Haya kaka, ni haki yako kikatiba kutoa maoni yako.
Vile vile kuacha mazuri yaliyotendwa na serikali ya awamu ya kwanza na kuchukuwa mabaya yaliyoachwa wakati huo.
- Najivunia amani yetu inayotokana na uelewa mdogo wa watanzania juu ya haki zetu na kutokuwa na ujasiri wa kuzidai.
- Najivunia kuwa mapato yoote tunayopata, yanaishia kununua mashangingi v8, safari za viongozi, warsha na makongamano.
- Najivunia mwizi wa kuku anafungwa miaka mingi, mwizi wa mabilioni anaundiwa tume au anaombwa kwa upole arudishe alichoiba.
- Najivunia Tanzania nchi yangu, kwakuwa Ukiwa kiongozi Tanzania, inalipa kuliko biashara yeyote duniani.
- Ni nchi ya kifalme, madaraka kwa kupeana..Nnauye, Kawawa, Mwinyi, Karume, Nchimbi, Msuya, hadi vijukuu watapata vyeo.
- Najuvunia TAKUKURU, ni ka-mbwa koko, kanakula tu vifaranga vyakuku vyenye mdondo na kufyata mkia kwa wakubwa.
- Najivunia nchi yangu kwakua intelijensia, haina mpango na rasilimali za taifa wala mikataba mibovu......chezea kuchakachua kura weye...utaijua intelijensia.
- Najivunia nchi yangu ni SHAMBA la BIBI, natamani niwe mzungu nipewe kitalu au mgodi......nshaanza kutumia karolait.
- Vijana maskani wanasemaga....."mwanaaaa....bora vita ije......kila mtu achukue chake.....maana huu ujinga, wachache wanajirundikia...!"
Kibanga Msese
Toka mwaka umeanza wewe ni kiboko ya yote,sijakusoma hata chembe1. Michezo....football, athletics, netball
2. Muziki...singeli, taarabu, bongo flavour.
3. Umahiri katika Lugha adhimu duniani.....kiswahili.....
4. Uvivu.........
Mlima ambao upo na Kenya.......Wadau hebu tuambizane ni jambo gani ambalo ukiliona au kulifikiria kama Mtanzania unajivunia popote ulipo duniani na pia jambo ambalo ukirifikiria popote pale ulipo katika ulimwengu huu unaona aibu kabisa kujitambulisha kama mtanzania.
Mimi kwa upande wangu najivunia yafuatayo.
1.Kuwa ndani ya Nchi ambayo ina mlima mrefu kuliko yote Africa.
2.Kuwa katika Nchi ambayo ina kila aina ya vivutio vya asili vya kila namna.
mi huwa naonaga aibu sana kila niionapo avatar yko!Wadau hebu tuambizane ni jambo gani ambalo ukiliona au kulifikiria kama Mtanzania unajivunia popote ulipo duniani na pia jambo ambalo ukirifikiria popote pale ulipo katika ulimwengu huu unaona aibu kabisa kujitambulisha kama mtanzania.
Mimi kwa upande wangu najivunia yafuatayo.
1.Kuwa ndani ya Nchi ambayo ina mlima mrefu kuliko yote Africa.
2.Kuwa katika Nchi ambayo ina kila aina ya vivutio vya asili vya kila namna.
Avatar yangu ina nini mkuu.mi huwa naonaga aibu sana kila niionapo avatar yko!