Ukweli wa kifo cha Kighoma Ally Malima ni upi?

Mbona sisi tuliofanya Mtihani wa Cambridge Overseas Schools Cerficate mwaka wa 1952 tulitumia namba na sio majina yetu? Kwani kulikuwa na Waziri aliyefuta utaratibu huo baada ya Uhuru?
Mkuu wangu hata sielewi ndicho nachozungumzia hapa wewe ulitumia namba, mimi nilitumia jina na sina sababu ya kudanganya. Tunachotaka kufahamu hapa ni kujaribu kurekebisha mfumo wa elimu nchini na sio kubishana juu ya udini. Mtu yeyote anayechukulia swala hili ktk udini ndiye anayetuvuruga..maana ukweli unasimama kwamba majina yanatumika na tumeona matokeo haya ya juzi yakionyesha majina ya watu.. Sasa kama ilikuwa tukitumia namba na sio majina ni lini NECTA wameacha kutumia namba wakarudi ktk majina? sipati jibu..Kwa kuongezeda tu mwaka 1969 wanafunzi walikaa mtihani wa darasa la saba kwenda sekondary la nane lilifutwa tokea hapo.
 
Zakumi,

..Ndalichako ametetea integrity ya zoezi la utungaji mtihani na usahihishaji.

..kuna watu wanadai hata ktk kusahihisha wamejaa wakatoliki wengi ambao wanawanyima maksi Waislamu.

..sasa ndiyo mimi nikaeleza kama mambo yako kama alivyobainisha Dr.Ndalichako basi huwezi kufanya udanganyifu zaidi ya kuiba mtihani wenyewe. zaidi nikaeleza hata ukiiba mtihani, ili ufaulu, you have to be a good student kwasababu maswali ya mtihani yana-cover material ya miaka 4 kwa o-levels na miaka 2 kwa a-levels.

..binafsi nilipokuwa jeshini nili-solve paper ya mtihani wa form 4 kwa madogo fulani, na nilikuwa very curious kuona matokeo yao yangekuwaje. well, matokeo yalipokuja vijana wale waliambulia div 4 na wengine wakabahatisha 3. ndiyo maana nime-conclude kwamba paper iliyoibiwa only helps the brighter and capable students.

Mkuu,

Huoni kuwa hata utungaji wenyewe unasababisha wizi. Chukua mfano shule ambazo hazina resources. Wanafunzi wa shule hizo nao wanapambana kwenye mitihani na wanafunzi wenye resources, je mitihani ikiibiwa utalalamika?

You can't have integrity when you don't have fairness. Na sababu kuwa ya kufanya mitihani ni ku-gauge elimu inavyotolewa hili kufanyike improvement. Kwenye mazingira ambayo mitihani inatolewa hili wachaguliwe wale wanaoitwa bora, wizi utafanyika tu.

Anyway, thread ni kuhusu Malima.
 
La muhimu ikiwa tunataka kuzungumzia swala hili with open mind tujiulize waziri mzima kama Kighoma Malima alilalamikia nini kuhusu ELIMU nchini na kwa nini?..Lazima kulikuwepo na sababu huyu hakuwa kichaa - kama haikuwa hili la namba je ni lipi alolisema? na kwa vigezo gani kuliko kuendelea kubishana wakati hatuna facts. Nakumbuka sana miaka ya 70s na 80s hata kuandika dini na kabila ya mtu ktk form za serikali zilipigwa vita sana tu.
 
Wengine wanasema Mke mkubwa wa marehemu hakujulishwa wala hakufurahishwa na Prof Malima Kuoa mke mwingine. kwa hiyo alisoma alibadiri

Malima alifunga Ndoa na toto la kinyamwezi waishio Mwanza lakini kwenye harusi aliwakilishwa na ndugu yake. Baada ya harusi honeymoon ndiyo uko walienda na mke mpya UK huku akiwa na mpango wa kuchukua mijihela yake.

Basi kumbe kupitia system pesa zilishapigwa stop na ile pressure ya kukosa mahela ndiyo ilimmaliza prof.

Alipo apumzike kwa amani
 
Mkuu mimi nakubaliana na wewe sana tu na ndivyo nilivyoelewa mimi kwamba tulishindwa kuendelea na masomo kwa sababu hatukuwa na shule za sekondary na vyuo vya kutosha.

Lakini inapofikia watu wanaanza kubishana kuhusu matumizi ya namba na majina, nafasi ya Malima ktk ELimu nchini ndipo naposhangaa na kujiuliza tena pengine kuna ukweli ktk madai ya Malima. haiwezekani kabisa waziri mzima aandike barua na kupinga mfumo wa Elimu nchini halafu watu waje kutetea hapa na kumwita yeye ndiye mdini na wasipinge hoja yake. Yeye alikuwa kichaa? Haya leo hii mimi Mkandara napinga kabisa mfumo wa elimu nchini unaounganisha serikali na CSSC naonekana kicha vile vile.. Lakini ukweli ni upi?.. kesho watu watakuja bishana vile vile kwamba serikali haiwajawahi kushirikiana na kanisa.

Ukweli ni kuwa kulikuwa na sekondari za kidini zilizotaka usajili lakini applications zao zilikuwa zimekaa tu wizara ya elimu bila kushughulikiwa kwa miaka mingi. Na wakati huo huo, serikali ilikuwa ina shule chache.

Hivyo Malima alipokuwa waziri alikata ukiritimba wa usajili. Hii ilisaidia taifa kwa ujumla. Kwa sababu namba ya watahiniwa iliongezeka mara mbili bila serikali kujenga shule ya sekondari.
 
Wengine wanasema Mke mkubwa wa marehemu hakujulishwa wala hakufurahishwa na Prof Malima Kuoa mke mwingine. kwa hiyo alisoma alibadiri

Malima alifunga Ndoa na toto la kinyamwezi waishio Mwanza lakini kwenye harusi aliwakilishwa na ndugu yake. Baada ya harusi honeymoon ndiyo uko walienda na mke mpya UK huku akiwa na mpango wa kuchukua mijihela yake.

Basi kumbe kupitia system pesa zilishapigwa stop na ile pressure ya kukosa mahela ndiyo ilimmaliza prof.

Alipo apumzike kwa amani

Mke mkubwa wa Malima ni Mkristo. Hiyo Alibadiri alisoma wapi?
 
Ukweli ni kuwa kulikuwa na sekondari za kidini zilizotaka usajili lakini applications zao zilikuwa zimekaa tu wizara ya elimu bila kushughulikiwa kwa miaka mingi. Na wakati huo huo, serikali ilikuwa ina shule chache.

Hivyo Malima alipokuwa waziri alikata ukiritimba wa usajili. Hii ilisaidia taifa kwa ujumla. Kwa sababu namba ya watahiniwa iliongezeka mara mbili bila serikali kujenga shule ya sekondari.
Mkuu wangu kisa na mkasa wa Malima ulitokana na elimu nchini..wala sio swala la namba hata kidogo isipokuwa watu wamelikuza hadi kufikia hapa. Ni sawa na leo mimi navyopiga vita muafaka wa elimu na Afya... hakuna Udini isipokuwa haifai na unaleta utengano baina yetu.

Tatizo lilitokana kweli na swala la UDINI pale Malima alipohoji inakuwaje Waislaam na Wanawake ndio wenye hesabu ndogo kuendelea na masomo ya kidato cha kwanza wakati hesabu yao ni nusu kwa nusu hasa baada ya azimio la Musoma kwa upande wa wananake? he said something is wrong.. Mwinyi akalikubali swala hili isipokuwa akalirudisha kwenye chama ili lizungumziwe kwa undani kuweza kuanzisha uchunguzi. Ndipo Malima akakutanishwa na mama yetu Mongela katibu wa chama na ndipo zogo lilipoanza. Binafsi nitasema mchawi wangu ni mama Mongela maana alichukulia swala hili kuwa ni UDINI badala ya kutazama undani japokuwa Malima alichoomba ni uchunguzi ufanyike.

Moto ulipowaka na kuwa mkubwa ndipo Malima alipoona bora ajikate hasa baada ya kuondolewa wizara ya elimu na kupelekwa Fedha ambako scandal baada ya scandal ilikuwa ni yeye utafikiri Sitta leo hii..Ilifikia hadi Kardnali Pengo akasema huyu Malima ni hatari sana anatakiwa ashughulikiwe!.. haya ni maneno yaliyotaka kwa Kardinali na sii mchezo wa kupuuza..Kighoma ndio kutoka CCM na kujaribu kuunda chama chake lakini alipigwa vita na ikasemekana ameingiza silaha nchini ili Waisaam wapambane na Wakristu.. Hizi tuhuma zote nazikumbuka vizuri tu kama jana mkuu wangu..Hii ndio CCM yetu tuloachiwa na mwalimu hutakiwi unazushiwa jambo kiasi kwamba hutamaniki tena na wakikushindwa Unaondolewa.

