Kachanchabuseta
JF-Expert Member
- Mar 8, 2010
- 7,269
- 675
"Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, wakati akifungua rasmi Bunge Jipya la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Bungeni, Dodoma, 30 Desemba 2005
Mheshimiwa Spika:
Nishati ni sawa na chembe za damu mwilini. Serikali ya Awamu ya Nne itatoa kipaumbele katika kuboresha na kuendeleza upatikanaji wa nishati ya uhakika na rahisi vijijini na mijini.
Tutapanua wigo na aina ya vyanzo vya umeme na nishati kwa jumla ili kuwa na nishati ya kutosha na yenye gharama nafuu kukidhi mahitaji ya uzalishaji viwandani, utoaji wa huduma za kijamii, na matumizi ya nyumbani.
Tutayashughulikia kwa kipaumbele cha juu matatizo ya sasa yahusuyo upatikanaji wa umeme nchini.
Mheshimiwa Spika:
Ilani ya CCM ya Uchaguzi wa Oktoba 2005 inasema wazi kuwa Serikali ya Awamu ya Nne itaharakisha mradi wa kupata umeme kutoka makaa ya mawe ya Mchuchuma. Na hivyo ndivyo tutakavyofanya.
Aidha, Serikali ya Awamu ya Nne itafufua mipango ya umeme wa Mto Rusumo na Stiglers Gorge. Tutaharakisha pia upatikanaji wa umeme kutoka gesi asilia ya Mnazi Bay.
Mheshimiwa Spika:
Lengo la Serikali ya Awamu ya Nne pia ni kuendeleza kazi ya kufikisha umeme katika miji mikuu ya wilaya isiyo na umeme hivi sasa, kuongeza kasi ya kupeleka umeme vijijini kupitia Mfuko wa Nishati Vijijini, na kuiunganisha Mikoa ya Kigoma na Ruvuma katika gridi ya Taifa.
Hotuba ya Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwenye Baraza la Eid-el-Fitr, Arusha, tarehe 24 Oktoba, 2006
Bahati mbaya sana kwa upande wa tatizo la umeme hakuna majawabu ya papo kwa papo. Hata kwa umeme wa dharura imetuchukua miezi isiyopungua mitano tangu tuanze mchakato wa kukodi mitambo ya kuzalisha umeme.
Ni sasa tu ndipo baadhi ya mitambo imewasili na baadhi kuanza kazi. Ni matumaini yetu kwamba ifikapo mwishoni mwa mwezi ujao au hata katikati karibu mitambo yote ya kukodi itakuwa imewasili na kuanza kuzalisha umeme.
Mitambo hii itakapoanza kuzalisha umeme, tutakuwa tumepata nafuu. Lakini, jawabu hasa litakuwa limepatikana hapo mwakani wakati mitambo mipya ya TANESCO ya Ubungo na Tegeta itakapokuwa imeanza kutoa umeme
Salamu za Mwaka Mpya za Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Watanzania, tarehe 31 Desemba, 2006
Mwaka 2006 ulikuwa mwaka wa aina yake. Upande mmoja ulikuwa mwaka wa mafanikio mengi mazuri na kuipatia Serikali yetu pongezi na sifa nyingi. Upande mwingine ulikuwa mwaka uliokuwa na matatizo machache makubwa ambayo yalileta usumbufu mkubwa na adha kwa watu wengi nchini.
Baadhi ya matatizo hasa ya ujambazi na umeme yaliwafanya baadhi ya wananchi kupunguza imani yao kwa utendaji wa Serikali na baadhi ya vyombo vyake. Bahati nzuri, kwa majaaliwa ya Mwenyezi Mungu tunaumaliza mwaka, matatizo ya ukame, njaa na umeme yakiwa hatunayo tena na ujambazi tumeudhibiti.
Tarehe 31 Januari, 2006, nilipoongea na Watanzania kupitia Wazee wa Mkoa wa Dar es Salaam nilieleza kuwa uzalishaji wa umeme katika mabwawa yetu ulipungua kutoka megawati 561 hadi megawati 167.5 tu.
Nilitahadharisha kuwa mgao wa umeme hauepukiki. Niliwasihi Wananchi wenzangu kuzidisha kumuomba Mungu atujalie mvua za kutosha ili baa la njaa liishe na tatizo la umeme lisichukue muda mrefu kuisha.
