Umuhimu wa nambari 3 kwenye maisha ya binadamu

Mokoyo

JF-Expert Member
Mar 2, 2010
15,145
5,553
Naomba kuuliza kuhusu umuhimu wa nambari 3 katika tamaduni za Kitanzania, aidha kihesabu au katika imani za watu (belief/religious systems)kwa mfano kwenye matambiko, nk. Kwa nini nadodosa hili? Naomba nitoe mifano.

Kwenye lugha ya Kiswahili tuna nafsi tatu: mimi, wewe, yeye; sisi, nyinyi, wao. Tulifikaje kwenye matumizi ya hizi nafsi zinazojumuishwa kwa nambari 3? Zaidi ya hapo, waandishi mashughuli kama washairi marehemu Shaaban Robert na Mathias Mnyampala waliandika aidha kwa makusudi au bila kujuwa kuhusu umuhimu wa nambari 3. Shaaban Robert aliandika kuelezea umuhimu wa ngazi tatu katika maisha ya mwanadamu: kuzaliwa, ndoa, na kifo (a triplet). Mathias Mnyampala aliandika hadithi nzuri kuhusu kisa cha mrina asali na wenzake wawili (also a triplet). Kulikoni washairi maarufu walilenga hii nambari 3?

Aidha, tamaduni nyingine duniani pia zimeipa hii nambari tatu umuhimu wa pekee. Marumi waliabudu miungu wakuu watatu vinyo hinyo majirani wao Magiriki. Mpaka hivi leo Wakristo wanaamini Utatu Mtakatifu (God the Father, the Son, and the Holy Spirit). Kuzaliwa kwa Yesu kuliashiliwa na nyota iliyowaongoza wafalme watatu (the three magi) hadi Yerusalemi. Na karne za mwanzo za enzi za Ukristo ziliashiria huo utatu mtakatifu hususan katika matumizi ya alama ya jich ndani ya “triangle.” The eye in the triangle representing God’s all-seeing eye.

Wajapani wanaamini kuwa Taoism ina mandhari tatu, mbingu, ardhi na bahari, na kila moja ina mtawala maalum. Wajerumani wana Imani katika utamaduni wao kuwa makabila matatu muhimu ya Kijerumani yalitokana na uzawa wa Mannus yaani Wodan, Thorr, na Donar. Linganisha hadithi hii na hadithi ya Wayahudi kwenye Mwanzo (Genesis) sura ya 9 aya ya 19).

Ni kutokana na maelezo hayo hapo juu ndo maana nauliza kama kuna anaelewa umuhimu wa namba 3 katika jamii zetu. Nahisi kuwa Watanzania pia tuliipa hii nambari 3 umuhimu wa pekee na ningependa kujuwa Zaidi. Kwa kutamatisha, ilikuwaje mama zetu waliamua kupika kwa kutumia mafiga matatu na siyo manne?

Naomba kuuliza.

NB: HUU MJADALA NIMEUTOA KWENYE MTANDAO MMOJA, NIKAONA UNAFAA KUJADILIWA HAPA. KWAHIYO MIMI SIO MWANDISHI.
 
mmhh ndugu yangu ukifatilia hayo manamba yatakuchanganya bure...kama alivosema Bonesmen kuna namba 7 nayo ina matukio mengi ukiwekewa hapo unaweza kubadili msimamo..vipi kuhusu 40?? unaweza pia kuielezea vipi kuhusu 12 ??
kwa mfano 40..mvua ya gharika ni sku 40,za mwizi ni 40,marehem kusomewa hitma ni siku40,kwa rezma ni siku 40,mtoto mchanga hutolewa nje baada ya sku 40,kwa waislamu mtume mohhamad(pbuh) alipewa utume baada ya miaka40,wazungu wanamsemo wao wanasema life start at 40,jesus alivofufuka alikaa dunian siku 40 kabla hajapaa mbinguni,nafkiri hata kibongobongo urais hupewi bila kuwa na miaka40, ...nafkiri wana jf wengine watakuja na nyongeza ya namba nyingine
 
mi niko tofauti kidogo tarehe za bahati kwangu ni zile zisizogawanyika kwa mbili hata tarehe mwezi mwaka nliyozaliwa pia haigawanyiki kwa mbili mi nadhani hizi ni imani ukiamini inakuwa
 
mmhh ndugu yangu ukifatilia hayo manamba yatakuchanganya bure...kama alivosema Bonesmen kuna namba 7 nayo ina matukio mengi ukiwekewa hapo unaweza kubadili msimamo..vipi kuhusu 40?? unaweza pia kuielezea vipi kuhusu 12 ??
kwa mfano 40..mvua ya gharika ni sku 40,za mwizi ni 40,marehem kusomewa hitma ni siku40,kwa rezma ni siku 40,mtoto mchanga hutolewa nje baada ya sku 40,kwa waislamu mtume mohhamad(pbuh) alipewa utume baada ya miaka40,wazungu wanamsemo wao wanasema life start at 40,jesus alivofufuka alikaa dunian siku 40 kabla hajapaa mbinguni,nafkiri hata kibongobongo urais hupewi bila kuwa na miaka40, ...nafkiri wana jf wengine watakuja na nyongeza ya namba nyingine

Nasupport usemacho mkuu. Hizi namba zipo nyingi tofauti tofauti na kila moja ikisimama ktk matukio fulani fulani.

Kwa hiyo mtoa mada angalia usije ukaachana na namba 3,ukajikuta unataka kujua kuhusu zingine.
 
Kila namba ina maana yake na chanzo chake ni Mungu mwenyewe tunaanza
Number
1.MUNGU NI MMOJA (UTAWALA SIKU ZOTE UTOKA KWA MMOJA )KAMA KUNA NCHI AU FAMILIA INATAWALIWA NA ZAIDI YA KIONGOZI MKUU MMOJA IKO HATALINI.
2.MAMLAKA ILIYOPO ULIMWENGUNI IMEGAWANYIKA MARA MBILI MBINGUNI NA DUNIANI TU
UTAULIZA VIPI ILE YA SHETANI IKO DUNIANI.
3.MUNGU NI UTATU NA MWANADAMU AMEGAWANYIKA KATIKA NAFSI TATU HIVYO KILICHO KAMILI HUWA NA SEHEMU TATU MUHIMU ANAVYOITAJI MWANADAMU NI MAJI,DAMU,MWILI.
4.HII NI MSALABA AMBAO UNA PANDE NNE IKIMAANISHA UKOMBOZI KWA WANADAMU DUNIANI AMBAKO KUNA PANDE KUU NNE SAA NYINGI ZA MAPUMZIKO UWA NI SAA NNE HIVYO PUMZIKO LILILETWA kwa msalaba
5.HUDUMA TANO ZENYE UKOMBOZI KAMA VILE UINJILSTI,UCHUNGAJI,UTUME,NABII,MWALIMU .KATIKA MALEZI HUWA TUNAFUNDISH,TUNAONYA,TUNAKEMEA,TUNALEA KWA UPOLE NA KUFUNZA TARATIBU,PIA,TUNAANDAA MAZINGIRA BORA.
6.TUNATUMIA SIKU SITA KUFANYA KAZI NA TUNAENDELEA KUFANYA KAZI KWANI HUKAMILIKA BAADA YA SIKU SITA KUISHA NDIO MAANA ILE YA SABA UTAPUMZIKA
7. KAMILIFU PUMZIKO BAADA YA KUKAMILISHA MAMBO YAKO.
KUUSU NANE NA TISA ZINA MUUNGANIKO NA ZINAITAJI KUELEZWA KIREFU HIVYO NAZIRUKA NTAZIELEZA WAKATI MWINGINE.
10.NI MUNGU KATIKA DUNIA YAANI SUFURI NI DUNIA.
JE UNA SWALI LOLOTE KUHUSU MASWALA YA KIROHO USISITE NIULIZE AU NITAFUTE FACEBOOK KWA NAMBA JINA JEREMIAH MATHAYO NA WHATSAP NO 0768936317
 
Unapoanza mashindano yoyote unahesabiwa hadi tatu, yaan 1.....2....3

Unapoanza kubeba kitu kizito unahesabu hadi tatu.

unapomtisha mtoto unahesebu hadi tatu. y 3?
 
Ukitaka kufanya jambo lolote lazima ufanye kwa namba. Na namba kuu kuliko zote lenye nguvu duniani ni 3. Ni maelezo marefu kuelezea humu jukwaani.
Mkuu tafadhali tafuta muda uweke hayo maelezo marefu hapa hata in summary form.
 
Back
Top Bottom