Ukweli ni upi kuhusu Oscar Kambona?

Wimbo huu tuliuimba sana tukiwa shule ya msingi, na baadaye hata JKT tukiwa kwenye zile zilizoitwa "ruti machi":
"Kambona aliagiza
Chipaka na Kamaliza,
Pindueni mkiweza,
Nitawapeni mapesa,
Nikitoka safarini Uingereza!"


Ndicho tulichofundishwa kuhusu Kambona. Naye pia alisababisha ionekane kuwa huo ndio uliokuwa ukweli (au labda ni kweli ndo ukweli wenyewe huo), kwani kipindi fulani (sikumbuki mwaka gani), ndege ilidondosha vipeperushi vyenye ujumbe kutoka kwa Kambona vikihimiza wananchi waigomee serikali ya Nyerere. Ilikuwa sikukuu sikumbuki sabasaba au nyingine, lakini baba yangu aliokota kimoja na hadi leo kipo nyumbani nimekihifadhi. Ukisoma kipeperushi hicho, kinaashiria alishawahi kudondosha vingine pia siku za nyuma, kwani ndani yake anadai kuwa Nyerere ni mwoga tu anayekimbia kivuli, kwani yeye (Kambona) angetaka kupindua nchi angelipua tu uwanja ambako Nyerere na kabineti yake walikuwa wanatazama ngoma za kienyeji kwenye sherehe ya uhuru siku alipodondosha vipeperushi vingine mbele yake kwa ndege bila kuguswa na mtu! Ati anadai Nyerere alikuwa anashangaa tu wakati watu wanagombea kuokota vipeperushi vya Kambona mbele yake! Kwenye hicho kipeperushi nilichotunza kuna picha ya Nyerere ameshika kichwa, chini yake kuna maneno "Jamani naomba msaada, mambo yamenizidi kimo". Mwisho wa kipeperushi kuna picha ya Kambona na maandishi "Ushindi kwa wananchi" na saini yake Oscar S. Kambona.

Hizo ndizo kumbukumbu nilizonazo kuhusu huyu aliyejiita wakati huo (alipokuwa mkimbizi), "mkombozi" Oscar Kambona.
 
Katika ku-balance story, msije hangaika kumuuliza Kawawa; huyu hajawahi kuwa na mawazo yake mwenyewe tangu nianze kumsikiliza. Atakachowaeleza ni hayohayo ya Nyerere ambayo tayari mnayajua.
Nimesoma ile article mara kibao, sijaona hata chembe ya chumvi. Alichofanya yule mwandishi ni kusimulia kile ambacho hakijawahi kusimuliwa.

Lazima tukiri kwamba pamoja na mazuri ya mzee wetu Nyerere, ndani ya nguo zake alikuwa ni mtu hatari sana hasa katika kuwafanya wanasiasa wenzake waonekana ovyo mbele ya jamii. communist style. Unakumbuka jinsi Amini alivyochafuliwa: mla watu, alionyeshwa akibeba nyama za watu na huku inzi wakimzonga, lakini wote sasa tunajuwa kwamba pamoja na ubaya wa Amini hakufikia kiwango cha kubeba nyama za watu kwenye mzegazega, huo ulikuwa ni umafia aliofanyiwa.

Pamoja na mapenzi yangu kwa Nyerere, nasikitika kwamba huyu mzee alijaribu kwa mafanikio makubwa kuua kila kipaji cha mtu yeyote mwingine aliyeibuka. As a result, yeye peke yake mpaka leo anaonekana ndiye aliyekuwa hero. Lakini sote tunajua ukweli kwamba isingewezekana yeye tu peke yake alete mazuri. Sasa swali la kujiuliza hao wengine walikuwa akina na nani na kwa nini hatuwajui?
 
Kitila, wewe naona ndo uko balanced zaidi hapa kuliko huyo "Nyerere Impostor"....

Nimefurahi hichi kipande cha Kawawa! Nimecheka sana. Dizaini jamaa alikuwa Yes Man wa Nyerere.

