Ukweli kuhusu Rwanda na Kagame kwa ujumla (tofauti na wengi wajuavyo)

Madesa wewe ni researchers wa ukweli au magumashi.

Ni kama una lako jambo vile, maana usingekuwa nalo story ingebalance, now its a one sided story from a 'researcher' ....

Ntakubishia si kwa sababu nimefika Rwanda bali taarifa yako haikidhi mizania ya mtafiti, ingawa pia mie sio mtafiti.

Kwa mfano:

1. Watu kujua wizara ya elimu iko wapi researcher Madesa anahusisha na kuelimika kwao???? Zaidi ya nusu ya watu mliowauliza walikiwa hawajui wizara iko wapi.
Ilikuwaje watu karibu ya nusu (wanaopajua wizarani) mliowauliza na bado hamkufika wizara ya elimu. Kama sio urongooo!!

2. Reseacher unashangaa enrolment rate ya 97%. Ulipata kujua gross enrolment rate ya Tanzania miaka ya 70?? Ulipata kusikia UPE?? Je sasa enrolement ya Tz ni ngapi ktk MDGs??? Unakimbilia kutupa story za marekani (eti hata marekani haijafikia 97%) ambako sie tunaona kwenye Tv tu.

3. Unasema swala la laptop haliwezekani kwa vile hakuna umeme wakati kuna samsung za kutumia sola hata kampuni ya Tigo wanagawa siku hizi.

4. Ni kweli wanyarwanda hawajui kinachoendelea serikalini?? Je watanzania tunajua kinachoendelea serikalini na kama twajua imetusaidiaje???

Sasa badala ya kuleta matokeo ya utafiti wako unaleta story za mtaani, mara mia wanaotujuza viota vya maraha ndani ya Kigali kuliko taarifa ya msomi ambaye hakuelimika....watafiti kama wewe ndio mmejaa Ikulu yetu ndio maana mambo hayaendi.

Samahani kama nitakukwaza...........

anatakiwa angalau akasome kitabu cha cothari.
 
Wewe ni muongo kama shetani! Mimi nilifanya kazi Ngara katika makambi mbalimbali ya wakimbizi wa Rwanda na kulikuwa na kambi maalum ambazo zimetengwa kwa ajili ya watusi na wahutu waliooana!

Kuanzia leo nitakuogopa kama ukoma!

wewe ndo muongo. mwisho wa kambi za wanyarwanda ngara ilikuwa 1998, sasa hivi ni 2012. hauoni tofauti? kagame kaua WAPINZANI WAKE wengi kupitia mahakama za GACHACHA. Wewe unaongelea maisha ya kambi za BENACO NA RUMASI. sasa hivi wapo kwa KAGAME.
 
Mkuu Madesa,

Nimejaribu kufuatilia thread yako kuhusu Rwanda nimeona umejaribu kukielezea kile ulichokiona Nchini Rwanda lakini ni vizuri nikuweke wazi ktk mambo ambayo nimeona umezidisha mno chumvi....

Kwanza mimi ni Mtanzania ambaye nimeishi Rwanda kwa zaidi ya Miaka 15...(Remera Jirani na Meg Gen Rwahama).na pia huwa naenda sana Rwanda kwa sababu kuna vitega uchumi vyangu..

1. Mradi ule wa Laptop haukufeli sababu ya Rushwa...Nadhani kwa sababu umekaa Rwanda utakuwa umepata picha kamili kwamba Rwanda nayo ikiwa kama mojawapo ya nchi za kiafrika ina Idadi kubwa ya maskini (Wahutu ni wengi na ndio maskini) kuliko watu wa Tabaka la kati na la juu..Hivyo ilifika kipindi uhalisia ukajitenga na njozi.
Nakusisitizia kwenye suala la Rushwa Rwanda iko makini na usiifananishe na hiki ki-nchi chetu ambacho kimefikia hatua kwamba ukiwa kiongozi ambaye si mla rushwa wala mtoa rushwa unaonekana kitu cha ajabu...

2.Kuhusu kutokujua ilipo wizara ya elimu hilo linaweza kutokea popote pale na ktk nchi yoyote ile...Mfano hapa Tanzania watu wengi hawaifahamu ilipo wizara ya elimu...Lakini Taasisi kama Baraza la Mitihani la Taifa na Chuo kikuu cha Dar es salaam hususani kampasi ya mlimani vinafahamika sana...Ina maana kwa mtu ambaye yupo Rwanda na hajui wizara flani ilipo anaweza akakuelekeza uende MINISTERI..sehemu ambayo kuna wizara karibu zote za nchi hiyo.

