GHIBUU
JF-Expert Member
- Jan 13, 2011
- 4,432
- 3,006
- Vibanda hivi vimejengwa bila kibali cha aina yeyote ile au ya umiliki wa ardhi. Na kama kipo tunaomba tuonyeshwe. Balozi Seif Ali Iddi anajua hilo, lakini amekurupuka na kuzungumza siasa zaidi ya kutaka kukamilisha agenda yake ya Tanganyika. Nina challenge balozi Seif Ali Iddi atuonyeshe hati miliki ya hao wamachinga wa hapo. Jamani, tuzungumze sheria, na haki, sio hamasa wala siasa au chuki.
- baada ya kuvamia, wamejenga kanisa, jambo lililowakera wananchi wazawa wa hapo. Balozi Seif Ali Iddi anisute kama sio kweli.
- wanakijiji/wazawa, walilalamika kwa serikali, za wilaya, mkoa na serikali kuu kuhusu kadhia hiyo, hakuna lililochukuliwa, smz imepuuza madai ya wananchi wake. Leo, yametokea mengine, wanajaribu kugeuza kibao kwa wenyeji. Uonevu gani huu, ndani ya nchi yetu. Madai ya wananchi yapo hai, tena kwa maandishi na kesi ipo, files zipo. Madai yao yapo halali kabisa, lakini walipuuzwa kwa sababu wao ni wenyeji, na wamekuzwa watu wageni wasiokuwa na hata saa moja ya kuishi Zanzibar. Sasa, OK, tujaalie SMZ iamue kuwalipa watoto wa wafalme, wataanzia wapi; any document ya kuhalilisha malipo au uhalali wa umiliki wao hapo, kisheria; tusiende kisiasa.
* Jamani, tunataka kuambiwa nini na Balozi Seif Ali Iddi, Charlie Chaplin. Nilisema awali kuwa huyu Seif NO.2 siye/hatufai. Na kadhalika Seif NO.1; pia ni mzigo kwetu kwa maslahi ya Zanzibar.
Hiyo ni SET NO .1
SET NO.2 ya mazungumzo yetu:
- hoteliers pia wamelalamika sana na watu hawa NO action. Kamisheni ya utalii pia wamekereka na watu hawa no action: kwa sababu wanaiharibu sekta yote ya utalii Zanzibar.Hoteli nyingi ama zinakosa biashara kwa kuwepo vibanda vile pale. How? wageni wao wanaibiwa, wanakuwa harrased na hotels zinakosa positve image/good image kwa kuzungukwa na vibanda hivyo. Hoteli ya fur star worth over 20m dollars, imezungukwa na kibanda cha shilingi elfu kumi. Uoza mtupu. Sekta ya utalii inakufa kutokana na wauza ugali na vinyago hawa. Hii ni serious, na naomba SMZ na nyie wote muitazame huko, kama angle ya biashara zaidi /sio siasa zaidi.
SET NO.3 ya amzungumzo yetu:
- biashara gani walikuwa wanafanya hawa watoto wa wafalme?
1. Kuuza Vinyago
2.Kuuza pombe/madawa ya kulevya
3.Uhalifu wa kupindukia.
4.Ukahba.
Katika uhalifu, iliwahi kukamatwa hata silaha katika mabanda hayo, ingawa polisi imebana kimya. Haya na mengine , mstahiki balozi seif ali iddi hataki kuyasema wala hatoyasema maisha.
Angalia ufedhuli wa watu hawa, jana wanasoma risala mbele ya Seif Ali Iddi na kusema kuwa kama serikali haitochukua hatua, wao watachukua hatua mikononi mwao. Huyu eti ni VP 2 wa nchi, na watu wanamwambia watavunja sheria, yeye na timu yake, wanacheka. Watu wanafikiria kulipiza kisasi, au kuuwa, au kufanya hujma, yeye mwenzetu anaona rahaaa, na anacheka kwa kuraha. Keli tumepata vingozi au tumepatikana.
Lakini yote hayo ya nini? Hayo ni mambo yamepanga na system. Inawezekana waliochoma moto ni serikali au hata hoteliers, au hata wengine xxxx! ili kukamilisha agenda yao. Mnaijua?
Jawabu: katiba mpya. Kwa vile mmeikataa, sasa wanabuni tension, ili kukamilisha agenda hiyo.
Bottomline: lazima katiba mpa iwe by 2014, kama alivyosema au anavyotaka JK.
Sasa Zanzibar kuanzia siku mliyoikataa mswada wa katiba mpya, mpaka 2014 mtaona mambo mengi ya ajabu ajabu popobawa atarudi, wale ramba ramba watarudi, vitisho, na visa, na mikasa mingi tu mtaiona. Ushindi lazima, na lazima katiba mpya ipite, na lazima Zanzibar tuifute katika ramani ya dunia kwa utaalamu na kisayansi.
Tusisahau kuwa katika kuchomwa moto vibanda hivi upo mkono wa kanisa.
Unajua huko nyuma sana, nilisema kwa sauti kubwa kuwa Seif NO.1 na NO.2 hawatufai, na ni lame duck niliambiwa sijui niko CUF, wengine wakasema mimi CCM. Ahhhh jamani: mimi atayesema ni CUF basi mimi ni CUF aliyekata kamba zizini; na atayesema mimi CCM; basi mimi ni CCM mfu sina mbele, sina nyuma. GNU, narudia tena haitufai; inazidi kutuletea matatizo.
- Na Maalim seif mwenyewe (menyewe .baba dogo veve, amekiri juzi jamat khan) kuwa hawawezi kutatua matatizo ya wananchi, na ametoa visingizio miteni kidogo. Mwisho hana la kusema anasingizia eti pirates wa Somalia, ndio wamesababisha kupanda kwa bei ya vyakula. Balahau bora sasa ukae na uandike vitabu vya comedy. Maalim Seif bora aungane na akina Chimbeni Kheri au Mr.Bean, watupatie tales za vichekesho.
Mwisho,nimesitikitika zaidi kuona waandishi kama Salma Said, naye amejaa tele katika hamasa na kuandika lugha mbovu kabisa, iweje yeye aandike neno vibanda vya wabara. si aseme tu, vibanda vya wafanya biashara yaani wazanzibari wote tumetekwa akili zetu na watu hawa.
Inasikitisha sana.