Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,316
- 33,112
HUDUMA muhimu katika maisha ya kila siku ya binadamu zimeonekana kupanda ghafla baada ya kukosekana kwa umeme visiwani Zanzibar . Moja ya huduma muhimu ni kule kupanda kwa mafuta Kutokana na tatizo hilo linalowafanya wakazi wa visiwani humo kushindwa kumudu gharama za matumizi hayo ambayo ni muhimu kwa maisha ya kila siku..
Tangu kukatika kwa umeme, kumebainiwa kuwa hali ya maisha imekuwa ngumu kwa wakazi na kwa wafanyabiashara ndogo ndogo wanaotumia umeme kwani wengi wao wamefunga biashara zao kutokana na tatizo hilo.
Biashara zilizoathirika na tatizo hilo la umeme ni pamoja na saluni za kiume na kike, vibanda vinavyotoa huduma mbalimbali vikiwamo vya vinywaji baridi, wauzaji wa samaki, baa, kumbi za starehe, nyumba za kulala wageni huku biashara ya teksi na daladala, zikionekana kusuasua na kuwa ngumu kutokana na ukosefu wa mafuta .
Hivyo mji huo umekumbwa na tatizo la miungurumo ya jenereta kila kona ambapo inakuwa kero kwa wagendi waiingiao visiwani humo.
Pia tatizo hilo limeonekana kusimamisha baadhi ya ajira kwa vijana visiwani humo.
Katika taarifa zilizozifikia nifahamishe ilidaiwa kuwa baadhi ya wakazi na maharusi hujenda Dar es Salaam kwa ajili ya matengenezo ya nywele kwa kuwa saloni nyingi visiwani kufungwa kutokana na aujosefu wa umeme.
http://www.nifahamishe.com/NewsDetails.aspx?NewsId=3777918&&Cat=1
Tangu kukatika kwa umeme, kumebainiwa kuwa hali ya maisha imekuwa ngumu kwa wakazi na kwa wafanyabiashara ndogo ndogo wanaotumia umeme kwani wengi wao wamefunga biashara zao kutokana na tatizo hilo.
Biashara zilizoathirika na tatizo hilo la umeme ni pamoja na saluni za kiume na kike, vibanda vinavyotoa huduma mbalimbali vikiwamo vya vinywaji baridi, wauzaji wa samaki, baa, kumbi za starehe, nyumba za kulala wageni huku biashara ya teksi na daladala, zikionekana kusuasua na kuwa ngumu kutokana na ukosefu wa mafuta .
Hivyo mji huo umekumbwa na tatizo la miungurumo ya jenereta kila kona ambapo inakuwa kero kwa wagendi waiingiao visiwani humo.
Pia tatizo hilo limeonekana kusimamisha baadhi ya ajira kwa vijana visiwani humo.
Katika taarifa zilizozifikia nifahamishe ilidaiwa kuwa baadhi ya wakazi na maharusi hujenda Dar es Salaam kwa ajili ya matengenezo ya nywele kwa kuwa saloni nyingi visiwani kufungwa kutokana na aujosefu wa umeme.
http://www.nifahamishe.com/NewsDetails.aspx?NewsId=3777918&&Cat=1