Halafu sikujua. Inavyoonekana kulikuwa na propaganda machine kabambe sana iliyokuwa na lengo moja tu nalo ni kumchafulia jina kabisa Idi Amin kama vile halikuwa halijachafuka bado(I still hate him with a passion, though)

Halafu kama sote tunakubaliana kwamba Nyerere naye alikuwa binadamu mwenye mapungufu kama sisi wote, kwa nini baadhi ya watu inakuwa vigumu kwao kuamini kwamba yeye hakupenda mtu yoyote kum-overshadow. Kwa kawaida binadamu wengi tuko territorial sana.
 
STORY HAS IT THAT ..hata sokoine was silenced by power brokers kutokana na style yake iliyo mu overshadow mwalimu..though hilo mwalimu halikumsumbua kwa kuwa tayari alitaka kuondoka..watu kama kawawa na msuya waliokuwa wakitegemea wamrithi nyerere wali m fix sokoine...

PIA NA HILI TUWAULIZE HAWA..anyway nchi nyingi wana utaratibu wa kuziweka archives za SECRET SERVICE na mambo mengine nyeti wazi for PUBLIC CONSUMPTION baada ya kipindi fulani..mfano marekani MAFAILI mengi ya siri ya miaka ya 60 yako wazi ..ili historia iwekwe sawa..hata hapo kenya baadhi ya taarifa za siri za serikali ya KENYATTA zimeanza kuwekwa wazi kwa awamu..na kuna kipindi NATION walitoa series ya baadhi ya taarifa.....utashangaa hadi leo kwetu mambo kama kifo cha karume[na uwaji wake wa watu kama hanga ]...ets bado ni kitendawili..ni udhaifu wa waandishi wetu au..?
 
Wanabodi,

Mimi nimekaa nje kwa muda nikiyasoma mawazo ya watu humu lakini yaonyesha wazi kuwa watu mnaanza kuamini ovyo habari ambazo zimetungwa na kufukizwa udi. nachowaomba someni Historia ya TANU na hasa zile zilizoandikwa kuhusu kina Sykes, Fundikira, Mwapachu na Nyerere utaona kuwa habari hii inapingana sana na maelezo yaliyokwisha tangulia.

Yaonyesha wazi siku hizi kwa sababu Wadanganyika ni wepesi wa kusahahu basi kila mtu anataka kudai kuwa bila yeye TANU ama Nyerere asingekuwa rais na kumfanya Nyerere kuonekana bingwa kuwashinda Watanzania wote akili. Mimi nachosema Nyerer alikuwa mtu mmoja haiwezekani kabisa huyu mtu akaweza kututawala sote nje kabisa ya matakwa ya wengi laa sivyo basi WAJINGA tulikuwa sisi na sio Nyerere aliyetuburuta mchangani tukafuata.

Ukisoma historia ya Kambona utakuta kila sehemu alozungumzia ilifanyika hivyo. Ni sera ya chama kujitangaza kwa hiyo kila mkoa alichaguliwa mtu kuongoza upatikanaji wa membership ili kujiandaa na Uchaguzi mkuu. Kambona alikikuta chama tayari kimesimama imara na wanachama wake waanzilishi walosoma kuliko yeye.

Hata madai ya kuwa chama kilikuwa hakina mpangilio nashindwa kabisa kuamini wakati yeye kawakuta wasomi tayari ndani ya chama hicho na ajabu ni kwamba nimesoma vitabu vingi vinavyohusiana na watu waliochangia kuzaliwa kwa TANU, Kambona ni mtu wa mwisho kabisa kutajwa. Hawa ni watu mbali mbali waliokuwepo ama kushiriki kikamilifu ktk kukijenga chama tena basi wengi walishangaa Kambona kupewa nafasi ile wakisema zilikuwa njama za Nyerere kuhakikisha anaweka watu aliowaona kuwa ni Yes Sir - wazembe.

