Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,299
- 33,082
Shija Felician,Kahama
UMEME wa mionzi ya jua[ Solar] unaoendelea kufungwa kwa ufadhili wa Mbunge wa Jimbo la Msalala, Ezekiel Maige katika baadhi ya Shule za Sekondari za Kata wilayani Kahama umeelezwa kuchangia mabadiliko makubwa kitaaluma kwa wanafunzi wake wa shule hizo.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wakazi wa Kata za Ngaya,Bulige na Kinaga ambako mradi huo umeanza kutekelezwa walisema kuwa wanafunzi katika Sekondari za Kata za vijijini vyake sasa wanasoma masomo ya ziada nyakati za usiku kwa kutumia mwanga wa umeme huo.
Walidai kuwa pamoja na mazingira magumu walioyonayo wanafunzi hao katika shule hizo za kata lakini tangu mradi huo uanze kutekelezwa kumejitokeza mabadiliko makubwa kwenye taaluma hali ambayo imeleta matumaini ya kufanya vizuri katika mitihani yao.
Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Kata ya Ngaya, Kafuru Songora alidai kuwa tangu kufungwa kwa umeme huo shuleni kwake wanafunzi wake hutoka madarasani saa tisa mchanana kurejea tena saa kumi na mbili jioni kujisomea hadi saa nne usiku hali ambayo imebadilisha hali ya taaluma iliyokuwa mbovu kabla ya umeme huo.
Ofisa Mtendaji wa Kata ya Ngaya, Stephen Manyanda alisema kuwa Serikali ya Kijiji hicho inafanya mkakati wa kuimarisha ulinzi katika eneo la shule hiyo ili kuhakikisha wanafunzi hao wanaosoma nyakati za usiku wanatoka salama.
Mbunge wa Jimbo la Msalala ambaye pia ni Waziri wa Maliasili na Utalii Ezekiel Maige alisema kuwa ataendelea kufanya mikakati ya kuweka umeme kwa kila shule pindi atakapopata wafadhili na kwamba tayari amefanya hivyo katika Shule za Sekondari za Ngaya,Bulige na Kinaga.
Umeme wa Jua kubadili sura ya maendeleo Sekindari za Msalala
UMEME wa mionzi ya jua[ Solar] unaoendelea kufungwa kwa ufadhili wa Mbunge wa Jimbo la Msalala, Ezekiel Maige katika baadhi ya Shule za Sekondari za Kata wilayani Kahama umeelezwa kuchangia mabadiliko makubwa kitaaluma kwa wanafunzi wake wa shule hizo.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wakazi wa Kata za Ngaya,Bulige na Kinaga ambako mradi huo umeanza kutekelezwa walisema kuwa wanafunzi katika Sekondari za Kata za vijijini vyake sasa wanasoma masomo ya ziada nyakati za usiku kwa kutumia mwanga wa umeme huo.
Walidai kuwa pamoja na mazingira magumu walioyonayo wanafunzi hao katika shule hizo za kata lakini tangu mradi huo uanze kutekelezwa kumejitokeza mabadiliko makubwa kwenye taaluma hali ambayo imeleta matumaini ya kufanya vizuri katika mitihani yao.
Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Kata ya Ngaya, Kafuru Songora alidai kuwa tangu kufungwa kwa umeme huo shuleni kwake wanafunzi wake hutoka madarasani saa tisa mchanana kurejea tena saa kumi na mbili jioni kujisomea hadi saa nne usiku hali ambayo imebadilisha hali ya taaluma iliyokuwa mbovu kabla ya umeme huo.
Ofisa Mtendaji wa Kata ya Ngaya, Stephen Manyanda alisema kuwa Serikali ya Kijiji hicho inafanya mkakati wa kuimarisha ulinzi katika eneo la shule hiyo ili kuhakikisha wanafunzi hao wanaosoma nyakati za usiku wanatoka salama.
Mbunge wa Jimbo la Msalala ambaye pia ni Waziri wa Maliasili na Utalii Ezekiel Maige alisema kuwa ataendelea kufanya mikakati ya kuweka umeme kwa kila shule pindi atakapopata wafadhili na kwamba tayari amefanya hivyo katika Shule za Sekondari za Ngaya,Bulige na Kinaga.
Umeme wa Jua kubadili sura ya maendeleo Sekindari za Msalala