Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,720
- 21,779
Lukuvi: Kiama cha wamachinga Okt 30
Na Hilary Komba
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam Bw. William Lukuvi ametangaza kuwa ifikapo Oktoba 30 mwaka huu wamachinga wawe wameondoka katika maeneo yasiyo rasmi vinginevyo timuatimua itaanza upya.
Bw. Lukuvi alisema hayo Dar es Salaam katika mazungumzoa yake na watendaji wa Manispaa ya Ilala wakiwamo wenyeviti wa serikali za mitaa, watendaji na madiwani juzi.
Alisema biashara zote ambazo zinafanywa katika maeneo yasiyo rasmi yakiwemo maeneo ya barabara zinatakiwa kuondoshwa kabla ya tarehe hiyo ambayo imetangazwa kwa lengo la kufanya jiji kuwa tofauti na lilivyo hivi sasa.
"Jiji la Dar es Salaam limekuwa chafu sana kutokana na uzembe wa kusimamia sheria, sasa wakati umefika kwa wakazi kubadirika na nitahakikisha jiji hili linakuwa safi na kufanana na halmashauri ya Moshi ambayo imetumia sheria zake kuyaweka mazingira katika hali ya usafi.
Alisema timuatimua hiyo itaziondosha biashara zote zinazofanywa katika maeneo yasiyorasmi zikiwemo biashara za maji ya kunywa ya chupa, nguo, miwa, machungwa na aina ya zote za vyakula.
Kwa mujibu wa Bw. Lukuvi shughuli hiyo ya timuatimua itafanywa na askari wa Jeshi la Polisi na wale wa jiji ambao watawakamata watakaokaidi kuondoka.
Alisema timuatimu hiyo pia itawakumba wenye gereji katika maeneo yasiyo rasmi, baa zinazopia muziki wa juu katika makazi ya watu, vyoo vinavyotiririsha maji ya vyooni, wanaocha magiari barabarani, kutupa taka ovyo, wanaojisaidia maeneo yasiyo rasmi.
Naye Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam Bw.Suileman Kova alisema jeshi lake limejipanga vizuri kwa kuwakamata na kuwafikisha watu wanaovunja sheria kwa kufanya biashara katika maeneo yasiyo rasmi.
Alisema shughuli hiyo haitakuwa nguvu ya soda, kwani yeye hapendi kushindwa jambo, hivyo machinga watakaokaidi amri yake hatawaonea huruma kwa sababu mpango huo ni wa kuliweka jiji katika mazingira ya usafi.
USHAURI
USI COPY KAMA HUJUI KU PASTE
Na Hilary Komba
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam Bw. William Lukuvi ametangaza kuwa ifikapo Oktoba 30 mwaka huu wamachinga wawe wameondoka katika maeneo yasiyo rasmi vinginevyo timuatimua itaanza upya.
Bw. Lukuvi alisema hayo Dar es Salaam katika mazungumzoa yake na watendaji wa Manispaa ya Ilala wakiwamo wenyeviti wa serikali za mitaa, watendaji na madiwani juzi.
Alisema biashara zote ambazo zinafanywa katika maeneo yasiyo rasmi yakiwemo maeneo ya barabara zinatakiwa kuondoshwa kabla ya tarehe hiyo ambayo imetangazwa kwa lengo la kufanya jiji kuwa tofauti na lilivyo hivi sasa.
"Jiji la Dar es Salaam limekuwa chafu sana kutokana na uzembe wa kusimamia sheria, sasa wakati umefika kwa wakazi kubadirika na nitahakikisha jiji hili linakuwa safi na kufanana na halmashauri ya Moshi ambayo imetumia sheria zake kuyaweka mazingira katika hali ya usafi.
Alisema timuatimua hiyo itaziondosha biashara zote zinazofanywa katika maeneo yasiyorasmi zikiwemo biashara za maji ya kunywa ya chupa, nguo, miwa, machungwa na aina ya zote za vyakula.
Kwa mujibu wa Bw. Lukuvi shughuli hiyo ya timuatimua itafanywa na askari wa Jeshi la Polisi na wale wa jiji ambao watawakamata watakaokaidi kuondoka.
Alisema timuatimu hiyo pia itawakumba wenye gereji katika maeneo yasiyo rasmi, baa zinazopia muziki wa juu katika makazi ya watu, vyoo vinavyotiririsha maji ya vyooni, wanaocha magiari barabarani, kutupa taka ovyo, wanaojisaidia maeneo yasiyo rasmi.
Naye Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam Bw.Suileman Kova alisema jeshi lake limejipanga vizuri kwa kuwakamata na kuwafikisha watu wanaovunja sheria kwa kufanya biashara katika maeneo yasiyo rasmi.
Alisema shughuli hiyo haitakuwa nguvu ya soda, kwani yeye hapendi kushindwa jambo, hivyo machinga watakaokaidi amri yake hatawaonea huruma kwa sababu mpango huo ni wa kuliweka jiji katika mazingira ya usafi.
USHAURI
USI COPY KAMA HUJUI KU PASTE