Kutokana na kujirudia kwa tatizo la mgao wa umeme unaoleta usumbufu mkubwa kwa watu na kuathiri uchumi wa taifa letu changa, nilielezea dhamira ya Serikali ya kuanza kuchukua hatua za dhati za kupunguza kutegemea mno umeme wa maji.
Nilieleza uamuzi wa Serikali wa kuongeza matumizi ya gesi asilia na makaa ya mawe kuzalisha umeme. Nafurahi kusema kuwa tumekwishachukua hatua muafaka.
Hotuba ya Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Kwenye Ufunguzi wa Mkutano wa Nane Wa CCM, Ukumbi wa Kizota, 03 Novemba 2007
Nishati
Mwezi mmoja tangu Serikali ya Awamu ya Nne ianze kazi ya kuwatumikia Watanzania, tulikumbana na tatizo kubwa la aina yake la ukosefu wa umeme.
Tatizo hilo lilisababishwa na ukame ambao haujawahi kutokea kwa miaka mingi hapa nchini. Maji katika mabwawa ya kuzalishia umeme yalikauka, hivyo uzalishaji umeme ukapungua sana na kwa baadhi ya vituo kusimama.
Kwa rehema za Mwenyezi Mungu mvua kubwa zilizonyesha Desemba, 2006, tatizo la umeme limeisha. Ili kuhakikisha tatizo hili halijirudii tulifanya uamuzi wa makusudi wa kuongeza wigo wavyanzo vya kuzalisha umeme badala ya kutegemea mno maji.
Kuanzia mwaka 2005 mpaka sasa tumeongeza kwa asilimia 60 umeme unaozalishwa kutokana na vyanzo vingine.
Kutokana na jitihada hizi, sasa hivi tuna ziada ya umeme kwenye gridi ya Taifa. Sio rahisi sasa katika miaka michache ijayo nchi yetu kupata tatizo la upungufu wa umeme kama lile labda kutokee dharura aina nyingine.
Changamoto iliyobakia sasa ni kuyaingiza maeneo mengi zaidi kwenye Gridi ya Taifa na kuwasambazia kwa umeme watu wengi zaidi. Mpaka sasa ni asilimia 10 tu ya Watanzania wanapata umeme, hivyo kuna kazi kubwa ya kufanya katika eneo hili.
Katika kutekeleza Ilani, tumeongeza kasi ya kusambaza umeme vijijini kwa kuanzisha Mfuko wa Nishati Vijijini. Mwaka huu, tumetenga shilingi bilioni 10 kwa ajili hiyo
Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, wakati akiwahutubia Wananchi wa Dodoma na Wabunge kwenye Ukumbi wa Kilimani, Dodoma tarehe 10 Juni, 2009
Mwisho kabisa, nawasihi viongozi wenzangu na wananchi kwa ujumla, tuwe wavumilivu na tuiunge mkono Serikali katika kutekeleza mkakati huu.
Tangu mwaka 2006, mambo hayakuwa mepesi sana, tumepitia misukosuko mikubwa kwa uchumi wetu: mgao mkubwa wa umeme, njaa, bei kubwa ya mafuta na bei kubwa za vyakula na sasa msukosuko huu wa aina yake.
Kwa kila tatizo tumepambana nalo kiume na kwa umakini mkubwa na kuvuka salama. Mshikamano wetu, umoja wetu ndiyo uliotufikisha hapo.
Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete katika Sherehe ya Uzinduzi wa Mradi wa Umeme wa Gesi wa Somanga-Fungu, 16 Agosti, 2010
Nakushukuru Mheshimiwa William Ngeleja, Waziri wa Nishati na Madini kwa kunialika katika hafla hii ya uzinduzi wa Mradi wa Umeme wa Gesi wa Somanga Fungu.
Mradi huu wa umeme ambao umezinduliwa leo, ni mwendelezo wa hatua za Serikali za kutekeleza sera zake za msingi za kuhakikisha kuwa wananchi wanapata nishati ya uhakika, yenye gharama nafuu, na isiyoharibu mazingira yetu
Changamoto ya kwanza iliyo mbele yenu ni ujenzi wa nyumba bora ili muweze kuunganishiwa umeme majumbani kwenu.
Serikali itafarijika sana endapo baada ya muda mfupi tutaambiwa kuwa, umeme huu ambao leo unaonekana ni mwingi kuliko mahitaji yenu, hautoshi kwa kuwa matumizi yamekuwa makubwa kuliko umeme uliopo. Hiyo itakuwa changamoto nzuri kwani itadhihirisha kuwa malengo ya mradi huu yamefikiwa.
Kikwete aahidi umeme mikoa ya KusiniLindi,19 October 2010
Mgombea Urais kupitia CCM, Rais Jakaya Kikwete, amesena tatizo la umeme lililokuwa linaikabili mikoa ya kusini sasa litabaki historia baada ya kufanikiwa kupatikana kwa umeme wa gesi ya asilia kutoka Songosongo.
Alisema wilaya ya Kilwa ambayo ilikuwa ina tatizo la umeme kwa muda mrefu, sasa ina umeme wa uhakika baada kupatikana kwa umeme huo
Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, katika Ibada ya Kumweka Wakfu Askofu Mteule Gervas John Nyaisonga wa Jimbo Katoliki Dodoma, tarehe 19 Machi, 2011, Dodoma
Jambo lingine ninalowaomba viongozi wa dini muendelee kuiombea nchi yetu ipate mvua za kutosha, mabwawa yajae, umeme upatikane na nchi iwe na chakula cha kutosha.
Kadhalika msichoke kuiombea nchi yetu amani na upendo miongoni mwa wananchi wake. Jambo kubwa la kusisitiza hapa ni kuwataka watu wapendane, washirikiane na kamwe wasibaguane kwa rangi, kabila, dini, jinsia, maeneo wanayotoka au itikadi za kisiasa.
Haya ni miongoni mwa mambo ya tunu ambayo Baba wa Taifa Mwl. Julius Nyerere alituachia Watanzania. Ndiyo siri ya amani na utulivu wa nchi yetu. Hatuna budi kuyaenzi na kuyaendeleza."
My take: Hizi Ngonjera hizi za Rais sio nzuri kwa mstakabali wa Taifa tokea 2005 mpaka sasa ni mikakati kwenda mbele.
Mheshimiwa Spika:
Nishati ni sawa na chembe za damu mwilini. Serikali ya Awamu ya Nne itatoa kipaumbele katika kuboresha na kuendeleza upatikanaji wa nishati ya uhakika na rahisi vijijini na mijini.
Tutapanua wigo na aina ya vyanzo vya umeme na nishati kwa jumla ili kuwa na nishati ya kutosha na yenye gharama nafuu kukidhi mahitaji ya uzalishaji viwandani, utoaji wa huduma za kijamii, na matumizi ya nyumbani.
Tutayashughulikia kwa kipaumbele cha juu matatizo ya sasa yahusuyo upatikanaji wa umeme nchini.
Mheshimiwa Spika:
Ilani ya CCM ya Uchaguzi wa Oktoba 2005 inasema wazi kuwa Serikali ya Awamu ya Nne itaharakisha mradi wa kupata umeme kutoka makaa ya mawe ya Mchuchuma. Na hivyo ndivyo tutakavyofanya.
Aidha, Serikali ya Awamu ya Nne itafufua mipango ya umeme wa Mto Rusumo na Stiglers Gorge. Tutaharakisha pia upatikanaji wa umeme kutoka gesi asilia ya Mnazi Bay.
Mheshimiwa Spika:
Lengo la Serikali ya Awamu ya Nne pia ni kuendeleza kazi ya kufikisha umeme katika miji mikuu ya wilaya isiyo na umeme hivi sasa, kuongeza kasi ya kupeleka umeme vijijini kupitia Mfuko wa Nishati Vijijini, na kuiunganisha Mikoa ya Kigoma na Ruvuma katika gridi ya Taifa.
Hotuba ya Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwenye Baraza la Eid-el-Fitr, Arusha, tarehe 24 Oktoba, 2006
Bahati mbaya sana kwa upande wa tatizo la umeme hakuna majawabu ya papo kwa papo. Hata kwa umeme wa dharura imetuchukua miezi isiyopungua mitano tangu tuanze mchakato wa kukodi mitambo ya kuzalisha umeme.
Ni sasa tu ndipo baadhi ya mitambo imewasili na baadhi kuanza kazi. Ni matumaini yetu kwamba ifikapo mwishoni mwa mwezi ujao au hata katikati karibu mitambo yote ya kukodi itakuwa imewasili na kuanza kuzalisha umeme.
Mitambo hii itakapoanza kuzalisha umeme, tutakuwa tumepata nafuu. Lakini, jawabu hasa litakuwa limepatikana hapo mwakani wakati mitambo mipya ya TANESCO ya Ubungo na Tegeta itakapokuwa imeanza kutoa umeme
Salamu za Mwaka Mpya za Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Watanzania, tarehe 31 Desemba, 2006
Mwaka 2006 ulikuwa mwaka wa aina yake. Upande mmoja ulikuwa mwaka wa mafanikio mengi mazuri na kuipatia Serikali yetu pongezi na sifa nyingi. Upande mwingine ulikuwa mwaka uliokuwa na matatizo machache makubwa ambayo yalileta usumbufu mkubwa na adha kwa watu wengi nchini.
Baadhi ya matatizo hasa ya ujambazi na umeme yaliwafanya baadhi ya wananchi kupunguza imani yao kwa utendaji wa Serikali na baadhi ya vyombo vyake. Bahati nzuri, kwa majaaliwa ya Mwenyezi Mungu tunaumaliza mwaka, matatizo ya ukame, njaa na umeme yakiwa hatunayo tena na ujambazi tumeudhibiti.
Tarehe 31 Januari, 2006, nilipoongea na Watanzania kupitia Wazee wa Mkoa wa Dar es Salaam nilieleza kuwa uzalishaji wa umeme katika mabwawa yetu ulipungua kutoka megawati 561 hadi megawati 167.5 tu.
Nilitahadharisha kuwa mgao wa umeme hauepukiki. Niliwasihi Wananchi wenzangu kuzidisha kumuomba Mungu atujalie mvua za kutosha ili baa la njaa liishe na tatizo la umeme lisichukue muda mrefu kuisha.
Kutokana na kujirudia kwa tatizo la mgao wa umeme unaoleta usumbufu mkubwa kwa watu na kuathiri uchumi wa taifa letu changa, nilielezea dhamira ya Serikali ya kuanza kuchukua hatua za dhati za kupunguza kutegemea mno umeme wa maji.
Nilieleza uamuzi wa Serikali wa kuongeza matumizi ya gesi asilia na makaa ya mawe kuzalisha umeme. Nafurahi kusema kuwa tumekwishachukua hatua muafaka.
Hotuba ya Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Kwenye Ufunguzi wa Mkutano wa Nane Wa CCM, Ukumbi wa Kizota, 03 Novemba 2007
Nishati
Mwezi mmoja tangu Serikali ya Awamu ya Nne ianze kazi ya kuwatumikia Watanzania, tulikumbana na tatizo kubwa la aina yake la ukosefu wa umeme.
Tatizo hilo lilisababishwa na ukame ambao haujawahi kutokea kwa miaka mingi hapa nchini. Maji katika mabwawa ya kuzalishia umeme yalikauka, hivyo uzalishaji umeme ukapungua sana na kwa baadhi ya vituo kusimama.
Kwa rehema za Mwenyezi Mungu mvua kubwa zilizonyesha Desemba, 2006, tatizo la umeme limeisha. Ili kuhakikisha tatizo hili halijirudii tulifanya uamuzi wa makusudi wa kuongeza wigo wavyanzo vya kuzalisha umeme badala ya kutegemea mno maji.
Kuanzia mwaka 2005 mpaka sasa tumeongeza kwa asilimia 60 umeme unaozalishwa kutokana na vyanzo vingine.
Kutokana na jitihada hizi, sasa hivi tuna ziada ya umeme kwenye gridi ya Taifa. Sio rahisi sasa katika miaka michache ijayo nchi yetu kupata tatizo la upungufu wa umeme kama lile labda kutokee dharura aina nyingine.
Changamoto iliyobakia sasa ni kuyaingiza maeneo mengi zaidi kwenye Gridi ya Taifa na kuwasambazia kwa umeme watu wengi zaidi. Mpaka sasa ni asilimia 10 tu ya Watanzania wanapata umeme, hivyo kuna kazi kubwa ya kufanya katika eneo hili.
Katika kutekeleza Ilani, tumeongeza kasi ya kusambaza umeme vijijini kwa kuanzisha Mfuko wa Nishati Vijijini. Mwaka huu, tumetenga shilingi bilioni 10 kwa ajili hiyo
Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, wakati akiwahutubia Wananchi wa Dodoma na Wabunge kwenye Ukumbi wa Kilimani, Dodoma tarehe 10 Juni, 2009
Mwisho kabisa, nawasihi viongozi wenzangu na wananchi kwa ujumla, tuwe wavumilivu na tuiunge mkono Serikali katika kutekeleza mkakati huu.
Tangu mwaka 2006, mambo hayakuwa mepesi sana, tumepitia misukosuko mikubwa kwa uchumi wetu: mgao mkubwa wa umeme, njaa, bei kubwa ya mafuta na bei kubwa za vyakula na sasa msukosuko huu wa aina yake.
Kwa kila tatizo tumepambana nalo kiume na kwa umakini mkubwa na kuvuka salama. Mshikamano wetu, umoja wetu ndiyo uliotufikisha hapo.
Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete katika Sherehe ya Uzinduzi wa Mradi wa Umeme wa Gesi wa Somanga-Fungu, 16 Agosti, 2010
Nakushukuru Mheshimiwa William Ngeleja, Waziri wa Nishati na Madini kwa kunialika katika hafla hii ya uzinduzi wa Mradi wa Umeme wa Gesi wa Somanga Fungu.
Mradi huu wa umeme ambao umezinduliwa leo, ni mwendelezo wa hatua za Serikali za kutekeleza sera zake za msingi za kuhakikisha kuwa wananchi wanapata nishati ya uhakika, yenye gharama nafuu, na isiyoharibu mazingira yetu
Changamoto ya kwanza iliyo mbele yenu ni ujenzi wa nyumba bora ili muweze kuunganishiwa umeme majumbani kwenu.
Serikali itafarijika sana endapo baada ya muda mfupi tutaambiwa kuwa, umeme huu ambao leo unaonekana ni mwingi kuliko mahitaji yenu, hautoshi kwa kuwa matumizi yamekuwa makubwa kuliko umeme uliopo. Hiyo itakuwa changamoto nzuri kwani itadhihirisha kuwa malengo ya mradi huu yamefikiwa.
Kikwete aahidi umeme mikoa ya KusiniLindi,19 October 2010
Mgombea Urais kupitia CCM, Rais Jakaya Kikwete, amesena tatizo la umeme lililokuwa linaikabili mikoa ya kusini sasa litabaki historia baada ya kufanikiwa kupatikana kwa umeme wa gesi ya asilia kutoka Songosongo.
Alisema wilaya ya Kilwa ambayo ilikuwa ina tatizo la umeme kwa muda mrefu, sasa ina umeme wa uhakika baada kupatikana kwa umeme huo
Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, katika Ibada ya Kumweka Wakfu Askofu Mteule Gervas John Nyaisonga wa Jimbo Katoliki Dodoma, tarehe 19 Machi, 2011, Dodoma
Jambo lingine ninalowaomba viongozi wa dini muendelee kuiombea nchi yetu ipate mvua za kutosha, mabwawa yajae, umeme upatikane na nchi iwe na chakula cha kutosha.
Kadhalika msichoke kuiombea nchi yetu amani na upendo miongoni mwa wananchi wake. Jambo kubwa la kusisitiza hapa ni kuwataka watu wapendane, washirikiane na kamwe wasibaguane kwa rangi, kabila, dini, jinsia, maeneo wanayotoka au itikadi za kisiasa.
Haya ni miongoni mwa mambo ya tunu ambayo Baba wa Taifa Mwl. Julius Nyerere alituachia Watanzania. Ndiyo siri ya amani na utulivu wa nchi yetu. Hatuna budi kuyaenzi na kuyaendeleza."
My take: Hizi Ngonjera hizi za Rais sio nzuri kwa mstakabali wa Taifa tokea 2005 mpaka sasa ni mikakati kwenda mbele.