Una Uwezo wa Kuzungumza Lugha Ngapi?

SHIEKA

JF-Expert Member
Dec 20, 2011
8,244
4,258
Je wewe waweza kuzungumza kwa ufasaha lugha ngapi? Lugha mbili?(ya kabila lako na kiswahili?) Lugha tatu? (ya kabila lako, kiswahili na kiingereza?) Lugha nne? (ya kikabila, kiswahili, kingereza na kifaransa/kispaniola/........?

Bwana mmoja mwingereza, Matthew Youlden anazungumza lugha tisa kwa ufasaha.

Msikilize kwenye video iliyopo kwenye tovuti hii:
10 Tips And Tricks To Learn Any Language
 
Kiswahili tu.... hiyo english hata ikiandikwa hapa naona uvivu kusoma
 
Kiswahili tu.... hiyo english hata ikiandikwa hapa naona uvivu kusoma
Ni kweli. English inatatiza wengi, ila mbona huna lugha ya kienyeji kwa mfano kinyaturu, kichagga nk?Au hukuzaliwa na kukulia kijijini?
 
Naongea na kuandika lugha NNE ila nilijaribu France ikawa ngumu maana hizo zingine nimejifunza kwa kukaa na wenyeji lakini kusomea ni ngumu kidogo
 
Mother tongue
Swahili
English
French

Pia kidogo Kiarabu na Spanish
 
Ikitokea umesafiri kwenda nchi za nje utawasilianaje na watu wa huko?
Ongeza ufahamu wa lugha moja ya nje kama vile kiingereza, kifaransa au kichina.

Sitaki kujua lugha yoyote zaidi ya Kiswahili. Nimegoma kabisa yani.
 
kihehe kinyakyusa kikinga kigogo kisafa kisukuma kijita kikerewe kiswahili kiingereza na hii imetoka kwa sababu mimi ni chotara
 
Back
Top Bottom