Umeme Juuu next week!

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,319
33,125
Inaelezwa kuwa gharama za kulipia umeme zitakwea hewani kwa asilimia tatu zaidi kuanzia Septemba mosi, mwaka huu, ili kulipia Mfuko wa Umeme Vijijini (REA), imefahamika.

Kwa mujibu wa tangazo lililotolewa jana na Ofisi ya Mawasiliano ya Shirika la Ugavi wa Umeme nchini (TANESCO), wateja wote wanaotumia umeme na wananchi wote kwa ujumla, watatakiwa kulipa ushuru wa asilimia tatu kwa ajili ya mfuko huo.

Tangazo hilo lililosambazwa kwenye vyombo mbalimbali vya habari jana, lilisema kuwa ushuru huo unatozwa kwa kuzingatia Tangazo la Serikali (GN) la Agosti Mosi, 2009 na ainisho la sheria ya Bunge kuhusu Wakala wa Umeme Vijijini (Rural Energy Act of 2005), kifungu namba 19 (3) ( c ) na (d).

“Ushuru huu ni kwa ajili ya Mfuko wa Umeme Vijijini ambao matumizi yake ni pamoja na kuongeza kasi ya usambazaji umeme vijijini na mafunzo kwa wajasiriamali ili kuboresha maendeleo ya jamii kwa kutumia nishati bora vijijini.

“Ushuru huu utakuwa ni asilimia tatu (3%) ya thamani ya umeme uliotumiwa katika mwezi husika, yaani juu ya gharama ya matumizi ya umeme,” ilisema sehemu ya tangazo hilo.

TANESCO kupitia tangazo lake hilo, imeeleza kuwa yenyewe itakuwa ni mkusanyaji tu wa ushuru huo, ambapo makusanyo yote yatakabidhiwa REA.

Kutokana na tangazo hilo, sasa katika ankara ya umeme mteja atapaswa kulipia asilimia 18 kama Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT), malipo kwa EWURA asilimia 1 na Mfuko wa Umeme Vijijini (REA), asilimia 3.

“Hii inatokana na upungufu wa nafasi katika fomu ya Ankara. Hata hivyo, kwa sasa tunatengeneza fomu mpya ambayo itaonyesha kila gharama peke yake. Tunategemea fomu hii itakuwa tayari kabla ya mwisho wa mwaka 2009,” ilisema sehemu ya tangazo hilo.


Source: DarHotWire.com
 
sasa mnatakaje?umeme wa bure?

Imawezekana kabisa kama kusingekuwa na richmond, merememta, radar, ndege ya raisi na chai ya billioni tisa, umeme ungekuwa wa bure. Kutokuwa na priorities ndiko kunakopandisha umeme.
 
suala hapa sio umeme wa bure... kila mwananchi anatakiwa kuachangia maendeleo ya umeme vijijini sio watumia waliopo sasa ambao ni wastani wa wateja 600,000. Tatizo la Tanzania wale wanaolipa kodi ndo huwa wanaendelea kukamliwa zaidi.... nadhani wangetafuta njia nyingine ya kupata hizo fedha za miradi yao...

kwa maana hiyo katika kila shilingi mia utakao tumia kununulia umeme, shilingi 21 zitakuwa ni kodi mbalimbali weka na service charge kwa mwezi ambayo ni sh 3000, kwa mlalahoi kama mimi ili niwashe bulb yangu ya sebuleni na chumbani ni lazima niwe na buku 10 !!!!!

mandeleo yaletwe na wote sio 600,000 tu!!!!!
 
Kupanda kwa bei kulitakiwa kuendane na huduma siyo bei inakuwa juu na umeme wenyewe ndo ule wa kukatika kila dakika.

Ni vizuri serikali na TANESCO watafute vyanzo ambavyo wanawe zalisha umeme kwa bei nafuu zaidi kuliko kulalia zaidi kwenye kuwakamua wananchi ambao ukiangalia kwa undani unakuta vipato ni vidogo sana.

Pia CCM wasiwakumbatie mafisadi maana ndo waliochangia hadi tumefika hapa.
 
Tulishazoea wapandishe watakavyo hata wakitaka asilimia mia sisi tutalipa tu kwani kuna la kujitetea? hata kama sitaki nitapata huduma hiyo muhimu kwa nani?
Wapandishe tu hamna noma tutalipa tu!
 
tulishazoea wapandishe watakavyo hata wakitaka asilimia mia sisi tutalipa tu kwani kuna la kujitetea? Hata kama sitaki nitapata huduma hiyo muhimu kwa nani?
wapandishe tu hamna noma tutalipa tu!

watanzania wote wangekuwa kama wewe nchi ingeendelea kwa haraka,matatizo yetu ni kuwa kila mtu ni mjuaji na mbishi hata kwa mambo ya faida,kila mtu ni "much know"
 
Tulishazoea wapandishe watakavyo hata wakitaka asilimia mia sisi tutalipa tu kwani kuna la kujitetea? hata kama sitaki nitapata huduma hiyo muhimu kwa nani?
Wapandishe tu hamna noma tutalipa tu!

Mchukia Fisadi!

Kwenye kupandisha bei ya umeme kwa asilimia 3% sio ufisadi au kwa manufaa ya tanesco bali ni katika kutekeleza sera ya CCM ya MAISHA BORA kwa kila Mtanzania!! Huna wa kumlaumu haya ni matunda ya kura zenu za kishindo zilizomweka JMK mtoto wa CCM madrakani!

Serikali ya CCM badala ya kubadili sheria ya kodi ili madini yachangie kwa kiwango cha maana katika kupeleka umeme vijijini wameona wawabebeshe ailimia 10% ya watanzania wanaopata huduma ya umeme kuwapelekea umeme Watanzania asilimia 90% wasiokuwa na umeme. Hii sio njia muafaka kwani watu wote waliohai wangepaswa kuchangia kama CCM imekosa mbinu!
Kazi ya kufanya electrification ni kubwa hizi mbinu za kichovu za hawa wahuni wa CCM plus a few members of parliament calling themselves opposition.
Kuna haja ya kutafakari na kuweka mpango mkubwa wa kufanya kazi hiyo.

What comes from the 3% is a pea nut assume ni Tshs 740m/= per month itachukua karne ngapi kupeleka umeme vijijini!!

Msichekelee this is national tragedy!!! Janga la kitaifa nyie CCM cant you use your grey matter!!!

Toeni mawazo msilalamike tujenge hoja na msiseme ufisadi ina maana serikali is a big fisadi or what?
 
Back
Top Bottom