Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,258
- 20,709
Jibu hayo maswali halafu uangalie nafasi yako hapo ulipo!....Naweza kuorodhesha matamanio ya mafanikio ya mwenzangu kimaisha..YES/NO? Najua mambo anayohofia mwenzi wangu kwa nyakati tofauti.......YES/NO? Najua kuhusu nyakati muhimu kwenye maisha ya mwenzi wangu,naweza kuzitaja kama ikihitajika wakati wowote.,..YES/NO? Naweza kuorodhesha mambo matatu anayoyapenda mwenzi wangu,nitayataja kirahisi..YES/NO? Huwa ninamgusa mpenzi wangu kwa upendo mara kwa mara.....................YES/NO? Maisha yetu kuhusu tendo la ndoa ni ya kuridhisha na ninayafurahia.......YES/NO? Hua napenda kuwa karibu nae nikiwa sina majukumu mengi..................YES/NO? Mwenzi wangu ni miongoni mwa marafiki wangu wakubwa sana...........YES/NO? Mwenzi wangu ananieleza kila anapopata jambo linalomsumbua..............YES/NO? Huwa nafurahia kutoka moyoni ushauri wake.YES/NO? Huwa najifunza mengi kutoka kwake pale ambapo hatujafikia muafaka kwenye mambo mbalimbali....YES/NO? Najihisi mwenye kauli yenye nguvu au muhimu kila tukifanya maamuzi..YES/NO? Huwa nakiri kwa upendo kila nikikosea....YES/NO? Hatununiani tunaposhindwa kuelewana...........YES/NO? Ni mzuri sana katika kuniliwaza pale ninapokereka au kuvunjika moyo,...YES/NO? Huwa tunashirikiana kwenye kila jambo tuklenga kuimarisha uhusiano wetu udumu sana.....YES/NO? Tunapobishana lengo sio kushinda bali muafaka na maelewano tu........YES/NO? Kuna mambo hatuwezi kuyapatia suluhu....YES/NO? Tunashiriki kwenye majukumu yetu kwa usawa....YES/NO? Tunashiriki kumbukumbu zetu nzuri kwa furaha.,...YES/NO? Kama majibu yako ya YES yanakaribia robo tatu,jua uhusiano wenu ni imara,kama ni chini ya hapo kuna kasoro kidogo,zirekebisheni.Kama YES ni chini ya robo,mnakaribiana kutengana!