Ukweli kuhusu Rwanda, watutsi, Paul Kagame na uchochezi wa mch. Mtikila

Tanzaniaist

Senior Member
Nov 29, 2011
161
156
Habari wanaJF..!

Kwa muda sasa kumekuwa na mijadala mingi ikiilenga Rwanda, Paul Kagame na hususani kabila la Watutsi..!
Na hili suala limekolezwa zaidi na mch.Christopher Mtikilia ambaye ni mwanasiasa hodari hapa nchini Tanzania na pia ni
Mwenyekiti wa Chama cha DP.,kupitia waraka wake ambao mimi nauona ni wa kichochezi,uwongo,chuki na propaganda
Zisizokuwa za msingi ambao wenye malengo ya kupotosha ama kuleta uchochezi na mauji.

Najua kuna baadhi watapingana na mimi lakini kwa wale waliosoma historia watanielewa.

Nianze kwanza,..nini chanzo cha uhasama baina ya Wahutu na Watutsi..?
Kabla ya Ukoloni makabila haya mawili walishabihana na hata kuwa na lugha moja Kinyarwanda upande wa Rwanda
na Kirundi upande wa Burundi ingawa watutsi ndio walikuwa watawala kwakuwa walikuwa na utajiri mwingi wa ng'ombe maarufu "ankole" na hata pia tukiangalia hapa Tanzania Ufalme wa Karagwe ulikuwa na mchanganyiko wa Watutsi, Utawala wa Bachwezi na tawala mbali mbali kanda ya ziwa kulikuwa na mchangiko wa watutsi kabla ya ukoloni mwaka 1885..!
Wakoloni waliikiingi na Mkakati ulioitwa "Wagawanye na uwatawale".,na ulifanikiwa sana Kama nchini Nigeria baina ya Wakristo na Waislamu, Kenya baina ya wakikuyu na wajaluo,wakalenjin. ndio maana hata hapa Tanzania mikoa yenye wakristo wengi ilipata sana fursa ya elimu,miondombinu kuliko mikoa yenye waislamu wengi.

Tukija Rwanda huko zilianza taratibu za kuangalia pua,muonekano ambako waligawanywa kama Watutsi na Wahutu na hata kuvalishwa vibao.,ambako wale walioitwa watutsi walipewa fusra kubwa sana kwenye elimu na utawala na wakoloni ambao walikuwa wajerumani kisha wabeligiji..! mwanzo hawa watu walikuwa kama familia,ukoo na kabila moja paka kuweza kuwa na lugha moja na hata pia vinasaba vinaonyesha watutsi wana mchanganyiko na wenzao wahutu..!

Uhasama mkubwa uliibuka pale mwaka 1959,..ambako watutsi wengi walihamia Uganda,Congo na Hata Tanzania mpaka mwaka 1994 ambako yalitokea mauji ya kimbari na kusababisha vifo vya watu zaidi ya 1,000,000. kwa kifupi hii ndo historia fupi ya watutsi unaweza ukapata habari nyingi zaidi ya hapa.

Tuje kwenye waraka wa Mchungaji Christopher Mtikila,..ambao hauna tofauti na waraka uliosambazwa mwaka 1994 na
kusababisha mauji ya kikatili, wanawake na watoto kubakwa, miondombinu ya uchumi kuharibiwa vibaya..,na mtu kama huyu mahali pake hapa duniani ni Jela tena kifungo cha Maisha na hata peponi ni Jehanamu. ni kitu kibaya sana kuona Binadamu anapenda kuona vifo au mvurugano wa nchi ambayo sasa hv ina amani wakirudi tena katika mapigano. Mchungaji Mtikila ametumia mifano mfu na ya uongo kutetea hoja zake.

1.Suala la wafugaji kuingia bonde la Burigi, hili ni tatizo la serikali yenyewe kutolinda mipaka yake kuanzia maafisa uhamiaji, na hata kuliibuka baadhi ya tuhuma wafugaji kuonga wenyeviti wa vijiji ili waweze kupitisha ngombe. na hili suala limekuwa sugu sana, mfano tukiangalia hata kwenye ziwa letu Victoria Wakenya na Waganda wanakuja kuvua kwenye maeneo yetu na hata mbunge wa Ukerewe Mh.Machemli alishawahi kuja kulalamika bungeni, na hata baharini tukikumbuka wale samaki wa Magufuli walikuja kuvua kwenye mwambao wetu wa Bahari., hili tatizo la wageni kuvamia Rasilimali zetu ni Tatizo la Serikali kushindwa kulinda mipaka yake dhidi ya wavamizi ndio tatizo la wafugaji wengi kutoka Rwanda na Hata Burundi kuvamia maeneo yetu ya hifadhi. ndio maana imekalia kimya waraka wa Mch.Mtikila
kwani kwenye maeneo ya mipaka kuna tatizo kubwa sana la Rushwa.. na ningependa nimdahamishe Mch.Mtikila wanaovamia Rasilimali zetu sio tu watutsi hata pia Wakenya na Waganda ziwa Victoria,Wachina Bahari ya Hindi ni muhimu Serikali kuzidisa ulinzi kwakuwa wana Polisi na Jeshi.

2.Suala la Kagame Kupendeza Wanyarwanda 35,000. hivi nchi yetu haina usalama wa Taifa, haina idara ya uhamiaji, haina idara ya intelejensia polisi. kumbuka kuna makabila ya wahaya,waangaza,muha na wanzinza ambao wamenyangika na watutsi hata kabla ya Ukoloni mwaka 1885. na kumbuka nchi yetu imetoka uraia kwa baadhi ya wakimbizi kutoka makambini ambao walikuwa wahanga wa vita. ndio maana nchi kama Canada,Norway na Sweden wametoa uraia sana kwa wasomali ambako kwa akili ya mch.Mtikila angemaanisha wale wametumwa na Al shabaab. Mch.Mtikila hujui maana ya vita.

3.Suala la ''Black Apartheid" na kufanisha watutsi na nyoka., hapa sitaki kuongea sana lakini Mzungu ama Mhindi atamcheka sana Mwafrika kama anambagua mwenzake kisa kabila,ama rangi au dini.,

4.Mwisho ni nikija kwa PAUL KAGAME, Historia yake inasemakana amwaka 1979 alihshiriki vita ya TANZANIA dhidi ya nduli IDD AMINI DADA chini ya YOWERI MUSEVENI akiwa upande wa Tanzania kisha kushirikiana na Museveni mwaka 1985 ambako alikuwa mkuu wa Intelejensia wa jeshi la Museveni, hadi kujiunga na jeshi la Uganda Museveni alipokuwa Rais na kupelekwa Grand Rapids Nchini marekani kwa mafunzo zaidi ya Kijeshi, ambako aliiwezesha jeshi lake la RPF kutumia mbinu mbadala kuliteka jiji la Kigali dhidi ya serikali ya kipindi hicho.., Mchungaji Mtikila una habari kwamba WATUTSI wengi ambao wewe unawaita NYOKA walishiriki kwenye vita ya Ukombozi wa Watanzania mwaka 1979 dhidi ya IDD AMINI akiwemo hayati mtutsi FRED RWIGEYMA na hata baadhi ya Kufa kwaajili ya Taifa letu wakati wewe ukiwa kwenye handaki umejificha. mwenzio PAUL KAGAME alizaliwa ndugu zake wakichinjwa na kujikuta amekulia kambini., its fair kumuita muuaji bila ushahidi wakati wewe umefaidi matunda ya amani chini ya mtu unayemdharau Baba wa Taifa., think twice Mtikila huku ukikumbuka maumivu ya kupigwa jiwe huko Tarime kwa uchochezi wako.


Ningependa Watanzania Tusishabikie vitu visivyokuwa na Msingi wakati nchi yetu ikiwa na Matatizo makubwa ya Ajira,Afya,Umeme,Maji,Miondombinu na N.k juzi wenzetu Brazil walipinga Matumizi makubwa ya maandalizi kombe la Dunia Nchini mwao,..sisi leo tunafurahia Serikali kupeleka Jeshi Nchini Congo.,wakati nyumba za Polisi zikiwa katika hali mbaya mfano zile kota za kariakoo msimbazi. ni masuala ya kujiuliza kitu gani kina faida nchini mwetu. kuna mtu hapa jamvini alitoa hoja watutsi watimuliwe nchini kwa msingi hiyo basi mikoa ya Kagera,Kigoma tuindoe kwenye ramani ya Tanzania kwani watutsi ni ndugu zao na hata lugha moja wanaongea. ikiwemo kirundi na kinyarwanda.

Tukiangalia Nchini zilizoendelea Kama MAREKANI,UMOJA WA FALME ZA KIARABU NA AFRIKA KUSINI, hizi nchi ni mchanganyiko wa mataifa mbali mbali, ww Mtanzania hujishughulishi anakuja Mkenya,Mnyarwanda anafanya maendeleo kwenye Nchi yako then unaaznisha maneno ya uchochezi wakati ni udhaifu wako wa kutojiendeleza. Tanzania ni nchi yenye rasimali kubwa sana ya ardhi lakini hatuitumii vizuri kuzalisha na kuongeza pato la Taifa kwanini wageni wasitutolee macho, mi naona waje tu kutusaidia kwasababu tumeshindwa.

Naona nianze na historia kwanza kwa faida ya wasomaji coz' naona hii ya kwako haija-expose vizuri chanzo cha uhasama kati ya Wahutu na Watusi!

HISTORIA FUPI: Hapo awali eneo ambalo hivi sasa ni Rwanda na Burundi hapakuwa na watu ambao wanafahamika kama Watusi hivi sasa; kwa maana hiyo, asili ya watu wa eneo hilo ni Wahutu!

Watusi walitokea Ethiopia, na kama ilivyokuwa enzi hizo, walipofika eneo ambalo sasa ni Rwanda na Burundi, Watutsi waliwavamia na kuwashinda vita wenyeji; Wahutu! Kimsingi, the guys(Tutsi) ni warriors since then kama yalivyo makabila mengi ya wafugaji....labda ni kwavile wameshazoea kufukuzana na wanyama wakali katika kulinda mifugo yao; tofauti na mkulima; yeye akimuona simba au chui atakimbia; by the way si simba wala chui anayekula mahindi lakini ukisusa mifugo kwa hao jamaa, imekula kwako (Hapo kwenye RED, tafsiri ni yangu kwahiyo msinidai ushahidi kwavile sina)!!!

Wakati wa ukoloni, Wakoloni waliwatumia sana Watusi kuwa-oppress Wahutu coz' Watutsi wao ndo walikuwa watawala. Inasemekana oppressing ya Watusi kwa Wahutu ilikuwa kubwa sana pengine kuliko sehemu zingine barani Afrika. Na wata Walipoingia Wabelgiji baada ya WWI, wakaendeleza hali hii, ya kuwatumia Watusi kuwa-opress Wahutu!

Lakini cha ajabu, wakati Wabelgiji wanakaribia kuondoka, wakaanza kuwaingiza baadhi ya Wahutu madarakani. Later on, kwa ushawishi wa kanisa Katoliki, Mchungaji wa Kihutu akatoa Waraka wa kuitaka Ubelgiji kukabidhi madaraka kwa Wahutu! Sujui kwanini RC waliwa-favor Wahutu, sina uhakika labda kwavile Wahutu walikuwa ni oppressed community or kutokana na ukweli kwamba kwa kawaida Wakulima walikuwa na muda wa kushiriki dini za wazungu kuliko Wafugaji na hivyo bila shaka Wakulima(Wahutu) wengi zaidi walikuwa wamempokea YESU kuliko Wafugaji Watutsi na hivyo RC kuamua kutoa upendeleo kwa waumini wao Na in fact, labda hapo ndipo unaweza kuona ni kwa vipi Kanisa lilihusika na mauaji ya kimbali kwa namna moja au nyingine!(Kwa mara nyingine, hapo kwenye RED, tafsiri ni yangu kwahiyo msinidai ushahidi kwavile sina)!!!!

Aidha, kufuatia Waraka huo, Wahutu wakaanzisha vyama vya kisiasa kama njia ya kujiandaa kutwaa mamlaka kutoka kwa Mkoloni Mbelgiji. Na historia inasema kwamba hata uanzishwaji wa vyama hivi ulisimamiwa na Kanisa!

Wakati Wabelgiji wamekaribia zaidi kuondoka, ukaitishwa uchaguzi ambapo (wengine wanasema wa kimagumashi) na chama cha Kihutu kikashinda! To make things even worse, pakapigwa kura ya kama Ufalme uendelee kuwapo au ufutwe! Tusisahau, ufalme ulikuwa unashikiliwa na Watusi wachache ambao ndo walikuwa wenye nguvu...this means that, mshindi huyu wa Kihutu alikuwa chini ya Ufalme wa Kitutsi! Hata hivyo, kama ilivyotarajiwa, wengi waka-vote against Monarch na hivyo Mhutu aliyechaguliwa akapata wasaa wa kujinafasi!! Na hivyo, mwanzoni tu mwa utawala wake akaanza kuwashighulikia Watutsi ambao walikuwa madarakani! Na katika kipindi kifupi, Watusi wakaonja joto ya jiwe kwani walishughulikiwa kila idara na wengi waliuawa na wengine wakaikimbia Rwanda! In short, ni kama walikuwa wanalipiza kisasi cha kuwa oppressed for centuries!

Hali hii ya uhasama iliendelea na kuja kuzalisha mauaji ya kimbali ya 1994 ambayo chanzo chake ni kutunguliwa kwa ndege ambayo ndani kulikuwa na Rais Habyarimana ambae alikuwa ni Mhutu!

SASA TURUDI KWENYE MADA:
Kwanza ni kweli kabisa uvamizi wa wageni ndani ya ardhi ya Tanzania unatokana na udhaifu ulio ndani ya uwezo wetu wenyewe! Hata hivyo, hilo hali-justify wageni kuingia na kutoka watakavyo! Huwezi kufika kwenye duka la mtu kisha ukaiba kwavile tu mwenyewe hajafunga! Ukikamatwa, utahukumiwa kwa wizi na wala hakuna atakayejali kwa utetezi kwamba ulikuta duka halijafungwa!!

Ni kweli pia kwamba mataifa uliyotaja ni ya watu wa mchanganyiko lakini kote huko kuna utaratibu wa mtu kuingia na sio tu kuingia utakavyo! Ukifanya hivyo na ukagundulika utawajibishwa! Na kama serikali imelala, raia wema wa nchi husika watapandisha sauti kulalamikia wahamiaji haramu! Labda tatizo la Mtikila ni aina ya lugha aliyotumia lakini kwa anayemfahamu hawezi kumshangaa!! Binafsi ningeshangaa endapo angetumia lugha ya kiungwana, lakini mtu ambae alipata kuita Mwili wa Baba wa Taifa kwamba ni mzoga sijui kama ni ajabu kuwaita Watusi ni nyoka! Nakumbuka miaka kadhaa iliyopita Mtikila huyu huyu alipata kum-refer Mkapa kwamba ni Mmakonde wa Musumbiji ambae anatakiwa kutiwa kwenye lori na wamakonde wenzake kisha wakamwage mpakani! Lakini tukichuja maneno yake mabovu na ya kibaguzi, bado hoja yake inabaki kuwa ya msingi na katu uozo wa mipakani usiwe justification!

Mwisho ningependa kuzungumzia hilo la eti Kagame alikuwa tayari kufa kwa ajili ya Tanzania! Hebu jisikie aibu kwa hoja kama hiyo kwani hata kama ni kweli Kagame alishiriki kwenye vita vya Kagera, katu hakufanya hivyo kwa maslahi ya Tanzania bali alifanya hivyo kwa maslahi ya Museveni....ilikuwa ni lazima Museveni apate nchi ili nae (Kagame)apate nafasi ya kuendeleza harakati zake!
 
Hutabadilisha ukweli wa kuwa Watutsi ni wapuuzi, wabaguzi hawataki utawala wa kidemokrasia wanataka wao kutawala. Hata wayahudi wana hata vitabu vya dini kuwahalalishia upuuzi kama wanayotaka Watutsi; lakini uzayuni itikadi yao ni kibaguzi sawa na ya Watutsi. Nazungumzia haya mimi ni Mtanzania wa asili lakini nimeshuhudia matendo ya hawa Watutsi walivvowatoroko dada zetu na watoto wetu kwa sababu si Watutsi.

Kaama wangekuwa wa maana wanashindwaje kushirikiana na makabila mengine kwenye utawala kupitia sanduku la kura halali?

Halafu kuegemea udhaifu wa CCM kuna mwisho mtatimuliwa tu kwa sababu hila zenu ziko wazi
 
Binafsi nilikuwa mshabiki saana wa Mch.Mtikila, ila sasa nimeshajidhalau kwanini nilikuwa shabiki wake, Si unakumbuka kichapo alichokipata Tarime? Nimegundua kweli ana akili zilizo mzidi baada ya kusikia ati tena katunga kitabu cha Marehemu Chacha Wangwe, wakati alipata kichapo afu akaomba msamaha, then anakuja na hoja ileile aliyoiombea msamaha!
 
Kagame is a hero of Tanzania during Idd Amin war,Where was this fool Mtikila during that war.He was hiding in the holes somewhere while Kagame and other soldiers were fighting for the respect and image of our country.I hate the guy who is using Mtikila to demonize Nyerere,No wonder his administration has turned out to be a total failure.
 
my brother,am sorry to say this to you.But,I think you dnt know anything kuhusu Kagame wala Museveni.
Usilete zile akili za kina " Membe" akiwaita malawi eti wenzetu?

Sisi watanzania nathani tuna kama mtindio wa akili vile.Muda mwingine namlaumu sana Mwl Nyerere kwa kutuzubaisha mno pamoja ni mtu ambaye nina heshima naye sana na kwa hilo naamini hakuwa na nia mbaya.
Ila nachoweza kusema akili zetu watanzania zimefungamana mno, labda tutupie lawama elimu na curriculums tulizonazo ambazo zinafinya uwezo wa kufikiria.

Nachoweza kukuambia ni kwamba usilete uchafu wako huku kama hujui unachokiongea. kama unaona kagame mjinga mwenzako ni mtu nenda ukaishi huko kwake.

nimesikitika sana kusoma upuuzi huu na nimepoteza muda wangu. please get a life!
 
my brother,am sorry to say this to you.But,I think you dnt know anything kuhusu Kagame wala Museveni.
Usilete zile akili za kina " Membe" akiwaita malawi eti wenzetu?

Sisi watanzania nathani tuna kama mtindio wa akili vile.Muda mwingine namlaumu sana Mwl Nyerere kwa kutuzubaisha mno pamoja ni mtu ambaye nina heshima naye sana na kwa hilo naamini hakuwa na nia mbaya.
Ila nachoweza kusema akili zetu watanzania zimefungamana mno, labda tutupie lawama elimu na curriculums tulizonazo ambazo zinafinya uwezo wa kufikiria.

Nachoweza kukuambia ni kwamba usilete uchafu wako huku kama hujui unachokiongea. kama unaona kagame mjinga mwenzako ni mtu nenda ukaishi huko kwake.

nimesikitika sana kusoma upuuzi huu na nimepoteza muda wangu. please get a life!


Mi nachojua Kagame ndo chanzo cha vita kule Congo kwa kuwaibia rasilimali zao na mwisho kuwaua.

Haimaanisha kuwa ni mzuri na tuendelee kumshabikia eti tu kisa alisaidia katika vita vya kumng'oa Iddi Amin.
 
Mimi naomba nisome comments Tu nisijitie ushabiki kwa mambo nisito na uelewa nayo. Ntakua mwanafunzi mtiifu na Nita analyze kila comment ili kupata upande nttakao simamia but so far nabaki neutral
 
Kuna kampeni ya kumchafua Nyerere kwa makusudi imeanzishwa muda mrefu tu na watu flani,Na hii inatokana na hasira za watu flani ambao walienguliwa katika kinyang'anyiro cha kugombea Urais kwa tiketi ya CCM mwaka 1995 ambapo Bw Mkapa alipewa mikoba ya kuiwakilisha CCM katika tiketi ya Urais.Hawa watu bado wana kinyongo na Nyerere na wanafanya kila wanaloweza kuifuta historia ya Nyerere katika vichwa vya Watanzania.Walichosahau katika mpango wao huo ni kwamba wao ni Wachafu na hawana Uzalendo hata kidogo Kwa Taifa hili.Kama wanadhani watafanikiwa katika mipango yao haramu ya kupuuza kila kitu Nyerere alikisimamia basi wanajidanganya sana.Ikifika mwaka 2015 tutawaonyesha hawa watu kwamba wafuasi wa Nyerere bado tupo wengi mno katika Nchi hii kwahiyo waendelee tu na mipango yao ovu.
 
usemalo mkuu ni kweli , kabisa huyu mtikila inawezekana katumwa ili mambo yachafuke waliomtuma wapate namna yakusema na kutuvamia, serikali ichukue hatua hasa maswala ya mipaka not else .
 
hata ukiandika kwa kalamu nyeupe huweza kumsafisha Kagame. Mtikila alitoa evidence, we sioni chochote hapa.

Uongo mwingine hata haufai, vita ya uganda iliisha kabla kagame hajajua hata risasi inafananaje. Soma hapa:

".....In 1978, Fred Rwigyema returned to western Uganda and reunited with Kagame.[SUP][18][/SUP] During his absence, Rwigyema had joined the rebel army of Yoweri Museveni, which was based in Tanzania and aimed to overthrow the government of Idi Amin. Rwigyema then returned to Tanzania and fought in the 1979 war in which Museveni's army, allied with the Tanzanian army and other Ugandan exiles, defeated Amin. Following Amin's defeat, and inspired by Rwigyema, Kagame and other Rwandan refugees pledged allegiance to Museveni, who was a cabinet member in the transition government. Kagame travelled to Tanzania where the Tanzanian government, which sought to protect the new Ugandan regime, trained him in espionage...."

Mengi zaidi kuhusu maisha yake soma wikipedia hapa: Paul Kagame - Wikipedia, the free encyclopedia
 
Unaposema Kagame aliisaidia Tanzania katika vita vya Nduli Idd Amini Dada, una maana Watanzania hawakuwepo? Kama walikuwepo, nini zaidi alichokifanya Kagame hadi awafukie watanzania wote mashujaa. Ina maana akina Mayunga, Wolden na wengine wengi waliongozwa na Kagame. Acheni kuwadhalilisha wapiganaji hodari wa Tanzania!
Mi nachojua Kagame ndo chanzo cha vita kule Congo kwa kuwaibia rasilimali zao na mwisho kuwaua.

Haimaanisha kuwa ni mzuri na tuendelee kumshabikia eti tu kisa alisaidia katika vita vya kumng'oa Iddi Amin.
 
Kumbe Kagame ni mmoja wa mashujaa wetu halafu hawa watu wengine wasaliti wanataka kuiandika historia upya?Hawatafanikiwa kamwe na Kagame atalindwa kwa gharama zote na Watanzania.Wanasiasa wasio wazalendo siku zote huwa wasaliti.Nilijua tu Kagame alikuwa innocent.
Wacha uongo wewe, Kagame alishiriki chini ya museven kwa lengo na tamaa za kitutsi kukamata dola. jwtz ilikua na uwezo wa kumtosha amin nje ya mipaka ya tz lakini waganda waliungana kumwondosha amin ndio maana jwtz likavuka mipaka kuwasaidia. Katika msafara wa mamba na kenge wako.
Kwa nini kagame na museveni ni waroho wa madaraka kama walivyo watutsi wote! Baada ya obote kushinda uchaguzi na museveni kushindwa vibaya alikataa matokeo na kuanzisha vita akiwashirikisha wakimbizi wa kitutsi kutoka rwanda. Walisababisha vifo vingi na maafa makubwa uganga. Walirudiarudia uongo mara nyingi na ni hodari sana wa propaganda hadi wengi kuamini obote na chama chake waliiba kura.
Si uongo 1959 kwa sababu za kihistoria watutsi walitendewa uovu mkubwa na wakawa wakimbizi kwa wingi , lakini kama walivyo wayahudi wamejenga uzalendo wa kimbari kwa lengo la kukamata dola popote wanapoishi maziwa makuu.
 
Kagame is a hero of Tanzania during Idd Amin war,Where was this fool Mtikila during that war.He was hiding in the holes somewhere while Kagame and other soldiers were fighting for the respect and image of our country.I hate the guy who is using Mtikila to demonize Nyerere,No wonder his administration has turned out to be a total failure.