Kwa hiyo, niijuavyo CCM mimi na yaliyowakuta kina Kolimba na Mwaikambo siwezi kupuuza ukweli kwamba Malima aliondolewa kama alivyoondolewa Sokoine, na wengine as long as walikuwa hatari kwa utawala wao. Sijaona mahala popote Kighoma Malima akisema yeye ndiye aliyeanzisha namba wala jambo jingine zaidi ya madai kwamba kuna mchezo unachezwa baraza la mitihani kupasisha watu kwenda kidato cha nne na bahati mbaya alokuwa akiwatetea ni Waislaam na Wanawake.
 
You can tell watu wanaong'ang'ania mfumo wa udini ni watu wenye identity crisis!
Hii kitu mikoani ndio imeanza kusikika baada ya uchaguzi wa 2010.
Prior to 2010 waislamu na wakristu tuliishi kwa upendo mkubwa sana mikoani, bonded by our forefathers tradition. We were one.
But now, they had to come these people who have no idea who they are.
I like to think hawa watu walichukuliwa miaka iileee kutoka bara kuja pwani destination Oman na kadhalika, but hawa watu hawakupata soko pale mnadani kunuliwa. Wakabakia tu huko visiwani na pwani.
Sasa wakapoteza identity yao, wapo kati kati.

We umeshaona wapi mhaya akamchukia au kumyima haki mhaya mwezake sababu ya dini? Ali Mufuruki ni successful mhaya and proud of it!
Hata wachaga, umeshaona wanachukiana sababu ya dini? IGP Said Mwema is as mchaga as they come! Mmachame.

Utaona tu wale wanaolialia kuonewa wanayao.
 
Mie ni mmoja wa watu ambao hatuungi mkono kabisa ubaguzi. Kelele za waislam zilinifanya nianze kutafuta tatizo liko wapi. Nilichokiona kwa macho yangu ni kuwa hamana mkazo wa elimu kwa watoto miongoni mwa wazazi wa kiislam, nimekaa vingunguti, buguruni kwa mnyamani na Segerea kwa nyakati tofauti. nilichoona vingunguti na buguruni ni kuwa haya ni maeneo yenye waislam wengi sana huko watoto wengi wa kike huacha shule darasa la tano na sita bila wasiwasi na ni kitu cha kawaida, hii hali ni tofauti kidogo na sehemu ambako kuna wakristo wengi kama segerea na Tabata kwa ujumla, nimefuatilia pia wale waislam tuliosoma nao katika level tofauti nimegundua wengi ni watu waliokulia ktk mikoa ambayo inazingatia elimu kama kilimanjaro, Mbeya Kagera n.k wakati tukiwa A-Level pale kibaha ktk darasa la watu 103 kulikuwa na waislam 21 na kati ya hao ni mmoja tu ndio alikuwa mtu wa mkoa wa pwani waliobaki walikuwa waislam wa kutoka Iringa, mbeya kilimanjaro, mwanza na wachache kutoka Tanga, dar, singida na kigoma. Nilichoona ni kuwa ktk mikoa ya pwani lifestyle na mila na desturi zinawaathiri watoto na hilo liko wazi iwe kwa wakristu au waislam, watoto wa kiislam hulelewa ktk misingi ya kuchukia elimu ya magharibi wakiiambatanisha na ukristo wakati wakristo hawana tatizo hilo. Aidha kuna dada yangu alihamia tandika akiwa na mtoto mdogo lakini kwa mazingira ya tandika ndani ya mwezi mmoja mtoto alibadilika sana kitabia kiasi kwamba ilibidi huyo dada arudi mkoani ili akamlee mtoto mpaka atakapofikisha umri wa kwenda shule ili kumwepusha asitumie muda mwingi kuchanganyikana na watoto wengi ambao matusi ni kama tai.

