Jagermaster
JF-Expert Member
- Nov 6, 2010
- 654
- 316
Mzee Mwanakijiji, baadhi yetu tulijaribu maisha ya Bongo tukashindwa. Tukajaribu na ughaibuni tukashindwa hatimaye tumerudi Bongo kama Mishen Town. Japo maisha ni magumu lani mara moja moja line zinafunguka.
Kwa watumishi wa umma, hakuna anaweza kuishi kwa kipato chake pekee. Kuanzia Mkuu wa nchi na mishe mishe za vijisafari chungu tele, sometime deal sio safari, deal ni per diem.
Huko chini ndio usisikie, bila vikao,warsha, semina, kongamano na mikutano, hakuna linalowezekana. Procurement ndio inasawazisha mambo yote mpaka chakula ya wazee. Hii imekuwa ndio mtindo wa maisha.
Sekta binafsi na mashirika ya kimataifa, multilateral organizations na maconglomerete ndizo zinaokua maisha ya kundi wanaloishi kwa mishahara yao, hawa wanalipwa kwa dola kuanzia 3,000 mpaka wa 30,000. Kundi hili ni wachache wenye bahati, CV/resume za mguvu ama technical know who na wenye majina makubwa, hawa life is good, the rest tunahangaika tuu kama nyie tena afadhali yenu hicho kibarua cha ziada kinapatikana, hapa Bongo, hata hiyo shughuli ya msingi kuipata ni issue.
Jamani mnatutisha tulio ughaibuni, kwa mtindo huo haturudi bongo