UN Employment Scam - Kuweni Macho

Tiba

JF-Expert Member
Jul 15, 2008
4,604
3,163
Wana JF,

Sometimes in January 2012, kuna tangazo la kazi kutoka shirika moja la UN - Commission for International Development (UNCFID). Kwenye tangazo hilo kulikuwa na kazi nyingi na duty station ilikuwa ni Geneva. Mimi nilivutiwa kuomba kazi mojawapo ambayo niliiona inaenda na proffile yangu. Nilipeleka maombi na baada ya wiki tatu nililetewa maswali ya interview na nilipewa siku nne niwe nimerudisha majibu. Nilifanya hivyo.

Baada ya wiki mbili tena, nilipokea simu ikinitaarifu kwamba nimefaulu written interview na kwamba sasa natakiwa kuhudhuria oral interview through telephone. Tulikubaliana wakati wa hiyo interview na wakati ulipofika walinipigia simu. Nilijibu maswali yao kama nilivyoweza, walikuwa watu watatu kwenye hiyo interviewing panel.

Tarehe 1 March 2012, nilipokea email kutoka kwao ikinitaarifu kwamba nimefaulu interview na hivyo wakanipa offer ya hiyo kazi. Waliniletea mkataba wa kazi ambao walinitaka ni-usign na kuwarudishia. Walinitaarifu kwamba ingawaje duty station yangu itakuwa ni Geneva, itabidi niende New York kwa muda wa mwezi mmoja kwa ajili ya in-deep training. Walinitaarifu kwamba agent wao angewasiliana na mimi ili kunipa taratibu za kuomba visa na mambo mengineyo. Walinitumia fomu za kujaza na kupeleka kwa huyo agent.

Baada ya kupeleka form hizo kwa agent (Miyake Corporation) walinijibu na kunipa taratibu za kupata visa ya kuingia Marekani huku wakisisitiza kwamba sipashwi kutafuta hiyo visa bila kupitia kwao. Gharama za hiyo visa ndizo ziliniacha mdomo wazi, ukitaka ya haraka ni USD 3,940 n a ile ya kawaida ni USD 2,750. Kwa gharama hizo machale yalinicheza na kuamua kuwaandikia kwamba hizo gharama ni kubwa na kwamba nitawalipa hizo hela baada ya kuwa nimeanza hiyo kazi au waniletee barua ya Mwaliko ili mimi niitumie kuomba visa mwenyewe. Walipopata hiyo email yangu, wakanitumia form wakisistiza nilipe kupitia account namba waliyonipa na kwamba nikifika New York nitarudishiwa gharama zangu zote na ofisi. Wakanitumia Reimbursement Claim Form.

Kabla ya kuwajibu, nililazimika kuzama kwenye internet kutafuta hilo shirika la UN linaloitwa UNCFID. Ajabu sikupata jibu lolote kuonyesha kwamba hilo shirika lina website. Nitakajaribu kuitafuta hiyo Miyake Corporation na kugundua kwamba kampuni hiyo ipo huko Marekani lakini haihusiki na travel agent hata kidogo. Lakini through searching (google) nikaja kugundua kwamba lile tangazo la kazi ilikuwa ni employment scam.

Nimelazimika kuileta hii habari hapa kwa kujua kwamba kuna uwezekano mkubwa kwamba kuna wana JF wengine waliomba hizi kazi na kwa sasa wako kwenye mchakato wa kuibiwa pesa zao na hawa matapeli. Kama sio wewe basi ni ndugu yako, be aware hawa ni wezi na hakuna shirika la UN linaitwa United Nations Commission For International Development.

Nawasilisha.

Tiba
 
Pole Mkuu umenusurika katika mdomo wa mamba...
Mara nyingi matapeli hawa wapo makini sana katika kugundua tamaa
za watu kisha huitumia tamaa yako mwenyewe kukuliza...
Ushauri kwa yeyote anayeona tangazo la kazi au jambo lolote
la kuvutia ni muhimu ukawasiliana na mamlaka husika kwa kufika
mwenyewe katika ofisi zao...ikatokea umekutana na mtu katika mamlaka hiyo
labda akawa kwenye njama moja ni vema ukatumia vema kamera ya simu yako
kuwapiga picha. rafiki yangu alitapeliwa T.sh 20ml kwa deal ya kuuziwa mini bus
aliwapiga picha wahusika ambao walimpeleka show room wakaingia makataba lakini
alipowapa hela walitoweka... picha alizowapiga kutumia simu yake zilisaidia walikamatwa
na akarejeshewa fedha zake.
 
Pole Mkuu umenusurika katika mdomo wa mamba...
Mara nyingi matapeli hawa wapo makini sana katika kugundua tamaa
za watu kisha huitumia tamaa yako mwenyewe kukuliza...
Ushauri kwa yeyote anayeona tangazo la kazi au jambo lolote
la kuvutia ni muhimu ukawasiliana na mamlaka husika kwa kufika
mwenyewe katika ofisi zao...ikatokea umekutana na mtu katika mamlaka hiyo
labda akawa kwenye njama moja ni vema ukatumia vema kamera ya simu yako
kuwapiga picha. rafiki yangu alitapeliwa T.sh 20ml kwa deal ya kuuziwa mini bus
aliwapiga picha wahusika ambao walimpeleka show room wakaingia makataba lakini
alipowapa hela walitoweka... picha alizowapiga kutumia simu yake zilisaidia walikamatwa
na akarejeshewa fedha zake.

Ni kweli mkuu nilishafikiria pa kuipata hiyo USD 2,750 lakini baadae nikashtuka. Nafikiri watu wanaopost nafasi za kazi hapa inabidi nao wawe wanakuwa na uhakika na hizo kazi sio kutuletea kanyabwoya hapa. Ningelizwa!!!

Tiba
 
aksante kwa taarifa mkuu, hawa jamaa ni mtapeli wa kimataifa, tuwe macho.
 
aksante kwa taarifa mkuu, hawa jamaa ni mtapeli wa kimataifa, tuwe macho.

Ni kweli kwamba hawa ni matapeli wa kimataifa, lakini UN infanya nini kuhakikisha jina lake halitumiki kwenye utapeli kama hivi? Kuna ukweli kwamba UN haikuliona hili tangazo la kitapeli na kuwaonya watu kwamba hiyo ni employment scam? Hawa watachafua credibility ya UN.

Tiba
 
Ndugu yangu pia aliponea chupuchupu baada ya kupitia hatua zote ulizotaja. Akaanza kukopa pesa ili kufanikisha hiyo ajira lakini akashauriwa na mkopwaji aende kwanza shirika lolote la UN akacheki uhalali wa hiyo kitu. Ndiko aliambiwa ni scam na amenusurika kuibiwa!
 
Wana JF,

Sometimes in January 2012, kuna tangazo la kazi kutoka shirika moja la UN - Commission for International Development (UNCFID). Kwenye tangazo hilo kulikuwa na kazi nyingi na duty station ilikuwa ni Geneva. Mimi nilivutiwa kuomba kazi mojawapo ambayo niliiona inaenda na proffile yangu. Nilipeleka maombi na baada ya wiki tatu nililetewa maswali ya interview na nilipewa siku nne niwe nimerudisha majibu. Nilifanya hivyo.

Baada ya wiki mbili tena, nilipokea simu ikinitaarifu kwamba nimefaulu written interview na kwamba sasa natakiwa kuhudhuria oral interview through telephone. Tulikubaliana wakati wa hiyo interview na wakati ulipofika walinipigia simu. Nilijibu maswali yao kama nilivyoweza, walikuwa watu watatu kwenye hiyo interviewing panel.

Tarehe 1 March 2012, nilipokea email kutoka kwao ikinitaarifu kwamba nimefaulu interview na hivyo wakanipa offer ya hiyo kazi. Waliniletea mkataba wa kazi ambao walinitaka ni-usign na kuwarudishia. Walinitaarifu kwamba ingawaje duty station yangu itakuwa ni Geneva, itabidi niende New York kwa muda wa mwezi mmoja kwa ajili ya in-deep training. Walinitaarifu kwamba agent wao angewasiliana na mimi ili kunipa taratibu za kuomba visa na mambo mengineyo. Walinitumia fomu za kujaza na kupeleka kwa huyo agent.

Baada ya kupeleka form hizo kwa agent (Miyake Corporation) walinijibu na kunipa taratibu za kupata visa ya kuingia Marekani huku wakisisitiza kwamba sipashwi kutafuta hiyo visa bila kupitia kwao. Gharama za hiyo visa ndizo ziliniacha mdomo wazi, ukitaka ya haraka ni USD 3,940 n a ile ya kawaida ni USD 2,750. Kwa gharama hizo machale yalinicheza na kuamua kuwaandikia kwamba hizo gharama ni kubwa na kwamba nitawalipa hizo hela baada ya kuwa nimeanza hiyo kazi au waniletee barua ya Mwaliko ili mimi niitumie kuomba visa mwenyewe. Walipopata hiyo email yangu, wakanitumia form wakisistiza nilipe kupitia account namba waliyonipa na kwamba nikifika New York nitarudishiwa gharama zangu zote na ofisi. Wakanitumia Reimbursement Claim Form.

Kabla ya kuwajibu, nililazimika kuzama kwenye internet kutafuta hilo shirika la UN linaloitwa UNCFID. Ajabu sikupata jibu lolote kuonyesha kwamba hilo shirika lina website. Nitakajaribu kuitafuta hiyo Miyake Corporation na kugundua kwamba kampuni hiyo ipo huko Marekani lakini haihusiki na travel agent hata kidogo. Lakini through searching (google) nikaja kugundua kwamba lile tangazo la kazi ilikuwa ni employment scam.

Nimelazimika kuileta hii habari hapa kwa kujua kwamba kuna uwezekano mkubwa kwamba kuna wana JF wengine waliomba hizi kazi na kwa sasa wako kwenye mchakato wa kuibiwa pesa zao na hawa matapeli. Kama sio wewe basi ni ndugu yako, be aware hawa ni wezi na hakuna shirika la UN linaitwa United Nations Commission For International Development.

Nawasilisha.

Tiba
Pole kwanza!!
=Kwanza hakuna UNCFID kuna UNCDF!
=Pili nikwamba wakitangaza kazi UN kokote duniani ikiwa nje yamahali ulipo Uelekezwa kwenda kwenye Office za UNDP zilizopo nchi husika!
Pili ukiisha fanyia interview kwa simu uenda kufanyiwa aral makao makuu ya UN nchi husika!
=Maswala ya visa ukiwa umemaliza interview zao UN makao makuu nchi husika ushughulikia malipo yote!!gharama zote visa kila kitu wao uwasiliana na watoa kazi na huwatumia account charge na wao un makaomakuu ya nchi husika ukugharamia kila kitu
=UN hatumiagi hata siku moja agent
Hizo ni tip chache kuhusiana na mrorongo wakazi za UN katika recruitment.
 
Ndugu yangu pia aliponea chupuchupu baada ya kupitia hatua zote ulizotaja. Akaanza kukopa pesa ili kufanikisha hiyo ajira lakini akashauriwa na mkopwaji anende kwanza shirika lolote la UN akacheki uhalali wa hiyo kitu. Ndiko aliambiwa ni scam na amenusurika kuibiwa!

Inaelekea tuko wengi kwenye hii trap!!! Inabidi tuwe macho sana na hawa matapeli. Sasa sijui ukikpoa USD 2,750 unakuja kuzilipa vipi ukigundua umeingizwa mjini?

Tiba
 
Pole kwanza!!
=Kwanza hakuna UNCFID kuna UNCDF!
=Pili nikwamba wakitangaza kazi UN kokote duniani ikiwa nje yamahali ulipo Uelekezwa kwenda kwenye Office za UNDP zilizopo nchi husika!
Pili ukiisha fanyia interview kwa simu uenda kufanyiwa aral makao makuu ya UN nchi husika!
=Maswala ya visa ukiwa umemaliza interview zao UN makao makuu nchi husika ushughulikia malipo yote!!gharama zote visa kila kitu wao uwasiliana na watoa kazi na huwatumia account charge na wao un makaomakuu ya nchi husika ukugharamia kila kitu
=UN hatumiagi hata siku moja agent
Hizo ni tip chache kuhusiana na mrorongo wakazi za UN katika recruitment.

Asante mkuu kwa kutufumbua macho. Mimi nilidhani nimeuchinja maana mshahara kwenye calculation sheet walionyesha ningekuwa napata USD 10,760 kwa mwezi baada ya makato na mkataba ulikuwa wa miaka 5. You can imagine!!!

Tiba
 
jamani,hiyo ni kweli,hata mm ilinikuta ila nilishtuka mapema walipoanza kusema kuwa stakiwi kwenda ubalozini ,nitume copy ya pport na details nyingine. So nilichofanya nilienda pale UNDP information desk kuuliza kama wanalitambua hilo shirika la UN wakadai halipo, na hata last yr pia limesumbua sana watu.

Pia nilienda hata ubalozi wa Swiss,tho wao hawakuwa na masaada,ila walisema UN office hapa ndo watajua.

So nilipojua ukweli niliwaandikia mail kuwaambia naomba watume infomation kwa UN hapa Tanzania ,kuthibitisha wao ni genuine,basi hadi leo hawajatuma tena email kwangu. Na hizi kazi hizi hizi,za January,ila mm skufanya oral interview bali written tu.

So wadau kwanza muwe maco kwani unaambiwa kazi zote za UN lazima zitangazwe kwenye website ila ya UN,na si kwa mitandao mingine(zaidi ya ile organisation husika). So tupende kufanya confirmation na ofic za UN hapa km wana taarifa na hizo kazi.
Tuwe macho jamani.
 
Back
Top Bottom