Mama Mdogo
JF-Expert Member
- Nov 21, 2007
- 2,961
- 2,138
Katika hali ya kushangaza, umeme haujakatika maeneo ya kwetu kuanzia jumatatu hadi leo. Siyo kawaida kwani tumekuwa na kawaida ya mgawo kila baada ya siku mbili. Wakati tunalijadili mitaani kwetu, wakasema, inabidi tuchunguze labda kuna Kigogo au Fisadi limehamia mitaa ya kwetu hivyo ujio wake umendoa mgawo.
Nimewapigia simu Tanesco kuwauliza kulikoni umeme haukatiki mitaa ya kwetu. Wakaniuliza kwa nini wewe unaulizia umeme kutokukatika, nikasema kuwa ninahofu kuwa kwa kunipa mfululizo mnaweza kunikatia tena mfululizo.
Wenzangu hebu nipeni uzoefu wenu wa huu mgao kwa wiki hii.Huu ni muujiza kupata umeme kwa wiki nzima bila kukatika wakati huu wa sakata la Ngeleja, kweli Tanzania ni zaidi ya uijuavyo!!!!
Nimewapigia simu Tanesco kuwauliza kulikoni umeme haukatiki mitaa ya kwetu. Wakaniuliza kwa nini wewe unaulizia umeme kutokukatika, nikasema kuwa ninahofu kuwa kwa kunipa mfululizo mnaweza kunikatia tena mfululizo.
Wenzangu hebu nipeni uzoefu wenu wa huu mgao kwa wiki hii.Huu ni muujiza kupata umeme kwa wiki nzima bila kukatika wakati huu wa sakata la Ngeleja, kweli Tanzania ni zaidi ya uijuavyo!!!!