Haya tazama sasa tumefikia hata habari za Idd Amin, hivi kweli miaka ya 1980 kulikuwepo na video zinazoonyesha Idd Amin akila watu?.. na kama kweli waliweza vipi kuzipiga hizo video kiasi kwamba nyie mliweza kuamini kuwa huyo mtu alikuwa Idd Amin na nyama za watu hadi hivi majuzi ndio mmekuja fahamu ulikuwa Uongo. Na ikiwa mliweza kuamini yale siwezi kushangaa kama mnaweza amini haya pia.

Nyerere alikuwa kiongozi wetu ambaye ktk uongozi wake kuna maamuzi mengi aliyafanya ambayo hayakuwa mazuri, kama tulivyokwisha kubaliana kuwa Nyerere alikuwa binadamu mwenye kuipenda nchi yake na pengine kuwa baba mwenye wivu. Makosa ya phapa na pale yapo mengi tu lakini mtu kama Kambona sina haja kabisa ya kumsikiliza kwani mpigania haki wa kweli kamwe hawezi kukimbia nchi! wenye uchungu na Uzalendo wengi huingia msituni.

Nachofahamu mimi Kambona alipokimbiliak London aliwahi ku win Lotto ya Uingereza ndipo utajiri wake ulipotokea.. hizi habari nyingine nazikuja zisikia hapa..
 
Nyani Ngabu,
Sina ushahidi hapa ila jaribu kuwasiliana na watu waliokuwa UK muda mrefu watakwambia vizuri maanake habari hizo tulizipata miaka ilee ya 277. Na kama unavyofahamu kuhusu Lotto ni jambo la kawaida kabisa mtu kushinda mamillioni.
 
Philemon Mikael said:
STORY HAS IT THAT ..hata sokoine was silenced by power brokers kutokana na style yake iliyo mu overshadow mwalimu..though hilo mwalimu halikumsumbua kwa kuwa tayari alitaka kuondoka..watu kama kawawa na msuya waliokuwa wakitegemea wamrithi nyerere wali m fix sokoine...

1.Kawawa na Msuya hawakuwa na influence na Usalama wa Taifa kiasi cha kuweza kutekeleza mpango wa kumuua Waziri Mkuu wa Tanzania, Edward Sokoine.

2.Katika masuala ya kiimla-imla kama Operesheni Vijiji vya Ujamaa, na kampeni dhidi ya Wahujumu, Mwalimu aliwaachia wasaidizi wake, Waziri Mkuu, kutekeleza kampeni hizo. He would usually set the tone[.."hakuna lingine ila kuwashughulikia maadui wa ndani"] na kuachia implementation kwa wengine.

3.Hali hiyo ilimfanya Mwalimu akwepe lawama pale mambo yanapoharibika. Labda mfumo wetu wa Uongozi[Raisi vs Waziri Mkuu] unamkinga Raisi kutokana na utekelezaji wa maamuzi ya serikali yake. Nadhani hiyo ndiyo sababu Mawaziri Wakuu kubomoka kisiasa Tanzania.

Kitila Mkumbo,
Kuhusu Mzee Kawawa kwa kweli umeshindilia msumari utosini. Kawawa alifikia mpaka kuiga msisitizo wa Mwalimu wakati akitoa hotuba. Kawawa alikuwa akisema "NDIYO...NDIYO" ktk hotuba zake kama Mwalimu Nyerere.
 
hold on a minute... sikuona hii ina maana kuna mtu alishawahi kuwa na "orodha ya mafisadi" na akapewa uwanja kumwaga madhambi ya Nyerere na Mwalimu mwenyewe alikuwa hai wakati huo akashindwa? Au alitishiwa kufungwa tena?

kumbukumbu zangu zinasema (naweza kuwa siko sahihi) pale jangwani kambona alimshutumu sana mwalimu kuhusu "ufisadi". kambona aliambiwa afute shutuma zake la sivyo atapelekwa mahakamani. hakufanya hivyo na mahakamani hakupelekwa. jee ni the same song being played today wapinzani na orodha ya mafisadi na kutishiwa kupelejwa mahakamani...
 
