Unaishi kwa kipato chako?

Mzee Mwanakijiji, baadhi yetu tulijaribu maisha ya Bongo tukashindwa. Tukajaribu na ughaibuni tukashindwa hatimaye tumerudi Bongo kama Mishen Town. Japo maisha ni magumu lani mara moja moja line zinafunguka.
Kwa watumishi wa umma, hakuna anaweza kuishi kwa kipato chake pekee. Kuanzia Mkuu wa nchi na mishe mishe za vijisafari chungu tele, sometime deal sio safari, deal ni per diem.

Huko chini ndio usisikie, bila vikao,warsha, semina, kongamano na mikutano, hakuna linalowezekana. Procurement ndio inasawazisha mambo yote mpaka chakula ya wazee. Hii imekuwa ndio mtindo wa maisha.

Sekta binafsi na mashirika ya kimataifa, multilateral organizations na maconglomerete ndizo zinaokua maisha ya kundi wanaloishi kwa mishahara yao, hawa wanalipwa kwa dola kuanzia 3,000 mpaka wa 30,000. Kundi hili ni wachache wenye bahati, CV/resume za mguvu ama technical know who na wenye majina makubwa, hawa life is good, the rest tunahangaika tuu kama nyie tena afadhali yenu hicho kibarua cha ziada kinapatikana, hapa Bongo, hata hiyo shughuli ya msingi kuipata ni issue.

Jamani mnatutisha tulio ughaibuni, kwa mtindo huo haturudi bongo
 
ukweli ni kwamba ni baadhi tu ya wafanyakazi wa sekta binafsi nchini ndio wanaweza ishi kwa vipato vyao kwani kidogo mishahara sekta binafsi ni afadhali lakini kwa serikalini mshahara wa graduate kama uko kwenye laki 5 au 6 there is no way huyu mtu akatimiza hata yale mahitaji ya msingi kwa mwezi huo, nadhan wanaokimbilia serikalini wanajua kua kule ulaji ni mwingi na kazi hamna kwani salalry inatoka kwenye kodi sio uzalishaji!
 
Mzee Mwanakijiji, baadhi yetu tulijaribu maisha ya Bongo tukashindwa. Tukajaribu na ughaibuni tukashindwa hatimaye tumerudi Bongo kama Mishen Town. Japo maisha ni magumu lani mara moja moja line zinafunguka.
Kwa watumishi wa umma, hakuna anaweza kuishi kwa kipato chake pekee. Kuanzia Mkuu wa nchi na mishe mishe za vijisafari chungu tele, sometime deal sio safari, deal ni per diem.

Huko chini ndio usisikie, bila vikao,warsha, semina, kongamano na mikutano, hakuna linalowezekana. Procurement ndio inasawazisha mambo yote mpaka chakula ya wazee. Hii imekuwa ndio mtindo wa maisha.

Sekta binafsi na mashirika ya kimataifa, multilateral organizations na maconglomerete ndizo zinaokua maisha ya kundi wanaloishi kwa mishahara yao, hawa wanalipwa kwa dola kuanzia 3,000 mpaka wa 30,000. Kundi hili ni wachache wenye bahati, CV/resume za mguvu ama technical know who na wenye majina makubwa, hawa life is good, the rest tunahangaika tuu kama nyie tena afadhali yenu hicho kibarua cha ziada kinapatikana, hapa Bongo, hata hiyo shughuli ya msingi kuipata ni issue.
Enzi hizi chocho zote zimezibwa, vyuma vimekaza
 
Hili swalil inaonekana sasa hivi linazidi kupata jibu lake... kuishi kwa kipato bila ufisadi kwa wengine ni ngumu sana. Labda wakulima tu ndio wanaishi kwa vipato vyao... wengine wetu kila mtu anavuta anapoweza...
 
Majibu ya swali hili aliyatoa mkuu BAK katika post namba 9 na mkuu Susuviri kama sijakosea jina katika post namba 10 na wachangiaji wengine wachache. Huwezi kumlipa mtu hela isiyotosha kwa mahitaji ya lazima na bado ukategemea asitafute namna ya kujitosheleza.
Poleni waajiriwa wa kima cha chini!
 
Kama huu uzi uliandikwa mwaka 2009 kipindi kile cha neema teletele vipi mwaka huu wa magufuli?? Nawaza kwa sauti
 
siyo kuhalalisha ndugu yangu bali kujaribu kufocus tatizo letu hasa ni nini? ndugu yangu Nyani ana msemo kuwa "Waafrika ndivyo tulivyo". Wengi wetu tunakerwa na ufujaji wa mali ya umma na matumizi mabaya ya ofisi (hasa inapohusu wanasiasa). Najaribu kuona kuwa yawezekana tunawanyoshea kidole kimoja wao, vitatu sisi wenyewe na kimoja Mungu shahidi yetu.

Swali la msingi ni kuwa hivi kweli ikiingia serikali makini ikakata mianya yote ya "kipato cha ziada" na kulazimisha watu kuishi kwa malipo yao ya mwezi, wangapi kati yetu wataipigia kura serikali hiyo?
Mzee mwanakijiji ulitabiri na leo imekua.
 
Kila Pahala Ulaji!​

KWAMBA kila mtu `hula' mahala pake pa kazi, hilo halikuwa geni, hususan ofisini kwetu.

Tangu `mnene' wa kwanza, mpaka `kapuku' wa mwisho, kila mmoja huketi mkao wa kula kwenye `wigo' unaomkinga asionekana na `vishingo' wasiokawia kuweka `mikingamo' ya kujaza michanga kitumbua cha mtu.

Ukitilia maanani mishahara-njiwa na marupurupu njaa yenye kupigwa paranja na wale watoza-ushuru wasio na simile, sera ikawa ni kutumia `bongo' katika nchi ya Ruksa, mradi tu usidakwe.

Madhali mtu umekabidhiwa ofisi na meza - na ruzuku au tuseme, kasma, hasa iliyonona, hukuwa na haja ya promosheni, wala ya kwenda shule eti kuongeza `unga.' Huo unga au mchele wa nyongeza unaugema na kuumega mumo humo - mradi tu penye unyonge upenyeze matonge, au penye udhia watupia rupia!

Kwa mtaji huo, wale ambao `ofisi' zao zilikuwa kavu, kwa maana ya kukosa pa kuchota, au cha kugema, walifanya kila namna ya kupata `transfa' ndogo ndogo huku na kule kwenye ofisi, bora mkono uende kimiani.

Kwa upande wangu, nilionekana kupendelewa zaidi. Hata madereva wenzangu wakati mwingine waliniambia bayana wakati tukisogoa.

"Mwenzetu unakatiwa mapande ya ulaji tu," alisema Bwana Shaibu, dereva wa bosi mkuu. "Miye kila wakati nipo na kingunge-mkuu wa ofisi! Nitaiba saa ngapi? Gari yenyewe Nissan Patrol. Roho juu kila wakati kuogopa majambazi. Hata `kusanya' siwezi!" Alilalama.

Wakati huo mimi naendesha gari la maji machafu. Nikipiga tripu mbili za kampuni, napiga tano za kwangu. Na kwa kuwa gari lile ni la kubeba (ashakum) kinyesi, wanene wa kampuni hawakutupa macho yao kwangu. Mradi ilikuwa ni ulaji mtupu wa kimyakimya. Hata madereva wenzangu hawakushtuka.

Machale yalianza kuwacheza waliposikia nimesimamisha `banda' pale bondeni.

Nikahamishiwa kwenye `kijiko' - gari la kuchimbia na kung'oang'oa - kwa imani sitakuwa na cha `kuhamisha.' Wakati huo mtindo wa kutumia `nyoka' - mipira ya kutolea petroli na dizeli - ulikuwa umedhibitiwa. Lakini huwezi kumdhibiti mwanadamu, hasa ngurumbili huyo anapokuwa wa Bongoland. Ulaji wa kwenye `kijiko' ukawa mkubwa zaidi, maana katika masaa ya kazi, nusu nayatumia nikiwa `kontrakta bubu.'

Mpaka walipostuka, nilishavuna vya kutosha. Siku nilipohamishiwa kwenye gari la kubeba wafanyakazi, wenzangu walijua wazi chizi limepewa manati, sokoni!

"Au mwenzetu unakula na wakubwa?" walinitania.

"Kwenda zenu! Nani asiyegema mahala pake pa kazi?" Niliwajibu kwa masikhara.

"Ah! Lakini wewe mwenzetu unawekwa kwenye vitengo vya ulaji tu!"

Na kweli. Kwenye gari hili la abiria kulikuwa na pesa za nje-nje tu.

Mara ya kwanza nilikuwa naogopa kuligeuza daladala-bubu (sanyasanya), hususan asubuhi, kwa vile "wanga wengi." Lakini kadiri nilivyoshika hatamu za uongozi wa basi lile, ndivyo nilivyozidi kujiamini.

"Kwanza wanene wote wa kampuni wanakaa uzunguni. Halafu wote wana magari. `Dili' zao zote na wazito wenzao. Huku uswahili watatafuta nini? Nyumba ndogo?"

Ikawa desturi.

Nikitoka kazini, baada ya `kuwatupa' wafanyakazi wenzangu, nilianza awamu mpya ya kupiga tripu za daladala ...

Hapakuwa na tatizo. Japo konda, ambaye pia alikuwa ndiye mpiga-debe na mpambe, alikuwa `anapiga panga.' Makusanyo, bado chuma cha siku lilikuwa la kuvutia.

Mungu akupe nini! Man'ake huo usiku `serikali inakuwa imelala' - hamna matrafiki, walau huko kwenye njia za uswahlini. Ukiona `tageti' waendea kwa wakati wako!

Na hapo sikutaka `kuchezea wakati'. Ukipata tumia, ukikosa jutia. Hata kitambi kikaanza kuchomoza.

Hicho pengine ndio kilichonisaliti. Maana maneno yakaanza `kutembea' chini chini. Tena madereva wenzangu wale wale! Utafikiri wao `hawali' kwenye magari yao! Mswahili bwana! Kwa kuchukia `maendeleo' ya mtu?!

Sikujali.

Wembe ni ule ule!

Siku moja nikaamua kumchukua `dei waka' dereva wa daladala fulani iliyo juu ya mawe. Siku hiyo kondakta nikawa mwenyewe - ili kuzuia `kupigwa panga' pesa zinazokusanywa.

Sanyasanya iliendelea kama siku zote. "Sanyasanya Trans" kama ilivyojulikana mtaani, iliendelea kudunda uswahilini. Na pesa nilizokusanya siku ile zilinifanya nijue ukubwa wa `panga' lililokata pesa siku zote.

Ni wakati wa tripu ya mwisho, ya kupata pesa za kujazia mafuta, kizungumkuti kilipoanza.

Wakati `nawachuna' abiria nauli, abiria aliyeketi kwenye kona kiti cha nyuma akakataa kulipa.

"Siti ya mwisho, bado mmoja!" nilisema. "Halo we mwenye kapelo leta `uchache' huo!"

Lakini yule jamaa aliyekuwa amevaa kofia iliyofunika uso staili ya `ukitaka kumuua nyani" alikuwa anapuuza kelele zangu.

Nilipojaribu kufikiri ni kitu gani ananiringia, nikahisi labda kitambi!

"Halo usiku unauweka! Ikiwa ni ubosi ni huko huko ofisini kwako!"

Lile jamaa lilinitazama tu.

Au linavuta bangi? Hata likivuta! Shauri yake! N'nachojali ni michuzi tu!

"Halo usitutishe na kitambi chako cha mapuya! Tumbo hilo la mataputapu linakufanya ujione booosi! Nakwambia hapa umefika." Nilifoka.

Abiria wengine walitukodolea macho. Tayari wengine walishaanza kuambukizwa `ufyatu' wa yule jamaa.

"Asipolipa yule na sisi hatulipi." Walidai.

Hapo ndipo wazimu wote ukanipanda kichwani. Mtu huyu hawezi kunifanyia mapuuza kwenye gari `langu' halafu nikamucha vivi hivi tu!

Nahisi hata yeye alibaini sasa yatakuwa mengine. Ndiyo maana akatoa noti ya nauli kabla sijaongea zaidi. Nikamrudishia chenji, pungufu ya shilingi mia tano.

"Na mimi nikikunyima chenji hii utajisikiaje?"

Hakusema kitu.

Nikanyoosha mkono nimpe hela yake.

Mara, Lo!

Akatoa miwani ya jua aliyovaa usiku ule. Kisha akainua kofia aliyovaa.

Mama yake na mama!

Kumbe ni bosi, `mnene mkuu' wa ofisi!!

"Hizi zitakuwa ni fitna za watu!" niliwaza.

Nilihisi kutaka kwenda haja papo hapo. Sijui gavana iliyookoa jahazi ilitoka wapi! Vinginevyo ingekuwa simulizi.

Nilichanganyikiwa.

Hata abiria wengine sikuweza kuchukua nauli zao.

Kesho yake niliitwa ofisini kwa mkuu.

"Kijana, maisha unayapeleka vibaya! Ungekuwa japo unaendesha mwenyewe, pengine ningeelewa, japo kidogo. Kosa ulilofanya unastahili adhabu kali!"

Ama kweli. Siku ya kutembea uchi ndiyo unayokutana na mkweo!

Hivi ninapokumegea stori bosi bado 'anafikiria' adhabu ya kutoa. Sijui bosi atatoa adhabu gani? Sijui atanihamishia ofisi yenye meza bila kasma? Au atanipeleka kusoma? Kunifukuza hawezi - maana ni urasimu mkubwa - ndiyo raha ya ajira ya umma. Mwenzenu niko roho juu!

mwisho.

Kwa hisani ya Chumvi Mtembezi


Amazon product ASIN 144866411X
 
Samahani Bosi lakini naona unatania maisha ya watu wa maeneo hayo, ama hujawahi kufika!
How can you possibly, sensibly say watu kule wanaishi maisha mazuri?!
% ngapi wana access na clean water? Je, huduma ya afya? Umeme? Transport? Akina mama wanakufa wakati wa kujifungua kisa mbali na huduma ya afya, ama wakienda hakuna wataalam. Hospitali daktari afanya upasuaji kwa kibatari- wagonjwa kibao wanakufa.
na nyumba walizojenga, ni nyumba bora au bora nyumba!
Acha kutania, maisha ni mabaya- watu hawana alternative, inabidi wayapende hivyo hivyo.
Achana na Alipotaja mkuu
Case Study Moshi Rural
 
Swali la msingi ni kuwa hivi kweli ikiingia serikali makini ikakata mianya yote ya "kipato cha ziada" na kulazimisha watu kuishi kwa malipo yao ya mwezi, wangapi kati yetu wataipigia kura serikali hiyo?
...🤔🤔🤔..wapo watakaoipigia kura tena wengi tu, subiri siku ya uchaguzi utaona.😂😂😂
 
The higher you go the hotter it became.....Mimi nilishaamua sichangii mchango wowote ambao sio wa matatizo na tatizo lenyewe liwe ni msiba au sort of that nature na mchango wenyewe ni mpaka niwe nazo....chakula ni dagaa, combat (maharage) na spinach au mcicha with ugali au mchele. Gari nimeliacha ni daladala kwa kwenda mbele...kama ni kariakoo - posta au ubungo -mwenge ninatembea.

Maisha ni magumu lakini inabidi tukomae nayo mpaka wazee huko juu wastaafu au wafe.
2012 JK
2020 JPM na hali bado n ile ileee
i thnk tatzo sio viongoz, tatzo ni ss wananchi+serikali kutotambua tatzo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
UKISIKIA "kuisoma NAMBA"
Maana yake halisi ndo hi
tapatalk_1581743534682.jpeg
tapatalk_1581743543682.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kila Pahala Ulaji!​

KWAMBA kila mtu `hula' mahala pake pa kazi, hilo halikuwa geni, hususan ofisini kwetu.

Tangu `mnene' wa kwanza, mpaka `kapuku' wa mwisho, kila mmoja huketi mkao wa kula kwenye `wigo' unaomkinga asionekana na `vishingo' wasiokawia kuweka `mikingamo' ya kujaza michanga kitumbua cha mtu.

Ukitilia maanani mishahara-njiwa na marupurupu njaa yenye kupigwa paranja na wale watoza-ushuru wasio na simile, sera ikawa ni kutumia `bongo' katika nchi ya Ruksa, mradi tu usidakwe.

Madhali mtu umekabidhiwa ofisi na meza - na ruzuku au tuseme, kasma, hasa iliyonona, hukuwa na haja ya promosheni, wala ya kwenda shule eti kuongeza `unga.' Huo unga au mchele wa nyongeza unaugema na kuumega mumo humo - mradi tu penye unyonge upenyeze matonge, au penye udhia watupia rupia!

Kwa mtaji huo, wale ambao `ofisi' zao zilikuwa kavu, kwa maana ya kukosa pa kuchota, au cha kugema, walifanya kila namna ya kupata `transfa' ndogo ndogo huku na kule kwenye ofisi, bora mkono uende kimiani.

Kwa upande wangu, nilionekana kupendelewa zaidi. Hata madereva wenzangu wakati mwingine waliniambia bayana wakati tukisogoa.

"Mwenzetu unakatiwa mapande ya ulaji tu," alisema Bwana Shaibu, dereva wa bosi mkuu. "Miye kila wakati nipo na kingunge-mkuu wa ofisi! Nitaiba saa ngapi? Gari yenyewe Nissan Patrol. Roho juu kila wakati kuogopa majambazi. Hata `kusanya' siwezi!" Alilalama.

Wakati huo mimi naendesha gari la maji machafu. Nikipiga tripu mbili za kampuni, napiga tano za kwangu. Na kwa kuwa gari lile ni la kubeba (ashakum) kinyesi, wanene wa kampuni hawakutupa macho yao kwangu. Mradi ilikuwa ni ulaji mtupu wa kimyakimya. Hata madereva wenzangu hawakushtuka.

Machale yalianza kuwacheza waliposikia nimesimamisha `banda' pale bondeni.

Nikahamishiwa kwenye `kijiko' - gari la kuchimbia na kung'oang'oa - kwa imani sitakuwa na cha `kuhamisha.' Wakati huo mtindo wa kutumia `nyoka' - mipira ya kutolea petroli na dizeli - ulikuwa umedhibitiwa. Lakini huwezi kumdhibiti mwanadamu, hasa ngurumbili huyo anapokuwa wa Bongoland. Ulaji wa kwenye `kijiko' ukawa mkubwa zaidi, maana katika masaa ya kazi, nusu nayatumia nikiwa `kontrakta bubu.'

Mpaka walipostuka, nilishavuna vya kutosha. Siku nilipohamishiwa kwenye gari la kubeba wafanyakazi, wenzangu walijua wazi chizi limepewa manati, sokoni!

"Au mwenzetu unakula na wakubwa?" walinitania.

"Kwenda zenu! Nani asiyegema mahala pake pa kazi?" Niliwajibu kwa masikhara.

"Ah! Lakini wewe mwenzetu unawekwa kwenye vitengo vya ulaji tu!"

Na kweli. Kwenye gari hili la abiria kulikuwa na pesa za nje-nje tu.

Mara ya kwanza nilikuwa naogopa kuligeuza daladala-bubu (sanyasanya), hususan asubuhi, kwa vile "wanga wengi." Lakini kadiri nilivyoshika hatamu za uongozi wa basi lile, ndivyo nilivyozidi kujiamini.

"Kwanza wanene wote wa kampuni wanakaa uzunguni. Halafu wote wana magari. `Dili' zao zote na wazito wenzao. Huku uswahili watatafuta nini? Nyumba ndogo?"

Ikawa desturi.

Nikitoka kazini, baada ya `kuwatupa' wafanyakazi wenzangu, nilianza awamu mpya ya kupiga tripu za daladala ...

Hapakuwa na tatizo. Japo konda, ambaye pia alikuwa ndiye mpiga-debe na mpambe, alikuwa `anapiga panga.' Makusanyo, bado chuma cha siku lilikuwa la kuvutia.

Mungu akupe nini! Man'ake huo usiku `serikali inakuwa imelala' - hamna matrafiki, walau huko kwenye njia za uswahlini. Ukiona `tageti' waendea kwa wakati wako!

Na hapo sikutaka `kuchezea wakati'. Ukipata tumia, ukikosa jutia. Hata kitambi kikaanza kuchomoza.

Hicho pengine ndio kilichonisaliti. Maana maneno yakaanza `kutembea' chini chini. Tena madereva wenzangu wale wale! Utafikiri wao `hawali' kwenye magari yao! Mswahili bwana! Kwa kuchukia `maendeleo' ya mtu?!

Sikujali.

Wembe ni ule ule!

Siku moja nikaamua kumchukua `dei waka' dereva wa daladala fulani iliyo juu ya mawe. Siku hiyo kondakta nikawa mwenyewe - ili kuzuia `kupigwa panga' pesa zinazokusanywa.

Sanyasanya iliendelea kama siku zote. "Sanyasanya Trans" kama ilivyojulikana mtaani, iliendelea kudunda uswahilini. Na pesa nilizokusanya siku ile zilinifanya nijue ukubwa wa `panga' lililokata pesa siku zote.

Ni wakati wa tripu ya mwisho, ya kupata pesa za kujazia mafuta, kizungumkuti kilipoanza.

Wakati `nawachuna' abiria nauli, abiria aliyeketi kwenye kona kiti cha nyuma akakataa kulipa.

"Siti ya mwisho, bado mmoja!" nilisema. "Halo we mwenye kapelo leta `uchache' huo!"

Lakini yule jamaa aliyekuwa amevaa kofia iliyofunika uso staili ya `ukitaka kumuua nyani" alikuwa anapuuza kelele zangu.

Nilipojaribu kufikiri ni kitu gani ananiringia, nikahisi labda kitambi!

"Halo usiku unauweka! Ikiwa ni ubosi ni huko huko ofisini kwako!"

Lile jamaa lilinitazama tu.

Au linavuta bangi? Hata likivuta! Shauri yake! N'nachojali ni michuzi tu!

"Halo usitutishe na kitambi chako cha mapuya! Tumbo hilo la mataputapu linakufanya ujione booosi! Nakwambia hapa umefika." Nilifoka.

Abiria wengine walitukodolea macho. Tayari wengine walishaanza kuambukizwa `ufyatu' wa yule jamaa.

"Asipolipa yule na sisi hatulipi." Walidai.

Hapo ndipo wazimu wote ukanipanda kichwani. Mtu huyu hawezi kunifanyia mapuuza kwenye gari `langu' halafu nikamucha vivi hivi tu!

Nahisi hata yeye alibaini sasa yatakuwa mengine. Ndiyo maana akatoa noti ya nauli kabla sijaongea zaidi. Nikamrudishia chenji, pungufu ya shilingi mia tano.

"Na mimi nikikunyima chenji hii utajisikiaje?"

Hakusema kitu.

Nikanyoosha mkono nimpe hela yake.

Mara, Lo!

Akatoa miwani ya jua aliyovaa usiku ule. Kisha akainua kofia aliyovaa.

Mama yake na mama!

Kumbe ni bosi, `mnene mkuu' wa ofisi!!

"Hizi zitakuwa ni fitna za watu!" niliwaza.

Nilihisi kutaka kwenda haja papo hapo. Sijui gavana iliyookoa jahazi ilitoka wapi! Vinginevyo ingekuwa simulizi.

Nilichanganyikiwa.

Hata abiria wengine sikuweza kuchukua nauli zao.

Kesho yake niliitwa ofisini kwa mkuu.

"Kijana, maisha unayapeleka vibaya! Ungekuwa japo unaendesha mwenyewe, pengine ningeelewa, japo kidogo. Kosa ulilofanya unastahili adhabu kali!"

Ama kweli. Siku ya kutembea uchi ndiyo unayokutana na mkweo!

Hivi ninapokumegea stori bosi bado 'anafikiria' adhabu ya kutoa. Sijui bosi atatoa adhabu gani? Sijui atanihamishia ofisi yenye meza bila kasma? Au atanipeleka kusoma? Kunifukuza hawezi - maana ni urasimu mkubwa - ndiyo raha ya ajira ya umma. Mwenzenu niko roho juu!

mwisho.

Kwa hisani ya Chumvi Mtembezi
Stori tamu Sana, umemaliza vizur

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom