Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
WanaJF:
Sasa ni wazi kabisa umaarufu wa CCM umeanza kupungua kwa kiasi cha kutisha kiasi kwamba hata zile shughuli za kitaifa zinalazimishwa kuwa ni za CCM. Leo hii JK alifungua barabara ya 60km kati ya Mwandiga na Manyovu mkoani Kigoma, katika hafla ambayo ilitekwa na CCM kwa kuwepo watu wa magwanda ya kijani ambao bila shaka walitayarishwa rasmi kupamba hafla hiyo.
Mbunge wa eneo hilo, Zitto Kabwe, alijikuta akihutubia na umati wa wana-CCM ingawa jimbo lake hilo wengi ni Chadema kwa vile mwaka jana tu walimchagua yeye Zitto wa chama hicho na kumbwaga yule wa CCM.
Kweli tutaona vituko vingi kutoka kwa wanamagamba wanapoelekea kupotea katika medani ya siasa hapa nchini!
Source CH ten news bulletin today.
Sasa ni wazi kabisa umaarufu wa CCM umeanza kupungua kwa kiasi cha kutisha kiasi kwamba hata zile shughuli za kitaifa zinalazimishwa kuwa ni za CCM. Leo hii JK alifungua barabara ya 60km kati ya Mwandiga na Manyovu mkoani Kigoma, katika hafla ambayo ilitekwa na CCM kwa kuwepo watu wa magwanda ya kijani ambao bila shaka walitayarishwa rasmi kupamba hafla hiyo.
Mbunge wa eneo hilo, Zitto Kabwe, alijikuta akihutubia na umati wa wana-CCM ingawa jimbo lake hilo wengi ni Chadema kwa vile mwaka jana tu walimchagua yeye Zitto wa chama hicho na kumbwaga yule wa CCM.
Kweli tutaona vituko vingi kutoka kwa wanamagamba wanapoelekea kupotea katika medani ya siasa hapa nchini!
Source CH ten news bulletin today.