Umri wa mpiga kura ubadilishwe

JoJiPoJi

JF-Expert Member
Aug 8, 2009
2,907
3,261
Robert Nyanda



Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ibadilishe sifa ya umri wa kupiga kura kutoka miaka 18 ya sasa na kuwa miaka 14 ili kutoa fursa kwa vijana wengi wenye umri huo kutumia haki yao ya msingi ya kupiga na kupigiwa kura.


Kampeni za uchaguzi mkuu wa Jamhuri ya Muungano na Zanzibar kwa nafasi za udiwani, ubunge na urais zilitia nanga Oktoba 30, 2010. Zilidhirisha umuhimu wa kubadilishwa kwa ibara ya 5 (1) ya Katiba yetu.


Katika kipindi chote hicho cha kampeni tulishuhudia wagombea wakijinadi kwa sera za vyama vyao na kutoa ahadi lukuki ili mradi kuwashawishi wapiga kura kuwachagua kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.


Kutokana na mwamko wa Watanzania katika uchaguzi ukihanikizwa na vyombo vya habari vilivyo kuwa bega kwa bega na wagombea katika harakati zao za kuomba ridhaa ya wananchi kuongoza.


Watu wengi walijitokeza katika kampeni hizo, hali iliyoonyesha mwamko wa kweli kwa Watanzania kuhusiana na mambo ya uchaguzi na kupelekea wanasiasa wengi hasa vijana kuamini kuwa utakuwa na mabadiliko makubwa.


Kampeni hizo zilishuhudia mchuano mkubwa sana kati CCM na CHADEMA kutokana na wagombea wake kuteka nyoyo za wengi na kutoa matumaini ya kuleta maisha bora kwa Mtanzania kwa kipindi cha miaka mitano endapo watawapa ridhaa ya kuwaongoza.


CCM ilimsimamisha Jakaya Kikwete wakati CHADEMA iliwakilishwa na Dk. Willbrod Slaa ambaye alikuwa akipata mapokezi makubwa wakati wa kampeni zake.


Umati mkubwa uliokuwa ukimlaki mgombea huyo, uliwafanya CCM kupata kiwewe na kuamini kuwa hali haikuwa kama ilivyotarajia kabla ya kampeni kuanza.
Huu umati uliokuwa ukijitokeza katika mikutano ya kampeni za wagombea wa udiwani, ubunge na urais ndiyo hasa msingi wa mada yangu leo.


Nimehudhuria mikutano mbalimbali ya wagombea kwa nafasi za urais na kwa haraka haraka niligundua kuwa kuna haja ya kubadili sheria ya uchaguzi kuhusu umri unaostahili kwa mpiga kura.
Ibara tajwa hapo juu inasema “Every Citizen who has attained 18 years is entitled to vote in any election”. Maana yake “Kila raia aliyetimiza umri wa mia 18 na mwenye akili timamu ana haki ya kupiga kura katika uchaguzi wowote”.


Ni ukweli usiopingika kuwa wengi wanaohudhuria katika mikutano hiyo ni vijana wa chini ya umri wa miaka 18 ambao kimsingi sheria ya uchaguzi haiwaruhusu kushiriki kupiga kura kwa kiongozi wanayemtaka.
Sheria hiyo inamtambua kama mtoto asiyekuwa na ufahamu mzuri wa mambo na hivyo hawezi kutoa uamuzi sahihi wa kura yake.


Sheria hii imepitwa na wakati na kwa hali hiyo inatakiwa kubadilishwa ili iendane na mazingira halisi ya Mtanzania wa sasa. Mabadiliko hayo yazingatie umri wa kuishi (life expectance) wa Mtanzania kwa sasa ambao ni kati ya miaka 47 na 50.


Nikirejerea nyuma kidogo wakati sheria hii inatungwa (1977), yawezekana ilizingatia zaidi umri wa kuanza na kumaliza elimu ya msingi ambayo kipindi hicho ilikuwa ya lazima. Lakini pia kumaliza elimu ya sekondari.
Kwa wakati huo haikuwa rahisi kwa mtoto kuanza darasa la kwanza akiwa na umri wa miaka mitano ama sita kama ilivyo sasa.


Tume ya uchaguzi kwa wakati huo yawezekana kabisa iliamini kuwa mtu mwenye akili timamu na mwenye uwezo wa kupiga kura ni yule ambaye ana umri wa kuwa sekondari, hata kama hakubahatika kusoma.
Kama elimu ya sekondari ndiyo ilikuwa kigezo cha mtu kupiga kura kwa wakati huo, basi kwa sasa hali ni tofauti kabisa, kwani umri wa kwenda shule umebadilika mno.


Sasa umri wa kwenda shule ni kati ya miaka mitano hadi saba kitu ambacho kinafanya watoto hawa kuhitimu Elimu ya msingi wakiwa na umri wa miaka 11 hadi 13. Na kwa mantiki hiyo basi umri wa kuanza sekondari ni kati ya mika 12 na 14.


Kwa mtazamo wangu, katika kipindi hiki cha vuguvugu la mabadiliko ya Katiba, napendekeza suala la umri wa mpiga kura uangaliwe upya.
Mfanye haya kwa kuzingatia umri wa kuishi wa Mtanzania ambao kwa sasa umekadiriwa kuwa ni chini ya miaka 40, fikirieni pia mabadiliko ya kimaumbile ya vijana ambao wanaonekana wazee hali wakiwa.


Pia zingatieni kuwa kijana ni taifa la leo na mtoto ni nguvu kazi mbadala.
 
Sijawafiki wazo hilo.

Umri wa miaka 14 bado ni watoto hata thamani ya kura yake hajaijuwa
 
Uhuru wa kuongea,
mkuu nadhani tukomae na idadi ndogo iliyojitokeza kuvote kulinganisha na waliojiandikisha, kuliko kuongeza umri wa piga kura
 
Wazo la chekechea hilo..!!!!

Nick nasikitika umewahi kumhukumu without giving support to your conclusion. Nadhani jamaa ana point ndani yake

Kama umefuatilia siasa hata za nje utagundua JP sio wa kwanza kuwa na wazo hili. Kuna wakati National Youth Rights Association |(NYRA) ya Marekani walipiga kelele sana juu ya kupunguzwa kwa umri wa mpiga kura. Walitoa sababu zao 10 za ni kwanini umri wa mpiga kura upunguzwe
Top Ten Reasons to Lower the Voting Age

  1. Youth suffer under a double standard of having adult responsibilities but not rights
  2. Youth pay taxes, live under our laws, they should have the vote
  3. Politicians will represent their interests if youth can vote
  4. Youth have a unique perspective, they'll never have those experiences again
  5. 16 is a better age to introduce voting than 18; 16 year olds are stationary
  6. Lowering the Voting Age will increase voter turnout
  7. If we let stupid adults vote, why not let smart youth vote?
  8. Youth will vote well
  9. There are no wrong votes
  10. Lowering the voting age will provide an intrinsic benefit to the lives of youth

Tembelea kwa maelezo zaidi National Youth Rights Association - Top Ten Reasons to Lower the Voting Age

Kwa mfano kama tunadhani wa umri wa miaka 16 hawajui thamani yao ya kura na wataiuza, je kuna watu wazima wangapi ambao tunalalamika watauza?

Pia angalia mabadiliko ya watoto kwa sasa, miaka 12 mpaka 14 kuitwa mama au baba ni juambo la kawaida.

Tunaweza kuangalia upya japo kwa ukweli kwa watoto wetu miaka 14 ni kidogo labda tungedhani 16
 
Bado watoto sana!Hata hawatajua wanamchagua nani na kwasababu zipi!
 
Nilibahatika kuangalia kama sikosei ni kipindi cha skonga cha eatv ch 5, ilikuwa aibu walikuwa wanahojiwa wanafunzi wa sekondari na miaka yao ilikuwa ina range 14-16 kuhusu mambo ya uchaguzi.
wengi wao hamna kitu kabisa
 
Nilibahatika kuangalia kama sikosei ni kipindi cha skonga cha eatv ch 5, ilikuwa aibu walikuwa wanahojiwa wanafunzi wa sekondari na miaka yao ilikuwa ina range 14-16 kuhusu mambo ya uchaguzi.
wengi wao hamna kitu kabisa

mimi napingana na wale wanaosema kupunguza umri kwa wapiga kula si sahihi,kabla ya yote naomba tuelewe kuwa wakati muda huu wa miaka 18 unawekwa uelewa wa watu ulikuwa unachelewa sana kutokana na hali ya kipindi kile,kwa sasa watoto wanaelewa mambo tofauti na watoto wa kipindi cha TANU,suala la utandawazi limechangia sana uelewa huo hasa luninga na wingi wa radio.

Suala la kuangalia kipindi cha sikonge eti ndiyo sababu mimi sikubaliani na Paulss kwa sababu tatizo si hao wanafunzi bali ni mfumo mzima wa utolewaji wa elimu ya uchaguzi,je ni vijana wangapi tena wenye familia kabisa ambao hawajui umuhimu wa kupiga kura?je haukuwai kukutana na watu wa aina hiyo!unakutana na kijana anasema haoni umuhimu wa kupiga kura!kama ni umri anazaidi ya miaka 30.

mimi nakubalina kuwa umri upunguzwe ila suala la kujadili ni mpaka umri upi,kwani kutoka 18 hadi 14 inaweza kuwa tatizo,binafsi tukianzia 16 si mbaya na hapo hapo tukazanie elimu ya uchaguzi iwe ya lazima kama matangazo ya ukimwi.

naomba watu waelewe kuwa kupunguza umri ni sehemu mojawapo ya maendeleo kwa taifa kwani hata nchi zingine umri wa maamuzi ni miaka 16,na anashangaza kukataa kupunguza umri wakati ndoa za miaka 15 zinakubaliwa kisheria hapa nchini,je ni lipi gumu, ndoa au kupiga kura?
 
mimi napingana na wale wanaosema kupunguza umri kwa wapiga kula si sahihi,kabla ya yote naomba tuelewe kuwa wakati muda huu wa miaka 18 unawekwa uelewa wa watu ulikuwa unachelewa sana kutokana na hali ya kipindi kile,kwa sasa watoto wanaelewa mambo tofauti na watoto wa kipindi cha TANU,suala la utandawazi limechangia sana uelewa huo hasa luninga na wingi wa radio.

Suala la kuangalia kipindi cha sikonge eti ndiyo sababu mimi sikubaliani na Paulss kwa sababu tatizo si hao wanafunzi bali ni mfumo mzima wa utolewaji wa elimu ya uchaguzi,je ni vijana wangapi tena wenye familia kabisa ambao hawajui umuhimu wa kupiga kura?je haukuwai kukutana na watu wa aina hiyo!unakutana na kijana anasema haoni umuhimu wa kupiga kura!kama ni umri anazaidi ya miaka 30.

mimi nakubalina kuwa umri upunguzwe ila suala la kujadili ni mpaka umri upi,kwani kutoka 18 hadi 14 inaweza kuwa tatizo,binafsi tukianzia 16 si mbaya na hapo hapo tukazanie elimu ya uchaguzi iwe ya lazima kama matangazo ya ukimwi.

naomba watu waelewe kuwa kupunguza umri ni sehemu mojawapo ya maendeleo kwa taifa kwani hata nchi zingine umri wa maamuzi ni miaka 16,na anashangaza kukataa kupunguza umri wakati ndoa za miaka 15 zinakubaliwa kisheria hapa nchini,je ni lipi gumu, ndoa au kupiga kura?

Ni asilimia ngapi ya watoto wana access na Luninga?

Naomba mfano wa nchi ambapo wapiga kura wake ni 14 (kwa faida yangu tu)
 
Ni asilimia ngapi ya watoto wana access na Luninga?

Naomba mfano wa nchi ambapo wapiga kura wake ni 14 (kwa faida yangu tu)

Naomba usome kwanza kabla ya kuandaa swali!nimesema kwa maoni yangu iwe miaka 16 sijatamka 14,nimesema 14 inaweza kuwa tatizo,kuhusu luninga sikuongelea luninga tu,nimesema na radio,mbona radio ukuuliza?kama si luninga itakuwa radio,na luninga si lazima wamiliki jiulize ni wangapi wanamiliki dstv lakini vijana wengi wanaongelea mipira ya ulaya!wanawezaje kufahamu?kwa umri nilionao kikatiba ifikapo 2015 naruhusiwa kugombea urais,sasa ni bora kujua umri wako kwani kama unabisha kuwa uelewa wa watoto umeongezeka kulinganisha na watoto wa miaka ya 1964 naomba msamaha sina jinsi ya kukuelimisha kwani umri wako utakuwa ni wa miaka ya 1990...hivyo uwezi kuelewa kwani utaki kuelewa bali umejiandaa kwa ubishi.
 
Tungeangalia historical reasons za kuopt 18 years kuwa ni umri wa franchise, baada ya hapo tutaona kama wazo hili ni sawa au la.
 
Back
Top Bottom