Ulikua ni Mdahalo au ni Mkutano wa CCM?

Ndallo

JF-Expert Member
Oct 1, 2010
7,619
4,292
Hatimaye imebakia siku moja wananchi kwenda kuwachagua viongozi wawapendao kuwaletea maendeleo kwa awamu ya pili baada ya viongozi wa vyama vyote saba baada ya kunadi sera zao. Kweli nimefuatilia sera za vyama vyote hadi kufikia jana baada ya kupata muda wa kuangalia mdahalo wa chama tawala hapo jana kupitia luninga ya TBC 1 kwa mgombea wa chama cha CCM! nimetafakari kwa kina baada ya kumsiliza JK akiwa anajibu maswali ya waandishi wa habari na sio wananchi kwa jinsi nilivyokua nategemea kuona mkutano huo nasio mdahalo kama nilivyokua nategemea kwa kua niliona kama jamaa alikua anahutubia na sio kutoa sera za ni nini atawafanyia wananchi kwa kipindi hiki anachomalizia kwa kutoa ahadi lukuki kama tulivyomsikia katika kampeni zake! Ndugu wanajanvi naomba kuuliza kweli ule ulikua ni mdahalo au ulikua ni mkutano wa CCM na wazee wa Dar es salaam?? Hembu changia hoja hii mwana JF!
 
Back
Top Bottom