Ukweli usioujua kuhusu uchaguzi wa meya jijini Arusha

Utaratibu unasema theluthi mbili ya wajumbe wawepo (i stand to be corrected),kama hawakushiriki,the whole thing does not make sense whether waliingia wakatoka wakarudi matokeo yakitangazwa,nakubaliana na wewe sheria haiko clear na CCM wanalijua hilo,lakini kwa upande mwingine,unafikiri mahakama ingetoa haki kwenye nchi hii ambapo CCM bado wana say kwenye kila chombo pamoja na mahakama??? Ngoja kuwe na separation/independence ya state organs then muwe na guts za kusema nendeni mahakamani.............i like your analysis though!
Na hilo ndiyo ambalo CCM wanachekelea kwalo, hawana jingine vingivevyo wanajua walishalost.
 
Nimepata nafasi ya kujua kwamba wewe ndie Hiza Tambwe!!! Karibu JF lakini hapa propaganda hazipiti hata kidogo!!!

Tiba
 
baada ya ccm kuchaguana, cdm walipanga kufanya uchaguzi na wao wachaguane na kufungua kesi lkn yote hayo hayakufanyika..kwanini?
unauliza kwa nn hawataki kwenda mahakamani? Unadhani kesi ingechukua mika mingapi? Je kutumia nguvu ya umma siyo njia sasa hihi kama ndiyo kwanini?
 
mzee huyu amefanya utafiti Arusha au alitega sikio,ninachojua ni walialikwa katika semina elekezi wakajikuta peke yao kumbe wenzao wanaendelea na uchaguzi,twambie source of your data mazee tufanyie utafiti au umemsikiliza HIZA TAMBALA MBOVU.
Ripoti ya kamati ya ulinzi na usalama.
 
Nimepata nafasi ya kujua kwamba wewe ndie Hiza Tambwe!!! Karibu JF lakini hapa propaganda hazipiti hata kidogo!!!

Tiba
Nijibu swali moja mkuu hivi ni kwa nini hamtaki kwenda mahakamani badala yake mkahamasisha maandamano japokuwa nakiri maandamano ni haki.
 
Sijatumika na sitatumika ila huo ndiyo ukweli ninaioufahamu. Kama huamini CDM hawawezi kwenda mahakamani mpaka kiama. Ukiona CDM hawaendi mahakamani jua mimi ni mkweli katika hili. Kwamba walitakiwa kukutana Olasiti Garden ni jambo la kushangaza, mimi nafahamu hawa jamaa walikuwa Equator Hotel iliyopo opposite na halmashauri.

Waende mahakama za ccm? Hizi ambazo zinachakachua kesi? Ili wapige danadana hadi 2014? Wachakachue hukumu kama ya kesi ya mzee wa vijisenti??? You must be kidding Zoba ooooo sorry ZOMBA.
 
2/3*32 = 21. Wao walikuwa 17, na CDM walihudhuria kisha wakatoa sasa wamlaumu nani. Hawakutimia kweli lakini walisusia.
Hiv wewe unatumia nin kuweka agument zako! Kwanza umejichanganya kusema walicheza rafu then unasema uchaguzi ulikuwa wa halali. Sasa unakuja na mahesabu ya darasa la kwanza yanayokuonyesha haukua halali mana hawakufikia 2/3. Sasa idad ni waliopiga kura au waliofika ukumbin alafu wakatoka hata bila kujiandikisha? Nin kitakuwa ushahidi kama idad ilifika 2/3? Hebu kaa ufikirie kabla hujapost hapa.
 
Chonde chonde wana chadema. someni alama za nyakati. Kama nilivyowahi kusema huko nyuma chadema wametengeneza uadui na mamlaka inayotawala kwa hiyo wasitarajie mteremko katika mambo yao. Inapofikia unasusa hata sherehe za UHURU wa nchi yetu basi jua matokeo ya baadaye na ujiandae vilivyo.

Msitarajie kuwa watakaokufa na kuumia kwa sababu ya propaganda zenu za kuingia IKULU kwa nguvu na umwagaji damu ni raia wasio na hatia pekee bali hata viongozi , watoto ,wake na au mahawara wao pia yatawapata madhara. Kuweni waangalifu sana na mtii amri/ushauri wa mamlaka inayotawala. Kama kuna mambo hayaendi sawa basi tumieni njia za kistaarabu pamoja na kwenda mahakamani kudai haki. Nabii SULEIMAN alisifika kwa HEKIMA na sio VISASI NA KUSUSA kike kike.

Chonde chonde, japo tunajua wazi kuwa KANISA lipo nyuma
peleka us huko, uhuru wa nchi ipi? Tanzania , Tanganyika au Zanzibar, cdm iko mbele ya kanisa, ccm, cuf iko nyuma kwako
 
Hahaaaa, sidhani kama kweli huo ndio utaratibu, maana ya column ni nini? ni sahihi za watu au watu kuwa pale physically? Je mjumbe anayefika kikaoni na mjumbe anayetoa udhuru kuwa hawezi kuja, ni sawasawa? Nadhani maana ya column kufikia ni watu kuwa pale physically na sio kutoa uzuru na kisha uzuru huo kutumika kama ndio column, nonsense.

La pili, ni mahakama ya nani hiyo unayopeleka hiyo kesi yako? Kesi ya Nyani unaipeleka kwa Ngedele? Si tumeona Mahakama ya Rufaa juzijuzi tu hapa inashindwa kutoa mwelekeo wa Mgombea Binafsi? Kwa vile Chadema ni chama makini, kwa hahika wanajua kuwa Kesi zote ziendazo mahakamani, tena hizi za kisiasa, zitakula kwao ndiyo maana wanatumia njia muafaka. Tunisia si tumeona? Kazi kwetu.
 
Ni kama vile umetoka kunywa maniii na kuja kuandika upuuzi wako hapa. Hunajipya ww kaa kimya.
Duuh ndugu yangu umepinda kinoma lakini haina noma. Hivi ukikuta home jamaa wamekuuibia kisha ukapata ushahidi aliyeniibia ni mzee wa Rula utanichekea au kuitisha maandamano ili nikamatwe?
 
Nijibu swali moja mkuu hivi ni kwa nini hamtaki kwenda mahakamani badala yake mkahamasisha maandamano japokuwa nakiri maandamano ni haki.

NO NEED TO HIRE A LAWYER if you can buy a judge brother!!!!!!!!!!! CCM bought a judge already
 
Duuh ndugu yangu umepinda kinoma lakini haina noma. Hivi ukikuta home jamaa wamekuuibia kisha ukapata ushahidi aliyeniibia ni mzee wa Rula utanichekea au kuitisha maandamano ili nikamatwe?
kama ni mimi, nitachukua mshale, shoka, na panga nakukufata..
 
Hahaaaa, sidhani kama kweli huo ndio utaratibu, maana ya column ni nini? ni sahihi za watu au watu kuwa pale physically? Je mjumbe anayefika kikaoni na mjumbe anayetoa udhuru kuwa hawezi kuja, ni sawasawa? Nadhani maana ya column kufikia ni watu kuwa pale physically na sio kutoa uzuru na kisha uzuru huo kutumika kama ndio column, nonsense.

La pili, ni mahakama ya nani hiyo unayopeleka hiyo kesi yako? Kesi ya Nyani unaipeleka kwa Ngedele? Si tumeona Mahakama ya Rufaa juzijuzi tu hapa inashindwa kutoa mwelekeo wa Mgombea Binafsi? Kwa vile Chadema ni chama makini, kwa hahika wanajua kuwa Kesi zote ziendazo mahakamani, tena hizi za kisiasa, zitakula kwao ndiyo maana wanatumia njia muafaka. Tunisia si tumeona? Kazi kwetu.
Mbona kesi ya jimbo la Segerea imekwenda mahakamani! Wangeenda kisha wakatumia nguvu kubwa kushinikiza isikiliswe haraka, usudhani majaji wanapenda kuharibu weledi wao kijinga jinga.
kuhusu column hilo ni kuwepo physically, sasa jamaa wameundiwa zengwe kuwa walisusia uchaguzi lakini ukweli walikuwa nje wanajipanga. Ni ukiangalia hauwa umepita muda mrefu tangu wabunge wa CDM wasusie hutuba ya JK.
 
Wana JF najua ni wengi wanajiuliza maswali mengi juu ya uhalali wa uchaguzi wa meya wa jiji la Arusha ambao umekuwa mjadala mpaka leo. Swali wengi wanalojiuliza je uchaguzi ulikuwa halali au si halali?
Nataka niweke wazi uchaguzi ule ulikuwa halali kabisa na taratibu zilifuatwa kabisa. Kabla ya uchaguzi kufanyika kulikuwa na utata wa mjumbe mmoja wa CCM Mary Chitanda kupiga kura kwa sababu yeye si mwakilishi wa mkoa wa Arusha. Yeye ni katibu wa CCM mkoa wa Arusha lakini kwa sasa yeye ni mbunge wa viti maalum mkoani Tanga. CCM ilikuwa na wajumbe 15 ie madiwani na huyo mwenye utata 1 jumla ni 16. CDM ilikuwa na wajumbe 14 pamoja na G. Lema mbunge.
Utata huu ulipelekea kuomba ufafanuzi, na ufafanuzi ulipatikana kuwa mjumbe yule yaani Mary Chitanda alikuwa halali kwa maandishi na siyo mdomo kwa vyama vyote, hiyo ilikuwa siku ya pili baada ya kuahirisha uchaguzi jana yake.
Hilo ndiyo jambo kuu lilikuwa likibishaniwa. Sasa endapo jambo hili lilipatiwa ufumbuzi kwa maandishi inakuwaje leo hii viongozi wa CDM waendeleze malumbano jukwaani?
Ni jambo lisilofichika kwa nini Mary Chitanda asiende kupiga kura Tanga badala yake Arusha. Hilo ndilo suala la msingi kabisa lakini majibu yake vile vile kisheria hakuna kipengele kinachomkataza kupiga kura kwani bado ni kiongozi wa wanaCCM Arusha, na kuzingatia sheria haimbani CCM wakaonelea basi ni vema wakaitumia loopwhole hiyo.
Tuachane na ubishi kama sheria haimkabi basi CDM hawana haja ya malumbano. Machoni pa watu itaonekana si halali lakini mbele ya sheria inaonekana sawa. Katika uchaguzi wa urais hakuna mahakama yenye uwezo wa kutengua mara baada ya matokeo kutangazwa na tume ya uchaguzi. Hapa tunajifunza mapungufu ya sheria zetu za bongo. Hili ni jambo lisilopingika kabisa na kwa hili linahitaji mabadiliko.
Uchaaguzi umekwisha na meya keshapatikana sasa kama sheria zilikikwa basi tukapate haki yetu mahakamani na siyo kwa mashinikizo ya jukwaani.
CDM ni chama makini lakini kimepotoka kwa hili kwa ndiyo maana yake hawataki kwenda mahakamani kwa sababu wanajua hawana jipya. Kinachofanyika saizi ni propaganga ya sintofahamu ya tukio hili kwa wananchi!
Ni kweli mara baada ya kupewa taarifa ya uhalali wa Mary Chitanda CDM walitoka nje kujadili wakawaacha wajumbe wengine 17 wakiwa ndani na kipindi hicho walishasaini tayari column ya mahudhurio! Ilipoonekana wamechelewa kurudi CCM hapo ndipo walipocheza rafu kwa kuendesha uchaguzi kwani tayari walikuwa na sababu zote za kushinda kesi. Sijui ni daftari au niiteje umesaini, kisha umetoka nje kujadili basi jamaa wakaendelea ndani na uchaguzi. CDM walishituka pindi matokeo yanatangazwa na kuja ukumbini wakiongozwa na mbunge wao Lema wakaambiwa nyie si MMESUSIA uchaguzi basi endeleeni ila viongozi wamepatikana.
Huo ndiyo ukweli wa uchaguzi wa meya Arusha.
Kwa kuwa ukweli huu umejificha kauli nyingi za kulaani zilitokea na kuzidi hasa baada ya maandamano kuzuiliwa na kupeleka vifo.
Kauli za kiburi toka kwa viongozi wa CCM akiwemo Makamba zikaamsha hisia kali. CCM ni kama walikuwa wanawakebehi CDM kwa sababu walijua hawana pa kushika mahakamani na ndiyo maana wanawashinikiza viongozi wa CDM waande huko ili haki ijulikane.
Usichokijua ni hiki, kwa nini wasiende mahakamani wafungue kesi kisha waitishe maandamano ili kushinikiza haki ya kusikilizwa kesi upesi. Kukataa kwao kwa kisingizio mahakama haitatenda haki kunatilisha mashaka na waelewe kuwa mashinikizo yao hayana direct impact badala yake yanawapa changamoto viongozi wa CCM.
Mwisho naalani kwa kauli moja kuwa nguvu iliyotumika kuzima maandamano yale ilikuwa kubwa mno na viongozi wetu wa serikali waache kutumika kisiasa. La Arusha latosha kuwa funzo.
Kikwete zlisema tukio la Arusha ndiyo mwanzo na mwisho naomba iwe kweli ingawaje nasikia Mbeya vijana wake wamekwisha ua tena!!!
MD usiichangane na thread yoyote ile, iweke ili watu wajue na ku challange pale wanapoona siyo sahihi.

Vyovyote utakavyoandika, Lowassa hayupo tayari kuona CHADEMA wanatawala Arusha, itakua ni mwisho wa miradi yake ya kifisadi....
 
wana jf najua ni wengi wanajiuliza maswali mengi juu ya uhalali wa uchaguzi wa meya wa jiji la arusha ambao umekuwa mjadala mpaka leo. Swali wengi wanalojiuliza je uchaguzi ulikuwa halali au si halali?
Nataka niweke wazi uchaguzi ule ulikuwa halali kabisa na taratibu zilifuatwa kabisa. Kabla ya uchaguzi kufanyika kulikuwa na utata wa mjumbe mmoja wa ccm mary chitanda kupiga kura kwa sababu yeye si mwakilishi wa mkoa wa arusha. yeye ni katibu wa ccm mkoa wa arusha lakini kwa sasa yeye ni mbunge wa viti maalum mkoani tanga. Ccm ilikuwa na wajumbe 15 ie madiwani na huyo mwenye utata 1 jumla ni 16. Cdm ilikuwa na wajumbe 14 pamoja na g. Lema mbunge.
Utata huu ulipelekea kuomba ufafanuzi, na ufafanuzi ulipatikana kuwa mjumbe yule yaani mary chitanda alikuwa halali kwa maandishi na siyo mdomo kwa vyama vyote, hiyo ilikuwa siku ya pili baada ya kuahirisha uchaguzi jana yake.
Hilo ndiyo jambo kuu lilikuwa likibishaniwa. Sasa endapo jambo hili lilipatiwa ufumbuzi kwa maandishi inakuwaje leo hii viongozi wa cdm waendeleze malumbano jukwaani?
Ni jambo lisilofichika kwa nini mary chitanda asiende kupiga kura tanga badala yake arusha. Hilo ndilo suala la msingi kabisa lakini majibu yake vile vile kisheria hakuna kipengele kinachomkataza kupiga kura kwani bado ni kiongozi wa wanaccm arusha, na kuzingatia sheria haimbani ccm wakaonelea basi ni vema wakaitumia loopwhole hiyo.
Tuachane na ubishi kama sheria haimkabi basi cdm hawana haja ya malumbano. Machoni pa watu itaonekana si halali lakini mbele ya sheria inaonekana sawa. Katika uchaguzi wa urais hakuna mahakama yenye uwezo wa kutengua mara baada ya matokeo kutangazwa na tume ya uchaguzi. Hapa tunajifunza mapungufu ya sheria zetu za bongo. Hili ni jambo lisilopingika kabisa na kwa hili linahitaji mabadiliko.
Uchaaguzi umekwisha na meya keshapatikana sasa kama sheria zilikikwa basi tukapate haki yetu mahakamani na siyo kwa mashinikizo ya jukwaani.
Cdm ni chama makini lakini kimepotoka kwa hili kwa ndiyo maana yake hawataki kwenda mahakamani kwa sababu wanajua hawana jipya. Kinachofanyika saizi ni propaganga ya sintofahamu ya tukio hili kwa wananchi!
Ni kweli mara baada ya kupewa taarifa ya uhalali wa mary chitanda cdm walitoka nje kujadili wakawaacha wajumbe wengine 17 wakiwa ndani na kipindi hicho walishasaini tayari column ya mahudhurio! Ilipoonekana wamechelewa kurudi ccm hapo ndipo walipocheza rafu kwa kuendesha uchaguzi kwani tayari walikuwa na sababu zote za kushinda kesi. Sijui ni daftari au niiteje umesaini, kisha umetoka nje kujadili basi jamaa wakaendelea ndani na uchaguzi. Cdm walishituka pindi matokeo yanatangazwa na kuja ukumbini wakiongozwa na mbunge wao lema wakaambiwa nyie si mmesusia uchaguzi basi endeleeni ila viongozi wamepatikana.
Huo ndiyo ukweli wa uchaguzi wa meya arusha.
Kwa kuwa ukweli huu umejificha kauli nyingi za kulaani zilitokea na kuzidi hasa baada ya maandamano kuzuiliwa na kupeleka vifo.
Kauli za kiburi toka kwa viongozi wa ccm akiwemo makamba zikaamsha hisia kali. Ccm ni kama walikuwa wanawakebehi cdm kwa sababu walijua hawana pa kushika mahakamani na ndiyo maana wanawashinikiza viongozi wa cdm waande huko ili haki ijulikane.
Usichokijua ni hiki, kwa nini wasiende mahakamani wafungue kesi kisha waitishe maandamano ili kushinikiza haki ya kusikilizwa kesi upesi. Kukataa kwao kwa kisingizio mahakama haitatenda haki kunatilisha mashaka na waelewe kuwa mashinikizo yao hayana direct impact badala yake yanawapa changamoto viongozi wa ccm.
mwisho naalani kwa kauli moja kuwa nguvu iliyotumika kuzima maandamano yale ilikuwa kubwa mno na viongozi wetu wa serikali waache kutumika kisiasa. La arusha latosha kuwa funzo.
Kikwete zlisema tukio la arusha ndiyo mwanzo na mwisho naomba iwe kweli ingawaje nasikia mbeya vijana wake wamekwisha ua tena!!!
Md usiichangane na thread yoyote ile, iweke ili watu wajue na ku challange pale wanapoona siyo sahihi.

mnahangaika kwa sasa baada ya kuona nguvu ya umma inatisha wauaji wakubwa nyie, kama ccm walikuwa wanajua wanakura za kutosha kwanini mizengwe namna hiyo???? Nyie mkubali tu wauaji na kama kuua tafuteni makontena ya risasi manake nguvu ya umma itaunguruma kila siku mtatetea mpaka mtashindwa -mlizoea watanzania ni vichwa vya wendawazimu lakini watanzania wameamuka. Kuna nini arusha??? Mpaka mnaua ili kupata meya??? Wewe mzee wa rula utakuwa rula kweli kwa kasi ya nguvu ya umma.
 
Back
Top Bottom