The Quonquerer
JF-Expert Member
- May 14, 2009
- 777
- 111
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Na Prudence Karugendo [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]LIPO wazo la kuunda Shirikisho la Nchi za Afrika Mashariki (EAC). Wazo hilo, kama siyo la kusadikika, linaenda mbele zaidi kutupa matarajio ya kuwa na nchi moja ya Afrika Mashariki hapo baadaye. [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Hili ni wazo lisilo na tofauti na lile lililoshikiwa bango na kiongozi wa kudumu wa Libya, Kanali Muammar Gaddafi, la kutaka kuwa na nchi moja ya Afrika. Wakati Gaddafi akiota nchi moja ya Afrika kila alalapo, rafiki yake Yoweli Kaguta Museveni wa Uganda naye amekuwa akiota nchi moja ya Afrika Mashariki kila alalapo. [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Na hawa viongozi marafiki wanalo jambo moja linalowafanya wasifanane tu bali kuonekana mapacha katika nyanja ya utawala, nalo ni kupenda kuwa watawala wa kudumu. Zamani watawala wa aina hiyo walikuwa wakijitawaza kuwa watawala wa maisha, ila kwa sasa neno hilo ni kama wanalionea aibu na kuamua kutumia njia nyingine ambayo bado inawahakikishia utawala wa kudumu (wa maisha). Wanajifanya wa kudumu badala ya wa maisha, kitu kinabaki kilekile. [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Kuhusu Shirikisho la Afrika Mashariki naona watu wanaliangalia kwa mitizamo tofauti tofauti. Wapo wenye mawazo kuwa shirikisho ambalo baadaye linaweza kugeuka kuwa nchi moja manufaa yake ni kuwa na nchi moja kubwa itakayokuwa imara kiuchumi, pengine kuwa na nguvu kubwa za kijeshi na kadhalika. [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Lakini kwa upande wangu nayakataa mawazo ya aina hiyo. Nayakataa katika misingi ya kwamba sisi watu wa eneo hili bado tuna roho dhaifu, roho zetu bado zinatawaliwa na umimi, roho hizi kamwe hazituwezeshi kujenga shirikisho. [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Tusiangalie penye shirikisho tukadhani hiyo ni neema inayoweza kutokea kila pahala kama inyeshavyo mvua. Shirikisho linajengeka katika mioyo ya watu waliojitoa na kuusahau umimi na kuliwaza shirikisho tu badala yake. [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Shirikisho linahitaji watu wenye roho za shirikisho, watu wanaowaza kishirikisho, kufikiria kishirikisho, kuamua kishirikisho. Watu wenye mtizamo wa sisi Afrika Mashariki, na wala siyo sisi Watanzania, sisi Wakenya au sisi Waganda na kadhalika. [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Tutakapokuwa tumefikia uungwana wa aina hiyo ndipo nitakapoamini kuwa suala la Shirikisho la Afrika Mashariki linaweza likaongelewa. Lakini kwa jinsi mambo yalivyo kwa sasa bado naona ni kama ndoto za Alinacha zinazotufanya tuwe na mawazo haya ya kusadikika. [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Udhaifu huo tulio nao ndio uliokuwa unanisukuma kulikataa shirikisho la nchi za Afrika Mashariki, udhaifu wa kutamani kitu kimoja wakati hatuna mawazo ya umoja. Ni wazi kwamba hatuna mawazo ya umoja kuanzia kwenye nchi zetu hizi moja moja, sasa mawazo ya kujenga umoja wa shirikisho tutayatoa wapi? [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Maana watu wenye mawazo ya umoja kamwe hawawezi kungangania madaraka iwe ni kwa mtu mmoja mmoja au chama. Unganganizi wa madaraka katika hizi nchi zetu zinazojigamba kuunda shirikisho unatoa picha gani? [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Hebu tuangalie yanayoendelea katika nchi zetu hizi. Kwa upande wa Tanzania kuna Chama cha Mapinduzi chenye tamaa ya kutawala milele, nchini Rwanda kuna Kagame mwenye tamaa ya kutawala milele, Uganda kuna Museveni ambaye naye anatamani kutawala milele. Kenya kuna Kibaki anayeshindwa na kukatalia Ikulu. [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Huo wote ni udhaifu unaoletwa na umimi. Na haijawahi kutokea udhaifu na udhaifu ukaunganishwa kikapatikana kitu kilicho imara. Sanasana kitakachopatikana ni udhaifu mkubwa zaidi. Na kama ni hivyo kwa nini tuungane kuutafuta udhaifu mkubwa zaidi? [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Nadhani kinachotushawishi, tulio wengi, kulitamani shirikisho na baadaye kuwaza nchi moja ni mafanikio ya nchi zilizoungana kama vile Amerika (USA). Ila tunasahau kuwa katika wengi kuna mengi, wapo vilevile wanaolitamani shirikisho kwa maslahi yao yaliyo tofauti kabisa na maslahi ya wananchi wa eneo hili. [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Wapo wanaotamani kutawala eneo kubwa ambalo ndani yake kuna mlima mkubwa kuliko yote Afrika, Kilimanjaro, ziwa kubwa kuliko yote Afrika, Victoria, na kadhalika. Sidhani kama hayo ndiyo mambo tunayoyatamani wananchi wa eneo hili katika shirikisho letu au katika nchi yetu, tunatamani zaidi ya hapo. Kwa ufupi tunatamani kuungana kwetu kutuboreshee maisha yetu. [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Kikwazo kinachojitokeza ni kwamba tunakosa uungwana wa kuliangalia shirikisho katika mtizamo wenye kuleta manufaa kwa watu wote wa Afrika Mashariki, na badala yake tunatawaliwa na uchu wa kila mmoja kuliangalia kutokea kwenye nchi yake na si ajabu hata kwenye mkoa wake akizingatia ni namna gani nchi yake au mkoa wake utakavyonufaika na shirikisho hilo. [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Tatizo hilo ndilo lililomfanya hata Waziri wa Kenya anayeshughulikia Uhusiano wa Afrika Mashariki, Amason Kingi, kuhoji usahihi wa Makao Makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kuendelea kubaki Arusha. Pamoja na hoja alizozitoa majuzi, kinachojitokeza zaidi ni yeye kutaka kuvutia upande wa nchi yake kwa kuona kuwa makao makuu kuendelea kubaki Arusha yanainufaisha zaidi Tanzania. [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Yeye anaona makao makuu ni bora yakawa Nairobi, sehemu ambayo umbali wake na Arusha ni wa pua na mdomo. Kwa hiyo Kingi hana mawazo ya Afrika Mashariki kichwani mwake, ila kilichomo ni Kenya yake. [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Rwanda nayo ikaja na madai yake ya kwamba Arusha ni pembeni mno. Kwa kujibu hoja hizo Waziri anayeshughulikia Uhusiano wa Afrika Mashariki wa Tanzania, Diodorus Kamala, naye akaonyesha udhaifu ule ule wa umimi. Yeye alionyesha kwamba iliyochokozwa ni Tanzania kana kwamba Makao Makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki yanapaswa kuwa mali ya Tanzania. [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Maana alivyoongea si kama mtu wa Afrika Mashariki bali zaidi kama Mtanzania. Hakuonyesha kutetea Makao Makuu yale kubaki Arusha kwa faida ya watu wa Afrika Mashariki, ila alionyesha wazi kutetea faida ya Tanzania. [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Sasa na tuangalie mvurugano huo, Wakenya wanasema Makao Makuu bora yawe Nairobi, Watanzania wanacharuka hawataki mjadala wowote kuhusu hilo. Wanadai Makao Makuu ni Arusha, basi. Eti mkataba unasema hivyo! Sijui huo ni mkataba wa kwenye Biblia! [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Wengine wana mawazo ya kwamba kwa vile Rwanda na Burundi ni washirika wapya katika jumuiya hiyo basi hawapaswi kuwa na kauli. Yote hiyo inachangiwa na umimi, kitu ambacho ni hasidi mkubwa wa ushirika au jumuiya, ambacho hakiwezi kutuacha tukafanikisha kitu kama hiki tunachojaribu kukiunda. [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Inabidi tuelewe kuwa kama kumeonekana umuhimu wa kuwashirikisha Rwanda na Burundi vilevile ni lazima upo umuhimu wa kusikiliza kauli zao. Ni ujinga kusema kwamba wao ni wageni hivyo wasitoe kauli hata kama ni ya manufaa. [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Pia wapo wenye mawazo ya kwamba ikiwezekana Rwanda na Burundi wanaweza wakafutwa tukabaki kama tulivyokuwa mwanzo, Tanzania, Uganda na Kenya. Ila tusisahau kwamba mawazo ya aina hiyo yanatuelekeza kwa Charles Njonjo, ukishaanza dhambi ya kufuta hutaacha mpaka uhakikishe unabaki peke yako. Kwa hiyo wenye mawazo ya kuzifuta Rwanda na Burundi kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki wajue ni kama wameishaifuta jumuiya yenyewe. [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Kama kweli tuna dhamira ya kuwa na shirikisho inabidi tujifunze kufanya mambo yetu kishirikisho kuanzia wakati huu. Maamuzi yetu yawe ya kishirikisho, mitizamo yetu iwe ya kishirikisho na fikira zetu ziwe za kishirikisho. Mfano mkataba unaosema kwamba makao makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki yatakuwa Arusha haujatoka kwa Mungu, kwa maana hiyo siyo haramu kuuongelea. [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Pengine wakati unasainiwa Rwanda na Burundi walikuwa hawajaonyesha nia yao ya kujiunga. Hivyo kujiunga kwao ni lazima kuonyeshe kuimarika kwa Jumuiya, na si kuimarika kwa kuongeza eneo la Jumuiya na idadi ya watu tu, bali pia mawazo. [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Sasa kwa nini mawazo yao ya kushauri ni wapi wanaona makao makuu yangefaa yawepo yapuuzwe kwa kigezo cha kwamba wao ni wageni? Kama wageni hawapaswi kuchangia lolote tumewakaribisha wa nini kwenye jumuiya yetu? [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Nikizungumza kama mtu anayeitakia heri Jumuiya ya Afrika Mashariki, ningeulizwa swali ni wapi naona panafaa kuwa makao makuu ya jumuiya hii, bila kuuma maneno, jibu langu lingekuwa Kampala. Si Arusha, Nairobi wala kwingineko. Hiyo ni kutokana na ninavyoijua jiografia ya eneo letu. Kampala ndipo sehemu inayofikika kwa urahisi kuliko sehemu zote kutokea pande zote za jumuiya hii. [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Nakizungumzia kwa kutumia njia zote za usafiri, barabara, reli, anga na hata usafiri wa majini. Kwa hiyo ni rahisi kwa kila mwanajumuiya kuyafikia makao makuu yake kiurahisi kuliko yalivyo sasa mjini Arusha. [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Wanaosema kwamba Arusha kunafaa inabidi watueleze sababu nzuri ya mtizamo wao, kulingana na mahitaji ya jumuiya, iliyo tofauti na muwamba ngoma, inayoweza kumfanya mtu wa Burundi kupaona Arusha ni sehemu sahihi kwake kuliko Kampala kwa mfano. [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Suala la amani kwa upande wa Arusha hilo halimo tena kwenye ajenda tukitilia maanani hali halisi ya usalama ilivyo katika mji huo ambao vivutio vyake vimeugeuza kuwa kitovu cha uharamia katika eneo hili la Afrika Mashariki. [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Najua kuna Watanzania wenzangu watakaonishangaa, lakini hapa mimi naongea kama mtu wa Afrika Mashariki nikijaribu kuuweka bayana ukweli. Kuupuuza ukweli huo itakuwa ni kuufanya mchakato mzima unaoendelea uonekane kama mchezo wa kuigiza au mpango wa kutegana ili kufanyiana hadaa. [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Na hicho ni kitu ambacho hakifai kwa watu ambao tayari wanajiona ni waungwana. Ni aibu kushindwa kuweka mambo katika mpangilio sahihi wakati huu ambao ni zaidi ya miaka 200 tangu wenzetu wafanye kitu kama kile kule Marekani. [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]prudencekarugendo@yahoo.com [/FONT]
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]0784989512[/FONT]