Tiba
JF-Expert Member
- Jul 15, 2008
- 4,604
- 3,163
Wana JF,
Sometimes in January 2012, kuna tangazo la kazi kutoka shirika moja la UN - Commission for International Development (UNCFID). Kwenye tangazo hilo kulikuwa na kazi nyingi na duty station ilikuwa ni Geneva. Mimi nilivutiwa kuomba kazi mojawapo ambayo niliiona inaenda na proffile yangu. Nilipeleka maombi na baada ya wiki tatu nililetewa maswali ya interview na nilipewa siku nne niwe nimerudisha majibu. Nilifanya hivyo.
Baada ya wiki mbili tena, nilipokea simu ikinitaarifu kwamba nimefaulu written interview na kwamba sasa natakiwa kuhudhuria oral interview through telephone. Tulikubaliana wakati wa hiyo interview na wakati ulipofika walinipigia simu. Nilijibu maswali yao kama nilivyoweza, walikuwa watu watatu kwenye hiyo interviewing panel.
Tarehe 1 March 2012, nilipokea email kutoka kwao ikinitaarifu kwamba nimefaulu interview na hivyo wakanipa offer ya hiyo kazi. Waliniletea mkataba wa kazi ambao walinitaka ni-usign na kuwarudishia. Walinitaarifu kwamba ingawaje duty station yangu itakuwa ni Geneva, itabidi niende New York kwa muda wa mwezi mmoja kwa ajili ya in-deep training. Walinitaarifu kwamba agent wao angewasiliana na mimi ili kunipa taratibu za kuomba visa na mambo mengineyo. Walinitumia fomu za kujaza na kupeleka kwa huyo agent.
Baada ya kupeleka form hizo kwa agent (Miyake Corporation) walinijibu na kunipa taratibu za kupata visa ya kuingia Marekani huku wakisisitiza kwamba sipashwi kutafuta hiyo visa bila kupitia kwao. Gharama za hiyo visa ndizo ziliniacha mdomo wazi, ukitaka ya haraka ni USD 3,940 n a ile ya kawaida ni USD 2,750. Kwa gharama hizo machale yalinicheza na kuamua kuwaandikia kwamba hizo gharama ni kubwa na kwamba nitawalipa hizo hela baada ya kuwa nimeanza hiyo kazi au waniletee barua ya Mwaliko ili mimi niitumie kuomba visa mwenyewe. Walipopata hiyo email yangu, wakanitumia form wakisistiza nilipe kupitia account namba waliyonipa na kwamba nikifika New York nitarudishiwa gharama zangu zote na ofisi. Wakanitumia Reimbursement Claim Form.
Kabla ya kuwajibu, nililazimika kuzama kwenye internet kutafuta hilo shirika la UN linaloitwa UNCFID. Ajabu sikupata jibu lolote kuonyesha kwamba hilo shirika lina website. Nitakajaribu kuitafuta hiyo Miyake Corporation na kugundua kwamba kampuni hiyo ipo huko Marekani lakini haihusiki na travel agent hata kidogo. Lakini through searching (google) nikaja kugundua kwamba lile tangazo la kazi ilikuwa ni employment scam.
Nimelazimika kuileta hii habari hapa kwa kujua kwamba kuna uwezekano mkubwa kwamba kuna wana JF wengine waliomba hizi kazi na kwa sasa wako kwenye mchakato wa kuibiwa pesa zao na hawa matapeli. Kama sio wewe basi ni ndugu yako, be aware hawa ni wezi na hakuna shirika la UN linaitwa United Nations Commission For International Development.
Nawasilisha.
Tiba
Sometimes in January 2012, kuna tangazo la kazi kutoka shirika moja la UN - Commission for International Development (UNCFID). Kwenye tangazo hilo kulikuwa na kazi nyingi na duty station ilikuwa ni Geneva. Mimi nilivutiwa kuomba kazi mojawapo ambayo niliiona inaenda na proffile yangu. Nilipeleka maombi na baada ya wiki tatu nililetewa maswali ya interview na nilipewa siku nne niwe nimerudisha majibu. Nilifanya hivyo.
Baada ya wiki mbili tena, nilipokea simu ikinitaarifu kwamba nimefaulu written interview na kwamba sasa natakiwa kuhudhuria oral interview through telephone. Tulikubaliana wakati wa hiyo interview na wakati ulipofika walinipigia simu. Nilijibu maswali yao kama nilivyoweza, walikuwa watu watatu kwenye hiyo interviewing panel.
Tarehe 1 March 2012, nilipokea email kutoka kwao ikinitaarifu kwamba nimefaulu interview na hivyo wakanipa offer ya hiyo kazi. Waliniletea mkataba wa kazi ambao walinitaka ni-usign na kuwarudishia. Walinitaarifu kwamba ingawaje duty station yangu itakuwa ni Geneva, itabidi niende New York kwa muda wa mwezi mmoja kwa ajili ya in-deep training. Walinitaarifu kwamba agent wao angewasiliana na mimi ili kunipa taratibu za kuomba visa na mambo mengineyo. Walinitumia fomu za kujaza na kupeleka kwa huyo agent.
Baada ya kupeleka form hizo kwa agent (Miyake Corporation) walinijibu na kunipa taratibu za kupata visa ya kuingia Marekani huku wakisisitiza kwamba sipashwi kutafuta hiyo visa bila kupitia kwao. Gharama za hiyo visa ndizo ziliniacha mdomo wazi, ukitaka ya haraka ni USD 3,940 n a ile ya kawaida ni USD 2,750. Kwa gharama hizo machale yalinicheza na kuamua kuwaandikia kwamba hizo gharama ni kubwa na kwamba nitawalipa hizo hela baada ya kuwa nimeanza hiyo kazi au waniletee barua ya Mwaliko ili mimi niitumie kuomba visa mwenyewe. Walipopata hiyo email yangu, wakanitumia form wakisistiza nilipe kupitia account namba waliyonipa na kwamba nikifika New York nitarudishiwa gharama zangu zote na ofisi. Wakanitumia Reimbursement Claim Form.
Kabla ya kuwajibu, nililazimika kuzama kwenye internet kutafuta hilo shirika la UN linaloitwa UNCFID. Ajabu sikupata jibu lolote kuonyesha kwamba hilo shirika lina website. Nitakajaribu kuitafuta hiyo Miyake Corporation na kugundua kwamba kampuni hiyo ipo huko Marekani lakini haihusiki na travel agent hata kidogo. Lakini through searching (google) nikaja kugundua kwamba lile tangazo la kazi ilikuwa ni employment scam.
Nimelazimika kuileta hii habari hapa kwa kujua kwamba kuna uwezekano mkubwa kwamba kuna wana JF wengine waliomba hizi kazi na kwa sasa wako kwenye mchakato wa kuibiwa pesa zao na hawa matapeli. Kama sio wewe basi ni ndugu yako, be aware hawa ni wezi na hakuna shirika la UN linaitwa United Nations Commission For International Development.
Nawasilisha.
Tiba