Umeyasikia ya Tatu Ntimizi?

rimbocho

Member
Jan 11, 2010
73
3
BAADHI ya wananchi wa Jimbo la Igalula ambao ni wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wametoa malalamiko kwa mwenyekiti wa chama hicho taifa kuhusu uongozi mbaya wa mbunge wao. Jimbo la Igalula linaongozwa na Tatu Musa Ntimizi.

Katika barua yao kwenda kwa Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Jakaya Kikwete, wananchi hao wanasema hawataki kumwona mbunge huyo akiendelea kuliongoza jimbo hilo. Jimbo la Igalula lilianzishwa rasmi mwaka 1995 baada ya kugawanywa kwa Jimbo la Tabora Kaskazini.


Baadhi ya tuhuma dhidi ya Ntimizi ni kwamba amekuwa akitumia nafasi yake ya uongozi kumlazimisha Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Tabora Vijijini kumpatia mwanaye Musa Ntimizi kazi za ukandarasi wa majengo na madaraja.


Inadaiwa kuwa Musa hana taaluma wala sifa za ukandarasi, isitoshe hata kampuni ya ukandarasi hana.


“Kwa mfano alipewa ukandarasi kujenga zahanati katika vijiji vya Imalakaseko, Igalula na Goweko pamoja na daraja la barabara ya Kigwa hadi Itundaukulu. Kibaya zaidi, baadhi ya watu aliokuwa anawapatia vibarua, hajawalipa fedha zao walizokubaliana hadi sasa,” inasema sehemu ya barua hiyo.


Wadai wa Mussa wametajwa kuwa ni pamoja na Ashura Mfaume na Ashura Selemani wanaodai Sh 35,000, ambao walipewa kazi ya kuponda kokoto zilizotumika kujenga Zahanati ya Goweko. Wengine ni Kajuna Daudi na Michael Malambo wanaodai Sh 84,000 kwa kazi ya kusomba mchanga na kufyatua matofali.


“Shule ya Sekondari Goweko inadaiwa kumdai pia Sh 405,000. Majengo ya Zahanati za Imalakaseko na Goweko bado hayajakamilika kujengwa hadi sasa, ingawa tayari ameshalipwa fedha kabla ya kumaliza kazi,” inasema barua hiyo.


Lakini pia, Mbunge Ntimizi anadaiwa kuwanyanyasa wananchi katika masuala mbalimbali ya kijamii. Kwa mfano, inadaiwa Machi 25 mwaka huu, mbunge huyo alizuia basi lililokuwa limewabeba wana-CCM kuelekea Goweko kwa ajili ya sherehe za kuwasimika makamanda wa UVCCM Wilaya ya Uyui.


Wananchi hao wanasema: “Mbunge Ntimizi, kwa kutumia madaraka yake, aliwaamuru polisi wa Tabora Mjini kumzuia mmiliki wa basi la NBS lililokuwa limekodiwa na CCM Wilaya kuwapeleka makamanda na viongozi wa CCM kuhudhuria sherehe hizo. Gari hilo lilizuiwa tangu saa mbili asubuhi hadi saa tisa alasiri liliporuhusiwa.”


Aidha, Mbunge Ntimizi anadaiwa kukopa Sh milioni 40 kutoka Mfuko wa Pembejeo kwa kutumia jina la mtoto wake, Saidi Rashidi Omari.


Hata hivyo, pembejeo hazikupelekwa Jimbo la Igalula na hivyo kuulazimu Mfuko wa Pembejeo Taifa kumshitaki mbunge huyo. Kesi hiyo namba Na. 19 ya mwaka 2006 iko Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam, wadaiwa ni Saidi Rashidi Omari na Tatu Ntimizi mwenyewe.


Inadaiwa pia kwamba mbunge Ntimizi amekuwa akivitumia vyombo vya dola kwa maslahi yake ili kuwasumbua wananchi ambao wamekuwa wakitangaza nia zao za kugombea ubunge wa jimbo hilo.


Baadhi ya wanachama wa CCM walioshitakiwa na Ntimizi kwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa, ni pamoja na Hanifa Tambulu, Athumani Rashid Mfutakamba, Katibu wa CCM (Uchumi), Suma Mamloo, Katibu wa CCM (W) Uenezi, Kapalu na Mwenyekiti wa CCM (W), Kazwika.


Kuna madai kuwa Tatu Ntimizi amekuwa akitoa fedha za kiasi cha Sh 2,000 kwa wajumbe wa nyumba 10, makatibu wa CCM wa matawi Sh 5,000 na makatibu wa kata Sh 10,000 kwa kumtumia Katibu wa Mbunge, Johnson Banda.


Baadhi ya wanachama wanaomlalamikia Ntimizi na namba zao za kadi za CCM katika mabano ni Miraji Mwalau (9999211), Shami Tandiko (35648), Idd Mlenge (1747271), Said Sumuni (594754), Shabani Mayega (35362) na Joha Hussein (862969). Wengine ni Salima Mbogo (432740), Hamisi Sukwa (35302), Issa Mtiliga (35304), Zainabu Hassan na Hadija Ramadhani (35303).
 
viongozi kama hawa ndo wanaichafua serikali. Kama wakigundulika ni kweli hamana haja ya kuwa nao katika uongozi zaidi ya kuwafukuza kazi na kuwafutia na uanachama kabisa. Hii imekuwa ni tabia ya viongozi walio wengi. Wanatumia vyeo vyao kujinufaisha wao wenyewe na ndiyo maana hata watoto wao hawana haja ya kusoma, kwani kila kitu wakitakacho wanapewa. Tunaelekea wapi? Yuko wapi mtoto wa maskini asiyekuwa nacho? Asiyetambuliwa? asiyethaminiwa? asiyeheshimika?
 
Kipindi hiki cha uchaguzi mbinu za kupata uongozi ni nyingi mno.
Isije ikawa ni sehemu ya technic ya kumng'oa huyo Tatu.
Nna mashaka.
 
Dada yangu Tatu Ntimizi amekuwa JUU kwenye ramani ya uongozi wa Tanzania kwa njia za ajabu sana.

Kuna siku nilisikia dada zangu wakimjadili jinsi anavypanda VYEO kwenye kazi ya UPOLISI. Ilikuwa anakwenda juu utafikiri miti ya Mikaratusi. Na hii ilikwenda hadi alipoamua kuingia kwenye SIASA. Mwaka 2005 kama sikosei alikuwa wa tatu kwenye uchaguzi ila majina yalipoenda Dodoma, lake ndiyo likarudi na wengine wakabwagwa. Mwaka huu pia amekuwa wa tatu ila nina HAKIKA kuwa jina lake halirudi.

Sababu ya kusema hivyo ni kuwa, nilishasikia majungu kuwa alikuwa akibebwa na jamaa fulani hivi. Ila jamaa mwenyewe sasa hivi yuko HOI kisiasa na mwenyewe anahitaji msaada. Sidhani kama atakuwa na nguvu ya kulazimisha tena Ntimizi jina lake lirudishwe. Wakirudisha basi CHADEMA nendeni mumchukue mshindi wa kwanza au wa pili na mtashinda wazi kabisa.

Kwa wanaofahamu hiyo story watakuwa tayari wameunganisha Dots. Na hii ndiyo ilinipa mwanga kwa nini alikuwa akipanda vyeo vya Polisi kwa speed ile. Vyeo vya Polisi kwa kweli wanapanda taaaratibu sana. Labda wewe kama unabebwa au unasoma saaana.
 
kwa kweli hata mimi niliwahi kusikia minong'ono kwambaa yupo mkulu alikuwa
anambeba. hata hivyo matokeo ya kura za maoni zinaonyesha kwamba
huyo mkulu na yeye inabidi apambane kivyake ili arudi ulingoni sasa sijui
kama safari hii atakuwa na stamina ya kumsaidia bibie pia. hata hivyo mambo ya siasa
za bongo ni magumu kiasi kutabirika.
 
CCM WAKIFANYA MAKOSA YA KUWARUDISHA WATU WALIOCHOKWA ITAKUWA PIGO KWAO............sawa na upinzani unavyookota makombo ya waliochokwa.......eg NJELU K.
 
Dada yangu Tatu Ntimizi amekuwa JUU kwenye ramani ya uongozi wa Tanzania kwa njia za ajabu sana.

Kuna siku nilisikia dada zangu wakimjadili jinsi anavypanda VYEO kwenye kazi ya UPOLISI. Ilikuwa anakwenda juu utafikiri miti ya Mikaratusi. Na hii ilikwenda hadi alipoamua kuingia kwenye SIASA. Mwaka 2005 kama sikosei alikuwa wa tatu kwenye uchaguzi ila majina yalipoenda Dodoma, lake ndiyo likarudi na wengine wakabwagwa. Mwaka huu pia amekuwa wa tatu ila nina HAKIKA kuwa jina lake halirudi.

Sababu ya kusema hivyo ni kuwa, nilishasikia majungu kuwa alikuwa akibebwa na jamaa fulani hivi. Ila jamaa mwenyewe sasa hivi yuko HOI kisiasa na mwenyewe anahitaji msaada. Sidhani kama atakuwa na nguvu ya kulazimisha tena Ntimizi jina lake lirudishwe. Wakirudisha basi CHADEMA nendeni mumchukue mshindi wa kwanza au wa pili na mtashinda wazi kabisa.

Kwa wanaofahamu hiyo story watakuwa tayari wameunganisha Dots. Na hii ndiyo ilinipa mwanga kwa nini alikuwa akipanda vyeo vya Polisi kwa speed ile. Vyeo vya Polisi kwa kweli wanapanda taaaratibu sana. Labda wewe kama unabebwa au unasoma saaana.

Embe dodo lililoivia mtini ni bora zaidi. Mkuu usemalo ni kweli kabisa huyu Tatu alikuwa ni kifutia machozi cha huyo bwana. Ni siku nyingi sana toka enzi alipokuwa Pinda wa wakati huo.
 
Embe dodo lililoivia mtini ni bora zaidi. Mkuu usemalo ni kweli kabisa huyu Tatu alikuwa ni kifutia machozi cha huyo bwana. Ni siku nyingi sana toka enzi alipokuwa Pinda wa wakati huo.
Duuh mshikaji umeamua utoboe kabisa,atapata mtu pressure hapa halafu iwe mshike mshike. Kwa hiyo jamaa alikuwa na mrs wawili mjengoni sio!!!!:love:
 
Hivi ni kweli mwanamke hawezi kupanda cheo au kupata ubunge bila ya kuwa na mwanamme wa kumbeba? Mbona shuleni huwa wanaendelea vizuri tu kitaaluma, kwa nini ikija kwenye kazi iwe lazima abebwe? Huo ni mfumo dume.

Jamani wacheni hizo. Kama alishindwa ubunge mwaka 2005 lakini akapatiwa sio yeye peke yake. Na nyinyi wanaume hata huko majimboni tu munawaonea wanawake na hiyo inaendelea mpaka leo.

Hebu angalia Shyrose Banji alivyokuwa akidhalilishwa na kupewa kila aina ya majina bila ya hata uthibitisho.
 
Mtanisamehe ndugu ila Sina Huruma kwa Wananchi kama hawa wanaolia lia lakini wakipewa Fursa wanawarudisha kwa Kishindo huku wakiwaimbia Mapambio. Mi nadhani wacha wapigike ili watie Akili
 
Kama kweli Tatu Ntimizi aliweza kuyafanya hayo yote yanayosemwa na hasa hili la "kumlazimisha Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Tabora Vijijini kumpatia mwanaye Musa Ntimizi kazi za ukandarasi wa majengo na madaraja"... inatisha sana! Ina maana serikali huko ni kaput kabisa... hakuna utawala bora hata kidogo.

Je vyombo vya dola vyenye kusimamia haya maswala ikiwemo TAKUKURU wamelala usingizi wa pono au wanamuogopa huyu mama kiasi gani? SHE MUST BE VERY POWERFUL THEN, WHICH I DONT WANT TO BELIEVE!

NADHANI mwenye tatizo siyo Tatu Ntimizi bali mfumo mzima ( if at all shutuma hizi ni za kweli).
 
Embe dodo lililoivia mtini ni bora zaidi. Mkuu usemalo ni kweli kabisa huyu Tatu alikuwa ni kifutia machozi cha huyo bwana. Ni siku nyingi sana toka enzi alipokuwa Pinda wa wakati huo.

Mkulu muhusika alipoamua kumuoa mshosti mwingine toka mle mle mjengoni, Tatu mwenyewe alitamka mjengoni kuwa "NIMEACHIA NGAZI"!!
 
Dada yangu Tatu Ntimizi amekuwa JUU kwenye ramani ya uongozi wa Tanzania kwa njia za ajabu sana.

Kuna siku nilisikia dada zangu wakimjadili jinsi anavypanda VYEO kwenye kazi ya UPOLISI. Ilikuwa anakwenda juu utafikiri miti ya Mikaratusi. Na hii ilikwenda hadi alipoamua kuingia kwenye SIASA. Mwaka 2005 kama sikosei alikuwa wa tatu kwenye uchaguzi ila majina yalipoenda Dodoma, lake ndiyo likarudi na wengine wakabwagwa. Mwaka huu pia amekuwa wa tatu ila nina HAKIKA kuwa jina lake halirudi.

Sababu ya kusema hivyo ni kuwa, nilishasikia majungu kuwa alikuwa akibebwa na jamaa fulani hivi. Ila jamaa mwenyewe sasa hivi yuko HOI kisiasa na mwenyewe anahitaji msaada. Sidhani kama atakuwa na nguvu ya kulazimisha tena Ntimizi jina lake lirudishwe. Wakirudisha basi CHADEMA nendeni mumchukue mshindi wa kwanza au wa pili na mtashinda wazi kabisa.

Kwa wanaofahamu hiyo story watakuwa tayari wameunganisha Dots. Na hii ndiyo ilinipa mwanga kwa nini alikuwa akipanda vyeo vya Polisi kwa speed ile. Vyeo vya Polisi kwa kweli wanapanda taaaratibu sana. Labda wewe kama unabebwa au unasoma saaana.

tingatinga..............
 
Na huyu pia? Mie nilisikia mwingine. Kumbe mleta habari wangu hakuwa sahihi sana au alikosea.
Kama ni huyu basi sasa naelewa kisa cha Sister kupanda vyeo miaka ya 80 wakati akiwa POLISI.
Dada zangu hao ambao wote ni Marehemu, walishangazwa sana na kupanda kwake.
Mie ndiyo nikaja kufahamu kuwa alikuwa Mnyamwezi.
Baadaye Wakamuongelea na Getrude Mongela ila wakasema jina la Getrude Ivongela?! Topic sikumbuki.
tingatinga..............
 
Sikonge, na Gertrude Mongella pia naye alipendelewa kwa vyeo vyote hivyo alivopata? Hamuwachi nyinyi!

Hatua nyengine basi muanze ku"declare" kwamba wanawake wote hawana akili na ni lazima wapewe upendeleo maalumu ndio waweze kufanikiwa.

Aah! munaniboa nyinyi wakati tulikuwa tunawapita nyinyi akina baba kwa mbali kiakili kuanzia primary mpaka vyuo vikuu!
 
Hilo nalo neno. Na mengine mengi yaja. CCM walikuwa wapi kuanzisha mfumo huu wa kura za maoni toka 1995? Labda haya yangetokea miaka hiyo na kutuepushia viongozi wa kupikwa!!!!!!
 
Hivi ni kweli mwanamke hawezi kupanda cheo au kupata ubunge bila ya kuwa na mwanamme wa kumbeba? Mbona shuleni huwa wanaendelea vizuri tu kitaaluma, kwa nini ikija kwenye kazi iwe lazima abebwe? Huo ni mfumo dume.

QUOTE]


....Tatu Abdalah alikuwa mwendesha mashtaka wa polisi na kati ya kesi alizowahi kusimamia ni ile kesi maarufu ya uhaini.....,baadaye alikuja kuteuliwa mkuu wa wilaya..na ni kipindi hicho pia alikuwa anatoka na waziri mkuu....wa wakati huo.....hilo halina ubishi hata kwenye hansard record zipo......."....kuna siku bungeni akiwa naibu waziri na baada ya waziri mkuu huyo kuwa amemuoa ANNA.....alipanda kujibu swali...the weddin had just ended ..alipoenda tu pale kwenye podium wabunge na mawaziri wenzake wakaanza kumcheka....kwa kuwa hakuolewa yeye...akajibu,"nilishaachia ngazi !!"

....sijui kuhusu utendaji wake kwa ujumla..na hatuwezi kuhusisha mahusiano na haki zake za msingi za kujamiiana....ila pale ardhi alikuwa akitumiwa sana na madalali wa viwanja......,anatamaa ya pesa ndogo ndogo!!...huyo mtoto wake ambaye ni mwenyekiti wa jumuia [alimshinda luoha kwa margin ndogo ]hapa dar......ni mfanyabiashara wa ajabu ajabu na anazo tuhuma nyingi za kuuza magari ya wizi ....na powder........naweza kuamini tuhuma za wana Ihagula....ambapo pia mama yake alikuwa anafikiria kumuachia jimbo!!!
 
Hivi ni kweli mwanamke hawezi kupanda cheo au kupata ubunge bila ya kuwa na mwanamme wa kumbeba? Mbona shuleni huwa wanaendelea vizuri tu kitaaluma, kwa nini ikija kwenye kazi iwe lazima abebwe? Huo ni mfumo dume.

QUOTE]


....Tatu Abdalah alikuwa mwendesha mashtaka wa polisi na kati ya kesi alizowahi kusimamia ni ile kesi maarufu ya uhaini.....,baadaye alikuja kuteuliwa mkuu wa wilaya..na ni kipindi hicho pia alikuwa anatoka na waziri mkuu....wa wakati huo.....hilo halina ubishi hata kwenye hansard record zipo......."....kuna siku bungeni akiwa naibu waziri na baada ya waziri mkuu huyo kuwa amemuoa ANNA.....alipanda kujibu swali...the weddin had just ended ..alipoenda tu pale kwenye podium wabunge na mawaziri wenzake wakaanza kumcheka....kwa kuwa hakuolewa yeye...akajibu,"nilishaachia ngazi !!"

....sijui kuhusu utendaji wake kwa ujumla..na hatuwezi kuhusisha mahusiano na haki zake za msingi za kujamiiana....ila pale ardhi alikuwa akitumiwa sana na madalali wa viwanja......,anatamaa ya pesa ndogo ndogo!!...huyo mtoto wake ambaye ni mwenyekiti wa jumuia [alimshinda luoha kwa margin ndogo ]hapa dar......ni mfanyabiashara wa ajabu ajabu na anazo tuhuma nyingi za kuuza magari ya wizi ....na powder........naweza kuamini tuhuma za wana Ihagula....ambapo pia mama yake alikuwa anafikiria kumuachia jimbo!!!


WAZIRI MKUU ALIEMUOA ANNA.....
YOU MEAN KAWAWA SIO??????NA ANNA NI ANNA ABDALLAH SIO?????

AMBAE LATER ALIOLEWA NA MSEKWA SIO??????

HAHA HA NILIWAHI ULIZA HAPA HII CCM FAMILLY TREE IKOJE???????
SIKUJIBIWA.....
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom