Asprin
JF-Expert Member
- Mar 8, 2008
- 68,012
- 95,355
Haaaa kumbe mchumba wako ni Serengeti lager eeee kweli kwaya masta tunae.
Ulishawahi kumjaribu. Usijaribu, hutamwacha.
Haaaa kumbe mchumba wako ni Serengeti lager eeee kweli kwaya masta tunae.
Wasalaamu salamuni, waungwana nawajia
Mababu wa mizimuni, walokwisha tangulia
Najongea kwa huzuni, najizuia kulia
ulimwengu wa mapenzi, buriani aagia
Ulimwengu wa mapenzi, buriani naagia
naondoka kwa majonzi, mlango najifungia
Si wangu nimemaizi, moyo nafungulia
Ninakupa zako mbawa, uruke unakotaka
Ninakupa zako mbawa, uruke unakotaka
Umeyataka mabawa, meupe yaso na taka
Nimechoka kupagawa, na penzi lenye mashaka
Ulimwengu wa mapenzi, nawaachia wenye bahati.
Ulishawahi kumjaribu. Usijaribu, hutamwacha.
Sijawahi kumjaribu na kamwe sitamjaribu.
Sijawahi kumjaribu na kamwe sitamjaribu.
MTM
Uamuzi nimetoa, nachelea urejea
wangu moyo nilitoa, yeye akauchezea
kitambo ningelitoa, subira nikarejea
ningeyajua ya moyo, katu singeliumia
Natizama pembe kona, faraja kuitafuta
Ili nipate kunona, mwili upate mafuta
nimekonda kila kona, kama mche wa ufuta
laiti ningeyajua, katu singeliumia
Ulimwengu wa mapenzi,hatuuachi twapumzika
Ndani ya mwaka au miezi,utampata unayemtaka
Mojawapo ya wanaokuenzi,Fidel80 aso na mipaka
Swali langu kwako moja,umeacha au wapumzika?
Wasalaamu salamuni, waungwana nawajia
Mababu wa mizimuni, walokwisha tangulia
Najongea kwa huzuni, najizuia kulia
ulimwengu wa mapenzi, buriani aagia
Ulimwengu wa mapenzi, buriani naagia
naondoka kwa majonzi, mlango najifungia
Si wangu nimemaizi, moyo nafungulia
Ninakupa zako mbawa, uruke unakotaka
Ninakupa zako mbawa, uruke unakotaka
Umeyataka mabawa, meupe yaso na taka
Nimechoka kupagawa, na penzi lenye mashaka
Ulimwengu wa mapenzi, nawaachia wenye bahati.
Shosti unaniangusha, kujiliza hadharani
Chati unampandisha, kakufanya hayawani
Bure unajikondesha, nakujishusha thamani
Amekufanya wa nini, mfanye wa kazi gani.
Mfanye wa kazi gani, amekufanya wa nini
Akipita mtaani, mvalie na miwani
Mmekutana ukubwani, majonzi sasa ya nini
Ulimwengu wa mapenzi, na wewe bado ni memba.
Na wewe bado ni memba, ulimwengu wa mapenzi
Hutakiwi kwenda Pemba, kuyatafuta mapenzi
Wanamuziki waimba, yalianza toka enzi
Aliye na niya hasa, penzi usimbanie.
Penzi usimbanie, aliye na niya hasa
Ila usikimbilie, Fidel Chrispin Masa
Hapana watamkie, usije wapa hamasa
Mbili zero moja mbili, ndoa zao watangaza.
Ndoa zao watangaza, mbili zero moja mbili
Hawajaenda angaza, wameahirisha mara mbili
Hapa nakupa mwangaza, silazimishi ukubali
Ukitala alosoma, jiulize pia why?
Jiulize pia why, ukitaka alosoma
Ningeshauri Bluray, ila kingereza chake noma
Anaongea in a way, tafsiri zinagoma
Pedejee sishauri, unless wahusudu.
Shosti unaniangusha, kujiliza hadharani
Penzi usimbanie, aliye na niya hasa
Ila usikimbilie, Fidel Chrispin Masa
Hapana watamkie, usije wapa hamasa
Mbili zero moja mbili, ndoa zao watangaza.
Lizy big up,nimeipenda sana hii,nimekugongea thanks kule.
Afwezeli, manake ulivokuwa mchoyo wa thanks kweli Lizy kakukuna.
Wewe salimia kwanza,ha ha ha mimi sio mchoyo wa thanks angalia kwenye details zangu idadi ya thanks nilizogongea watu halafu linganisha na za kwako hapo ndo tutajua nani mchoyo wa thanks.
Hahaha! Nilijua tu lazima uchungulie manake hupitwi. Salama lakini? Shemeji hajambo?
Si unajua unapoleta mada lazima uwe na full info sasa nilipoona umeniita mchoyo nikaanza uchunguzi,nikagundua kuwa umeleta mada bila kuifanyia uchunguzi,Sisi tu wazima,mimi na familia yangu na shemeji yako pia mzima kabisa.
Poa msalimu shemeji. Akikuletea za kuleta usisahau kuniPM. Hahahaha