Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,529
Jana nimejiuliza sana kwa nini Tanzania tunahangaika na ukosefu wa umeme kila mwaka na hata kuzorotesha uchumi n kukua kwa maendeleo? nikajiuliza ni mvua, mabwawa au mitambo? Nikapata tamati kuwa ni watu au kwa maneno sahihi ni Uongozi pofu na mbovu.
Leo hii nadamka asubuhi nasoma gazeti, nakutana na hii kauli ya Waziri Mkuu Pinda anayesema tukaribishe wawekezaji!
Je Tanzania si kuna IPTL, Songas, Agreko, Kiwira,Richmond, Dowans, Tanesco na Ewura na wengine wengi ukiongezea majenereta? Sasa kama tuna makampuni na taasisi zote hizi, kwa nini tuendelee kusema tunahitaji wazalishaji wapya wa umeme?
Kwani mahitaji yetu ni kiasi gani kwa mwaka? je mabwawa ya maji ya Kidatu, Handeni, Wami, Nyumba ya Mungu, Mtera, Kihansi na hata hili jipya la Ruhiji yana uwezo wa kuzalisha umeme wa kiasi gani?
Je gesi, mafuta, makaa ya mawe, jua na upepo zinatuzalishia megawati ngapi kila siku au kila mwaka kukidhi mahitaji ya Taifa?
Hivi kweli Tanzania tuna sera kamambe ya kujijenga katika miundombinu kama Umeme, Barabara, Maji, Simu, Bandari, Reli na mengineyo ambayo ni muhimu kwa kujenga Taifa lenye uchumi imara au kama suala la Umeme na Nishati tunakimbilia kusema "njooni wawekezaji"?
Leo hii nadamka asubuhi nasoma gazeti, nakutana na hii kauli ya Waziri Mkuu Pinda anayesema tukaribishe wawekezaji!
Je Tanzania si kuna IPTL, Songas, Agreko, Kiwira,Richmond, Dowans, Tanesco na Ewura na wengine wengi ukiongezea majenereta? Sasa kama tuna makampuni na taasisi zote hizi, kwa nini tuendelee kusema tunahitaji wazalishaji wapya wa umeme?
Kwani mahitaji yetu ni kiasi gani kwa mwaka? je mabwawa ya maji ya Kidatu, Handeni, Wami, Nyumba ya Mungu, Mtera, Kihansi na hata hili jipya la Ruhiji yana uwezo wa kuzalisha umeme wa kiasi gani?
Je gesi, mafuta, makaa ya mawe, jua na upepo zinatuzalishia megawati ngapi kila siku au kila mwaka kukidhi mahitaji ya Taifa?
Hivi kweli Tanzania tuna sera kamambe ya kujijenga katika miundombinu kama Umeme, Barabara, Maji, Simu, Bandari, Reli na mengineyo ambayo ni muhimu kwa kujenga Taifa lenye uchumi imara au kama suala la Umeme na Nishati tunakimbilia kusema "njooni wawekezaji"?
Pinda ataka wawekazajii wa umeme
Na Mwandishi Wetu
WAZIRI Mkuu wa Tanzania, Mizengo Pinda amezita nchi wananchama wa Mamlaka za Udhibiti wa Huduma za Umeme Kusini mwa Afrika (Rera) kuvuta wawekezaji katika sekta ya umeme ili kuondoa tatizo kubwa la umeme linalozikumba nchi wanachama wa Jumuiya ya Biashara Kusini mwa Afrika (SADC).
Pinda aliishauri Rara kuweka mikakati imara
itakayozewezesha nchi wanachama kupunguza tatizo la upatikanaji wa nishati hiyo kwa sababu inawezekama juhudi na maarifa vikifanyika.
Waziri Pindi alitoa changamoto hiyo jana wakati akifungua Mkutano wa Tano wa Mwaka wa Rare unaofanyika katika
Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC).
Afrika ndiyo yenye kiwango kidogo cha upatikanaji wa umeme ambacho ni sawa na asilimia 25 tu, hali mbaya zaidi ni vijijini ambapo wakazi zaidi ya asilimia 75
huishi ambao hupata umeme wa asilimia mbili tu, alisema Waziri.
Alitoa mfano wa Nchi za SADC ambazo zilipigania Uhuru wa Nchi hizo na kufanikiwa na kwamba iwapo Nchi hizo
zitaunganisha nguvu zao kwa kugawana vyanzo hivyo ni wazi watashinda.
Baadhi ya changamoto alizozitoa Waziri Mkuu katika kukabiliana na tatizo hilo ni kupanua huduma hizo kwa
kutumia nguvu za maji, makaa ya mawe, gesi asilia na mafuta.
Pia alizitaka nchi wananchama wa jumuiy hiyo kukabiliana na changamoto kadhaa kama uhaba fedha kwa ajili ya kugharamia miradi hiyo, ufundi, miundombinu na kuepukana na utegemezi zaidi katika umeme unaotokana na maji ambao sasa si wa uhakika.
Naye Waziri wa Nishati na Madini,
William Ngeleja alisema lengo kuu ni kuangalia ni jinsi ya kuunganisha nguvu katika kukabiliana na tatizo hilo.
Ni wakati muafaka kwa nchi zetu kuhakikisha kwamba huduma
hiyo inaboreshwa na inakuwa endelevu, alisema Ngeleja.
Awali, Mwenyekiti wa Bodi ya Mamla ya Udhibiti wa Maji na Nishati (Ewura), Simon Sayore alisema lengo ni kuhakikisha kuwa tatizo la uhaba wa umeme
katika nchi hizo.
Mkutano huo unawakutanisha wadau 150 wa kutoka nchi wanachana wa Rera na wasiowanachama kutoka nchi za Mozambique, Zambia, Malawi, Nigeria, Lesotho, Afrika Kusini, Namibia, USA, Norway, Madagascar, Angola, Botwsana, Uganda, Kenya and Tanzania.