Lunyungu
JF-Expert Member
- Aug 7, 2006
- 8,873
- 1,894
Date::10/26/2009'Huu si wakati wa kubeza Kilimo Kwanza'
Na Mwandishi Wetu
MWENYEKITI wa Mtandao wa Wadau wa Kilimo wa Asasi za Kiraia (Ansaf), James Davey amesema huu si wakati muafaka wa kuanza kukosoa dhana ya "Kilimo Kwanza" na badala yake utumike katika kufanikisha mapinduzi ya sekta hiyo muhimu nchini.
Davey, ambaye pia ni mkurugenzi mkazi wa shirika la Concern, aliwaambia waandishi wa habari jana jijini Dar es salaam akisema: "Tunafurahi kuona dhamira njema ya serikali katika kuendeleza kilimo... naona kuna fursa nzuri hata kama kuna kasoro kadhaa, lakini huu ni msingi na mahali pazuri pa kuanzia."
Davey, ambaye alikuwa akieleza yaliyojiri katika mkutano wa tatu wa mwaka wa mtandao huo uliofanyika mjini Dodoma hivi karibuni, alisema kwamba mkutano huo umeainisha mapendekezo manne yatakayowezesha mafanikio ya dira ya Kilimo Kwanza.
Akieleza mapandekezo hayo Mjumbe wa Ansaf, Salum Shamte alisema kwamba lengo la kwanza ni uratibu wa tasnia ya kilimo katika ngazi ya wilaya ambako jukumu la msingi ni kuwaunganisha wakulima na asasi za kiraia sawia na rasilimali watu na taaluma.
Alisema nyingine ni kuwezesha uendelezaji wa mlolongo wa kuongeza thamani akisema kwamba umefika wakati kwa sekta ya kilimo kulenga zaidi masomo badala ya kuishia katika uzalishaji pekee.
Azimio jingine la mkutano huo lilikuwa ni kuboresha ubia baina ya taasisi binafsi na za serikali akitoa mfano wa Mipango ya Kuendeleza Kilimo Ngazi za Wilaya (Dadp) inavyotoa fursa ya kushirikishwa kwa sekta binafsi, lakini ikikabiliwa na tatizo kubwa la maofisa wa ugani ambao wapo katika sekta binafsi.
Alisema jambo jingine muhimu ni kuwa na mipango ya kimkakati ya muda mfupi, wa kati na mrefu ya kuendeleza kilimo hasa katika ngazi za wilaya. "Katika hili ndipo utekelezaji mzima wa dhana ya Kilimo Kwanza unapokuja. Kubadili dhana ya kuendeleza kilimo kutoka kile cha kawaida cha kujikimu na kuwa cha kibiashara kwa kukiongezea thamani," alisema Shamte ambaye pia ni mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Katani Ltd.
Facebook
MWENYEKITI wa Mtandao wa Wadau wa Kilimo wa Asasi za Kiraia (Ansaf), James Davey amesema huu si wakati muafaka wa kuanza kukosoa dhana ya "Kilimo Kwanza" na badala yake utumike katika kufanikisha mapinduzi ya sekta hiyo muhimu nchini.
Davey, ambaye pia ni mkurugenzi mkazi wa shirika la Concern, aliwaambia waandishi wa habari jana jijini Dar es salaam akisema: "Tunafurahi kuona dhamira njema ya serikali katika kuendeleza kilimo... naona kuna fursa nzuri hata kama kuna kasoro kadhaa, lakini huu ni msingi na mahali pazuri pa kuanzia."
Davey, ambaye alikuwa akieleza yaliyojiri katika mkutano wa tatu wa mwaka wa mtandao huo uliofanyika mjini Dodoma hivi karibuni, alisema kwamba mkutano huo umeainisha mapendekezo manne yatakayowezesha mafanikio ya dira ya Kilimo Kwanza.
Akieleza mapandekezo hayo Mjumbe wa Ansaf, Salum Shamte alisema kwamba lengo la kwanza ni uratibu wa tasnia ya kilimo katika ngazi ya wilaya ambako jukumu la msingi ni kuwaunganisha wakulima na asasi za kiraia sawia na rasilimali watu na taaluma.
Alisema nyingine ni kuwezesha uendelezaji wa mlolongo wa kuongeza thamani akisema kwamba umefika wakati kwa sekta ya kilimo kulenga zaidi masomo badala ya kuishia katika uzalishaji pekee.
Azimio jingine la mkutano huo lilikuwa ni kuboresha ubia baina ya taasisi binafsi na za serikali akitoa mfano wa Mipango ya Kuendeleza Kilimo Ngazi za Wilaya (Dadp) inavyotoa fursa ya kushirikishwa kwa sekta binafsi, lakini ikikabiliwa na tatizo kubwa la maofisa wa ugani ambao wapo katika sekta binafsi.
Alisema jambo jingine muhimu ni kuwa na mipango ya kimkakati ya muda mfupi, wa kati na mrefu ya kuendeleza kilimo hasa katika ngazi za wilaya. "Katika hili ndipo utekelezaji mzima wa dhana ya Kilimo Kwanza unapokuja. Kubadili dhana ya kuendeleza kilimo kutoka kile cha kawaida cha kujikimu na kuwa cha kibiashara kwa kukiongezea thamani," alisema Shamte ambaye pia ni mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Katani Ltd.
Tuma maoni kwa Mhariri