Ukweli kuhusu Rwanda na Kagame kwa ujumla (tofauti na wengi wajuavyo)

Madesa

Member
Nov 30, 2011
17
30
Ukweli wa machache nnayo yajua mimi ni huu,

ELIMU:

Ule mradi wa laptop moja kwa kila mwanafunzi umefeli kwa sababu ya Rushwa na ilikuwa ni ndoto kutimia kwani zaidi ya nusu ya shule zao hazina umeme, walikuwa wana system kama ya kwetu kutoa mikopo lakini kuanzia mwaka jana serikali imejitoa kudhamini wanafunzi wa elimu ya juu hivyo basi wazazi wanatakiwa wawalipie watoto zao sual hilli limeleta mtafaruku mkubwa Rwanda ila kwa kuwa sheria zao haziruhusu maandamano hakuna aliyepinga hadharani,Wanyarwanda wengi hawajui chochote kinachoendelea kwenye serikali yao, ntafafanua,

Mwaka juzi nilikuwa Rwanda tukiwa tunafanya research ni kuhusu elimu chini ya NGO moja iliyokuwa inataka kujenga shule vijijini.
Maajabu ni kwamba zaidi ya nusu ya watu tuliowauliza watuelekeze wizara ya Elimu ilipo walikuwa hawajui ilipo na cha zaidi vijana wa Kigali wengi wao walitupoteza na kutupeleka mahali ambapo sio au wizara tofauti kabisa, mwisho wa siku kwa tabu sana na hapo napo tulipata ajabu la pili, tulikutana na naibu waziri wa elimu mama mmoja mrembo sana na tulichotaka kutoka kwake ni kutaka kujua ni wapi kuna uhaba wa shule ili tukajenge huko, mama yule akasema kwa yeye Rwanda ni moja hawezi akataja eneo kwani akisema kusini watu wa mashariki watakasirika?!! Mwisho wa siku akasema hajui ni maeneo gani twende ila akatushauri twende kwa wa kuu wa viijij au tewnde ubalozi wa Marekani kuna mtu wa USAID anaye husika na elimu huyo ana data zote za Rwanda, tukasema haya, swali la pili kwake likawa je ni asilimia ngapi ya wanafunzi wanaandikishwa shule kwa mwaka akasema 97% na hiyo 3% inayobaki ni ya watoto ambao wanamapungufu akimaanisha vilema, jamani hata nchi za ulaya na Marekani hawajafikia 97% huo ni uongo mtupu na hakujua kuwa zaidi ya mwezi mzima tulikuwa viunga vya Kigali tukiwahoji watoto wa mitaani ambo hawasomi, Jamani Rwanda si kama tusomavyo kuna omba omba wengi kama miji yetu watoto wa mitaani wapo kila kituo cha daladala wakisumbua abiria kuomba pesa.

Turudi ubalozi wa USA, huko tukakutana na huyo jamaa wa elimu, ofisa yule akasema yeye naye kusema ukweli hajawahi kutembelea kijiji chochote kile analetewa data tu hivyo basi tutafute njia nyingine ya kupata data hizo, nikajua labda ni mpango wa kutokutaka kutupa data lakini si kweli wale watu wanashinda ofisini tu hawajui nini kipo mtaani na hata Kagame nae yupo hivyo hivyo.

UHALISIA WA RWANDA:

Ni nchi mojawapo ambayo wananchi wake wanaishi kwa hofu vibaya mno, ukiwa Rwanda huruhusiwi kuongelea vita ya wahutu na watutsi eti serikali imekataza inataka isahau ila makabila haya mawili yana chuki ambayo si rahisi kusahauluka kuna siku nilikuwa kwenye daladala na rafiki yangu mmoja toka Kenya nikawa namuuliza maswali kuhusu Wahutu yule jamaa hakunijibu na abiria wote walinigeukia kutaka kujua nani kataja neno hilo ikanibidi niongee kiswahili ili kuonyesha mimi ni mgeni na nikasameheka kwa hilo,siku nyingine nikamuuliza msichana wa Kitutsi kama ipo siku anaweza akaolewa na Mhutu akasema hilo halitatokea kamwe kwa chuki aliyonayo na nikagundua kuwa hata NGO iliyonipeleka pale members wote ni watutsi!!! na wakasema kama wahutu walishawahi kuongoza NGO hiyo na hakukuwa na Mtutsi, pata picha, kila ikifika saa kumi jioni Kagame anapeleka majeshi mtaani eti kulinda amani mpaka kesho yake, utaona matruck ya jeshi ya kimwaga askari mitaani wakiwa kwenye mstari mmoja na mikononi wana AK47, fingers on the triger, staili hiyo Kigali inaitwa SINGLE FILE SYSTEM hasa na vijana.

Rwanda naweza kusema ni koloni la Marekani na nchi inayopumua kwa misaada ya USA hakuna nchi East & Central Africa yenye international NGOs kama ile, wananchi wengi wameajiliwa huko, kuna kampuni kubwa chache sana na makampuni hayo yanamilikiwa na wamarekani na hata maofisa wake wengi wamesomea huko akiwa yeye mmoja wapo na kwa taarifa yenu ni kuwa raisi na rafiki zake wanamiliki kampuni karibuni zote kubwa za Rwanda kupitia kampuni yao ambayo kazi yake ni kununua kampuni nyingine.hivyo basi ni miongoni mwa matajiri wakubwa kabisa nchini kwake.

Jamani Rwanda kumetapakaa umasikini mambo yote mnayosoma kutoka Rwandan media yote yamekuwa screened by the government, Rwanda hakuna freedom of media, na sidhani kama kuna private tv/radio zaidi ya mbili,kama moja ipo, ile nchi inaendeshwa na misaada zaidi ya 80%,kodi zao ziko juu zaidi ya kwetu, kuna stori nilipewa kuwa wahisani walikuja kukagua mradi wa barabara na serikali haikutekeleza hilo walichokifanya ni kufumua lami nzuri na kuweka nyingine ili kuonyesha pesa ilipoenda, mpaka mwaka juzi walimu walikuwa wanalipwa wastani wa 42$ kwa mwezi,mpo hapo?

Mpaka leo hakuna anayemjua mrithi wa Kagame ila kuna tetesi anaweza akawa mtoto wake ambaye yupo USA in one of the best millitary academy ambako amesomea baba yake, kama umeshawahi kusikia kule kuna upinzani wa kweli basi tujadili, ana kashfa ya kuwapoteza wapinzani wake na juzi juzi Uganda ililalamika kuwa anatuma majasusi wake nchini humo.

Kwakuwa muda umenitupa kwa leo naishia hapa, ila ukipatamuda vuka mpaka hata kwa wiki 1 tu ukajionee nilichosema ila jiandae kwa matumizi kwani chakula ni gharama nadhani mara tatu ya hapa na hapa sizungumzii kwenye hotel kubwa, asante.
 
paul-kagame.jpg
 
So you mean mwalimu anapokea 67,200tsh uki-exchange kwa rate ya 1600. Hiyo kali na chakula kama ni mara 3 ya apa kwetu hao jamaa wanaishije sasa?

Ila kagame mbabe nadhani ni kwa manufaa ya nchi yake.
 
Hakuna amani ya kweli kwa mujibu wa ripoti yako...

Nami sishangai,kwa nchi iliyokuwa marred na vita,si ya wenyewe kwa wenyewe tu,bali hasa vya kikabila,itachukua miongo hiyo sumu kutoweka...
 
Madesa, angalia upande mwingine wa shilingi uone jinsi wasomi wanavyoiona Rwanda:

The small African nation of Rwanda recently announced that it had cut poverty by 12% in six years, from 57% of its population to 45%. That equals roughly a million Rwandans emerging from poverty -- one of the most stunning drops in the world.

It's a remarkable achievement for Rwanda, which has emerged from civil war and a bloody ethnic genocide in the 1990s. How did it happen? The Times quizzed Paul Collier, director of the Center for the Study of African Economies at Oxford University, about the numbers.


Are there any doubts that the drop is real?

No doubts; I know the economics professor who did the data analysis, and he is highly experienced and painstaking, so it is genuine.


How did Rwanda cut its poverty so much?
There were one or two helpful events, notably the rise in world coffee prices, which pumped money into the rural economy, but, of course, overall the global economy since 2005 has not provided an easy environment for success. Hence, most of the achievement is likely due to domestic policies.Rwanda is the nearest that Africa gets to an East Asian-style "developmental state," where the government gets serious about trying to grow the economy and where the president runs a tight ship within government built on performance rather than patronage.There were strong supporting policies for the rural poor -- the "one cow" program [that distributed cows to poor households free of charge], which spread assets, and the improvements in health programs.Alongside this, the economy was well managed, with inflation kept low, and the business environment improved, both of which helped the main city, Kigali, to grow. Growth in Kigali then spread benefits to rural areas -- the most successful rural districts were those closest to Kigali.

