Mtu wa Pwani
JF-Expert Member
- Dec 26, 2006
- 4,184
- 671
katika kipindi hiki cha karibuni, tumeshuhudia mambo mengi, likiwamo la kuzungumzia na kuchangia muswada unaotarajiwa kupelekwa bungeni hivi karibuni kwa ajili ya kuweka ramani ya kutupeleka kwenye katiba mpya.
pia tumeshuhudia chama tawala ambacho ndicho kilichohusika kwa kiasi kikubwa na muungano wetu, kikiwa katika harakati za kujivua gamba.
sasa kwenye muswaada ambao unajadiliwa kuna mengi yamesemwa, na hasa kuhusu muungano wetu. wako wanaoona kuwa na uwakilishi sawa katika uundwaji wa katiba hii mpya sio sahihi kwa kuwa nchi moja ina watu wengi na eneo kubwa kuliko nyengine. kutokana na hoja hio wao wanaona ni kuwadhulumu wengi kwa kuamuliwa mambo yao na wachache.
baada ya kutafakari nimegundua hoja ingekuwa hivi, kwa vile serikali ya jamhuri wa muungano ndani yake mna serikali ya tanganyika, sio sawa kwa wazanzibari kuwaamulia watanganyika mambo yao. maana wao hayawahusu, wao wana katiba yao na huko wanapanga mambo yao.
sasa ili hili lisiwe kikwazo imefika wakati sasa tanganyika kujivua gamba na kubaki Tanganyika mbali na tanzania mbali, ili watanganyika waunde katiba yao kwa mujibu watakavyo, na baada ya hapo ndio tukae wazanzibari na watanganyika kuunda katiba ya jamhuri ya tanzania
na nnaamini kama tanganyika ikijivua gamba matatizo mengi ya muungano yatapatiwa ufumbuzi.
pia tumeshuhudia chama tawala ambacho ndicho kilichohusika kwa kiasi kikubwa na muungano wetu, kikiwa katika harakati za kujivua gamba.
sasa kwenye muswaada ambao unajadiliwa kuna mengi yamesemwa, na hasa kuhusu muungano wetu. wako wanaoona kuwa na uwakilishi sawa katika uundwaji wa katiba hii mpya sio sahihi kwa kuwa nchi moja ina watu wengi na eneo kubwa kuliko nyengine. kutokana na hoja hio wao wanaona ni kuwadhulumu wengi kwa kuamuliwa mambo yao na wachache.
baada ya kutafakari nimegundua hoja ingekuwa hivi, kwa vile serikali ya jamhuri wa muungano ndani yake mna serikali ya tanganyika, sio sawa kwa wazanzibari kuwaamulia watanganyika mambo yao. maana wao hayawahusu, wao wana katiba yao na huko wanapanga mambo yao.
sasa ili hili lisiwe kikwazo imefika wakati sasa tanganyika kujivua gamba na kubaki Tanganyika mbali na tanzania mbali, ili watanganyika waunde katiba yao kwa mujibu watakavyo, na baada ya hapo ndio tukae wazanzibari na watanganyika kuunda katiba ya jamhuri ya tanzania
na nnaamini kama tanganyika ikijivua gamba matatizo mengi ya muungano yatapatiwa ufumbuzi.