Soma comment yangu hapo juu na ufuatilie link. Kagame tumemfundisha jeshi baada ya vita vya kagera. Kipindi hicho cha vita hakujua chochote. Hajawahi kutoa msaada wowote kwa Tz. Hana tofauti na Osama aliefundishwa na Marekani halafu akawageuka. Hata roho zao zinafanana. Tena Osama anaweza kuwa na nafuu
 
Huna hoja yenye mashiko yakuni shawishi kuku sadiki zaidi naona nijinsigani ulivyo mzalendo kwa taifa lako la Rwanda. Umeshindwa kupinga kwakutumia ushahidi yale aliyo yasema mzalendo na shujaa wetu wa Tanzania, hivyo wewe ni kati ya wale 35000 alio wazungumzia mzalendo Mtikila. Nenda kamwambie hiyo muuwaji (kagame) mbinu zake tushazijua michozoyake michafu tushaisoma hivyo tunamlia timeng tu kabla hatuja muonesha kilicho mtoa kanga manyoya.
 
Mkuu kusema wakoloni waliwapa elimu wakristo kuliko waislamu ni muendelezo wa uchochezi unaolekea kuota mizizi!
Inawezekana una lengo jema ktk makala yako hii lakini umenitia shaka uelewa wako wa historia kwa hii kauli yako!
1) tambua huu mtandao unatembelewa na watu wasiopungua laki 2 kwa siku hivyo lazima uwe makini na kalamu yako
2) Simama kwenye ukweli maana hayo maafa unayoona Mtikila anachochea kama alivyosema Mh Kagame pia kupitia maandiko yako unafanya kile kile!
 
Nimeishia hapo tu uliposema elimu kuwa kwa wakristi wengi kupita waislam ilikuwa ni kuwagawa waTanzania.

Wewe ni PINDA Mkubwaa kwa kuandika Hisia zako.

1. Kama unataka historia ya Wahutu na Watusi kwa nini unaanzia alipo kuja Koloni, Inamaana kabla ya Mkoloni maisha hayakuwepo?

2. Unasahau kuwa Wamision walipokuja walikuja na Hizo shule kwa maana walikuwa wana eneza Elimu Dunia na Dini. Waarabu walipokuja walieneza Dini tu Bila Elimu na Hilo Linaendelea mpaka leo kwani Waislam tunakomaa na Elimu Ahera wakati Wakristo wanakomaa na zote Ahera na Dunia.

3. Alafu huo waraka ndio mnauona leo? Mbona upo sikunyingi sana humu? Mlikuwa wapi sikuzote watanzania nyinyi kumtetea Kagame, Ghafla juzijuzi mmekuja humu wengiwengi kujibu hoja.

Mwisho nachojifunza wewe ni Mnyarwanda tena Mtusi na umekuja humu baada kutumwa na Kagame, Naona mnakuja kupima Kina cha Maji ila kamuambieni Kagame Amenoa asifikiri kila mtu ni Kichwa cha NaZi.
Kama ungekuwa Mtanzania huna haja ya Kujiita Tanzanianist ili sisi tukuamini.
 
Mkuu kusema wakoloni waliwapa elimu wakristo kuliko waislamu ni muendelezo wa uchochezi unaolekea kuota mizizi!
Inawezekana una lengo jema ktk makala yako hii lakini umenitia shaka uelewa wako wa historia kwa hii kauli yako!
1) tambua huu mtandao unatembelewa na watu wasiopungua laki 2 kwa siku hivyo lazima uwe makini na kalamu yako
2) Simama kwenye ukweli maana hayo maafa unayoona Mtikila anachochea kama alivyosema Mh Kagame pia kupitia maandiko yako unafanya kile kile!

Huyu ni Mamluki wa Kagame, walikuwa wapi sikuzote kumtetea? Kagame humu? Kuna opic ngapi humu za kumponda kagame na zimekuwapo miaka yote na hatukuwaona hawa watu, Leo ghafla wapo kibao, Wanatoka wapi hawa!
 
Huyu ni Mamluki wa Kagame, walikuwa wapi sikuzote kumtetea? Kagame humu? Kuna opic ngapi humu za kumponda kagame na zimekuwapo miaka yote na hatukuwaona hawa watu, Leo ghafla wapo kibao, Wanatoka wapi hawa!

Yangu macho ila kumbuka Kagame ana mkono mrefu hahaha!
 
Back
Top Bottom