When you say well managed, what do you mean? What choices did the government make that were signs of good management?
Basically, [President Paul] Kagame built a culture of performance at the top of the civil service. Ministers were well paid, but set targets. If they missed the targets there were consequences. Each year, the government holds a whole-of-government retreat where these performances are reviewed: good performance rewarded, and poor performers required to explain themselves.
An example is the strategy to improve Rwanda's rating on the World Bank's "Doing Business" annual rating, where over the course of six years the country moved from around 140th to 60th in the world rankings. Each component of the ratings was assigned each year to an appropriate minister. So over time, a cadre of government officials has been built up who believe in their ability not just to strategize but to get things done.

What changes can you see now in Rwanda?
Some changes are obvious to the eye -- houses that now have tin roofs instead of thatch. Thatch may look prettier, but the world over, a decent roof is one of the first changes people make when they start the ascent out of poverty. Some of the changes are psychological -- a sense that things really can improve, and a sense that individual families can do something about their circumstances.

What can other countries learn from Rwanda -- or is its story so unique that it can't be copied?
They can learn a lot. If Rwanda can do this well, with all its disadvantages -- landlocked, legacy of conflict, no natural resources -- other African countries should be able to do even better.


Do you think Rwanda can continue to reduce poverty at the same rate in the coming years?

The government has now set its sights on getting the country to middle-income levels. This will require a change in the growth strategy. So far, growth has come primarily from doing better the things that Rwanda is doing already. To reach middle income, new activities will need to be introduced and the economy diversified. Rwanda needs pioneer investors and aid to support them with public infrastructure; I hope that it gets them. If it does, then, yes, poverty can continue to fall fast.

Source: Los Ageles Times, February 16, 2012
 
So you mean mwalimu anapokea 67,200tsh ukiexchange kwa rate ya 1600.Hiyo kali na chakula kama ni mara 3 ya apa kwetu hao jamaa wanaishije sasa?
Ila kagame mbabe nadhani ni kwa manufaa ya nchi yake.
no co hvy pesa ya rwanda ipo juu ukicompare na tshs! Last tyme niliexchange tshs 100,000 kwa faranga ya rwanda 35,000 so anavyosema chakula ni mara tatu ya huku itc true coz rate yao ipo juu sana! Sahani ya msosi mzuri ni 5000 ya rwanda ambapo ukichange ktk pesa ya tz ni kama 14,000 hv! Na hawana mzaha na kodi! Wanatoza kodi kupita maelezo!
 
Wewe ni muongo kama shetani! Mimi nilifanya kazi Ngara katika makambi mbalimbali ya wakimbizi wa Rwanda na kulikuwa na kambi maalum ambazo zimetengwa kwa ajili ya watusi na wahutu waliooana!

Kuanzia leo nitakuogopa kama ukoma!
 
Kaka acha kuposha watu, usidhani wewe ndo umefika rwanda tu!mambo mengi uliyoyaandika sio kweli!
 
Hakuna lolote Rwanda, Angola, Mozambique, Botswana are in list of fastest growing economy.

CCM wamekutuma ili utupooze!

Lib must

nyinyi ndio zero brain wa JF, I was at the ICTR in Arusha for a mission sponsored by UN,cku moja tukiwa ktk workshop za capacity building, kila section ya tribunal ilikuwa inaeleza kazi zake na mambo mengine, dakika za mwisho baada ya kufight sana..defence lawyer mmja anaitwa peter hebert akapata nafac akaja kutoa semina, alimwa mambo mengi sana, kutokana na ufinyu wa muda aliopewa akafunguka mafuta tukabaki midomo wazi,

anachosema mleta mada ni cha kweli wala c uzushi,tafuta,Kagame haguswi, ukimgusa ur dead nchi yoyote, maprof kibao ambao walikuwa upande wa defence pale ICTR hatuanao tena including mbongo mwenze2 Mwaikasu na wengine wengi waliojaribu kuleta ukweli wa mabo hadharani.

mlolongo wa waandishi wa habari hatunao tena kutokana na kuhoji uongozi wa huyu bwana, they are dead.
Kwataarifa yako we kijana Genocide in Rwanda has been defined to mean the killing of tutsi by hutu, kupunguza makali imeongezwa also the killing of moderate hutus by hutu extremists.

Peter hebert aliuza maswali simple sana ktk presentation yake, akasema na nakuu,
1-"WE ARE SPEAKING OF JUSTICE TO THE RWANDAN PEOPLE, BUT WHY THE PROSECUTION IS ONE SIDED"
2-"IF THE VIOLENCE BROKE OUT AFTER THE DEATH OF PRES. HABRYARIMA, WHOSE PLANE WAS SHOT DOWN IN KIGALI, AND ALL EVIDENCE REVEAL THAT RPF UNDER GENERAL KAGAME ARE RESPONSIBLE FOR THE DEATH, WHY THE INTERNATIONAL COMMUNITY IS SILENT ON THIS MATTER"
ukiunganisha haya mambo unapata ukweli wa kagame akiwa ktk close ties na USA, hawezi kuguswahata cku moja mpaka washindwane,

ukita kujua ukweli kuhusu rwanada usisome magazeti, just go in there see by urself and if u can come out and speak.

ukitaka kujua mengi ingia "www.blacklawyers.com/peter hebert"
 
nyinyi ndio zero brain wa JF, I was at the ICTR in Arusha for a mission sponsored by UN,cku moja tukiwa ktk workshop za capacity building, kila section ya tribunal ilikuwa inaeleza kazi zake na mambo mengine, dakika za mwisho baada ya kufight sana..defence lawyer mmja anaitwa peter hebert akapata nafac akaja kutoa semina, alimwa mambo mengi sana, kutokana na ufinyu wa muda aliopewa akafunguka mafuta tukabaki midomo wazi,

anachosema mleta mada ni cha kweli wala c uzushi,tafuta,Kagame haguswi, ukimgusa ur dead nchi yoyote, maprof kibao ambao walikuwa upande wa defence pale ICTR hatuanao tena including mbongo mwenze2 Mwaikasu na wengine wengi waliojaribu kuleta ukweli wa mabo hadharani.

mlolongo wa waandishi wa habari hatunao tena kutokana na kuhoji uongozi wa huyu bwana, they are dead.
Kwataarifa yako we kijana Genocide in Rwanda has been defined to mean the killing of tutsi by hutu, kupunguza makali imeongezwa also the killing of moderate hutus by hutu extremists.

Peter hebert aliuza maswali simple sana ktk presentation yake, akasema na nakuu,
1-"WE ARE SPEAKING OF JUSTICE TO THE RWANDAN PEOPLE, BUT WHY THE PROSECUTION IS ONE SIDED"
2-"IF THE VIOLENCE BROKE OUT AFTER THE DEATH OF PRES. HABRYARIMA, WHOSE PLANE WAS SHOT DOWN IN KIGALI, AND ALL EVIDENCE REVEAL THAT RPF UNDER GENERAL KAGAME ARE RESPONSIBLE FOR THE DEATH, WHY THE INTERNATIONAL COMMUNITY IS SILENT ON THIS MATTER"
ukiunganisha haya mambo unapata ukweli wa kagame akiwa ktk close ties na USA, hawezi kuguswahata cku moja mpaka washindwane,

ukita kujua ukweli kuhusu rwanada usisome magazeti, just go in there see by urself and if u can come out and speak.

ukitaka kujua mengi ingia "www.blacklawyers.com/peter hebert"

Acha kuchanganya mada hapa! Kinachojadiliwa hapa ni maendeleo ya Rwanda katika sekta mbalimbali na si Kagame alimuua Habyarimana au wahutu kuuwa watusi. Jadili elimu, kilimo, viwanda nk
 
kama ni hivyo for sure let us expect for another Libya like thing!
 
Je unajua kuwa mwaka jana Kagame aliwaita watutsi wote wanaosoma vyuo vikuu vya ndani na Nje ya Nchi kuwanong'oneza kuhusu kutawala daima na kuwapa mafunzo ya kijeshi?!!

Kagame na serikali yake wanatawala NGOs zote Rwanda kila NGOs lazima iwe registered kila mwaka! na kueleza wanafanya nini! Anawalazimisha NGOs watoe "handouts" misaada midogo midogo kwa wananchi nchi ili kuwapumbaza. NGO moja imelazimishwa kununua ng'ombe wa maziwa kwa wananchi.

Dictator Kagame amegundua namna ya kuishi na wazungu ili kujenga umaarufu.
 
Acha kuchanganya mada hapa! Kinachojadiliwa hapa ni maendeleo ya Rwanda katika sekta mbalimbali na si Kagame alimuua Habyarimana au wahutu kuuwa watusi. Jadili elimu, kilimo, viwanda nk
Maendeleo katika nchi ya wanaochinjana siyo maendeleo! maendeleo katika yenye ubaguzi wa kikabila siyo maendeleo pole ndugu!!
 
25 Reactions
Reply
Back
Top Bottom