Hekaheka za kuanzisha vijiji vya ujamaa, jambo tulilojaribu kuiga kutoka uchina utekelezaji ulikuwa mbovu maana watu walihamishwa kiholela matokeo yake kukatokea njaa ya 1974 tukaishia kupanga foleni za unga wa yanga na kuimbishwa nyimbo za "kilimo cha kufa na kupona"...
 
heshima mkuu, mengi uliyosema nakubaliana nayo. hata hivyo kuna machache ambayo naweza toa mtazamo wangu

Mwandishi wa makala hiyo kuibalance angeweza kabisa kwenda kufanya interview na watu wengine ambao wanahusika katika hii issue. Kuna watu wapo waulizwe, aulizwe Malecela, aulizwe Kawawa, wapo viongozi wanaojua historia yetu kwanini inaogopwa kuulizwa? Kwanini maneno ya Kambona yachukuliwe kama msaafu kamili?

jee mutaamini atayosema mzee malecela hususan akiunga mkono mazuri yanayosemwa kuhusu kambona? isije ikawa watu wakasema anachuki kwa maana na yeye dhoruba aimeipata



Kuna mambo kadhaa ambayo ni ya kweli (facts)

d. Kambona baada ya kutangazwa Azimio la Arusha aliondoka Tanzania na kwenda kuishi Uingereza akijipa uhamisho. That is a fact..

je ni kweli alikimbia azimio la arusha au kuna zaidi ya azimio?

e. Wakati vyama vingi vimeanza Kambona alirudi nyumbani na kujaribu kuwasha moto aliodhania kauacha. Haukuwaka. That is a fact.

binafsi nadhani hapa kambona alifanya kosa la kimkakati. yeye aliamini kabisa umaarufu aliokuwa nao wakati akiondoka bado upo akasahau nguvu ya propaganda iliyofanywa kummaliza kisiasa. kizazi alichokikuta "active" ni kile ambacho kiliishaimbishwa nyimbo kuhusu ubaya wa kambona bila kujua upande wa pili washilingi. matokeo yake ni ndio huko unakokuita kudoda

Nasikitika kuwa hakuna mtu aliyepata nafasi ya kumuuliza Mwalimu "what happened to Kambona and why did you exile him". Hata hivyo wapo watu wanalojua jibu hilo ndio maana nimesema "waulizwe". Kwanini hamtaki hilo?

kweli hili ni bahati mbaya. lakini usisahau pia wapo ndugu wa kambona ambao nao walipata kibano kwa kuwa tuu walikuwa na uhusiano na kambona. wanaweza tafutwa na kuulizwa pia
 
kumbukumbu zangu zinasema (naweza kuwa siko sahihi) pale jangwani kambona alimshutumu sana mwalimu kuhusu "ufisadi". kambona aliambiwa afute shutuma zake la sivyo atapelekwa mahakamani. hakufanya hivyo na mahakamani hakupelekwa. jee ni the same song being played today wapinzani na orodha ya mafisadi na kutishiwa kupelejwa mahakamani...

alitoa shutuma gani dhidi ya Mwalimu?
 
Kuna JF member moja kasema ati watu walizuiwa kuagiza magari madogo, hili sio kweli. Ukweli ni kwamba kodi ya magari madogo ilikuwa ni kubwa sana kiasi kwamba wenye uwezo wa kufanya hivyo walikuwa watanzania wachache sana. Mimi nawafahamu wachache ambao waliweza kulipia na kuwa na hayo magari. Mwenye hiyo sheria kama ilikuwepo atuwekee hapa.

Swala jingine ni la passport, kweli zilikuwa zinatolewa tu kama unasababu ya msingi ya kusafiri nje ya nchi na wengi walikuwa wanapata lakini ukija kuomba na ukaonekana huna sababu ya msingi ulikuwa hupati kutokana na vijana wengi hasa miaka chini ya 25 waliopoteza maisha yao kwa kuzamia meli. Wengi waliweza kupata kwa njia moja au nyingine, nakumbuka wakati ule vijana wengi walikuwa wanakwenda buja na kuleta mashati ya juliana n.k. wakati ule kusafiri kwa ndege ilibidi utume maombi benki kuu ili uweze kupata foreign currency, hili lilikuwa kuanzia mwaka 1978 kama sikosei na sio kipindi chote ambacho mchonga alikuwa madarakani. Vile vile lazima kupata muhuri wa customs wakati ule kuomyesha kwamba unalipa kodi (matatizo mengi ya wakati huo ilikuwa ni pamoja na kuvunjika kwa jumuiya ya Afrika mashariki 1977, vita ya Iddi Amin iliyokuwapo 1978 kama sikosei n.k) Nyerere alipohutuba taifa alisema tufunge mkanda kwa miezi 18. wengi walitafsiri alimaanisha miaka 18.

Mwalimu hakupenda watanzania wasome - Kama ni kweli wengi tu tusingeweza kuwa hapa tulipo, shule za dini zilitaifishwa ili WTZ wasiende shule - MAKUBWA HAYA. Siye yeye aliyeanzisha hata elimu ya ngumbaru?

Njia kuu za uchumi kumilikiwa na serikali - Huu ndio ulikuwa msingi wakati ule na nakumbuka mabasi ya Kamata, Shirika la reli mabasi yake tuliyabatiza rab na mikoani kulikuwa na mabasi kama vile KAUDO kule Dodoma, UDA Dar es Salaam n.k.

MAFUTA HAYAKUUZWA JUMAPILI - Wakati wa vita ya nduli utumiaji wa mafuta ulikuwa ni mkubwa na jambo lililokubaliwa ni kubana matumizi ya mafuta na kupunguza gharama, hivyo iliamuliwa magari yasitembee siku za jumapili kuanzia saa saba mchana isipokuwa teksi na kwa shughuli muhimu kama dharura imetokea, sasa nalo hili unapoamua kubana matumizi ni lazima ufikirie ufanye nini, Je lilifanikiwa? wenye takwimu watupatie. Mwalimu alikuwa kiongozi kwa miaka takriban 23 katika hiyo alipata mafanikio makubwa katika nyanja za nyumbani na ugenini. Jukumu lake lilikuwa kuongoza.

Kambona sikuona mafanikio aliyoleta Tanzania, kama kuna vitabu ameandika wanaofahamu watujulishe huenda tukavisoma.
 
Wanabodi,

...lakini mtu kama Kambona sina haja kabisa ya kumsikiliza kwani mpigania haki wa kweli kamwe hawezi kukimbia nchi! wenye uchungu na Uzalendo wengi huingia msituni...

heshima mkuu.
nadhani wapo wanamapinduzi wa kweli waliokimbia nchi zao bila kuingia mstuni. mzee utakuwa huwatendei haki kwa kusema kwamba kwa vile hawakuingia msituni basi hawana uchungu na wala si wazalendo. wanamapinduzi wa aina hii huamini katika njia nyingine za mapambano kuliko ile ya msituni. wamefanikiwa au la hilo ni kitu kingine, lakini uchungu wanao.
 
sijui kama nasoma/naelewa vyema thread hii inakoelekea. naona kama kuna baadhi wanaamini lengo ni kutothamini mchango mkubwa wa mwalimu (kama nimekosea naomba radhi), la hasha.

nadahani lengo ni kuleta hadharani upande wa pili wa historia ya kambona ambayo wengi wetu tulikuwa hatuijui.
 
Kafara, kuna kitu ambacho ni chuki dhidi ya Mwalimu. Chuki ambayo inajificha katika kubalance "mazuri ya Mwalimu". Nitakuwa mwongo mkubwa nikisema Mwalimu hakufanya makosa ya uongozi au kimkakati. Kwa kiongozi kijana ambaye hakuwa na uzoefu wa aina yoyote hata yeye mwenyewe alikiri na ninakuu "kwani sisi Miungu bwana, lazima tulifanya makosa; tumepewa taifa tu hatuna hiki wala lile; kuna mazuri tuliyoyafanya na kuna mabaya tuliyoyafanya; jukumu la awamu zinazofuata ni kuyaacha mabaya na kushikilia mazuri. Tatizo hawa wanaacha mabaya na mazuri pia!" Uwanja wa Sokoine 1995.

Sasa, kuna makosa yalifanywa? absolutely? kuna maamuzi ambayo asingechukua absolutely. I'm no fool ninaelewa limitations za wanadamu na madhaifu yao. Ninaelewa hofu za viongozi na hasa wale watawala walioanza kutawala miaka ya vita baridi. Lakini any attempt to demonize Mwalimu for his human failures or his strategic miscalculations would prove to be futile.

In an open forum, or a public arena of ideas, ukweli lazima ujulikane. The only way to find out is to carry academic study or an learned research on the first 10 years of independence. Tunavyo vyuo vikuu na tunawatu wanaitwa "wasomi"... why not carry a balanced, fair, independent and transparent study on Mwalimu and the Exiles? what really happened and what didn't happen? Kwa sababu kama kweli Kambona, Babu na wengine walitendewa vile walivyotendewa waliporudi walikuwa na uwezo wa kuandika au kusema kilichotokea, they never did except zile hadithi za myths na legends zao.. on this one I'm still skeptic.

I'm skeptic si kwa sababu ya mapenzi yangu kwa Mwalimu, la hasha. I'm skeptic kwa sababu that is the nature of any fair minded person. Kwa sababu nisivyokubali kuwa Mwalimu hakuwa na makosa yoyote ndivyo hivyo hivyo sijashawishika kukubali mabaya anayorundikiwa.
 
mwkjj,

kama binadamu mwalimu wapo wale aliowakwaza aidha kutokana na udhaifu wake binafsi au kwa kupotoshwa na vyombo vya dola. hivyo naamini kabisa watakuwepo walionachuki dhidi yake. huo ni ubinadamu.

hata hivyo itakuwa si haki kujaribu kufumba macho na kujidai kutoona mengi mazuri ambayo mwalimu ameyafanyia nchi yetu. hivyo uliyosema mengi kuhusu yaliyomsibu mwalimu wakati akichukua nchi na kuteleza kwake/kwao naafiki kabisa.

bahati mbaya sidhani kama kuna kumbukumbu za kimaandishi nyingi kuhusu kambona. sina hakika kama kambona aliandika kitabu kuhusu mchango wa watu mbali mbali wakati wa harakati za uhuru. na naamini huu ni udhaifu mkubwa kwa wanasiasa wetu (hili lilishazungumzwa sana kwenye hii forum, na nadhani fmes aliashiria kuwa anamhamasisha mmoja wa wazee vingungwe wa siasa za tanzania kuandika).

katika hali hii nadhani utafiti wa "kisomi" kuhusu kambona na wengine itabidi kukubali kuanzia kwenye simulizi.

nje ya mada: jee unakumbuka kuna wakati kulikuwa na madai ya picha ya awali ya uongozi wa kwanza wa tanu kuwa "doctored?" kuna mzee (simkumbuki jina)alikuwa amefutwa! ndo siasa hizo
 
Naona mjadala unapamba moto lakini tunasahau kwamba zama za Nyerere kila kitu kilikuwa kinafanyika kwa malengo maalum. Lengo la Nyerere zama hizo ilikuwa ni kuhakikisha kwamba jamii inamkubali yeye na kila kitu anachokianzisha. Mifano michache ya kuonyesha jinsi watanzania tulivyokuwa tunaaminishwa na kupewa vitu vya upande mmoja tu ni kama hii:

Moja, mitaala ya shule za msingi na sekondari ya masomo ya historia na siasa viliandaliwa kwa kuangalia serikali na chama (TANU & ASP na CCM) wanataka nini. Tulikaririshwa imani za chama (TANU na CCM) na vikao vya chama. Tulifundishwa katiba ya CCM, wakati katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo ni muhimu sana mtu aijue hatukufundishwa. Kwa hiyo hata vitabu vya siasa na historia ya TANU viliandikwa kwa mtazamo huo huo wa kumuonyesha Nyerere kama hero na ndiyo maana wengine waliochangia, michango yao haionekani kama ni mikubwa sana kuliko mchango wa Nyerere. Kwa hiyo ninachokifikiria mimi ni kwamba tukitumia vitabu vya historia vilivyoandaliwa na makada wa TANU na CCM zama hizo, hatuwezi kuwa na balanced history ambayo haimpendelei wala kumuonea mhusika. Hapa naomba niunganishe mfano wa Afrika ya Kusini, ukisoma historia ya vitabu vilivyoandikwa na makaburu wakati wa utawala wao, vitakuwa vinatukuza makaburu na kuonyesha kwamba makaburu ndiyo wenye haki ya kuishi Afrika ya Kusini na kutawala. Lakini leo hii kuna vitabu ambavyo viko wazi zaidi na mtu akisoma vinatoa balanced information ambayo haipendelei upande wowote.

Mbili, tuliaminishwa kwamba CCM ni baba na mama (japo Nyerere alikanusha wakati akistaafu siasa), maana bila ya kuwa mwanachama wa CCM huwezi kupata baadhi ya mambo muhimu. Mfano, kuingia Mlimani/Muhimbili ilikuwa ni lazima upate recommendation ya Mwenyekiti wa Tawi lako la CCM. Kibaya zaidi, mwenyekiti mwenyewe ni darasa la saba, hapo utake usitake lazima ukawapigie magoti. Sijui impact ya kukosa recommendation, na sometimes watu walikuwa wanaulizwa hata kadi za CCM na UVCCM. Tukiwa JKT wale tuliokuwa hatuna kadi za CCM tulilazimishwa kukata kadi za CCM. Si ajabu hata kuomba kazi ilikuwa lazima uwe na kadi ya CCM na ndiyo maana kulikuwa na matawi ya CCM kwenye mashirika ya umma. Kwa hiyo lengo la hayo yote lilikuwa ni kui-praise CCM na Nyerere. Unaposema zidumu fikra sahihi za Mwenyekiti wa CCM (Nyerere) ulikuwa na maana gani? Ina maana yeye huwa hakosei hata kidogo, je, alikuwa ni Mungu mtu? Baada ya Nyerere kung'atuka CCM sikusikia tena hiyo kauli, hapo kuna walakini, ina maana wenyeviti wengine waliofuatia hawakuwa na fikra sahihi!!!??? Baada ya kukubali hiyo kauli ya fikra sahihi za mwenyekiti wa CCM unategemea kuna mtu angejitokeza kupinga pendekezo la mwenyekiti (Nyerere) kwenye kikao??? Nyerere ana mazuri lakini pia tukubali kwamba alijikweza sana na kuwafanya wenzake wengi wasionekane kama wana hoja au mchango mkubwa kwenye chama na nchi na ndiyo akina Kambona wako gizani na siyo nuruni.

Nina uhakika kwamba kuna watu wanajua mengi kuhusu Kambona lakini kwa sababu za kwao binafsi hawawezi kuyasema wanayoyajua. Na ndiyo maana kwenye vitabu hatuoni huo upande wa pili wa Kambona. Kama kuna mwana CCM ambaye si mnafiki nadhani anaweza kuja kutuambia kwamba hapa kuna ukweli au hakuna ukweli, lakini vitabu vya historia vilivyoandikwa zama za Nyerere haviwezi kutupatia huo ukweli, bali vitatupatia upande wa Nyerere na tena mazuri yake tu, lakini siyo mabaya yake na matumizi mabaya ya dola ya vyombo vya habari.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom