Katavi
Platinum Member
- Aug 31, 2009
- 41,983
- 12,701
Licha ya kukwapuliwa simu na vipesa ndani ya daladala lakini matukio haya mawili sitayasahau.....
1..Siku moja j/pili nimetoka zangu kanisani mida ya saa saba, nikaamua kwenda kupunga upepo ufukweni. Nikashuka pale sokoni feri na kuanza kutembea taratibu kuelekea pande zile ilipo "white house". Ghafla mvua ikaanza kunyesha, ikabidi nijisitiri chini ya mti maana ilikuwa kubwa. Muda kidogo ile mvua iliongezeka na mara nikaona raia kama wanne wakija upande niliopo. Wakaja mpaka pale nilipo nao wakajifanya wanajikinga na mvua katika ule mti, sikuwa na wasiwasi(mbele ya ikulu ulinzi wa kutosha). Ghafla nilipigwa bonge la mtama na kabla sijatua chini nikatiwa kabari ya hatari, na wengine wakaanza kunisachi na kuchukua kila kilichokuwa mfukoni. Nashukuru Mungu hawakuchukua coins 250, ambayo ilinisaidia kiasi kama nauli ya kurudia nyumbani Mbezi.
2..Tukio la pili lilinitokea miaka 11 iliyopita, napita vichochoro vya Ubungo maziwa ili nitokee ubungo stendi ya daladala nirudi zangu Mbezi. Ghafla akatokea jamaa nyuma yangu akaniambia "dogo simama nikuulize", kwa kumuona alivyo sikuwa na wasiwasi kabisa. Aliponifikia nilishangaa napigwa mtama na jamaa wengine wawili sikujua wametokea upande gani wakaanza kunisachi. Walichukua kila kitu hadi viatu, nusura wanivue hadi jinzi na tisheti kama si wapita njia wengine kutokea na wale jamaa kukimbia. Ilibidi "nijitoe fahamu" na kutembea pekupeku hadi Mbezi kwa mguu(hii siku sitaisahau), na sikumsimulia mtu yeyote huu mkasa mpaka leo hapa JF..
Hawa watu ni balaa...Hivi umewahi kukumbwa na hawa jamaa???
1..Siku moja j/pili nimetoka zangu kanisani mida ya saa saba, nikaamua kwenda kupunga upepo ufukweni. Nikashuka pale sokoni feri na kuanza kutembea taratibu kuelekea pande zile ilipo "white house". Ghafla mvua ikaanza kunyesha, ikabidi nijisitiri chini ya mti maana ilikuwa kubwa. Muda kidogo ile mvua iliongezeka na mara nikaona raia kama wanne wakija upande niliopo. Wakaja mpaka pale nilipo nao wakajifanya wanajikinga na mvua katika ule mti, sikuwa na wasiwasi(mbele ya ikulu ulinzi wa kutosha). Ghafla nilipigwa bonge la mtama na kabla sijatua chini nikatiwa kabari ya hatari, na wengine wakaanza kunisachi na kuchukua kila kilichokuwa mfukoni. Nashukuru Mungu hawakuchukua coins 250, ambayo ilinisaidia kiasi kama nauli ya kurudia nyumbani Mbezi.
2..Tukio la pili lilinitokea miaka 11 iliyopita, napita vichochoro vya Ubungo maziwa ili nitokee ubungo stendi ya daladala nirudi zangu Mbezi. Ghafla akatokea jamaa nyuma yangu akaniambia "dogo simama nikuulize", kwa kumuona alivyo sikuwa na wasiwasi kabisa. Aliponifikia nilishangaa napigwa mtama na jamaa wengine wawili sikujua wametokea upande gani wakaanza kunisachi. Walichukua kila kitu hadi viatu, nusura wanivue hadi jinzi na tisheti kama si wapita njia wengine kutokea na wale jamaa kukimbia. Ilibidi "nijitoe fahamu" na kutembea pekupeku hadi Mbezi kwa mguu(hii siku sitaisahau), na sikumsimulia mtu yeyote huu mkasa mpaka leo hapa JF..
Hawa watu ni balaa...Hivi umewahi kukumbwa na hawa jamaa???