kibananhukhu
JF-Expert Member
- Jul 6, 2009
- 366
- 161
Mimi ninafundisha Ujasiriamali. Nimekwisha fundisha wanafunzi zaidi ya elfu tatu ambao nimewaweka katika "data bank" ya chuo changu pamoja na aina za biashara wanazozifanya. Wengi wao ni wanachama wa SACCOS ambao wanaweza kukopa kati ya shilingi milioni mbili hadi milioni 30 kutegemea mishahara yao na hupashwa kulipa mikopo hiyo kwa kipindi hadi miaka mitatu.
Nina wazo la kuwatafutia masoko kwa pamoja, kuwashauri wazalize kwa makundi na washirikiane katika mengi kibishara kukabiliana na madalali na walanguzi wa kati. Nina wazo pia la kuwashauri waagize bidhaa nje kwa pamoja, na ikibidi hata kuwa na duka moja wafanyabiashara watano watano wale wanaoelewana vizuri marafiki ili kuchangia gharama.
Ninaomba mwenye uwezo wa kutafuta masoko kwa bidhaa zozote hususani zinazopatikana tanzania wanishauri au waniunganishe kwani nina watu wanaokopesheka. Ushauri wowote kuhusu mada hii utapelekea kujikomboa kiuchumi. Kwani hadi mwishoni mwa mwaka huu nitakuwa nimewafundisha wanachama wa SACCOS zaidi ya elfu 5 katika taasisi yetu na wote watakuwa katika data bank zetu pamoja na biashara zao.
Naamini pia wao watakuwa ni soko la wao kwa wao kwa baadhi ya bidhaa hivyo soko kubwa litahitajika pia.
Je, Nishaurini, wazo hili ni zuri? Kuna wazo mbadala? Kuna ushauri wowote katika mafunzo ninayoyafanya kwani mwisho wa siku lengo ni asilimia kuwa ya wanafunzi waboreshe na kuanzisha biashara kitaaluma.
Asanteni sana kwa mawazo yanu mtakayonipatia na nipo tayari kushirikiana na yeyote.