PakaJimmy
JF-Expert Member
- Apr 29, 2009
- 16,203
- 8,724
Mwana jamvi,
Wewe binafsi umeshawahi kuishi kijijini?
Ninaposema kuishi kijijini ninamaanisha kuwepo huko, kushiriki majumuiko mbalimbali, sherehe na kazi zote za uzalishaji za huko.
Nia ya swali langu ni kujaribu kujua hasa wakati tunapojadili masuala kama ya kumkomboa mkulima(peasant), au asilimia 80 ya watanzania kuishi vijijini, tunaongea kwa uchungu na kujua kiukweli maisha ya vijijini yalivyo?
Pia tunaongelea KILIMO KWANZA,ambapo kwa kiasi kikubwa kinatekelezwa vijijini.
Usikute watu wanajiita Mzee Mwanakijiji, Ng`wana Madaso, au Balantanda, kumbe wamezaliwa, kukulia, na kusomea mijini, na hawajaonja pepo ya kijiji!. Nina shaka na watu kama Bluray, Firstlady, Kigogo,bht na wengine, kama wanajua jembe, kama si kuliona kwenye nembo ya sisiemu!
Mimi binafsi nimezaliwa, kukulia, na kusomea kijijini.
Nimechunga mbuzi na kondoo, nikaokota kuni msituni ,na kucheza dimbadimba! Nimetembea pekupeku kwa kadiri ya muongo mmoja, thats me!
Umeishi kijijini, na una kisa chochote? tupe basi!
Wewe binafsi umeshawahi kuishi kijijini?
Ninaposema kuishi kijijini ninamaanisha kuwepo huko, kushiriki majumuiko mbalimbali, sherehe na kazi zote za uzalishaji za huko.
Nia ya swali langu ni kujaribu kujua hasa wakati tunapojadili masuala kama ya kumkomboa mkulima(peasant), au asilimia 80 ya watanzania kuishi vijijini, tunaongea kwa uchungu na kujua kiukweli maisha ya vijijini yalivyo?
Pia tunaongelea KILIMO KWANZA,ambapo kwa kiasi kikubwa kinatekelezwa vijijini.
Usikute watu wanajiita Mzee Mwanakijiji, Ng`wana Madaso, au Balantanda, kumbe wamezaliwa, kukulia, na kusomea mijini, na hawajaonja pepo ya kijiji!. Nina shaka na watu kama Bluray, Firstlady, Kigogo,bht na wengine, kama wanajua jembe, kama si kuliona kwenye nembo ya sisiemu!
Mimi binafsi nimezaliwa, kukulia, na kusomea kijijini.
Nimechunga mbuzi na kondoo, nikaokota kuni msituni ,na kucheza dimbadimba! Nimetembea pekupeku kwa kadiri ya muongo mmoja, thats me!
Umeishi kijijini, na una kisa chochote? tupe basi!