jogi
JF-Expert Member
- Sep 25, 2010
- 25,558
- 25,322
wakuu, kuna taarifa kuwa mnamo tarehe 8 august 2011 majira ya saa mbili mbili usiku katika kituo cha polisi magomeni umeme ulikatika, kuna mahabusu aliletewa chakula, kituoni palikuwa na polisi wa kike tu, wawili, akisha pokea chakula alienda kufungua lango la mahabusu ili amtoe muhusika apate kula, alipomalizia kufungua komeo, mahabusu walivamia lango na kumkumba nalo wp, alianguka chini, chakula kikatawanyika, mahabusu 16 kwa escaping velocity wakatokomea gizani wakimpita wp counter asijue la kufanya, haijaweza kufahamika mara moja askari polisi wanaume walikuwa wapi hadi kituo kikubwa kama magomeni kubaki na askari polisi wa kike tena bila silaha. yeyote ajuaye zaidi ya haya kuhusu habari hii ana nafasi ya kumwaga nyuzz hapa, sikuisikia popote gazetini wala redioni. Nawasilisha