti alinyoa kipara akapigwa suspension ya wiki mbili mpaka nywele ziote.

Kuna jamaa mtundu alikuwa mcheza serekasi alimweza siku moja, ukaguzi usafi ni kila thursday anakagua ndefu,kucha,mikanda mipana n.k akamkuta jamaa kwa makusudi kavaa laba za kike ticha kamvua kakatiza huku jamaa akimfuata akisema nipe viatu vya mama! sitosahau hiyo vunja mbavu
ni hadith nyingi ntantoa nyingine naogopa kujaza ukurasa.

eeh! Hii balaa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom