Unaishi kwa kipato chako?

Kutokana na hali ngumu ya kiuchumi imenilazimu kuanza kibarua kingine ku "supplement" ajira yangu kuu. Gharama ya nyuma, makadi kibao, na vitu vingine ninavyolipia ambavyo hata sivihitaji imenifanya nijikute nabadilisha sana mtindo wa maisha.

a. Hakuna kwenda sinema kila weekend;
b. Hakuna kula out (imebidi nijifunze kupika kitu kingine zaidi ya wali na maharage ya makopo)
c. Hakuna kwenda mjini kwa gari (naendesha hadi Mall, napaki nakuchukua UDA - SmartBus) siku nikiwa na mizunguko mingi


Sasa tatizo kubwa lililopo nikilinganisha na nilipokuwa nyumbani ni kuwa hapa kwenye kibarua kikuu na hata hicho cha pili "hakuna mitkasi" ya kuweza kusupplement kipato changu na hasa shughuli nyingi nizifanyazo. Wakati mwingine hali inakuwa ngumu na ninatamani kungekuwa na "njia" ya mkato ya "kibongo bongo" kuweza kujipatia "kipato cha ziada" bila kuhenyeka sana.

Sasa hili limenifanya nijiulize mtumishi wa umma au hata sekta binafsi (ambaye si mmiliki) anatumia njia gani kusupplement kipato chake na kuafford lifestyle yake? Hivi kwa kipato chako peke yake unaweza kumudu maisha yako au itabidi ufanye mabadiliko makubwa ya jinsi unavyoishi? Je yawezekana kumbe wengi wetu tukipewa nafasi ya kula, tutatafuna bila kukaribishwa na kumegua bila hata kunawa mikono? Je yawezekana baadhi yetu ambao tunatamani kushika nafasi fulani ya kiuongozi tuna upotential fisadism wa aina fulani?

Endapo mianya yote ya ulaji ikifungwa (no per diems, posho nyingine kama za vikao, za safari, za hali ngumu n.k) utafanya nini? Itakuwaje kama bosi wako anataka uwepo kazini kweli kwa masaa nane na usiende kushughulikia "miradi" yako wakati wa kazi? Vipi kama yule mtu wa supply akiamu kuzingatia sheria na kuhakikisha kitu hakitoki isipokuwa kwa saini na kwa idadi kamili; yaani njia zote za ujanja za kujipatia kipato zikibanwa utaweza kuishi kwa kipato chako au kutafuta shughuli nyingine halali katika muda wako wa ziada?

Je yawezekana tunaishi katika utamaduni wa kijanja janja kiasi kwamba ufisadi siyo suala la wenye nguvu tu bali pia watu wa chini ambao maisha yao yote wamejifunza "kuula" na hivyo kila mtu anapopata nafasi ya kutumikia kitu cha kwanza anachofikiria ni jinsi gani nafasi hiyo itampa kipato zaidi ya kile kilichoko kwenye mkataba?

Bila njia za ujanja ujanja tunaweza kweli kuishi kwa kipato chetu cha kawaida.

Heshima mbele mkuu MMJ.
Tunaweza kuishi maisha mazuri kwa pato halali kama tutazingatia yafuatayo.
{1}Kupanga matumizi kutokana na pato lako halali.
Pengine hili linaweza kuwa tatizo kubwa kwa watanzania wengi,mara nyingi tunapenda kutumia fedha zetu bila kuangalia pato letu halisi.Ninaposema kupanga matumizi kutokana na pato halali,maana yake ni kuanzia nyumba tunazopanga,vyakula tunavyokula,usafiri tunaotumia na nk.

{2}Kuwa mbunifu kuongeza pato kwa njia halali.hii itategemea zaidi na utaalamu wa mtu kwa mfano mimi nilikuwa mhasibu GTEA ingawa kampuni imeshindwa kufanyakazi sijawahi kutetereka kwasababu nililikuwa natumia ujuzi wangu kufunga mahesabu kwa kampuni zaidi ya tatu.

{3}Kusave fedha hata kama ni kidogo kwaajili ya kuwekeza.Hili nalo ni tatizo kubwa kwa watanzania wengi.Hatuna utamaduni wa kusave tunapenda kutumia hata kama pato tunazopata litaongezeka ndivyo matumizi yetu yanavyoongezeka.
 
siyo kuhalalisha ndugu yangu bali kujaribu kufocus tatizo letu hasa ni nini? ndugu yangu Nyani ana msemo kuwa "Waafrika ndivyo tulivyo". Wengi wetu tunakerwa na ufujaji wa mali ya umma na matumizi mabaya ya ofisi (hasa inapohusu wanasiasa). Najaribu kuona kuwa yawezekana tunawanyoshea kidole kimoja wao, vitatu sisi wenyewe na kimoja Mungu shahidi yetu.

Swali la msingi ni kuwa hivi kweli ikiingia serikali makini ikakata mianya yote ya "kipato cha ziada" na kulazimisha watu kuishi kwa malipo yao ya mwezi, wangapi kati yetu wataipigia kura serikali hiyo?

Mwanakijiji,

Unataka kuongea nini hapa? Ukitumia njia za mkato kuongezea pato lako ni wizi tu sawa na wa akina Chenge.

Kama unaongeza pato kwa kufanya kazi zaidi au kuwa na kazi zaidi ya moja nitaelewa lakini sio kuanza kuhamisha vifaa vya kampuni au kushinda kwenye miradi yako badala ya kufanya kazi uliyoajiriwa. Kama unatimiza majukumu yako yote na bado una muda kidogo wa kufanya mambo yako mengine hapo mimi sina tatizo.

Unapozembea kazi unatesa wateja wako, unamwingizia hasara mwajiri wako na pia unawatesa wafanyakazi wenzako ambao inabidi wafanye kazi zaidi shauri ya uzembe wako.
 
Mwanakijiji,

Unataka kuongea nini hapa? Ukitumia njia za mkato kuongezea pato lako ni wizi tu sawa na wa akina Chenge.

Kama unaongeza pato kwa kufanya kazi zaidi au kuwa na kazi zaidi ya moja nitaelewa lakini sio kuanza kuhamisha vifaa vya kampuni au kushinda kwenye miradi yako badala ya kufanya kazi uliyoajiriwa. Kama unatimiza majukumu yako yote na bado una muda kidogo wa kufanya mambo yako mengine hapo mimi sina tatizo.

Unapozembea kazi unatesa wateja wako, unamwingizia hasara mwajiri wako na pia unawatesa wafanyakazi wenzako ambao inabidi wafanye kazi zaidi shauri ya uzembe wako.

Mtanzania huu mjadala nimeupenda sana kuliko mijadala mingine tuliyoifanya hapa kwani huu unatuangalia sisi wenyewe na attitudes zetu kuhusu kazi, kuwajibika, usawa, uzalendo na mipango ya baadaye. Hadi hivi sasa kuna kila dalili kuwa hali ngumu ya maisha/tamaa ya maisha bora zaidi inawafanya watu kujaribu kujitajirisha kwa njia za mkato na kwa harraka.

Hata hivyo bado swali la msingi halijaangaliwa kwa kina kuwa endapo chama au mwanasiasa akijitokeza na kusema anataka kuziba mianya hii ya wizi, na ujanja ujanja mtu huyo/watu hao wataungwa mkono au wataonekana wanajaribu kuwanyang'anya watu 'halali' yao?
 
Naona bado sijakufahamu vizuri, labda tujadili hili kwa mifano halisi kwa yale yanayotokea kila siku katika sehemu mbalimbali za kazi.

Mfano wakusanyaji kodi za kila siku(service charge) wa Manispaa, hasa sokoni(marikiti). Hawa wana tabia ya kuwa na vitabu viwili viwili ya stakabadhi, ambapo kimoja ni kwa ajili ya mapato yake na kimoja ni kwa ajili ya kupeleka mapato ofisi kwake. Aina hii ya wizi unawaweka katika kundi gani? na aina hii ya ufisadi ukuhalalishwa utaisadia vipi Manispaa na serikali kuu kwa pamoja?

Wala sisemi mapato kama hayo ya rushwa, nazungumzia yale yanayozungumziwa kama posho, perdiems ma hata malipo mengine halali ambayo yanapatikana kwa ujanjaujanja kama ku-inlfate bei za vitu. nazungumzia fedha ambazo zimo katika bajeti lakini hazijawekwa moja kwa moja kama sehemu ya mapato la lazima ya mfanyakazi
 
Mtanzania huu mjadala nimeupenda sana kuliko mijadala mingine tuliyoifanya hapa kwani huu unatuangalia sisi wenyewe na attitudes zetu kuhusu kazi, kuwajibika, usawa, uzalendo na mipango ya baadaye. Hadi hivi sasa kuna kila dalili kuwa hali ngumu ya maisha/tamaa ya maisha bora zaidi inawafanya watu kujaribu kujitajirisha kwa njia za mkato na kwa harraka.

Hata hivyo bado swali la msingi halijaangaliwa kwa kina kuwa endapo chama au mwanasiasa akijitokeza na kusema anataka kuziba mianya hii ya wizi, na ujanja ujanja mtu huyo/watu hao wataungwa mkono au wataonekana wanajaribu kuwanyang'anya watu 'halali' yao?

Mzee Mwanakijiji,

Haya mambo yote ni possible ili mradi hao wakubwa wawe fair wanapotaka ku implement change. Haina maana wao wanajipangia per diem kubwa huku wanaacha wafanyakazi wa chini wanafunga mikanda.

fairness ni kitu muhimu sana unapotaka kufanya changes kubwa kama hizi.

Wakisema wote tufunge mikanda ili kuijenga nchi yetu naamini wengi tutakubali ila na wao waache kununua mashangingi yasiyo na maana na ujinga mwingine mwingi ambao umewajaa viongozi wetu.

Mfano mzuri huku majuu watu wengi middle class wako happy kulipa tax zaidi kama inatumika vizuri na kusaidia wananchi wengine ambao hawana bahati ya kuwa na plenty kama wao.

Tatizo la Tanzania nimewahi kukutana na watu wengi ambao wanaona raha kuwa matajiri kwenye umaskini. Mimi ni bora kuliko maskini kwenye utajiri, kuliko kuzungukwa na omba omba kila sehemu mpaka inakuwa shida.
 
Pasco, nimeshindwa 'kukuelewa'.

Inawezekanaje mwandishi 'aliyehongwa' kuweza ku retain/maintain objectivity?

Mwandishi anamtumikia nani? mwajiri? mtoa habari? au msomaji (mteja)? Kama serikali inatakja kufanya uwezeshaji basi iwe ni kwa vyombo vya habari kwa ujumla na si kwa individual journalists. Hii kwa kiasi inaweza kupunguza bias.

Investigative journalism kwa maoni yangu inatakiwa igharimiwe na chombo cha habari chenyewe and then wana-recover hiyo cost kutoka kwa msomaji (mteja).

Safari,semina, makongamano etc yasiyo na tija nadhani ndio hasa maana halisi ya ufisadi.
.
Jamani wana JF wenzangu, lazima tukubali kuwa Tanzania is a poverty stinking nation, yaani ni nchi yenye umasikini uliokithiri left, right and centre. Hivyo vibahasha vya 20,000 kwa waandishi sio hongo, they are nothing, ni nauli tuu and they have nothing to do with the story. Nakubaliana na wewe kwa mtu wa kawaida kusikia kuna vibahasha vya waandishi, anaweza akachanganya na hongo kwa waandishi bongo, wanapokea hivyo vibahasha kila siku na wanaandika very objective stories na sometimes very critical. Ili kuthibitisha bahasha has nothing to do with story, wako waliovamia fani hii ya uandishi wa habari kwa ajili tuu ya kuvuta hivyo vibahasha na hawaandikii chombo chochote (makanjanja).
Vyombo vya habari vyote Tanzania ni masikini,ukiondoa vile vya umma vinavyoweza chotewa toka hazina, vingine vyote ni masikini tuu hata hivi imara kama ITV na vyombo vya habari vya IPP vinavyoonekana angalau vinawalipa vizuri waandishi wake, bado ni masikini tuu na bila kuwezeshwa hawana jeuri ya kuzama ndani ya serious investigative journalism. Bila uwezeshaji, hakuna chombo cha habari cha bongo, kina jeuri ya kutuma reporter katika mikutano ya kimataifa ndio maana serikali imekubali kusaidia reporting ya UN General Assembly.
Naomba unielewe, uwezeshaji kwa waandishi sio hongo, ila pia nakiri, hongo kwa waandishi ipo!.
 
Sina muda wa kuchambua uliyotasema yote lakini nilichonukuu ni summary ya fikra zako - very sad way of thinking and this is what is causing Tanzania to go to the dogs! Kama wewe ungekuwa kweli fukara wa Rukwa ambaye unategemea 40,000 ya bahatibahati ungeweza kusema hivyo, but I am sure the poor do not say that, save for those who sell their mothers, fathers, sistrers, brothers, daughters and sons who are albinos to be slaughtered for the color of their skin. Unapoiba na vijidili vyako na kuwauza ndugu zako maalbino or any obnoxious deal na kusema eti 'the end justifies the means' You are basically saying 'screw every other human being as long as I can live the life I want, even if I cannot afford it' . It is your right but it is to be condemned and it is despicable.
I think that from this point of view you are right, you are like the mafisadiz that we are all complaining about! At least you are honest. I personally am ready to say that I have never accepted bribery and have only been forced to give in unusual circumstances. And I am proud of it and I let everyone know, hata nikiitwa bwege!
Sina nia ya kujitetea ila huo ndio ukweli wa maisha ya Mtanzania kama mimi na wengine wengi, our life is a constant struggle for existace ili angalau mkono uende kinywani. Kama tafsiri ya yako kwa masikini anayelala njaa akaokota embe limeanguka kwenye mwembe wa mtu ulioko kando ya barabara akalila, marawenye mwembe kamuona na kumwitia mwizi, watu wakajitokeza bila kuuliza wakapiga, wakamwagia mafuta ya taa, wakanchoma moto 'mwizi' na wewe ukakubali mwizi huyo ni sawa na wale wanaotumia kalamu kukwapua mabilioni, walipojulikana, wakapewa muda wa kurejesha, huku wakitayarishiwa vip room gerezani. Kama yule wa embe ni fisadi, na mimi nakiri kuwa ni fisadi wa embe lakini sio fisadi wa EPA.
Naendelea na Struggle for Existance na ili nisurvive, I have to be the fittest lakini mwisho wa siku, the end itajustfy the means nilizotumia kusurvive while the unfortunate ones by then wamesha perish.
Nakiri Susuviri kwa hayo uliyoyasema, wewe ni miongoni mwa wachache mliobarikiwa kuifuata falsafa ya Nyerere kwa vitendo. Watu wa Nyerere type ndio wanaqendelea kuishia (Abel Mwanga) na bado wapo, wakina Kaduma, Prof.Shivji, Jaji Warioba na wengine wengi ambapo as days go by, hamtaweza kusurvive kwenye unjust system iliyopo na mtaperish without leaving any mark, ikimaanisha you are not fit to survive na sisi tunaokubali struggle, tutakaoendelea kustruggle to reach a point only the fittest will survive na tutakuja kuhukumiwa au kupongezwa kwa kusurvive huku tukiwa justified by being there till the end and not by the means tulizo tumia. The End Justify The Means
 
unapouliza mtu anaishi kwa kipato chake kuna swali la pili la msingi linafuta. kipato kipi? halali au kisicho halali. mfano mzuri ni wafanyakazi wa serikali mishara yao tunaijua lakini life style is quite opposite!!!
 
Sina nia ya kujitetea ila huo ndio ukweli wa maisha ya Mtanzania kama mimi na wengine wengi, our life is a constant struggle for existace ili angalau mkono uende kinywani. Kama tafsiri ya yako kwa masikini anayelala njaa akaokota embe limeanguka kwenye mwembe wa mtu ulioko kando ya barabara akalila, marawenye mwembe kamuona na kumwitia mwizi, watu wakajitokeza bila kuuliza wakapiga, wakamwagia mafuta ya taa, wakanchoma moto 'mwizi' na wewe ukakubali mwizi huyo ni sawa na wale wanaotumia kalamu kukwapua mabilioni, walipojulikana, wakapewa muda wa kurejesha, huku wakitayarishiwa vip room gerezani. Kama yule wa embe ni fisadi, na mimi nakiri kuwa ni fisadi wa embe lakini sio fisadi wa EPA.
Naendelea na Struggle for Existance na ili nisurvive, I have to be the fittest lakini mwisho wa siku, the end itajustfy the means nilizotumia kusurvive while the unfortunate ones by then wamesha perish.
Nakiri Susuviri kwa hayo uliyoyasema, wewe ni miongoni mwa wachache mliobarikiwa kuifuata falsafa ya Nyerere kwa vitendo. Watu wa Nyerere type ndio wanaqendelea kuishia (Abel Mwanga) na bado wapo, wakina Kaduma, Prof.Shivji, Jaji Warioba na wengine wengi ambapo as days go by, hamtaweza kusurvive kwenye unjust system iliyopo na mtaperish without leaving any mark, ikimaanisha you are not fit to survive na sisi tunaokubali struggle, tutakaoendelea kustruggle to reach a point only the fittest will survive na tutakuja kuhukumiwa au kupongezwa kwa kusurvive huku tukiwa justified by being there till the end and not by the means tulizo tumia. The End Justify The Means

Pasco my brother, najua umekata tamaa and forgive my previous harsh remarks, you have not seen better, ndiyo maana umeform opinion that it's the Jungle law that rules.
But let me tell you, ndugu yangu, unapoishi kwa kufuata principle unalala vizuri sana!
Mwenzetu Ngongo amezungumzia suala moja muhimu sana- unajipangia maisha yanayoendana na kipato chako. Hii ni point muhimu. Nasikitika sana kuona vijana ambao wanaona aibu kwa sababu hawana simu ya mkononi. Tunaweza wengi wetu tukaona that it is a basic human right kuwa na simu ya mkononi lakini ukweli ni kwamba it is not a right but a priviledge. Sasa unakuta binti anajiuza eti apate simu ya mkononi au kijana anaiba alafu wakitoa umaskini kama excuse tunawasapoti, that is wrong. The same applies to those so-called mafisadi (I am abit wary of these labeling maana nakumbukia enzi zile za ulanguzi mtu ukiwa na toothpaste 2 unaitwa mlanguzi)
Anyway, the corrupt politicians and fake businessmen who steal and swindle people are not different, yet because they stole big we celebrate them because they proved to be 'smarter' and they 'beat the system'. That is a wrong approach.
Katika ishu hii nina mengi sana ambayo ningeweza kusema because actually Mwanakijiji is right, it goes to the heart of the issues in Tanzania starting from corruption to killing of albinos etc. Maybe one of these I will write my book about this! :)
 
Kutokana na hali ngumu ya kiuchumi imenilazimu kuanza kibarua kingine ku "supplement" ajira yangu kuu. Gharama ya nyuma, makadi kibao, na vitu vingine ninavyolipia ambavyo hata sivihitaji imenifanya nijikute nabadilisha sana mtindo wa maisha.

a. Hakuna kwenda sinema kila weekend;
b. Hakuna kula out (imebidi nijifunze kupika kitu kingine zaidi ya wali na maharage ya makopo)
c. Hakuna kwenda mjini kwa gari (naendesha hadi Mall, napaki nakuchukua UDA - SmartBus) siku nikiwa na mizunguko mingi


Sasa tatizo kubwa lililopo nikilinganisha na nilipokuwa nyumbani ni kuwa hapa kwenye kibarua kikuu na hata hicho cha pili "hakuna mitkasi" ya kuweza kusupplement kipato changu na hasa shughuli nyingi nizifanyazo. Wakati mwingine hali inakuwa ngumu na ninatamani kungekuwa na "njia" ya mkato ya "kibongo bongo" kuweza kujipatia "kipato cha ziada" bila kuhenyeka sana.

Sasa hili limenifanya nijiulize mtumishi wa umma au hata sekta binafsi (ambaye si mmiliki) anatumia njia gani kusupplement kipato chake na kuafford lifestyle yake? Hivi kwa kipato chako peke yake unaweza kumudu maisha yako au itabidi ufanye mabadiliko makubwa ya jinsi unavyoishi? Je yawezekana kumbe wengi wetu tukipewa nafasi ya kula, tutatafuna bila kukaribishwa na kumegua bila hata kunawa mikono? Je yawezekana baadhi yetu ambao tunatamani kushika nafasi fulani ya kiuongozi tuna upotential fisadism wa aina fulani?

Endapo mianya yote ya ulaji ikifungwa (no per diems, posho nyingine kama za vikao, za safari, za hali ngumu n.k) utafanya nini? Itakuwaje kama bosi wako anataka uwepo kazini kweli kwa masaa nane na usiende kushughulikia "miradi" yako wakati wa kazi? Vipi kama yule mtu wa supply akiamu kuzingatia sheria na kuhakikisha kitu hakitoki isipokuwa kwa saini na kwa idadi kamili; yaani njia zote za ujanja za kujipatia kipato zikibanwa utaweza kuishi kwa kipato chako au kutafuta shughuli nyingine halali katika muda wako wa ziada?

Je yawezekana tunaishi katika utamaduni wa kijanja janja kiasi kwamba ufisadi siyo suala la wenye nguvu tu bali pia watu wa chini ambao maisha yao yote wamejifunza "kuula" na hivyo kila mtu anapopata nafasi ya kutumikia kitu cha kwanza anachofikiria ni jinsi gani nafasi hiyo itampa kipato zaidi ya kile kilichoko kwenye mkataba?

Bila njia za ujanja ujanja tunaweza kweli kuishi kwa kipato chetu cha kawaida.

Mwanakijiji:

Kwa maoni yangu binafsi kujiongezea kusiko rasmi ni utamaduni uliojengeka kwa muda mrefu kwa watanzania wengi. Na kama mishahara itaongezwa na kufikia kiwango cha kumudu mahitaji yetu. Watanzania bado wataendelea kuiba. Watu wanaofanyakazi BOT au TRA wanashida gani? Lakini wengi hawachelewi kuvuta.

Kilichonifanya niachane na ubongobongo wangu ni kuwa kazi ninazofanya, wana-keep records. Na kila mwajiri anafanya background checks. Hivyo nimehamua kuokoka kwa sababu ya kulinda profession yangu.

Lakini ningekuwa Tanzania inawezekana nisingebadilika kwa sababu ni waajiri wachache wanaochukua kumbukumbu za waajiri waliotangulia.
 
Mhmmm please let us look at the comparisons we are making. Some are misleading. Kama USA tiketi ya sinema ni USD 7 na Tanzania tiketi ni Tshs. 8,000 then it is cheaper in Tanzania hasa ukiangalia market exchange ya USD kwa sasa ambayo inafikia hata Tshs 1350 kwa dola. Hivyo huko marekani gharama ya tiketi moja kwa pesa ya Tanzania ni Shs. 9,450.00. Sasa ni wapi wanaangalia sinema kwa bei ya juu, Tanzania au Marekani?
 
siyo kuhalalisha ndugu yangu bali kujaribu kufocus tatizo letu hasa ni nini? ndugu yangu Nyani ana msemo kuwa "Waafrika ndivyo tulivyo". Wengi wetu tunakerwa na ufujaji wa mali ya umma na matumizi mabaya ya ofisi (hasa inapohusu wanasiasa). Najaribu kuona kuwa yawezekana tunawanyoshea kidole kimoja wao, vitatu sisi wenyewe na kimoja Mungu shahidi yetu.

Swali la msingi ni kuwa hivi kweli ikiingia serikali makini ikakata mianya yote ya "kipato cha ziada" na kulazimisha watu kuishi kwa malipo yao ya mwezi, wangapi kati yetu wataipigia kura serikali hiyo?

Mkuu Mwanakijiji hao uliyoandika ni sahihi kabisa.
Sikumbuki mwaka lakini,nakumbuka mgomo wa wafanyakazi uliopangwa na Mpangala ukafeli miaka ya nyuma. Niliongea na mama mmoja sekretari wa mkuu wa mkoa akasema yeye pamoja na mshahara kuwa mdogo lakini hawezi goma kwa kuwa anafidia kipato chake kwa kuongea na dereva wa lori la hapo mkoani na wanafanya trip za mchanga then wanagawana. Analetewa mkaa kwa bei ya porini. Serikali yote haya inajua, lakini inaelewa pale itakapoamua kuziba mianya hii ndipo watakapotambua hasira za wananchi.

Kwa upande wa pili hatua a kudhibiti mianya ya ulaji (ingawa ni ndoto)itakuwa na faida sana kwa sisi watanzania. Kwani pesa zitaweza kukusanywa katika kapu vizuri bila kuvuja si kama ilivyosasa, then serikali itakuwa na pesa ya kutosha kutoa mishahara mizuri wa watanzania. hivi sasa watu wanajichukulia kabla a kunawa mikono wala kukaribishwa.

Lakini serikali ya CCM kwa kutambua haya yote, wameitumia nafasi hii ya kukaa kimya kama rushwa ili wananchi wasisikie makali ya maisha na kuwapigia kelele. Mwakijiji wakibana mianya bila kuongeza mishahara nchi haitakalika, maandamano na migomo haitaisha mpaka kieleweke.

 
Mwanakijiji,

.."mapato ya ziada" ya wafanyakazi yanalipwa na serikali.

..serikali inapaswa kuboresha mishahara na mafao ya watumishi wake ili wasilazimike kujitafutia "mapato ya ziada."

..hatua hiyo iende sambamba na kuweka sheria kali dhidi ya watumishi wadokozi na wabadhirifu.

..tufike mahali kwamba mtumishi wa umma aogope kudokoa na kuleta uzembe kazini.
 
MJ kama una miaka chini ya 40 basi ningejushauri ku invest on yourself. Kama una degree au masters basi soma software zenye market kama SAP n.k . Vilevile unaweza kusoma certification courses kama project mgmt, CPA, CMA, n.k. Vilevile Invest kwenye uraia kama huna kwani kuna nafasi nyingi za serikali zinakuja. Mawazo yangu ni kwa wanaoishi USA.
 
Kila Pahala Ulaji!​

KWAMBA kila mtu `hula' mahala pake pa kazi, hilo halikuwa geni, hususan ofisini kwetu.

Tangu `mnene' wa kwanza, mpaka `kapuku' wa mwisho, kila mmoja huketi mkao wa kula kwenye `wigo' unaomkinga asionekana na `vishingo' wasiokawia kuweka `mikingamo' ya kujaza michanga kitumbua cha mtu.

Ukitilia maanani mishahara-njiwa na marupurupu njaa yenye kupigwa ‘paranja’ na wale watoza-ushuru wasio na simile, sera ikawa ni kutumia `bongo' katika nchi ya Ruksa, mradi tu usidakwe.

Madhali mtu umekabidhiwa ofisi na meza - na ruzuku au tuseme, kasma, hasa iliyonona, hukuwa na haja ya promosheni, wala ya kwenda shule eti kuongeza `unga.' Huo unga au mchele wa nyongeza unaugema na kuumega mumo humo - mradi tu penye unyonge upenyeze matonge, au penye udhia watupia rupia!

Kwa mtaji huo, wale ambao `ofisi' zao zilikuwa kavu, kwa maana ya kukosa pa kuchota, au cha kugema, walifanya kila namna ya kupata `transfa' ndogo ndogo huku na kule kwenye ofisi, bora mkono uende kimiani.

Kwa upande wangu, nilionekana kupendelewa zaidi. Hata madereva wenzangu wakati mwingine waliniambia bayana wakati tukisogoa.

"Mwenzetu unakatiwa mapande ya ulaji tu," alisema Bwana Shaibu, dereva wa bosi mkuu. "Miye kila wakati nipo na kingunge-mkuu wa ofisi! Nitaiba saa ngapi? Gari yenyewe Nissan Patrol. Roho juu kila wakati kuogopa majambazi. Hata `kusanya' siwezi!" Alilalama.

Wakati huo mimi naendesha gari la maji machafu. Nikipiga tripu mbili za kampuni, napiga tano za kwangu. Na kwa kuwa gari lile ni la kubeba (ashakum) kinyesi, wanene wa kampuni hawakutupa macho yao kwangu. Mradi ilikuwa ni ulaji mtupu wa kimyakimya. Hata madereva wenzangu hawakushtuka.

Machale yalianza kuwacheza waliposikia nimesimamisha `banda' pale bondeni.

Nikahamishiwa kwenye `kijiko' - gari la kuchimbia na kung'oang'oa - kwa imani sitakuwa na cha `kuhamisha.' Wakati huo mtindo wa kutumia `nyoka' - mipira ya kutolea petroli na dizeli - ulikuwa umedhibitiwa. Lakini huwezi kumdhibiti mwanadamu, hasa ngurumbili huyo anapokuwa wa ‘Bongoland’. Ulaji wa kwenye `kijiko' ukawa mkubwa zaidi, maana katika masaa ya kazi, nusu nayatumia nikiwa `kontrakta bubu.'

Mpaka walipostuka, nilishavuna vya kutosha. Siku nilipohamishiwa kwenye gari la kubeba wafanyakazi, wenzangu walijua wazi chizi limepewa manati, sokoni!

"Au mwenzetu unakula na wakubwa?" walinitania.

"Kwenda zenu! Nani asiyegema mahala pake pa kazi?" Niliwajibu kwa masikhara.

"Ah! Lakini wewe mwenzetu unawekwa kwenye vitengo vya ulaji tu!"

Na kweli. Kwenye gari hili la abiria kulikuwa na pesa za nje-nje tu.

Mara ya kwanza nilikuwa naogopa kuligeuza daladala-bubu (sanyasanya), hususan asubuhi, kwa vile "wanga wengi." Lakini kadiri nilivyoshika hatamu za uongozi wa basi lile, ndivyo nilivyozidi kujiamini.

"Kwanza wanene wote wa kampuni wanakaa uzunguni. Halafu wote wana magari. `Dili' zao zote na wazito wenzao. Huku uswahili watatafuta nini? Nyumba ndogo?"

Ikawa desturi.

Nikitoka kazini, baada ya `kuwatupa' wafanyakazi wenzangu, nilianza awamu mpya ya kupiga tripu za daladala ...

Hapakuwa na tatizo. Japo konda, ambaye pia alikuwa ndiye mpiga-debe na mpambe, alikuwa `anapiga panga.' Makusanyo, bado chuma cha siku lilikuwa la kuvutia.

Mungu akupe nini! Man'ake huo usiku `serikali inakuwa imelala' - hamna matrafiki, walau huko kwenye njia za uswahlini. Ukiona `tageti' waendea kwa wakati wako!

Na hapo sikutaka `kuchezea wakati'. Ukipata tumia, ukikosa jutia. Hata kitambi kikaanza kuchomoza.

Hicho pengine ndio kilichonisaliti. Maana maneno yakaanza `kutembea' chini chini. Tena madereva wenzangu wale wale! Utafikiri wao `hawali' kwenye magari yao! Mswahili bwana! Kwa kuchukia `maendeleo' ya mtu?!

Sikujali.

Wembe ni ule ule!

Siku moja nikaamua kumchukua `dei waka' dereva wa daladala fulani iliyo juu ya mawe. Siku hiyo kondakta nikawa mwenyewe - ili kuzuia `kupigwa panga' pesa zinazokusanywa.

Sanyasanya iliendelea kama siku zote. "Sanyasanya Trans" kama ilivyojulikana mtaani, iliendelea kudunda uswahilini. Na pesa nilizokusanya siku ile zilinifanya nijue ukubwa wa `panga' lililokata pesa siku zote.

Ni wakati wa tripu ya mwisho, ya kupata pesa za kujazia mafuta, kizungumkuti kilipoanza.

Wakati `nawachuna' abiria nauli, abiria aliyeketi kwenye kona kiti cha nyuma akakataa kulipa.

"Siti ya mwisho, bado mmoja!" nilisema. "Halo we mwenye kapelo leta `uchache' huo!"

Lakini yule jamaa aliyekuwa amevaa kofia iliyofunika uso staili ya `ukitaka kumuua nyani" alikuwa anapuuza kelele zangu.

Nilipojaribu kufikiri ni kitu gani ananiringia, nikahisi labda kitambi!

"Halo usiku unauweka! Ikiwa ni ubosi ni huko huko ofisini kwako!"

Lile jamaa lilinitazama tu.

Au linavuta bangi? Hata likivuta! Shauri yake! N'nachojali ni michuzi tu!

"Halo usitutishe na kitambi chako cha mapuya! Tumbo hilo la mataputapu linakufanya ujione booosi! Nakwambia hapa umefika." Nilifoka.

Abiria wengine walitukodolea macho. Tayari wengine walishaanza kuambukizwa `ufyatu' wa yule jamaa.

"Asipolipa yule na sisi hatulipi." Walidai.

Hapo ndipo wazimu wote ukanipanda kichwani. Mtu huyu hawezi kunifanyia mapuuza kwenye gari `langu' halafu nikamucha vivi hivi tu!

Nahisi hata yeye alibaini sasa yatakuwa mengine. Ndiyo maana akatoa noti ya nauli kabla sijaongea zaidi. Nikamrudishia chenji, pungufu ya shilingi mia tano.

"Na mimi nikikunyima chenji hii utajisikiaje?"

Hakusema kitu.

Nikanyoosha mkono nimpe hela yake.

Mara, Lo!

Akatoa miwani ya jua aliyovaa usiku ule. Kisha akainua kofia aliyovaa.

Mama yake na mama!

Kumbe ni bosi, `mnene mkuu' wa ofisi!!

"Hizi zitakuwa ni fitna za watu!" niliwaza.

Nilihisi kutaka kwenda haja papo hapo. Sijui gavana iliyookoa jahazi ilitoka wapi! Vinginevyo ingekuwa simulizi.

Nilichanganyikiwa.

Hata abiria wengine sikuweza kuchukua nauli zao.

Kesho yake niliitwa ofisini kwa mkuu.

"Kijana, maisha unayapeleka vibaya! Ungekuwa japo unaendesha mwenyewe, pengine ningeelewa, japo kidogo. Kosa ulilofanya unastahili adhabu kali!"

Ama kweli. Siku ya kutembea uchi ndiyo unayokutana na mkweo!

Hivi ninapokumegea stori bosi bado 'anafikiria' adhabu ya kutoa. Sijui bosi atatoa adhabu gani? Sijui atanihamishia ofisi yenye meza bila kasma? Au atanipeleka kusoma? Kunifukuza hawezi - maana ni urasimu mkubwa - ndiyo ‘raha’ ya ajira ya umma. Mwenzenu niko roho juu!

mwisho.

Kwa hisani ya Chumvi Mtembezi
 
Mtanzania huu mjadala nimeupenda sana kuliko mijadala mingine tuliyoifanya hapa kwani huu unatuangalia sisi wenyewe na attitudes zetu kuhusu kazi, kuwajibika, usawa, uzalendo na mipango ya baadaye. Hadi hivi sasa kuna kila dalili kuwa hali ngumu ya maisha/tamaa ya maisha bora zaidi inawafanya watu kujaribu kujitajirisha kwa njia za mkato na kwa harraka.

Hata hivyo bado swali la msingi halijaangaliwa kwa kina kuwa endapo chama au mwanasiasa akijitokeza na kusema anataka kuziba mianya hii ya wizi, na ujanja ujanja mtu huyo/watu hao wataungwa mkono au wataonekana wanajaribu kuwanyang'anya watu 'halali' yao?


Mkjj huwezi zungumzia kuziba mianya ya wiziwizi bila kurekebisha ujira unaolipwa kwa kazi zinazofanywa, hebu fikiria dereva wa ubalozi anayelipwa say millioni moja na dereva wa serikali anayelipwa laki moja nani atapiga kidebe? ni wazi kuwa wa serikali atapiga kidebe tofauti na mwenzie ambaye anakipato safi na atahakikisha anakilinda kwani madereva ni wengi na hawalipwi kama inavyotakiwa, hivyo basii naungana na aliyewahi kuona tatizo hili mapema na kuandika kuwa "KILA MTU NA KA-MHOGO KAKE"
 
Mhmmm please let us look at the comparisons we are making. Some are misleading. Kama USA tiketi ya sinema ni USD 7 na Tanzania tiketi ni Tshs. 8,000 then it is cheaper in Tanzania hasa ukiangalia market exchange ya USD kwa sasa ambayo inafikia hata Tshs 1350 kwa dola. Hivyo huko marekani gharama ya tiketi moja kwa pesa ya Tanzania ni Shs. 9,450.00. Sasa ni wapi wanaangalia sinema kwa bei ya juu, Tanzania au Marekani?

.....hihihihihii....i like this analysis....hihihihihihi
 
MJ kama una miaka chini ya 40 basi ningejushauri ku invest on yourself. Kama una degree au masters basi soma software zenye market kama SAP n.k . Vilevile unaweza kusoma certification courses kama project mgmt, CPA, CMA, n.k. Vilevile Invest kwenye uraia kama huna kwani kuna nafasi nyingi za serikali zinakuja. Mawazo yangu ni kwa wanaoishi USA.

........MJ bonge la ushauri huo........at times...mambo mengine ya kibongo you just have to give up........for a while.......to revert on them later.......
 
Mhmmm please let us look at the comparisons we are making. Some are misleading. Kama USA tiketi ya sinema ni USD 7 na Tanzania tiketi ni Tshs. 8,000 then it is cheaper in Tanzania hasa ukiangalia market exchange ya USD kwa sasa ambayo inafikia hata Tshs 1350 kwa dola. Hivyo huko marekani gharama ya tiketi moja kwa pesa ya Tanzania ni Shs. 9,450.00. Sasa ni wapi wanaangalia sinema kwa bei ya juu, Tanzania au Marekani?

is Quality of theaters being factored in?!those $7-$8 offers advanced watching experience IMAX ddts 7.1 channels etc,i bet if i take a theater in TZ and put it in US it wont sell its tickets for higher than $5.

interesting point is that we are being forced to consume OLD technnology at the same price that the "world" is paying for super ultra new technology.that matters too!

so,BEI ya ticket TZ is very expensive compare to US,factoring quality of media presented and selection of movies available.
 
Back
Top Bottom