Mhache
JF-Expert Member
- Jun 20, 2008
- 345
- 24
Mimi ni Mtanzania, nilifanikiwa kupata safari ya kuja Finland kwa ajili ya masomo ya muda mfupi toka tarehe 01/09/2009 na niatrudi Tanzania mwezi ujao. Nimebahatika kutembelea maeneo mengi ya katika nchi ya Finland kama Turku, Tampere, Helsinki na kadhalika. Pia nilipata bahati ya kutembela Norway and Capenhagen. Jambo lililonifurahisha ni usafi wa nchi hizi. Ni ngumu sana kuona rundo la taka kama ilivyo katika jiji la Dar es Salaam. Mtu anatembea na uchafu masafa marefu mpaka aone sehemu ya kutupa taka.
Mapipa ya kutupia taka yapo kila mahali, hata kwenye misitu. Nikajiuliza ingekuwa ni Dar, wauza vyuma chakavu wangekuwa walishayabeba. Mapipa yenyewe hayajatobolewa kama tunavyofanya Tanzania. Mara ya kwanza nilifikiri ni mapipa ya maji safi, kumbe ni kwa ajili ya taka. Mimi mwenyewe nilikuwa naona aibu kimoyo moyo. Sijui tufanye nini ili jiji la Dar liwe safi. Ukiwa nchi za Ulaya utafikiri hakuna kufa, jinsi watu wanavyojali.
Mapipa ya kutupia taka yapo kila mahali, hata kwenye misitu. Nikajiuliza ingekuwa ni Dar, wauza vyuma chakavu wangekuwa walishayabeba. Mapipa yenyewe hayajatobolewa kama tunavyofanya Tanzania. Mara ya kwanza nilifikiri ni mapipa ya maji safi, kumbe ni kwa ajili ya taka. Mimi mwenyewe nilikuwa naona aibu kimoyo moyo. Sijui tufanye nini ili jiji la Dar liwe safi. Ukiwa nchi za Ulaya utafikiri hakuna kufa, jinsi watu wanavyojali.