3.Kuhusu kutapakaa kwa wanajeshi jijini Kigali..sidhani kama ni Issue...Kwani Rwanda wamejifunza kutokana na makosa ikifika saa 12 jioni kuna Doria zilizo serious...Tofauti na hapa kwetu ambapo unakuta Majambazi wanakusanya fedha mchana kweupe na kituo cha polisi kipo umbali ambao hauzidi hata mita 500...Na ni nadra sana kukuta walevi wanaendesha magari Rwanda kwani ndugu yangu lazima utapimwa Alcohol uliyonayo..

Hawa jamaa wametuzidi...wao wapo serious kwenye mambo yaliyo serious....full stop.

Mkuu mbezibeach 2
Hapo napo pana shida tena ile wizara haipo MINISTERI na wengi wao hujua hivyo na nakumbuka niliuliza mpaka wanafunzi wa school of finance and bness ya Kigali wahakujua ilipo, na kuhusu rushwa kwa kweli wamejitahidi lazima na hili utaliuona ukianzia mpakani ila bado ipo ndani ya some gvt officials ila na kuhusu ule mradi wa laptop unahusishwa na rushwa ya yule waziri aliyeongeza cha juu kwa kila laptop itakayoletwa na supplier ila dili likabumbuluka na kuishia kukimbia makucha ya mkuu(fuatilia hili) na vilevile wanyarwanda wengi hawachukulii wale askari kama walinda amani wanasema wanawatisha mno, hata mimi kwa kweli huwa sina amani nikiwaona ingawa ni askari waungwana.

Nakumbuka kuna mtanzania mwenzangu siku moja alikamatwa na wale wanajeshi eti kisa kapiga picha maeneo ya pale Kigali stand bado mi nadhani ile ni amani ya kulazimishwa haitokani na upendo wa wananchi, eti kuna prof wa Oxford anasema Rwanda iko juu kiuchumi kwa sababu ya kahawa inayozalisha hivi jamani hili nalo linataka kuwa mwanauchumi kung'amua?ni kiasi gani wanachozalisha na Uganda nao wasemaje?halafu kingine mbona yale makampuni makubwa ya kahawa pale yanamilikiwa na wamarekani?(kodi?).

Ni kweli kuna mazuri ya kujifunza kutoka kwa majirani zetu lakini si kwa kiasi hiki waandishi wetu wanavyoandika baada ya kusoma kutoka kwenye vyombo vya habari vya Rwanda, hivi kuna CHANNEL FIVE Rwanda?na kwa nini haipo kama haipo?
 
wewe ndo muongo. mwisho wa kambi za wanyarwanda ngara ilikuwa 1998, sasa hivi ni 2012. hauoni tofauti? kagame kaua WAPINZANI WAKE wengi kupitia mahakama za GACHACHA. Wewe unaongelea maisha ya kambi za BENACO NA RUMASI. sasa hivi wapo kwa KAGAME.

Mahakama za GACACA zinaruhusiwa kutoa hukumu ya kifo? Hizo ni mahakama za kijadi na kuna aina fulani ya makosa ndio husikilizwa kesi zake lengo likiwa ni kupunguza msongamano wa kesi na watuhumiwa wa makosa ambayo ni less grave wasikae jela (ambazo zilikuwa zimefurika watuhumiwa wakati fulani). Kesi zote kubwa hupelekwa mahakama za juu ambazo ni za kawaida. Ingekuwa hivyo UN ingekubali kesi zilizosalia Arusha zipelekwe Rwanda? Kwani sababu ya kuanzisha ICTR ilikuwa nini?

Fanya utafiti mkubwa. Mbona habari za Rwanda nyingi zipo kwenye public domain?
 
Rwanda ni maskini tena sana.
:Rwanda asilimia kubwa wanategemea kilimo, na kule sehemu ya kulima hawana hata ya kufuga mifugo. ndo maana unasikia wanyarwanda mifugo yao wanafugia Tanzania(ngara na karagwe).
:Wanyarwanda hawapo huru. ni kama wafungwa. Ukitaka kusafiri lazima utoe taarifa serikalini. kwa mfano, wafanya biashara wa mpakani wakitaka kuja kununua vitu vyao Tanzania wanaacha kitambulisho mpakani pale Rusumo hadi atakapo rudi. Ukabila bado upo, sema hawasemi hadharani kuogopa kukamatwa.
 