Mwisho nishauri kuwa kama watu tuna dhamira ya dhati ya kuondoa tofauti kubwa iliyopo kati ya wakristo na waislam pana haja ya kwanza kuyaadress matatizo yanayosababisha hali hiyo. Kuhusu malalamiko ya waislam kuwa waislam wanaonewa ni rahisi tu kuyaondoa, kwanza tujaribu kubalance idadi ya waislam na wakristo ktk maswala ya kusahihisha mitihani, halafu zianzishwe program za chemsha bongo kushindanisha wanafunzi wa shule tofauti zitakazokuwa zinarushwa ktk TVs kama ilivyo kwa Zain Africa challenge, pamoja na kuwapa changamoto wanafunzi na kuwajengea confidence lakini pia kila mtu atakuwa akiona tofauti ilyopo kati ya mwanafunzi anayesoma Marian girls, st. fransis na Mazinde na yule anayesoma kirinjiko, kibohehe na alharamain na pia tutajionea tofauti kati ya wanaosoma serikalini na wanaosoma private schools. Hapo tutakuwa ktk nafasi ya kutambua kama wanafunzi wa kikristo wanajua kweli au wanapendelewa na vilevile tutajua kama wanafunzi hawajui mambo kweli au wanaonewa ktk marking.
 
Mie ni mmoja wa watu ambao hatuungi mkono kabisa ubaguzi. Kelele za waislam zilinifanya nianze kutafuta tatizo liko wapi. Nilichokiona kwa macho yangu ni kuwa hamana mkazo wa elimu kwa watoto miongoni mwa wazazi wa kiislam, nimekaa vingunguti, buguruni kwa mnyamani na Segerea kwa nyakati tofauti. nilichoona vingunguti na buguruni ni kuwa haya ni maeneo yenye waislam wengi sana huko watoto wengi wa kike huacha shule darasa la tano na sita bila wasiwasi na ni kitu cha kawaida, hii hali ni tofauti kidogo na sehemu ambako kuna wakristo wengi kama segerea na Tabata kwa ujumla, nimefuatilia pia wale waislam tuliosoma nao katika level tofauti nimegundua wengi ni watu waliokulia ktk mikoa ambayo inazingatia elimu kama kilimanjaro, Mbeya Kagera n.k wakati tukiwa A-Level pale kibaha ktk darasa la watu 103 kulikuwa na waislam 21 na kati ya hao ni mmoja tu ndio alikuwa mtu wa mkoa wa pwani waliobaki walikuwa waislam wa kutoka Iringa, mbeya kilimanjaro, mwanza na wachache kutoka Tanga, dar, singida na kigoma. Nilichoona ni kuwa ktk mikoa ya pwani lifestyle na mila na desturi zinawaathiri watoto na hilo liko wazi iwe kwa wakristu au waislam, watoto wa kiislam hulelewa ktk misingi ya kuchukia elimu ya magharibi wakiiambatanisha na ukristo wakati wakristo hawana tatizo hilo. Aidha kuna dada yangu alihamia tandika akiwa na mtoto mdogo lakini kwa mazingira ya tandika ndani ya mwezi mmoja mtoto alibadilika sana kitabia kiasi kwamba ilibidi huyo dada arudi mkoani ili akamlee mtoto mpaka atakapofikisha umri wa kwenda shule ili kumwepusha asitumie muda mwingi kuchanganyikana na watoto wengi ambao matusi ni kama tai.

Mwisho nishauri kuwa kama watu tuna dhamira ya dhati ya kuondoa tofauti kubwa iliyopo kati ya wakristo na waislam pana haja ya kwanza kuyaadress matatizo yanayosababisha hali hiyo. Kuhusu malalamiko ya waislam kuwa waislam wanaonewa ni rahisi tu kuyaondoa, kwanza tujaribu kubalance idadi ya waislam na wakristo ktk maswala ya kusahihisha mitihani, halafu zianzishwe program za chemsha bongo kushindanisha wanafunzi wa shule tofauti zitakazokuwa zinarushwa ktk TVs kama ilivyo kwa Zain Africa challenge, pamoja na kuwapa changamoto wanafunzi na kuwajengea confidence lakini pia kila mtu atakuwa akiona tofauti ilyopo kati ya mwanafunzi anayesoma Marian girls, st. fransis na Mazinde na yule anayesoma kirinjiko, kibohehe na alharamain na pia tutajionea tofauti kati ya wanaosoma serikalini na wanaosoma private schools. Hapo tutakuwa ktk nafasi ya kutambua kama wanafunzi wa kikristo wanajua kweli au wanapendelewa na vilevile tutajua kama wanafunzi hawajui mambo kweli au wanaonewa ktk marking.
Mkuu wangu samahani sana... wewe na Kaburu hamna tofauti kabisa mana maeno hyaya tumeyasikia sana toka kwao.. mada hii inamhusu Malima, hao Waislaam wanahusu vipi hadi uwaone wao hawana mkazo na elimu. Kwa Ukristu wako ndio umekufanya kweli uweke mkazo ktk elimu? hii kweli inaingia akilini kisha hao hao waislaam walalamikie elimu ambayo hawaitaki? akili gani hii mkuu wangu..
Hivi kesho ukisilimu na kuwa Muislaam utabadidilisha mtazamo wako ktk elimu? Au mimi nikbatizwa basi nitafikiria tofauti ktk elimu ya wanangu...Acheni ujinga tuzungumzie yaliyomsibu Malima na sio waislaam maana wewe mwenyewe unaonyesha umesoma lakini hujaelemika. Umegubikwa na Ubaguzi sawa na kaburu.
 
Mkuu wangu kisa na mkasa wa Malima ulitokana na elimu nchini..wala sio swala la namba hata kidogo isipokuwa watu wamelikuza hadi kufikia hapa. Ni sawa na leo mimi navyopiga vita muafaka wa elimu na Afya... hakuna Udini isipokuwa haifai na unaleta utengano baina yetu.

Tatizo lilitokana kweli na swala la UDINI pale Malima alipohoji inakuwaje Waislaam na Wanawake ndio wenye hesabu ndogo kuendelea na masomo ya kidato cha kwanza wakati hesabu yao ni nusu kwa nusu hasa baada ya azimio la Musoma kwa upande wa wananake? he said something is wrong.. Mwinyi akalikubali swala hili isipokuwa akalirudisha kwenye chama ili lizungumziwe kwa undani kuweza kuanzisha uchunguzi. Ndipo Malima akakutanishwa na mama yetu Mongela katibu wa chama na ndipo zogo lilipoanza. Binafsi nitasema mchawi wangu ni mama Mongela maana alichukulia swala hili kuwa ni UDINI badala ya kutazama undani japokuwa Malima alichoomba ni uchunguzi ufanyike.

Moto ulipowaka na kuwa mkubwa ndipo Malima alipoona bora ajikate hasa baada ya kuondolewa wizara ya elimu na kupelekwa Fedha ambako scandal baada ya scandal ilikuwa ni yeye utafikiri Sitta leo hii..Ilifikia hadi Kardnali Pengo akasema huyu Malima ni hatari sana anatakiwa ashughulikiwe!.. haya ni maneno yaliyotaka kwa Kardinali na sii mchezo wa kupuuza..Kighoma ndio kutoka CCM na kujaribu kuunda chama chake lakini alipigwa vita na ikasemekana ameingiza silaha nchini ili Waisaam wapambane na Wakristu.. Hizi tuhuma zote nazikumbuka vizuri tu kama jana mkuu wangu..Hii ndio CCM yetu tuloachiwa na mwalimu hutakiwi unazushiwa jambo kiasi kwamba hutamaniki tena na wakikushindwa Unaondolewa.

Kwa hiyo, niijuavyo CCM mimi na yaliyowakuta kina Kolimba na Mwaikambo siwezi kupuuza ukweli kwamba Malima aliondolewa kama alivyoondolewa Sokoine, na wengine as long as walikuwa hatari kwa utawala wao. Sijaona mahala popote Kighoma Malima akisema yeye ndiye aliyeanzisha namba wala jambo jingine zaidi ya madai kwamba kuna mchezo unachezwa baraza la mitihani kupasisha watu kwenda kidato cha nne na bahati mbaya alokuwa akiwatetea ni Waislaam na Wanawake.
Mkuu wakati ule kardinali alikuwa sio Pengo alikuwa anaitwa Laurian Lugambwa.
 
