John Mnyika
JF-Expert Member
- Jun 16, 2006
- 712
- 1,240
NB: WAKATI NAANDIKA TAARIFA HII KWA UMMA TAREHE 28 OKTOBA 2011 DOLA MOJA ILIKUWA 1800, PAMOJA NA HATUA ZA KIFEDHA ZA BENKI KUFANIKIWA KIDOGO KUSHUSA MPAKA 1700 KWA KIWANGO CHA LEO BADO HATUJAWEZA KUREJEA KWENYE KIWANGO CHA KARIBUNI CHA CHINI YA 1600.
PIA, HATUA TATU ZILIZOCHUKULIWA NA BENKI KUU ZINA MADHARA MAKUBWA KATIKA MZUNGUKO WA FEDHA NCHINI IKIWEMO KUPUNGUA KWA UPATIKANAJI WA MIKOPO KATIKA BENKI ZA KIBIASHARA HALI AMBAYO ITAKUWA NA MADHARA KWENYE UZALISHAJI SIKU ZA USONI. HIVYO, NI MAONI YANGU KWAMBA SUALA LA KUHUSISHA KWA KARIBU SEKTA YA MADINI KWENYE JUHUDI ZA KUKABILIANA NA MFUMUKO WA BEI NA KUIMARISHA SARAFU YETU BADO LINAHITAJI MJADALA ENDELEVU WENYE KUWEZESHA HATUA ZA HARAKA KUCHUKULIWA.
TAARIFA KWA UMMMA-28/10/2011: Pamoja na kuchukua hatua za dharura za kuchochea ongezeko la uzalishaji katika kilimo na viwanda na kuwezesha udhibiti wa bei ya bidhaa muhimu kukabiliana na kupanda kwa gharama za maisha kunakosababishwa na mfumuko wa bei na kuporomoka kwa sarafu ya Tanzania pamoja na; serikali inapaswa kuitumia sekta ya madini katika kunusuru uchumi wa taifa na maisha ya wananchi.
Izingatiwe kwamba mfumuko wa bei nchini pamoja na kusababishwa na kupungua kwa uzalishaji unachangiwa pia na nakisi ya bajeti pamoja na udhaifu katika matumizi ya serikali wakati kuporomoka kwa sarafu kunatokana pia na ongezeko la mahitaji ya fedha za kigeni kwa ajili ya ongezeko la uagizaji wa mafuta na malighafi nyingine toka nje.
Hatua tatu za kifedha ambazo zimechukuliwa na benki kuu katika kipindi cha takribani wiki moja hazijaweza kuimarisha sarafu yetu badala yake imeendelea kuporomoka kutoka dola moja kubadilishwa kwa 1600 mpaka 1800; hali ambayo inahitaji hatua za ziada na za haraka kuchukuliwa na mamlaka zingine za kiserikali kwa kushirikiana na sekta binafsi.
Kati ya hatua hizo ni Wizara ya Nishati na Madini kushirikiana na Wizara ya Fedha pamoja na benki kuu kuitumia sekta ya madini katika kunusuru uchumi wa nchi kwa kurejea mapendekezo ya bajeti mbadala za kambi ya upinzani kwa mwaka wa fedha 2011/2012.
Kati ya hatua hizo ni pamoja na Wizara ya Fedha na Benki Kuu kutumia sera, sheria na kanuni husika kufanya majadiliano ya haraka na makampuni ya madini yaweze kuzingatia taratibu za kutunza sehemu kubwa ya fedha za nje (walau 60%) kwenye benki za ndani ili kusaidia kwa dharura kudhibiti kuporomoka kwa shilingi ya Tanzania.
Hatua nyingine ni Wizara ya Nishati na Madini kushirikiana kwa haraka na Wizara ya Fedha na Benki Kuu kutunza sehemu hifadhi yetu ya fedha za kigeni katika mfumo wa madini hususani dhahabu kutokana na thamani ya mauzo ya madini kuongezeka wakati sarafu ya Tanzania ikizidi kuporomoka.
Hatua ya ziada ni kutoza sehemu kubwa ya mrabaha kwa dhahabu badala ya kutoza kwa fedha pekee; na kutoza mapema mrabaha huo kwa asilimia nne kabla ya kukokotoa baadhi ya gharama kama Sheria ya Madini inavyohitaji badala ya asilimia tatu baada ya kuondoa baadhi ya gharama kama ilivyo sasa hatua ambayo itachangia katika kuongeza pato la taifa na kuimarisha sarafu yetu.
Hatua ya nyongeza ni kwa serikali kuelekeza mapato mengine yaliyopatikana katika sekta ya madini katika kutekeleza mpango maalumu wa dharura wa kuongeza uzalishaji na kupunguza madeni yenye kuongeza mfumuko wa bei na kuporomosha shilingi ya Tanzania. Mathalani vyombo vya habari vya kitaifa na kimataifa tarehe 27 Oktoba 2011 vimeeleza kwamba kampuni ya Anglo-Gold Ashanti italipa kodi ya mapato ya kampuni kiasi cha dola milioni 50 (ambayo ni takribani bilioni 90) kwa kiwango cha sasa cha kubadilisha fedha na kwamba tayari imeshalipa bilioni 8.6 katika katika kiasi hicho ikiwa ni mara ya kwanza toka kampuni hiyo ianze uchimbaji wenye tija zaidi ya miaka kumi iliyopita.
Haya ni mapato hayako kwenye bajeti ya serikali 2011/2012 hivyo serikali inapaswa kutumia mapato hayo kama bajeti ya nyongeza ya kutekeleza mpango wa dharura na kupanua wigo wa kuyataka makampuni mengine ikiwemo African Barrick Gold (ABG) yenye migodi mikubwa minne ambayo yote hailipi kodi ya mapato ya kampuni. Hatua hii iende sambamba na kupunguza matumizi ya anasa pamoja na kuvitumia vyanzo mbadala vya mapato vilivyoelezwa na kambi ya upinzani ili kupata fedha za nyongeza za kuingiza katika mpango wa dharura wa kudhibiti mfumuko wa bei na kuporomoka kwa shilingi. Hata hivyo, udhibiti wa ziada unahitajika katika kutekeleza mipango yote ya dharura ili kuepusha mianya ya ufisadi kama ilivyokuwa katika miradi ya kufua umeme IPTL, Alstorm Power Rentals, Richmond na fedha za kuchochea uchumi (Stimulus Package).
Itakumbukwa kwamba tarehe 23 Oktoba 2011 nilifanya mkutano na waandishi wa habari kutaka hatua za dharura kuchukuliwa na Rais Kikwete na bunge kuhusu kupanda zaidi kwa gharama za maisha kunakochangiwa na mfumuko wa bei na kuporomoka kwa kasi kwa shilingi ya Tanzania.
Katika mkutano huo nilitahadharisha kwamba hali ngumu ya maisha kutokana mfumuko wa bei ambao umefikia asilimia 16.8 na kuporomoka kwa sarafu yetu ambapo sasa imefikia dola moja ya Marekani inabadilishwa kwa zaidi ya 1800 ni tishio kwa uchumi na usalama wa nchi na maisha ya wananchi.
Katika mkutano huo nilieleza kwamba bidhaa zinazochangia kwa kiwango kikubwa mfumuko wa bei ni vyakula na nishati hususani matatizo ya umeme na gharama kubwa za mafuta na gesi asilia. Aidha, kuporomoka kwa thamani ya shilingi kunachangiwa na mahitaji makubwa ya dola miongoni mwa waagizaji wa bidhaa toka nje na urari hasi wa biashara kutokana na upungufu wa mauzo ya bidhaa zetu katika masoko ya kimataifa.
Kwa hali hiyo nilishauri hatua za dharura za Rais na Bunge katika kuongeza uzalishaji na usambazaji hususani wa vyakula katika soko la ndani, kuwezesha wazalishaji wadogo na wa kati katika kilimo na viwanda kuongeza mauzo ya nje na kuharakisha matumizi ya gesi asilia na utekelezaji wa mpango wa dharura wa umeme.Juhudi hizo ziende sambamba na kampeni maalumu ya kuhamasisha watanzania kununua bidhaa za ndani na serikali kutekeleza mkakati wa kupunguza manunuzi yake ya nje kwa bidhaa na huduma ambazo zinapatikana nchini. Kadhalika, kwa upande wangu nilieleza kusudio la kuwasilisha bungeni muswada wa sheria ya udhibiti wa bei ya bidhaa muhimu hususani za chakula ili kukabiliana na ukiritimba katika soko na kuweka mfumo wa kupunguza gharama za maisha kwa watanzania wa kipato cha chini.
Kwa upande mwingine, nilieleza kwamba kwa kuwa mfumuko wa bei unachangiwa pia na matatizo katika mfumo wa bajeti na matumizi ya serikali kutokana na ufisadi, ubadhirifu, matumizi ya anasa, mikopo isiyokuwa na udhibiti, kushuka kwa mapato ya serikali ikiwemo kupungua kwa fedha toka washirika wa kimaendeleo kutokana na matatizo ya kifedha katika ukanda wa ulaya; hivyo hatua za dharura za kibajeti na kimfumo zinahitajika kwa kuhusisha serikali na bunge badala ya kuachia hatua za kisera za fedha za benki kuu pekee.
Wenu katika utumishi wa umma,
John MnyikaMbunge wa Ubungo na
Waziri Kivuli wa Nishati na Madini
28/10/2011
PIA, HATUA TATU ZILIZOCHUKULIWA NA BENKI KUU ZINA MADHARA MAKUBWA KATIKA MZUNGUKO WA FEDHA NCHINI IKIWEMO KUPUNGUA KWA UPATIKANAJI WA MIKOPO KATIKA BENKI ZA KIBIASHARA HALI AMBAYO ITAKUWA NA MADHARA KWENYE UZALISHAJI SIKU ZA USONI. HIVYO, NI MAONI YANGU KWAMBA SUALA LA KUHUSISHA KWA KARIBU SEKTA YA MADINI KWENYE JUHUDI ZA KUKABILIANA NA MFUMUKO WA BEI NA KUIMARISHA SARAFU YETU BADO LINAHITAJI MJADALA ENDELEVU WENYE KUWEZESHA HATUA ZA HARAKA KUCHUKULIWA.
TAARIFA KWA UMMMA-28/10/2011: Pamoja na kuchukua hatua za dharura za kuchochea ongezeko la uzalishaji katika kilimo na viwanda na kuwezesha udhibiti wa bei ya bidhaa muhimu kukabiliana na kupanda kwa gharama za maisha kunakosababishwa na mfumuko wa bei na kuporomoka kwa sarafu ya Tanzania pamoja na; serikali inapaswa kuitumia sekta ya madini katika kunusuru uchumi wa taifa na maisha ya wananchi.
Izingatiwe kwamba mfumuko wa bei nchini pamoja na kusababishwa na kupungua kwa uzalishaji unachangiwa pia na nakisi ya bajeti pamoja na udhaifu katika matumizi ya serikali wakati kuporomoka kwa sarafu kunatokana pia na ongezeko la mahitaji ya fedha za kigeni kwa ajili ya ongezeko la uagizaji wa mafuta na malighafi nyingine toka nje.
Hatua tatu za kifedha ambazo zimechukuliwa na benki kuu katika kipindi cha takribani wiki moja hazijaweza kuimarisha sarafu yetu badala yake imeendelea kuporomoka kutoka dola moja kubadilishwa kwa 1600 mpaka 1800; hali ambayo inahitaji hatua za ziada na za haraka kuchukuliwa na mamlaka zingine za kiserikali kwa kushirikiana na sekta binafsi.
Kati ya hatua hizo ni Wizara ya Nishati na Madini kushirikiana na Wizara ya Fedha pamoja na benki kuu kuitumia sekta ya madini katika kunusuru uchumi wa nchi kwa kurejea mapendekezo ya bajeti mbadala za kambi ya upinzani kwa mwaka wa fedha 2011/2012.
Kati ya hatua hizo ni pamoja na Wizara ya Fedha na Benki Kuu kutumia sera, sheria na kanuni husika kufanya majadiliano ya haraka na makampuni ya madini yaweze kuzingatia taratibu za kutunza sehemu kubwa ya fedha za nje (walau 60%) kwenye benki za ndani ili kusaidia kwa dharura kudhibiti kuporomoka kwa shilingi ya Tanzania.
Hatua nyingine ni Wizara ya Nishati na Madini kushirikiana kwa haraka na Wizara ya Fedha na Benki Kuu kutunza sehemu hifadhi yetu ya fedha za kigeni katika mfumo wa madini hususani dhahabu kutokana na thamani ya mauzo ya madini kuongezeka wakati sarafu ya Tanzania ikizidi kuporomoka.
Hatua ya ziada ni kutoza sehemu kubwa ya mrabaha kwa dhahabu badala ya kutoza kwa fedha pekee; na kutoza mapema mrabaha huo kwa asilimia nne kabla ya kukokotoa baadhi ya gharama kama Sheria ya Madini inavyohitaji badala ya asilimia tatu baada ya kuondoa baadhi ya gharama kama ilivyo sasa hatua ambayo itachangia katika kuongeza pato la taifa na kuimarisha sarafu yetu.
Hatua ya nyongeza ni kwa serikali kuelekeza mapato mengine yaliyopatikana katika sekta ya madini katika kutekeleza mpango maalumu wa dharura wa kuongeza uzalishaji na kupunguza madeni yenye kuongeza mfumuko wa bei na kuporomosha shilingi ya Tanzania. Mathalani vyombo vya habari vya kitaifa na kimataifa tarehe 27 Oktoba 2011 vimeeleza kwamba kampuni ya Anglo-Gold Ashanti italipa kodi ya mapato ya kampuni kiasi cha dola milioni 50 (ambayo ni takribani bilioni 90) kwa kiwango cha sasa cha kubadilisha fedha na kwamba tayari imeshalipa bilioni 8.6 katika katika kiasi hicho ikiwa ni mara ya kwanza toka kampuni hiyo ianze uchimbaji wenye tija zaidi ya miaka kumi iliyopita.
Haya ni mapato hayako kwenye bajeti ya serikali 2011/2012 hivyo serikali inapaswa kutumia mapato hayo kama bajeti ya nyongeza ya kutekeleza mpango wa dharura na kupanua wigo wa kuyataka makampuni mengine ikiwemo African Barrick Gold (ABG) yenye migodi mikubwa minne ambayo yote hailipi kodi ya mapato ya kampuni. Hatua hii iende sambamba na kupunguza matumizi ya anasa pamoja na kuvitumia vyanzo mbadala vya mapato vilivyoelezwa na kambi ya upinzani ili kupata fedha za nyongeza za kuingiza katika mpango wa dharura wa kudhibiti mfumuko wa bei na kuporomoka kwa shilingi. Hata hivyo, udhibiti wa ziada unahitajika katika kutekeleza mipango yote ya dharura ili kuepusha mianya ya ufisadi kama ilivyokuwa katika miradi ya kufua umeme IPTL, Alstorm Power Rentals, Richmond na fedha za kuchochea uchumi (Stimulus Package).
Itakumbukwa kwamba tarehe 23 Oktoba 2011 nilifanya mkutano na waandishi wa habari kutaka hatua za dharura kuchukuliwa na Rais Kikwete na bunge kuhusu kupanda zaidi kwa gharama za maisha kunakochangiwa na mfumuko wa bei na kuporomoka kwa kasi kwa shilingi ya Tanzania.
Katika mkutano huo nilitahadharisha kwamba hali ngumu ya maisha kutokana mfumuko wa bei ambao umefikia asilimia 16.8 na kuporomoka kwa sarafu yetu ambapo sasa imefikia dola moja ya Marekani inabadilishwa kwa zaidi ya 1800 ni tishio kwa uchumi na usalama wa nchi na maisha ya wananchi.
Katika mkutano huo nilieleza kwamba bidhaa zinazochangia kwa kiwango kikubwa mfumuko wa bei ni vyakula na nishati hususani matatizo ya umeme na gharama kubwa za mafuta na gesi asilia. Aidha, kuporomoka kwa thamani ya shilingi kunachangiwa na mahitaji makubwa ya dola miongoni mwa waagizaji wa bidhaa toka nje na urari hasi wa biashara kutokana na upungufu wa mauzo ya bidhaa zetu katika masoko ya kimataifa.
Kwa hali hiyo nilishauri hatua za dharura za Rais na Bunge katika kuongeza uzalishaji na usambazaji hususani wa vyakula katika soko la ndani, kuwezesha wazalishaji wadogo na wa kati katika kilimo na viwanda kuongeza mauzo ya nje na kuharakisha matumizi ya gesi asilia na utekelezaji wa mpango wa dharura wa umeme.Juhudi hizo ziende sambamba na kampeni maalumu ya kuhamasisha watanzania kununua bidhaa za ndani na serikali kutekeleza mkakati wa kupunguza manunuzi yake ya nje kwa bidhaa na huduma ambazo zinapatikana nchini. Kadhalika, kwa upande wangu nilieleza kusudio la kuwasilisha bungeni muswada wa sheria ya udhibiti wa bei ya bidhaa muhimu hususani za chakula ili kukabiliana na ukiritimba katika soko na kuweka mfumo wa kupunguza gharama za maisha kwa watanzania wa kipato cha chini.
Kwa upande mwingine, nilieleza kwamba kwa kuwa mfumuko wa bei unachangiwa pia na matatizo katika mfumo wa bajeti na matumizi ya serikali kutokana na ufisadi, ubadhirifu, matumizi ya anasa, mikopo isiyokuwa na udhibiti, kushuka kwa mapato ya serikali ikiwemo kupungua kwa fedha toka washirika wa kimaendeleo kutokana na matatizo ya kifedha katika ukanda wa ulaya; hivyo hatua za dharura za kibajeti na kimfumo zinahitajika kwa kuhusisha serikali na bunge badala ya kuachia hatua za kisera za fedha za benki kuu pekee.
Wenu katika utumishi wa umma,
John MnyikaMbunge wa Ubungo na
Waziri Kivuli wa Nishati na Madini
28/10/2011