Kama tuna researchers wa namna hii, bac tuna zaidi ya safari ndefu jamani kufikia huko kwenye social development kupitia kwa social researcher wa aina hii. Yaani wee unajiita researcher then unatoa conclusion just kwa kumuuliza mschana ikiwa aweza kuolewa na mhutu/mtusi? Yaani unatoa conclusion ya ujinga wa watu kwa kuwa wee umetoka ulikotoka then ukafikia lets say manzese na kuwauliza wakazi ulioamua mwenyewe wakuonyeshe ilipo Wizara ya elimu na wao kusema hawaijui then ukawapa na ujinga watanzania wote!? enh are you researcher? Na je ingelikuwaje ikiwa mtu wa kwanza kumuuliza angelikuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu ya Rwanda, then angekuonyesha halafu ungelikuja hapa kukonkudi kuwa jamaa wameerevuka sana sio?
Sijui ujumbe wako hasa ni nini kwa watanzania lakini tunachotaka kukwambia ni kwamba hakuna aliyesema kuwa Rwanda ni developed country lah, ila tukubaliane kwamba indicators za kuendelea zinazoonekana Rwanda zinaiacha mbali mno Tanzania. Fortunately Rwanda ni miongoni mwa nchi nilizotembelea mara nyingi kabla na baada ya mauaji ya 1994 hivyo hakuna ubishi kuwa the guys are doing well. Na kwanini hukuuliza juu ya mfumo wa uundaji wa vyama vya hiari lazima uhusishe wahutu na watutsi ndipo upate usajili, au huliju hili? Na vipi ule mfumo wa kuainisha maeneo vivutio kwa uwekezaji mijini kisha kuwafidia wakazi wake kama ilivyofanyika pale round-about kubwa panapojengwa kituo cha kuassemble computer accessories? Na vipi hili shirika lao la Ndege Rwandair express unalielezaji, je na yale majengo blue yanayokuwa kila kona tofauti na kule bongo ambapo lazima Samoar/Jamhuri/Ghana/Pamba? Kajipange halafu uje tena mkuu.
 
Mahakama za GACACA zinaruhusiwa kutoa hukumu ya kifo? Hizo ni mahakama za kijadi na kuna aina fulani ya makosa ndio husikilizwa kesi zake lengo likiwa ni kupunguza msongamano wa kesi na watuhumiwa wa makosa ambayo ni less grave wasikae jela.



Mkuu lengo lilikuwa hilo la kuianzisha lakini sivyo ilivyo fanya kazi. ile mahakama iliwalenga Kuwaangamiza WAHUTU TU, ndo maana hamna MTUTSI hata mmoja aliye hukumiwa iwe RWANDA(GACHACHA) au ARUSHA(ICTR).
 
Kama tuna researchers wa namna hii, bac tuna zaidi ya safari ndefu jamani kufikia huko kwenye social development kupitia kwa social researcher wa aina hii. Yaani wee unajiita researcher then unatoa conclusion just kwa kumuuliza mschana ikiwa aweza kuolewa na mhutu/mtusi? Yaani unatoa conclusion ya ujinga wa watu kwa kuwa wee umetoka ulikotoka then ukafikia lets say manzese na kuwauliza wakazi ulioamua mwenyewe wakuonyeshe ilipo Wizara ya elimu na wao kusema hawaijui then ukawapa na ujinga watanzania wote!? enh are you researcher? Na je ingelikuwaje ikiwa mtu wa kwanza kumuuliza angelikuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu ya Rwanda, then angekuonyesha halafu ungelikuja hapa kukonkudi kuwa jamaa wameerevuka sana sio?
Sijui ujumbe wako hasa ni nini kwa watanzania lakini tunachotaka kukwambia ni kwamba hakuna aliyesema kuwa Rwanda ni developed country lah, ila tukubaliane kwamba indicators za kuendelea zinazoonekana Rwanda zinaiacha mbali mno Tanzania. Fortunately Rwanda ni miongoni mwa nchi nilizotembelea mara nyingi kabla na baada ya mauaji ya 1994 hivyo hakuna ubishi kuwa the guys are doing well. Na kwanini hukuuliza juu ya mfumo wa uundaji wa vyama vya hiari lazima uhusishe wahutu na watutsi ndipo upate usajili, au huliju hili? Na vipi ule mfumo wa kuainisha maeneo vivutio kwa uwekezaji mijini kisha kuwafidia wakazi wake kama ilivyofanyika pale round-about kubwa panapojengwa kituo cha kuassemble computer accessories? Na vipi hili shirika lao la Ndege Rwandair express unalielezaji, je na yale majengo blue yanayokuwa kila kona tofauti na kule bongo ambapo lazima Samoar/Jamhuri/Ghana/Pamba? Kajipange halafu uje tena mkuu.
 
Mkuu lengo lilikuwa hilo la kuianzisha lakini sivyo ilivyo fanya kazi. ile mahakama iliwalenga Kuwaangamiza WAHUTU TU, ndo maana hamna MTUTSI hata mmoja aliye hukumiwa iwe RWANDA(GACHACHA) au ARUSHA(ICTR).

Angalia victim wengi walitoka upande upi na utapata jibu la swali lako. Watawala walikuwa Wahutu, kwa hiyo sio ajabu kukuta washitakiwa wengi ni Wahutu maana mauaji yaliwalenga Watusi na moderate Wahutu. Unataka na victims wapelekwe mahakamani (GACACA, ICTR or otherwise)? Unataka kutuambia kuwa UN wangehamishia kesi zilizobaki Rwanda kutoka Arusha kama hayo madai yako ni ya ukweli?
 
Kuna rafiki yangu mrwanda, alishaniambia mengi yanyosemwa kwenye media si kweli, ni propaganda za serikali.
 
Kuna rafiki yangu mrwanda, alishaniambia mengi yanyosemwa kwenye media si kweli, ni propaganda za serikali.


watu wengi mnamshambulia mtoa mada na kuacha kuangalia/kujadili yaliyomo katika post yake. Mimi sijafika rwanda lakini naishi na wanyarwanda nje ya tanzania (wako huku kimasomo). Kwa muda niliokaa nao na kuzungumza nao Rwanda kuna tatizo kubwa-Uhuru wa watu kujieleza na hata kuishi uko mikononi mwa Kagame. Kwa maelezo ya huyu jamaa; yeye ni daktari; Rwanda hakuna mtu anayerusuhiwa kueleza matatizo ya nchi hiyo kwa mtu wa nje (mf. huyu jamaa haruhusiwi kusema kuwa kuna ugonjwa/mlipuko wa kipindupindu, ni waziri wa afya pekee anayeweza kufanya hivyo. sababu moja ya kufanya hivyo ni kuepuka ku discourage wageni). Kila anaposafiri nje ya nchi; watu wa usalama wa taifa wanafanya uchunguzi kujua umeenda wapi, kufanya nini na ulipokuwa huko umeongea na nani-hii aliambiwa na rafiki yake aliyeko UWT baada ya kutoka safari moja alipoenda Zambia. Ukiwa rwanda (mtoa mada amesema na huyu jamaa alinieleza hivyo) mkisha kuwa zaidi ya watu wawili hakuna atakayethubutu kuongelea siasa au uchumi/maendeleo ya rwanda (hofu kubwa ni kuwa katika kila watu watatu uwezekano mkubwa miongoni mwao yupo shushushu). pamoja na mambo mazuri tunayosoma kuhusu Rwanda; kuna mengi ambayo yamejificha; ukisoma makala nyingi (vyombo vya habari vya marekani nauingereza)utaona wanahusisha ukuaji wa uchumi wa Rwanda na kupanda kwa bei ya kahawa; Lakini inashangaza hali hiyo imetokea kwa Rwanda tu, na sio Tanzania, Uganda, Ethiopia nk. Wanyarwanda pia hawajawa wamoja ndani na nje ya Rwanda; ulaya (na hakika pia hali iko hivyo marekani nk) bado hawa jamaa wana socialize kikabila-Bar/pub za wahutu na watutsi hawachanganyiki.
 
