Ukweli Kuhusu UDOM huu hapa

Chunguza waliotoa thanks kwa mleta topic.
Kwanza wamepinga hapohapo wamekubaliana.
Kizungumkuti.
 
Hivi mnatumia methodology gani kujua dini ya mtu?
unamwangalia usoni? au unaangalia jina lake au mnafanyaje wandugu?


Hata mie sielewi, nimeenda kwenye website nimeona majina tu sijaona DINI!!!!!!!!

Hawa watakuwa ni wanafunzi wa Sheikh Yahaya, wanaTABIRI.
 
Mleta hoja umejaa vioja!
Upo chuo cha MUM?

Mlalamikaji alisema mishahara inatolewa kwamisingi ya udini?
Huyo msilamu aliye na cheo cha kugawa fedha za mishahara anatumia rungu lake vibaya,anawapendelea wajahedina kuliko wagalatia.

Top brass yote hapo UDOM ni urafiki kati yao na JK, MKAPA yupo kama kivuli tuu, hicho cheo hakihitaji,wala hakimnyimi kula,Top hapo ni Pr.Kikula

Angalia posts anazoshika kikulla ndio utajua nini kipo kati yake na JK.

I hate majahudina.

Wale wale

Tatizo linakuja hata pale mambo ya kawaida ya Siasa yanapozungumzwa hapa bodini, kuna baadhi ya watu humu ndani ni wadini wakubwa na lazima waingize falsafa zao za kibaguzi wa kidini. Kuna baadi ya watu na heshima zao humu ndani zikishaingizwa habari zitakazohusishwa na dini, wanageuka wapayukaji na kuongea vitu visivyo na maana na kuonyesha rangi zao za ukweli za kibaguzi wa kidini.

Nakumbuka ile habari ya uongozi wa University of Dodoma, mletaji habari alisema wazi kuwa uongozi wa chuo umejaa waislamu na wanatumia udini kupeana mishahara mikubwa. Na ilitokea baadhi ya watu wakaunga mkono ile habari bila ya kuwa na ushahidi wowote na kukurupuka kutoa shutuma mbalimbali.

Badilikeni nyinyi wadini mnatia kinyaa na kunuka kimawazo kama mashimo ya vyoo.

Mkuu hapa umenena. Kwa muda mrefu sasa jamiiforums imeanza kupoteza dira kutokana na mijadala mbalimbali kuhodhiwa na mantiki, utashi na matusi ya udini. Imetoka wapi hii? Kuna baadhi ya mijadala ya maana inaanzishwa na haipiti muda kidogo wanatokea wanabaraza fulani wanaofahamika vyema na kuleta "hoja" zao zilizotopea chuki, dharau na za uchochezi ambazo hazina mchango wowote chanya katika majadiliano kwenye baraza kama hili.

Hivi humu jamvini kuna moderators? Basi naombeni mfanye kazi na kuwajibika, kuna "michango" mingi ya kubomoa kuliko kujenga. Msitumie malengo ya jamiiforums ya kuchochea na kuimarisha matumizi ya haki za msingi za binadamu kama sababu ya kufumbia macho hawa wachangiaji na "michango" yao. Pamoja na kwamba kila mtu ana uhuru na haki ya kusema, moderators tafadhali simameni imara kuhakikisha baadhi hawapotoshi maana halisi ya uhuru huu kwa kuutumia bila ya uwajibikaji. Baadhi ya hii "michango" ya hawa wanabaraza haifai hata kuwa katika jukwaa la dini humu ndani, maana ni kashfa kwa jamii ya wastaarabu na watanzania kwa ujumla.


Mamkwe,
Umetbibitisha tu kuwa ni kweli kile chuo cha UDOM kimeshikwa na Waislaam. Huyu Mchaga Kinabo (kama sikosei) kapewa cheo cha Academic. Huko yeye anadeal na wanafunzi, waalimu, masomo, nk wakati huyu anayeshukiwa kuwa MDINI yaani Pro. S. Mlacha na Kikula, ndiyo Maboss wenyewe na ndiyo wameshika MPINI. Hapo ongeza Bilal ambaye ubabe wake ulionekana wakati Mkapa ni Waziri wa Sayari na Elimu ya Juu na yeye ni Katibu Mkuu. Akipata tatizo badala ya kwenda kwa Mkuu wake Mkapa, alikuwa anaenda moja kwa moja Ofisi ya Jirani yaani IKULU.

Hao Waalimu na viongozi Waislaam wanaweza kuwa wachache ila unyanyasaji wao ukawa wa kutisha.

Kama jamaa wanapata UBABE kutoka kwa Kikwete basi itakuwa ni too bad. Nasema kama wanatumia huo UISLAAM kujifanyia mambo kienyeji, itakuja kuwa mbaya sana kwao huko miaka ya baadaye. Hii aliifanya Prof. Kigoma Malima wakati akiwa Waziri wa Fedha. Alikuwa akitoa misamaha ya kodi kwa Waislaam kama kawa. Upuuzi huo akaja kuufanya Mkapa na genge lake na matokeo yake akina Mramba tunawaona Kisutu.

JIPANGE na uje hapa UPYA.

Jamani tuache kujaribu kuchafua watu, hivi Prof. Kikula unamfahamu vizuri? Sio kila mwenye imani tofauti na mimi na wewe ana malengo hasi na sisi.
 
Hizi dini zinachosha wajomba,haya mambo ya kupendeleana kwa ajiri ya dini au ukabila yapo sana TZ,yaaani kweli sielewi kabisa ndio maana sina hata cha kuandika naona michosho tuu!
 
Siku za hivi karibuni imewahi kuandikwa juu ya madai ya udini, ukabila, ukanda, ubabe katika Chuo Kikuu cha Dodoma. Mimi kama Mtanzania mwenye uchungu na taifa langu niliamua kuzifanyia kazi tuhuma hizo nzito. Niliamua kufanya hivyo kwa kuwa natambua athari za udini, ukabila, na ubaguzi wa aina nyingine katika jamii. Nchi nyingi zimejikuta katika mapambano ya kumwaga damu kutokana na aina mbalimbali za ubaguzi. Katika kuzifanyia kazi tuhuma hizo nilifanya uchunguzi na kubaini yafuatayo:-

Udini Uongozi wa UDOM

Chancellor: H. E. Benjamin W. Mkapa (catholic)
Vice Chancellor: Prof. Idris Kikula (Muslim)
Chairman of Council: Hon. Dr. M. G. Bilal (Muslim)
Deputy Vice Chancellor (Academic): Prof. L. Kinabo (catholic)
Deputy Vice Chancellor ( Administration) Prof. S. Mlacha ( Muslim)

Viongozi wengine wa ngazi za juu UDOM

Principal - College of Education: Prof. K.M. Osaki (catholic)
2 Deans of Schools in the College are all Christians

Principal - College of Humanities: Prof. C. M. Rubagumya (Christian)
2 Deans of Schools in the College are all Christians

Principal- College of Informatics: Prof. N. Mvungi (Christian - Protestant)
2 Deans of Schools in the College are all Christians

Dean of Student (Christian)

Dean, School of Natural Science (Christian)
Dean, School of Medicine (Christian)
Dean, School of Nursing ( Christian)

Source: (UDOM Prospectus and Website)

Wafanyakazi - Wanataaluma - Christians 96%
- Muslim 4%

Wafanyakazi Waendeshaji - Christians 86%
- Muslim 14%

Wanafunzi - Christians 92%
- Muslim 8%

(Source UDOM Website, newpapers, announcements of student admission)

Inashangaza sana kuona mtu mzima mwenye akili zake timamu kuzusha kwamba UDOM ni Chuo cha Waislam kwa kuwa kuna viongozi watatu Waislam bila kuyafanyia kazi madai yake. Bila shaka watu hao na wapambe wao hawalitakii mema Taifa letu.

Waungwana, kutokana na uchungu nilionao juu ya jambo hili bado nitaendelea kufanya utafiti kuhusu muundo wa uongozi katika vyuo na taasisi nyingine za umma na kumwaga data hapa uwanjani kwa madhumuni ya kuwasuta wote wasiotaka mwananchi wa dini au kabila fulani apewe madaraka hata kama ana uwezo. Ukweli ni kwamba viongozi wa UDOM hawakuteuliwa kwa sababu ya dini zao bali uwezo wao ambao kwa kiasi kikubwa unajidhihirisha kwa jinsi ulivyofaulu kubadilisha mandhari ya vilima vya Chimwaga na vitongoji vyake, pamoja na ramani ya nchi yetu katika dunia ya elimu ya juu. Ujenzi wa UDOM umesaidia sana kuinua kiwango cha elimu kwa vijana wanaomaliza kidato cha sita. Vijana wa wakulima na masikini wengine wa Tanzania ambao sasa wanasoma UDOM wangeishia kuwa wapiga debe kwenye vituo vya daladala kwa kukosa sehemu za kujiendeleza. Wanaobeza na wabeze, lakini mimi naifagilia nchi yangu na serikali yake kwa ujenzi wa UDOM bila kujali itikadi za Chama. Wanaosoma UDOM ni Watanzania haijalishi ni wanachama wa CHADEMA, CUF, TLP, CCM, NCCR, au ANR.

Watanzania tuamke, tuache kutumiwa kwa madai ya udini, ukabila, jinsia, kanda nk. Tusipokuwa makini tutajikuta kama majirani zetu.

Naamini JF ni kijiwe cha watu wenye busara, ni vizuri kikatumika kutoa taarifa zilizofanyiwa kazi. Nitasikitika sana endapo JF itageuzwa kuwa kijiwe cha majungu

Hongera kwa kuwapa elimu watanzania waachane na majungu wachape kazi kujenga taifa letu
 
Waungwana Habari za udini hazifai kutajwa na kujadiliwa na jamii ya watu makini kinachotakiwa ni kueleza mapungufu ya mtu fulani mwenye cheo fulani kwani upungufu au uimara wa mtu hauletwi na dini ila ni mtu mwenyewe.

Tukianza na dini tutaelekea kwenye kabila then tumalizie na jinsia.
 
Haya mambo ya dini sasa yamekuwa too much hapa JF kila siku kutafutana uchawi. Nadhani umefika wakati sasa post zote zenye mirengo ya kidini zikapelekwa kwenye forum maalum ya mambo haya, na hapa tuachieni tuchape siasa kwa kwenda mbele.

Mshindwe wadini wote!
huko tuendako, tukifanikiwa kuushinda ufisadi, tutasambaratishwa na udini
 
Wanafunzi - Christians 92%
- Muslim 8%

Jamani mambo mengine kweli yanachekesha,hivi hamjui kwamba mtu anaweza kuwa na jina la dini fulani lakini si wa dini ile?
halafu katika swala la admission ya wanachuo kama wakristo kwa mfano hawaja-apply utawalazimisha kuwapa admission ili tu uwiano uwe sawa?
na hata kama wame-apply na grade zao ziko chini,utawapa admission kwa kulazimisha ili kuogopa watu wa dini moja wasizidi.
Labda nieleweshwe au kuna watu maalumu hapo UDOM wanabania watu wa dini fulani wasipate nafasi hata kama wana sifa?

Vinginevyo ianzishwe programme maalumu ya pre-entry kama ya UD ya wanawake wasiokidhi viwango vya direct entry,ili kuwepo na uwiano wa dini pia.
 
Mamkwe,
Umetbibitisha tu kuwa ni kweli kile chuo cha UDOM kimeshikwa na Waislaam. Huyu Mchaga Kinabo (kama sikosei) kapewa cheo cha Academic. Huko yeye anadeal na wanafunzi, waalimu, masomo, nk wakati huyu anayeshukiwa kuwa MDINI yaani Pro. S. Mlacha na Kikula, ndiyo Maboss wenyewe na ndiyo wameshika MPINI. Hapo ongeza Bilal ambaye ubabe wake ulionekana wakati Mkapa ni Waziri wa Sayari na Elimu ya Juu na yeye ni Katibu Mkuu. Akipata tatizo badala ya kwenda kwa Mkuu wake Mkapa, alikuwa anaenda moja kwa moja Ofisi ya Jirani yaani IKULU.

Hao Waalimu na viongozi Waislaam wanaweza kuwa wachache ila unyanyasaji wao ukawa wa kutisha. Mbona Rwanda na Burundi Watusi walikuwa 10% ila ubabe wao ulikuwa wa kutisha. Wageruman walikuwa wachache tu ila wakatutawala.
Kama jamaa wanapata UBABE kutoka kwa Kikwete basi itakuwa ni too bad. Nasema kama wanatumia huo UISLAAM kujifanyia mambo kienyeji, itakuja kuwa mbaya sana kwao huko miaka ya baadaye. Hii aliifanya Prof. Kigoma Malima wakati akiwa Waziri wa Fedha. Alikuwa akitoa misamaha ya kodi kwa Waislaam kama kawa. Upuuzi huo akaja kuufanya Mkapa na genge lake na matokeo yake akina Mramba tunawaona Kisutu.

JIPANGE na uje hapa UPYA.

Mdini ni wewe! unakerwa na uislamu na post zako zimesheheni chuki dhidi ya uislam.

Hebu isome tena post yako uone ulivyo mdini, kwa akili yako kuwa na waislam 3 uongozi wa juu ni udini (isomeke uislamu) sasa je na hivyo vyuo vingine vilivyobaki ambavyo sio tu viongozi watatu wa juu ni wakristo bali WOTE ni wakristo huoni udini?

Wewe wafahamika hapa kwa chuki zako kwa waislam na kwako hakuna jema kutoka kwa waislam, lakini dini hii imepingwa na makafiri wakubwa kuliko wewe lakini bado ni dini inayo kuwa kwa kasi kuliko dini zote duniani. Endelea na chuki zako mgalatia wewe
 
Unajua ukisikia kuna UDINI maana yake kuna UISLAMU.

Jana nilikuwa nasoma Thread moja kuhusu Udini NSSF kwa swahiba wangu Dr Ramadhani Dau. Utaona waziri Prof Kapuya, na a lot of bla bla.

Jamani WAKATOLIKI nyie tu ushike kila pahala, wakishika waislam basi Nongwa.

hakika chuki zenu dhidi ya waislamu na Uislam zitaiweka pabaya nchi yenu. Na Uislam hamtauweza hata mkifanya nini, kwani umejengwa kwa misingi madhubuti sana. Tieni kila aina ya fitna lakini uislamu utapaa tu.
 
Mamkwe tunashukuru kubainisha ukweli. Sasa tuleteee data kama hizo za SUA, UCLAS, Muhimbili na UDSM.
tulinganishe na kupata ukweli wa mambo.

Allah akubariki saaaaaaaaana
 
Hoja zingine ziko so light yaani jamani hili nalo la kubishana....nenda kwenye taasisi zote utaona wakristu wengi kuliko waislamu....yaani ni katika hali ya kawaida bila kuhusisha upendeleo.Nchi hii population yetu ya watu kama milioni 40 ina waislamu wengi kuliko wakristu ila wasomi wengi zaidi ni wakristu...kama hutaki shauri yako huu ndo ukweli hasa unaosababisha kuwe na wakristu wengi katika kila sector nchi hii. Kwa hiyo suala hapa ni kwa waislamu kusoma,haitoshi tu kwenda madrasa jamani...tupate na elimu dunia ili tuweze kupata nafasi nyingine za kiutendaji katika serikali yetu.
 
Ukiona watu wanaanza kutumia majukwaa ya dini kuingia katika siasa ujue wamefilisika kisiasa. Vyama vya siasa kuingiza masuala ya dini kwenye ilani zao za uchaguzi ndio chanzo cha haya yote. Viongozi wetu wanatafuta cheap popularuty kwa ku influence makundi fulani katika jamii bila kufikiria kwanza athari zake.

Huu ni sawa na wendawazimu wa kufikiria ni kwa jinsi gani wataendelea kubaki madarakani hata kama ni kwa gharama kubwa kwa jamii na kuhatarisha utengamano wa nchi.

Hisia za kidini zimeletwa na watawala wetu kwani mpaka sasa huwezi kusikia mtu akikemea kwa nguvu na nia moja chokochoko za kidini.
 
Mdini ni wewe! unakerwa na uislamu na post zako zimesheheni chuki dhidi ya uislam.

Hebu isome tena post yako uone ulivyo mdini, kwa akili yako kuwa na waislam 3 uongozi wa juu ni udini (isomeke uislamu) sasa je na hivyo vyuo vingine vilivyobaki ambavyo sio tu viongozi watatu wa juu ni wakristo bali WOTE ni wakristo huoni udini?

Wewe wafahamika hapa kwa chuki zako kwa waislam na kwako hakuna jema kutoka kwa waislam, lakini dini hii imepingwa na makafiri wakubwa kuliko wewe lakini bado ni dini inayo kuwa kwa kasi kuliko dini zote duniani. Endelea na chuki zako mgalatia wewe


kwa kweli haya mambo yanahitaji kutazamwa na kutafutiwa suluhu afisini ukipiga nyimbo za gospel hakuna anaesema fungua quran mdini

ukipanda mabasi ya mikoani utasikia nyimbo za gospel ukifungua quran hapatoshi

hili tuliangalieni sana kama ni kweli tunapenda haki basi utaona wazi kuwa jamii ya wakristo haiwatendei haki waislam na inajaribu kuwafanya waonekane ni class 2 ktk nchi yao
 
Uongo ni kitu kibaya sana especially uongo wa kutunga wenye nia za hila hila. Hata hivyo udini pia ni kitu kibaya sana sana. Tujiangalie tusifikiri tumesimama kumbe ndo tunaanguka. Mambo ya aina hii hayako sustainable kwa individuals na kwa Taifa letu. Tuanze kuangalia dunia yetu kwa jicho pana. Hili la udini na uongo hili litatuangusha wenyewe. Time will tell
 
ki ukweli watanzania sio wadini bali hutumia huo udini kwa manufaa mengine maana ni wachache sana ktk maisha yao ukifuatilia ndio kweli wnafuata hizo dini zao ila wengi ni wahini wahuni na ni watu wa kawaida sana nadhani inafaa sasa tufuate siasa za cuba au communist countries
 
no wonder kila kwenye vita (sehemu nyingi) ni kwasababu ya watu kama nyie... Somalia, boko haram(nigeria), afghanistan, iraq, sudan....

Mnaboa sana na analysis zenu hizi za kidini bila kufikiria nje ya box kwanini inakuwa hivyo.


chuki na udini umekujaa, najua hampendi kuambiwa ukweli hasa pale hila zenu zinapofichuliwa.

Sehemu zote hizo zenye vita ni kwa sababu ya uroho wa wagalatia dhidi ya mali za waislam walizjaaliwa na mola muumba.

Hapa kin achotakiwa ni kujibu hoja kwa hoja sio kushutumu na kutukana kwa sababu tu hoja zilizowasilishwa umeshindwa kuzijibu.

Waleta hoja wakiziwasilisha bila data mnasema uzushi, wakiweka data mnasema analysis zinaboa sasa mnatakaje?????.

Hapo ndo inpodhihirika hila na chuki dhidi ya uislam.
 
Back
Top Bottom