Mzawa Halisi
JF-Expert Member
- Feb 25, 2009
- 637
- 361
Ukisikia kumkoma nyani giladi ndio huku.
Kudos kanda2.
Yaani umefunika, umeweka sawa kila kitu. Analysis yako imekuwa very extensive. Duh! kumbe jamaa zetu ndivyo walivo. Nafasi zote wamehodhi wao.
The point ambayo watu wanaikosa humu ni moja tu. Waislamu hawapaswi kuonekana kwenye sehemu zozote za maendeleo na elimu. Wao wameshatengewa kazi zao ambazo ni upishi, usafi na udereva.
Hii inchi sasa inaelekea kubaya na wenyewe wameshasema kama HAWADANGANYIKI. Unajuwa facts kama hizi wakizipata wale jamaa zangu pale Mtambani, Kichangani au Kwa Mtoro bdio watazdi kuchanganyikiwa, si unauwa Jazbii walivyo.
Binafsi napinga udini kwa misingi yeyote ile. Taasisi za umma zinapaswa kuendeshwa na watu wenye sifa bila kujali dini zao. Mtu yeyote anapigia debe udini anapaswa alaaniwe na waTz wa dini zote, kwani leo hii akiwa mkristo atawabagua waislamu, lakini baadaye atakwenda kubagua wakristo wenzake kwa misingi ya madhehebu, baadaye ukabila, ukoo nk nk.
Kuna mtu yeyote ana facts katika nafasi zote walizoshika wakristo ni waislamu wangapi walikuwa denied nafasi hizo based on dini zao? Na tunaweza tukarudi nyuma zaidi, je kwenye mtihani wa darasa la saba ratio ya kufaulu ya wakristo na waislamu ikoje? tukaendelea hivyo hata kufikia vyuo vikuu. Kwa sababu naamini uchaguzi wa kazi zenye kuhitaji utaalamu ni kiwango cha elimu/ujuzi stahili kwa kazi inayoombwa, sasa kama ratio ya wanafunzi wanaomaliza elimu ya juu kati ya waislamu wakristo na dini zingine ni mfano 1:7:2, no wonder kwenye soko la ajira rasmi itakuwa katika mtazamo huohuo.
Udini kwa mtazamo wangu ni matokeo vilevile ya kukosekana kwa uzalendo, kunapokosekana uzalendo tunatafuta kitu kingine cha kutuunganisha na ndiyo tunapata dini, kabila, kanda na vitu kama hivyo. Sasa nani wa kulaumiwa kwa kutupeleka watanzania kutokuwa na moyo wa utaifa kama si viongozi wetu ambao na wakristo, waislamu na wapagani.