Acha kuchanganya mada hapa! Kinachojadiliwa hapa ni maendeleo ya Rwanda katika sta mbalimbali na si Kagame alimuua Habyarimana au wahutu kuuwa watusi. Jadili elimu, kilimo, viwanda nk

Wewe hujaelewa mada, mleta mada ameongelea rwanda in general, amejumuisha vitu kama uhuru wa vyombo vya habari, uhuru wa watu wa rwanda ndani ya inchi yao na vit2 vingine, ndio maana mada inasema ukweli kuhusu rwanda,mimi si mbishani,I just added weight to corroborate what has been presented by my colleague,nimechangia mada kiusahihi kabasa kwa kuongeza ukweli kuhusu rwanda, nilichoweka ni kuendeleza kutoa data kuhusu rwanda, tatizo letu watanzania ni wavivu kutafuta ukweli wa mambo, kutafakari vitu unavyoambiwa, kazi kubishana kivyama hata mada zisizohusu vyama, mnageuza jukwaa kama sehemu ya mipasho, I wish upate access ktkjukwaa la premium members ujifunze kuwa great thinker mkuu, acha mipasho, jadili hoja,changia mada toa ushahidi wa unachoongea ndio kusudio la jf,Invisible amegonga thanks ktk mada hii,ujue ni mada nzuri kujadiliwa ndugu yangu
 
Angalia victim wengi walitoka upande upi na utapata jibu la swali lako. Watawala walikuwa Wahutu, kwa hiyo sio ajabu kukuta washitakiwa wengi ni Wahutu maana mauaji yaliwalenga Watusi na moderate Wahutu. Unataka na victims wapelekwe mahakamani (GACACA, ICTR or otherwise)? Unataka kutuambia kuwa UN wangehamishia kesi zilizobaki Rwanda kutoka Arusha kama hayo madai yako ni ya ukweli?

kilichopo ICTR na Gacaa ni kiini macho, inaonyesha ni kwa jinsi gani mambo yamepangwa, ICTR ilianzishwa ili kuprosecute wahusika wa vita za rwanda na si wahusika wa serekari iliyokuwa madarakani kwa wakati vita inafanyika, moja ya maswali ambayo jumuiya ya kimataifa imefeli kujibu na haitaki ni hili la prosecution kuwa ya upande mmoja, ktk kesi za mwanzo kabisa zilizokuwa hot ni ya AKAYESU,na JEAN KAMBANDA(Tafuta ICTR Jurisprudence au ingia humanrights watch/ictr jurisprudence), ambazo maamuzi yake yalidhibitisha kuwa kulikuwa na vita ndani nchini rwanda(Internal Armed Conflict)sasa kama kulikuwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe, inakuwaje genocide iwe defined interms kama mauaji ya upande mmoja,
 
Ukweli wa machache nnayo yajua mimi ni huu,

ELIMU:

Ule mradi wa laptop moja kwa kila mwanafunzi umefeli kwa sababu ya Rushwa na ilikuwa ni ndoto kutimia kwani zaidi ya nusu ya shule zao hazina umeme, walikuwa wana system kama ya kwetu kutoa mikopo lakini kuanzia mwaka jana serikali imejitoa kudhamini wanafunzi wa elimu ya juu hivyo basi wazazi wanatakiwa wawalipie watoto zao sual hilli limeleta mtafaruku mkubwa Rwanda ila kwa kuwa sheria zao haziruhusu maandamano hakuna aliyepinga hadharani,Wanyarwanda wengi hawajui chochote kinachoendelea kwenye serikali yao, ntafafanua,

Mwaka juzi nilikuwa Rwanda tukiwa tunafanya research ni kuhusu elimu chini ya NGO moja iliyokuwa inataka kujenga shule vijijini.
Maajabu ni kwamba zaidi ya nusu ya watu tuliowauliza watuelekeze wizara ya Elimu ilipo walikuwa hawajui ilipo na cha zaidi vijana wa Kigali wengi wao walitupoteza na kutupeleka mahali ambapo sio au wizara tofauti kabisa, mwisho wa siku kwa tabu sana na hapo napo tulipata ajabu la pili, tulikutana na naibu waziri wa elimu mama mmoja mrembo sana na tulichotaka kutoka kwake ni kutaka kujua ni wapi kuna uhaba wa shule ili tukajenge huko, mama yule akasema kwa yeye Rwanda ni moja hawezi akataja eneo kwani akisema kusini watu wa mashariki watakasirika?!! Mwisho wa siku akasema hajui ni maeneo gani twende ila akatushauri twende kwa wa kuu wa viijij au tewnde ubalozi wa Marekani kuna mtu wa USAID anaye husika na elimu huyo ana data zote za Rwanda, tukasema haya, swali la pili kwake likawa je ni asilimia ngapi ya wanafunzi wanaandikishwa shule kwa mwaka akasema 97% na hiyo 3% inayobaki ni ya watoto ambao wanamapungufu akimaanisha vilema, jamani hata nchi za ulaya na Marekani hawajafikia 97% huo ni uongo mtupu na hakujua kuwa zaidi ya mwezi mzima tulikuwa viunga vya Kigali tukiwahoji watoto wa mitaani ambo hawasomi, Jamani Rwanda si kama tusomavyo kuna omba omba wengi kama miji yetu watoto wa mitaani wapo kila kituo cha daladala wakisumbua abiria kuomba pesa.

Turudi ubalozi wa USA, huko tukakutana na huyo jamaa wa elimu, ofisa yule akasema yeye naye kusema ukweli hajawahi kutembelea kijiji chochote kile analetewa data tu hivyo basi tutafute njia nyingine ya kupata data hizo, nikajua labda ni mpango wa kutokutaka kutupa data lakini si kweli wale watu wanashinda ofisini tu hawajui nini kipo mtaani na hata Kagame nae yupo hivyo hivyo.

UHALISIA WA RWANDA:

Ni nchi mojawapo ambayo wananchi wake wanaishi kwa hofu vibaya mno, ukiwa Rwanda huruhusiwi kuongelea vita ya wahutu na watutsi eti serikali imekataza inataka isahau ila makabila haya mawili yana chuki ambayo si rahisi kusahauluka kuna siku nilikuwa kwenye daladala na rafiki yangu mmoja toka Kenya nikawa namuuliza maswali kuhusu Wahutu yule jamaa hakunijibu na abiria wote walinigeukia kutaka kujua nani kataja neno hilo ikanibidi niongee kiswahili ili kuonyesha mimi ni mgeni na nikasameheka kwa hilo,siku nyingine nikamuuliza msichana wa Kitutsi kama ipo siku anaweza akaolewa na Mhutu akasema hilo halitatokea kamwe kwa chuki aliyonayo na nikagundua kuwa hata NGO iliyonipeleka pale members wote ni watutsi!!! na wakasema kama wahutu walishawahi kuongoza NGO hiyo na hakukuwa na Mtutsi, pata picha, kila ikifika saa kumi jioni Kagame anapeleka majeshi mtaani eti kulinda amani mpaka kesho yake, utaona matruck ya jeshi ya kimwaga askari mitaani wakiwa kwenye mstari mmoja na mikononi wana AK47, fingers on the triger, staili hiyo Kigali inaitwa SINGLE FILE SYSTEM hasa na vijana.

Rwanda naweza kusema ni koloni la Marekani na nchi inayopumua kwa misaada ya USA hakuna nchi East & Central Africa yenye international NGOs kama ile, wananchi wengi wameajiliwa huko, kuna kampuni kubwa chache sana na makampuni hayo yanamilikiwa na wamarekani na hata maofisa wake wengi wamesomea huko akiwa yeye mmoja wapo na kwa taarifa yenu ni kuwa raisi na rafiki zake wanamiliki kampuni karibuni zote kubwa za Rwanda kupitia kampuni yao ambayo kazi yake ni kununua kampuni nyingine.hivyo basi ni miongoni mwa matajiri wakubwa kabisa nchini kwake.

Jamani Rwanda kumetapakaa umasikini mambo yote mnayosoma kutoka Rwandan media yote yamekuwa screened by the government, Rwanda hakuna freedom of media, na sidhani kama kuna private tv/radio zaidi ya mbili,kama moja ipo, ile nchi inaendeshwa na misaada zaidi ya 80%,kodi zao ziko juu zaidi ya kwetu, kuna stori nilipewa kuwa wahisani walikuja kukagua mradi wa barabara na serikali haikutekeleza hilo walichokifanya ni kufumua lami nzuri na kuweka nyingine ili kuonyesha pesa ilipoenda, mpaka mwaka juzi walimu walikuwa wanalipwa wastani wa 42$ kwa mwezi,mpo hapo?

Mpaka leo hakuna anayemjua mrithi wa Kagame ila kuna tetesi anaweza akawa mtoto wake ambaye yupo USA in one of the best millitary academy ambako amesomea baba yake, kama umeshawahi kusikia kule kuna upinzani wa kweli basi tujadili, ana kashfa ya kuwapoteza wapinzani wake na juzi juzi Uganda ililalamika kuwa anatuma majasusi wake nchini humo.

Kwakuwa muda umenitupa kwa leo naishia hapa, ila ukipatamuda vuka mpaka hata kwa wiki 1 tu ukajionee nilichosema ila jiandae kwa matumizi kwani chakula ni gharama nadhani mara tatu ya hapa na hapa sizungumzii kwenye hotel kubwa, asante.

Nina hofu sana kama kweli hiyo NGOs inweza kwenda moja kwa moja kwa wananchi tena wa vijijini na kuanza kuuliza maswali hayo. 2. siamini pia kama naibu waziri anaweza kutoa majibu mepesi kiasi hicho. mtoa maada ana lake jambo!
 
Je unajua kuwa mwaka jana Kagame aliwaita watutsi wote wanaosoma vyuo vikuu vya ndani na Nje ya Nchi kuwanong'oneza kuhusu kutawala daima na kuwapa mafunzo ya kijeshi?!!

Kagame na serikali yake wanatawala NGOs zote Rwanda kila NGOs lazima iwe registered kila mwaka! na kueleza wanafanya nini! Anawalazimisha NGOs watoe "handouts" misaada midogo midogo kwa wananchi nchi ili kuwapumbaza. NGO moja imelazimishwa kununua ng'ombe wa maziwa kwa wananchi.

Dictator Kagame amegundua namna ya kuishi na wazungu ili kujenga umaarufu.

Bora 'Dictator' Kagame anajua kuishi na wazungu, hata inafikia point wananchi wanaweza kupewa ng'ombe wa maziwa.
Sasa huyu baba mwanaasha wenu pamoja na kujikomba kote kwa wazungu amepata nini?
Kagame amejitahidi kwa kiwango chake, uwezi kumfananisha na jamaa yetu!
 
Intelijinsia ya Kagame inaogopesha! Nahofu asiwe amepenyeza majasusi hadi TISS,Polisi na JWTZ! Acha Wanyarwanda waogope maana wananusa kuliko tai weusi!
 
Wewe ni muongo kama shetani! Mimi nilifanya kazi Ngara katika makambi mbalimbali ya wakimbizi wa Rwanda na kulikuwa na kambi maalum ambazo zimetengwa kwa ajili ya watusi na wahutu waliooana!

Kuanzia leo nitakuogopa kama ukoma!

Unamuogopa bure, ukweli ni huo. Hakujawahi kuwa na kambi ya wakimbizi zilizowahifadhi watusi na wahutu waliooana. Nitajie kambi hiyo ya wakimbizi iliitwaje.
 
Kuna rafiki yangu mrwanda, alishaniambia mengi yanyosemwa kwenye media si kweli, ni propaganda za serikali.

Kuna rafiki yangu mrwanda alishanambia mengi yanayosema kwenye media ni kweli wala si propaganda za serikari!
 
Madesa, angalia upande mwingine wa shilingi uone jinsi wasomi wanavyoiona Rwanda:
The small African nation of Rwanda recently announced that it had cut poverty by 12% in six years, from 57% of its population to 45%. That equals roughly a million Rwandans emerging from poverty -- one of the most stunning drops in the world.
Laiti ungemwelewa mtoa mada, basi wala usingeleta hii hoja....hebu angalia hapo kwenye red...."Rwanda, recently annocuned....!" Hivi unapata shida gani hapo kufahamu kwamba huo si uhalisia bali ni serikali ndio ilitangaza?! Kama umemsoma vizuri mtoa mada, anasema kwamba baada ya kwenda kwa mtu wa USAID, huyo jamaa wa USAID akasema kwamba "analetewa tu data...!"
It's a remarkable achievement for Rwanda, which has emerged from civil war and a bloody ethnic genocide in the 1990s. How did it happen? The Times quizzed Paul Collier, director of the Center for the Study of African Economies at Oxford University, about the numbers.
Yaani remarkable achievement from wht the government announced!"
Are there any doubts that the drop is real?
No doubts; I know the economics professor
who did the data analysis, and he is highly experienced and painstaking, so it is genuine.
Hapa nashawishika kumwamini mtoa mada. Hoja yangu ni ile ile, kwamba mtoa mada alipokutana na mtu wa USAID, akaambiwa huyo mtu yeye uletewa tu data!! hapa tena, tunamuona Professor akisema " I know the economics professor who did the data analysis....!" Huyo Economic Professor ndie alifanya Data Analysis; so who collected the data?! How realiable were the collected/submitted data?! Don' you know the difference between Data Collection and Data Analysis?! Kwa Bahati , mie nimeshawahi kufanya yote hayo mawili na kwa ujumla wake; yaani, Data Collection, Data Analysis as well as Data Collection and Analysis! Hilo la pili ni kwamba, kuna mtu mwingine kabisa ambae amekusanya Data, tena si ajabu hata kumfahamu humfahamu na wewe unaishia tu kufanya data analysis!! Data Collector ndie anayeuona ukweli ambao si lazima auandike sawa na alivyouona!! Therefore, kama huyo bwana alifanya Data Analysis na si yeye aliyefanya Data Collection, then hapo hamna genuity yoyote coz' kwani we're not sure kama huyo Data Collector alifanya hiyo kazi professionally au alijifungia tu chumbani na kupika hizo data! Na hata anapomalizia " so it is genuine" inaonesha wazi kwamba haja-base kwenye scientific conclusion!!
My take: Ukiona wazungu wanakusifia sana, basi ujue hapo kuna tatizo. Rwanda wanasifiwa sana na wazungu kutokana na kuondoa urasimu....hata mimi nawasifia sana kwa hilo! Hata hivyo, lazima tukumbuke kwamba hivyo ndivyo watakavyo wazungu kwa nchi za wenzao...yaani waingie tu na kutoka kadri watakavyo lakini si wewe ufanye hivyo kwenye nchi zao! Ngoja leo serikali ya JK iondoe restrictions za kuingia nchini "kufanya uwekezaji!" Ngoja leo serikali ya JK iondoe Visa restriction kwa hao wanaojiita wawekezaji....ngoja leo pasiwe na restriction ktk upatikanaji wa ardhi....na mambo mengine kama hayo! I am telling you, within one months, itatangazwa kwamba TZ ndio sehemu bora kabisa duniani katika kufanya uwekezaji (katika kuiibia)!! Huyu JK leo anayeesemwa vibaya, atasifiwa kila mahali na wazungu! Ni nani asiyekumbuka jinsi Ben Mkapa alivyokuwa anasifiwa na wazungu hadi kupewa cheo cha Mwenyekiti Mwenza wa Utandawazi?! Hili lilifanyika baada ya kuwa Mkapa ameuza mashirika yote na kuruhusu wazungu wachukue kila tone la dhahabu kwa ujira mdogo!! YUle Morgan Tsivangrai (not sure wit spelling) wa Zimbabwe wakati akiwa kiongozi wa wafanyakazi alikuwa anapondwa sana na wazungu na kuambiwa si lolote si chochote na kwamba hajasoma!! Enzi hizo alikuwa mwiba mkali kwa wazungu kwavile ndio walikuwa wawekezaji wakubwa hususani kwenye kilimo! In short walikuwa hawampendi kabisa! Baadae wazungu hao hao wakaja kuwa rafiki mkubwa wa Morgan baada ya Morgan kuondoka kwenye uharakati na kumpinga Mugabe ambae aligeuka kuwa mwiba kwa wazungu! In short, ukiona kiongozi yeyote wa dunia ya tatu anasifiwa sana na wazungu basi fahamu kwamba hapo kuna tatizo! Wazungu kamwe hawatakuja kumsifia kiongozi yeyote anayeenda kinyume na matakwa yao hata kama anafanya hivyo kwa maslahi ya wananchi wake! Hivyo basi, ukweli unabaki pale pale kwamba Rwanda si lolote si chochote.Kama mwezi mmoja hivi uliopita nilikutana na dada mmoja Mnyarwanda ambae yeye mambo yake si mabaya! Alikuja Dar kwa mapumziko...niliongea nae mengi sana kuhusu Rwanda, ajabu ni kwamba yale tunayoyasikia kwenye vyombo vya habari ni tofauti kabisa na jinsi dada yule alivyonieleza!
 
Wewe huna tofauti na "wajinga" wenzio wanaodai kuwa Rwanda imeendelea eti kwa sababu ka-nchi ni kadogo!
 
Back
Top Bottom