Nemesis
JF-Expert Member
- Feb 13, 2008
- 5,462
- 4,364
Askari mmoja ana gharimu kiasi gani kwa kazi maalumu? Posho yake na gharama za mabomu ya machozi
Gharama za utawala ni kiasi gani,ikiwemo vikao vya kupanga jinsi ya askari hao kugawanyika na kufanya kazi yao?
Watu wa usalama nao hulipwa bei gani kwa ajili ya kukaa vijiweni kunywa pombe kwa siku kwa lengo la kupeleleza?
Tukipiga mahesabu hayo tunaweza kujua ni askari wangapi wanahitajika ili kutumia milioni 100 na tunaweza kukadiria pana askari wangapi huko hivi sasa na hatimaye tutapata jibu kama habari hii ni ya kweli au imeongezewa chumvi
Kule kwetu Zanzibar waliwahi kumwagwa kwa maelfu, nadhani walitumia vijisenti vingi
Asha
Bi Asha posho za vikao ni nyingi hasa kwa wahadhiri. Katika kikao chochote kilicho chini ya Halmashauri ya Chuo (University Council) posho kwa wajumbe ni sh 150,000/= kila mmoja. Vikao vya Kamati ni kuanzia sh 60,000/= sijui kama zimebadilika hizi ni rate za mwaka 2000.