Kuna uwezekanao kabisa serikali moja kupandisha bei ya bidhaa fulani ili kurekebisha bajeti yake. Hii hutokea sana katika nchi zzenye vyanzo finyu vya kongeza mapato ya serikali. Hivyo kulinganisha kiwango cha kuongezeka kwa bidhaa nchi tofauiti kutaonyesha jinsi serikali hiyo inavyotegemea chanzo hicho. Kwa mfano wako huu wa soda, mimi naishi EU, bei ya coke ya kopo ml 300 ilikuwa euorcent 49 2004 na sasa ni cent 54. Kwa hiyo jibu lako kuhusu kuongezeka kwa bidhaa za mlaji sehemu nyingi zimeongezeka. Mkate toka cet 49 mpaka cent 62 huku niishiko. sasa Tanzania mkate ni bei gani au umeongezeka vipi wewe unajua. Kama unafuatilia mabo ya uchumi pale mafuta yalipopanda sana nchi za magharibi waliutaka OPEC kuongeza uzalishaji ili bei ipungue., demand vs supply principle. OPEC walikataa kwa kuziambia nchi zipunguze kodi inayotozwa kwenye mafuta kwani nchi nyingine kodi ilifikia 70%. Wakagoma kusikiliza ushauri huo na bei ikapungua kwa kuwa speculants walijua imefika kikomo. Kwa maana hiyo serikal zinachangia mwongezeko wa bei wa bidhaa fulani fulani ilikuziba nakisi kwenye bajeti zao. Kila nchi ina economic indicator zake, zinazofuatwa na Marekani au THE Gx zaweza kutokuwa na maana kwenye uchumi wetu, japo kutokana na utegemezi wetu zinaweza kuleta nakisi kwenye bajeti yetu na kusababisha Mfumuko wa bei. Matumizi yasiyo na sababu au udhibiti mbovu wa mapato kwa serikali iliyoko madarakani unachangia kuleta mfumuko wa bei. Ushabiki au la serikali yeyote lazima ichague je uchumi utaongoza siasa au siasa itaongoza uchumi. Uchumi ukiongoza siasa kuna uhakika wa kukua au kuwa stable. Mfano Kenya kama siasa ingeongoza uchumi machafuko ya kisiasa yaliyotokea yangewaacha pabaya. Siasa kuongoza uchumi , mfano Tanzania toka vita ya Nduli hatujatengemaa wala kuzinduka kutoka kwenye mtizamo huo
Excellent view