Mkuu wakati ule kardinali alikuwa sio Pengo alikuwa anaitwa Laurian Lugambwa.
Samahani sasa nikitaka kum address Pengo natakiwa niseme? sijui mkuu wangu nilidhani unatumia cheo chake cha leo hata ktk maswala ya zamani.
 
This thread embodies a pure African disposition i.e gossiping, prying and meddling. Only in Africa where you'll find people discussing dead bodies instead of spending time on pondering weighty matters. Poor AFRICANS.
 
Mkuu wangu samahani sana... wewe na Kaburu hamna tofauti kabisa mana maeno hyaya tumeyasikia sana toka kwao.. mada hii inamhusu Malima, hao Waislaam wanahusu vipi hadi uwaone wao hawana mkazo na elimu. Kwa Ukristu wako ndio umekufanya kweli uweke mkazo ktk elimu? hii kweli inaingia akilini kisha hao hao waislaam walalamikie elimu ambayo hawaitaki? akili gani hii mkuu wangu..
Hivi kesho ukisilimu na kuwa Muislaam utabadidilisha mtazamo wako ktk elimu? Au mimi nikbatizwa basi nitafikiria tofauti ktk elimu ya wanangu...Acheni ujinga tuzungumzie yaliyomsibu Malima na sio waislaam maana wewe mwenyewe unaonyesha umesoma lakini hujaelemika. Umegubikwa na Ubaguzi sawa na kaburu.
Mkandara bana. Siyo vizuri kumuita mwenzako kaburu.
 
Mie ni mmoja wa watu ambao hatuungi mkono kabisa ubaguzi. Kelele za waislam zilinifanya nianze kutafuta tatizo liko wapi. Nilichokiona kwa macho yangu ni kuwa hamana mkazo wa elimu kwa watoto miongoni mwa wazazi wa kiislam, nimekaa vingunguti, buguruni kwa mnyamani na Segerea kwa nyakati tofauti. nilichoona vingunguti na buguruni ni kuwa haya ni maeneo yenye waislam wengi sana huko watoto wengi wa kike huacha shule darasa la tano na sita bila wasiwasi na ni kitu cha kawaida, hii hali ni tofauti kidogo na sehemu ambako kuna wakristo wengi kama segerea na Tabata kwa ujumla, nimefuatilia pia wale waislam tuliosoma nao katika level tofauti nimegundua wengi ni watu waliokulia ktk mikoa ambayo inazingatia elimu kama kilimanjaro, Mbeya Kagera n.k wakati tukiwa A-Level pale kibaha ktk darasa la watu 103 kulikuwa na waislam 21 na kati ya hao ni mmoja tu ndio alikuwa mtu wa mkoa wa pwani waliobaki walikuwa waislam wa kutoka Iringa, mbeya kilimanjaro, mwanza na wachache kutoka Tanga, dar, singida na kigoma. Nilichoona ni kuwa ktk mikoa ya pwani lifestyle na mila na desturi zinawaathiri watoto na hilo liko wazi iwe kwa wakristu au waislam, watoto wa kiislam hulelewa ktk misingi ya kuchukia elimu ya magharibi wakiiambatanisha na ukristo wakati wakristo hawana tatizo hilo. Aidha kuna dada yangu alihamia tandika akiwa na mtoto mdogo lakini kwa mazingira ya tandika ndani ya mwezi mmoja mtoto alibadilika sana kitabia kiasi kwamba ilibidi huyo dada arudi mkoani ili akamlee mtoto mpaka atakapofikisha umri wa kwenda shule ili kumwepusha asitumie muda mwingi kuchanganyikana na watoto wengi ambao matusi ni kama tai.

Mwisho nishauri kuwa kama watu tuna dhamira ya dhati ya kuondoa tofauti kubwa iliyopo kati ya wakristo na waislam pana haja ya kwanza kuyaadress matatizo yanayosababisha hali hiyo. Kuhusu malalamiko ya waislam kuwa waislam wanaonewa ni rahisi tu kuyaondoa, kwanza tujaribu kubalance idadi ya waislam na wakristo ktk maswala ya kusahihisha mitihani, halafu zianzishwe program za chemsha bongo kushindanisha wanafunzi wa shule tofauti zitakazokuwa zinarushwa ktk TVs kama ilivyo kwa Zain Africa challenge, pamoja na kuwapa changamoto wanafunzi na kuwajengea confidence lakini pia kila mtu atakuwa akiona tofauti ilyopo kati ya mwanafunzi anayesoma Marian girls, st. fransis na Mazinde na yule anayesoma kirinjiko, kibohehe na alharamain na pia tutajionea tofauti kati ya wanaosoma serikalini na wanaosoma private schools. Hapo tutakuwa ktk nafasi ya kutambua kama wanafunzi wa kikristo wanajua kweli au wanapendelewa na vilevile tutajua kama wanafunzi hawajui mambo kweli au wanaonewa ktk marking.

Kibona,

Watu hawaendi shule for the sake of going to school. Umetoa mfano kuwa watu waliokwenda nao shule walitoka kilimanjaro, Mbeya Kagera.

Ina maana waKristo wote wanatoka kilimanjaro, Mbeya Kagera. Je Mkristo wa Dodoma asiye na shule, na yeye inabidi ajivunie usomi wa waKristo wa Kilimanjaro, Mbeya Kagera?

Wasukuma ni kabila lenye idadi ya watu wengi Tanzania, je kulikuwa na wasukuma wangapi shuleni kwenu?

Ninaye rafiki yangu hapa kutoka Kagera. Anasema wao wana-IQ kubwa kwa sababu wanakula ndizi. Wakati nakuja kusoma naye hapa hakuwa ni mwenye stellar performance. Lakini kupata scholarship ilibidi asaidiwe na jamaa zake. Na kama kuna fairness asingepata hiyo scholarship.

Na katika kundi nililokuja nalo, 1/3 walikuwa wanatoka Kagera na wote hawakuwa na stellar performance.

Toeni elimu iliyo-fair kuanzia msingi muone kama watindiga, wazinza, wazaramo watashindwa kwenda shule?
 
Kibona,

Watu hawaendi shule for the sake of going to school. Umetoa mfano kuwa watu waliokwenda nao shule walitoka kilimanjaro, Mbeya Kagera.

Ina maana waKristo wote wanatoka kilimanjaro, Mbeya Kagera. Je Mkristo wa Dodoma asiye na shule, na yeye inabidi ajivunie usomi wa waKristo wa Kilimanjaro, Mbeya Kagera?

Wasukuma ni kabila lenye idadi ya watu wengi Tanzania, je kulikuwa na wasukuma wangapi shuleni kwenu?

Ninaye rafiki yangu hapa kutoka Kagera. Anasema wao wana-IQ kubwa kwa sababu wanakula ndizi. Wakati nakuja kusoma naye hapa hakuwa ni mwenye stellar performance. Lakini kupata scholarship ilibidi asaidiwe na jamaa zake. Na kama kuna fairness asingepata hiyo scholarship.

Na katika kundi nililokuja nalo, 1/3 walikuwa wanatoka Kagera na wote hawakuwa na stellar performance.

Toeni elimu iliyo-fair kuanzia msingi muone kama watindiga, wazinza, wazaramo watashindwa kwenda shule?

Zakumi,

..ndiyo maana mimi nasema tatizo siyo namba za mtihani kama wanavyodai "washabiki" wa Prof.Malima.

..tatizo liko ktk quality of education. kuna disparity kubwa kati elimu inayotolewa, say Kagera na ile inayotolewa maeneo ya pembezoni kama Sumbawanga etc etc.
 
Malima alikuwa mdini,alitaka ku inject hiyo aliposhika rungu la wizara katibu wa chama/ccm wakati huo akaliona!
 
Akiwa waziri wa fedha alikwapua fedha kibao za wananchi na kupeleka nje ya nchi (switzland). Halafu aliunda chama chake cha siasa chenye harufu kali ya udini. Inasemekana wakubwa waliiona hiyo na kuandaa mipango ya kuzirejesha fedha hizo nchini. Mungu bariki mipango ilifanikiwa na fedha zote zilirejeshwa BoT. Babu wa watu alipoenda kuchukua hela kiasi ili aendelee na mipango yake ya kuimarisha chama aliambiwa hakuna kitu. Alishikwa na mshtuko mkubwa kiasi cha mwili kushindwa kuhimili. Akakata roho palepale. That's all about Malima.

Ninavyojua Swiss accounts huwa ni za siri, sasa ilikuwaje waka trace pesa na kuruhusiwa kuzitoa?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom