Ukweli kuhusu mgomo na madai ya madaktari Tanzania

Kibanga Ampiga Mkoloni

JF-Expert Member
Aug 9, 2007
18,697
8,843
Katibu wa Jumuiya hiyo, Dk Edwin Chitega alitaja madai yaliyowasilishwa katika kamati hiyo kuwa ni:-

1. Hali bora ya mazingira ya utoaji afya nchini,
2. Ongezeko la mishahara,
3. Posho za kufanya kazi katika mazingira magumu,
4. Posho za kufanya kazi katika mazingira hatarishi
5. Posho za kuitwa kazini.


Yaliyotekelezwa kwa mujibu wa PINDA Bungeni ni:-

1. Kuongeza malipo ya uchunguzi wa mwili wa marehemu kwa madakari ambapo wasaidizi sasa watalipwa Sh50,000 na madaktari Sh100,000.
2. Serikali ilikubali kuwaondoa mawaziri na
3. Watendaji wengine wa wizara hiyo,
4. Imeongeza malipo ya kuitwa kwa dharura
5. Mengine kadhaa.

Update 1/7/2012

Kutokana na hotuba ya RAISI madai ya madaktari ni 12 :-

1.Posho ya kuitwa kazini (on call allowance) iwe asilimia 10 ya mshahara.
2.Posho ya kufanya kazi katika mazingira hatarishi (Risk allowance) iwe asilimia 30 ya mshahara.
3.Madaktari wapatiwe nyumba grade A au posho ya makazi ambayo iwe asilimia 30 ya mshahara.
4.Posho ya kufanya kazi katika mazingira magumu iwe asilimia 40 ya mshahara.
5.Madaktari walipwe posho ya usafiri ya asilimia 10 ya mshahara au wakopeshwe magari.
6.Madaktari wanaoanza kazi walipwe mshahara wa shilingi 3,500,00/= kwa mwezi.
7.Madaktari wapatiwe Green Card za Bima ya afya.
8.Hatua za kinidhamu zichukuliwe dhidi ya Watendaji Wakuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii.
9.Viongozi wa Kisiasa kulazimisha kupewa rufaa nje.
10.Madaktari waliofukuzwa warudishwe kazini.
11.Huduma za afya ziboreshwe nchini.
12.Posho ya uchunguzi wa maiti iongezwe.


Mambo saba waliokubalina kwa mujibu wa Raisi :-

Katika mambo hayo 12 pande zote mbili zilifikia muafaka na kukubaliana wa pamoja kwa mambo saba.
1. Ni kuhusu usafiri wa kwenda na kurudi kazini. Serikali ilieleza kuwa upo utaratibu kwa mujibu wa Waraka wa Utumishi wa Serikali Na. 3 wa mwaka 2011 wa kuwakopesha wafanyakazi wa Serikali fedha za kununulia magari au pikipiki, samani na matengenezo ya magari. Ilikubaliwa kuwa madaktari waitumie fursa hiyo.

2. Ni kuhusu madaktari kupatiwa Green Card za Bima ya Afya. Jambo hili lilikubaliwa na Serikali na Wizara ya Afya imekwishachukua hatua za utekelezaji wake.

3. Ni kuhusu hatua za kinidhamu kuchukuliwa dhidi ya Watendaji Wakuu wa Wizara ya Afya. Kwa pamoja walikubaliana kuwa suala hilo liko nje ya mamlaka ya Kamati yao ya pamoja, waziachie mamlaka husika za uteuzi. Uongozi wa juu wa Wizara umebadilishwa na sasa kuna uongozi mpya. Lakini, jambo la kustaajanisha hata Waziri mpya wa Afya alipowataka waonane kuzungumzia hoja walikataa kumuona. Kwanza walisema hawaoni sababu kwa vile wameyazungumza na Kamati yake kwa miezi mitatu bila ya mafanikio

4. Walilokubaliana ni kuhusu viongozi kulazimisha kupewa rufaa ya kutibiwa nje. Walikubaliana mambo mawili. Kwanza, kwamba maelekezo ya Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda kuwa madaktari wazingatie maadili ya kazi zao na kukataa kutoa rufaa kwa mtu asiyestahili awe kiongozi au asiwe kiongozi. Pili, walikubaliana kuwa hospitali zilizopo ziboreshwe ili viongozi watibiwe hapa nchini. Ukweli ni kwamba kufanya hivyo ndiyo sera ya Serikali. Nililieleza hili mwezi Desemba 30, 2005 katika hotuba yangu ya kuzindua Bunge baada ya kuchaguliwa kwa mara ya kwanza kuongoza nchi yetu.

Tumeiongeza sana bajeti ya sekta ya afya kutoka shilingi bilioni 300 2005/2006 hadi shilingi trilioni 1.2 mwaka 2011/12 na imekuwa ya tatu baada ya miundombinu na elimu. Tumeziimarisha hospitali za Mikoa kwa vifaa tiba na wataalamu wa afya. Kazi inaendelea katika hospitali za Wilaya. Tumewekeza katika Hospitali ya Muhimbili. Hospitali hiyo ilivyo leo sivyo ilivyokuwa miaka sita nyuma. Na kazi inaendelea hasa katika maeneo ambayo tunapeleka wagonjwa nje. Matunda yake yanaanza kuonekana kwa upande wa figo, moyo, kinywa na mipango inaendelea kwa upande wa ubongo na mishipa ya fahamu. Tunaendelea kuimarisha mafunzo ya madaktari na madaktari bingwa, yote kwa nia hiyo hiyo. Hivi sasa Chuo Kikuu cha Sayansi ya Tiba,Muhimbili kinachukua wanafunzi wengi zaidi ya ilivyokuwa siku za nyuma na makazi mapya ya chuo yanaendelea kuandaliwa ili kuchukua wanafunzi wengi zaid. Mwaka 2005 tulikuwa na madaktari bingwa 46 mwaka huu tunao 520.

5. Ambalo pande zote mbili zilikubaliana ni kuhusu madaktari waliofukuzwa. Hawa ni wale Interns waliokuwa wamerudishwa Wizarani kutoka Muhimbili na kupangiwa hospitali za Temeke, Ilala, Mwananyamala na Lugalo. Hili ni jambo ambalo lilikuwa limemalizika kitambo na wote walikuwa wamerudi Muhimbili.

6.Ni kuhusu mapendekezo mbalimbali yaliyotolewa na madaktari kuhusu kuboresha huduma ya afya. Mapendekezo hayo yalihusu kutathmini sera na mpango wa afya ya msingi, bajeti ya afya kuwa asilimia 15 ya bajeti ya Serikali, kuwepo na utaratibu mzuri wa kuajiri madaktari na kuboresha viwango vya ubora wa madaktari na kadhalika. Serikali imeyaafiki mapendekezo hayo na yatafanyiwa kazi.

7. Ambalo pande zote walilokubaliana ni kuhusu kuongeza posho ya uchunguzi wa maiti. Hili ni jambo jipya halikuwepo mwazoni. Hata hivyo, Serikali imelikubali na posho hiyo imeongezwa kutoka shilingi 10,000/= hadi kufikia shilingi 100,000/= kwa daktari na shilingi 50,000/= kwa wasaidizi wake.


Mambo matatu yapo 50/50 ni :-

1.Ni suala la kufanya kazi katika mazingira hatarishi. Serikali imekubali hoja ya kuchukua hatua ya kuwalinda madaktari wanaofanya kazi katika mazingira hatarishi. Serikali iliwaeleza kuwa watumishi wa kada zote za afya watapatiwa chanjo dhidi ya maambukizi ya Hepatitis B na fedha zimetengwa katika bajeti ya 2012/13.

Aidha, Serikali imeeleza dhamira ya kurudisha posho ya mazingira hatarishi kwa watumishi wa umma wanaostahili. Utekelezaji wake utafanyika baada ya uchambuzi wa kina wa kubainisha mazingira hatarishi ni yepi, viwango stahiki viwe vipi na nani hasa wahusike. Madaktari wamekataa hili la kufanya uchambuzi, wanataka kiwango kiwe kama wanavyotaka wao, yaani asilimia 30 ya mshahara na kianze mara moja.



2. Ambalo wamekubaliana nusu nusu ni kuhusu nyumba za kuishi. Serikali imekiri wajibu wake wa kuwapatia madakari nyumba za kuishi. Aidha, imeeleza mpango ulioanza wa kujenga nyumba 700 za madaktari kote nchini na kwamba hivi sasa ujenzi wa nyumba 90 unaendelea, 50 katika mkoa wa Mtwara na 40 katika mkoa wa Rukwa.

Kwa maeneo ambayo madaktari wanalipwa posho ya pango Serikali imesema waajiri wataendelea kufanya hivyo kwa mujibu wa taratibu zilizopo kwa watumishi wa umma wenye stahili ya kupewa nyumba. Jambo hilo limekataliwa na Madakari na kutaka lazima walipwe asilimia 30 ya mshahara kama posho ya nyumba. Serikali kwa upande wake imeona vigumu kufanya hivyo na kuwasihi wakubali wanayotendewa wafanyakazi wengine wote wa umma.

3. Ni kuhusu posho ya kufanya kazi katika mazingira magumu. Pande zote mbili ziliafikiana kuwa yapo baadhi ya maeneo nchini yanayo mazingira magumu kwa watumishi wa umma hivyo hatua zichukuliwe kuwasaidia watumishi hao. Serikali imekubali wajibu wa kuweka utaratibu wa kuboresha maisha ya watumishi katika maeneo hayo. Kwa ajili hiyo, Serikali itatoa mwongozo kwa mamlaka za ajira kuhusu namna ya kuwasaidia watumishi hao kupunguza makali ya maisha katika kila eneo badala ya kutegemea posho peke yake.

Kuhusu posho, Serikali imeeleza kuafiki kuwepo posho ya aina hiyo ila itatekelezwa baada ya kufanya uchambuzi wa kuainisha mazingira husika, kutambua watumishi waliopo na gharama zake.
Madaktari hawajakubali kusubiri zoezi la uchambuzi lifanyike, wanataka Serikali ilipe posho hiyo sasa. Tofauti hapa si posho hiyo kuwepo, bali ni rai ya Serikali ya kubaini maeneo yenyewe na kupanga aina ya hatua na viwango vya posho kulingana na mazingira halisi ya maeneo. Madaktari hawaoni haja ya kufanya hayo.



Mambo mawili hawajakubaliana:-
1.Ni posho ya kuitwa kazini (on call allowance). Kwanza sina budi kueleza kuwa Serikali imekubali kuongeza posho hiyo. Tangu Februari, 2012 posho iliongezwa kutoka shilingi 10,000/= hadi shilingi 25,000/= kwa daktari bingwa (Specialist), shilingi 20,000/= kwa dakari mwenye usajili wa kudumu (Registrars) na shilingi 15,000/= kwa madaktari waliohitimu ambao wapo katika kipindi cha mafunzo kazini (Interns). Viwango hivyo vya posho vinatumika hivi sasa.

Madaktari kwa upande wao hawakukubali uamuzi huo wa Serikali na kusisitiza walipwe asilimia 10 ya mshahara. Ugumu wa kukubali pendekezo la madakari ni kuwa sharti la malipo haya ni mtu kuitwa kazini. Ukitaka ilipwe kiwango cha mshahara ina maana kuwa hata kama daktari hakupangwa kuitwa au alipangwa na hakutokea aendelee kulipwa. Hili haliwezi kuwa sahihi kufanya. Linaweza kuwafanya baadhi ya madaktari kutokutimiza wajibu wao kwa vile wana hakika mwisho wa mwezi malipo yako pale pale.

2. Muafaka haukufikiwa baina ya Serikali na madaktari ni kuhusu mshahara wa kuanzia kazi wa daktari. Madaktari wanataka uwe shilingi 3,500,000/= wakati Serikali inasema kiasi hicho hatukiwezi. Serikali imeeleza utayari wake wa kuongeza mshahara kwa kati ya asilimia 15 mpaka 20 kama ambavyo itafanya kwa watumishi wote wa umma katika mwaka huu wa fedha. Kwa kiwango cha sasa cha mshahara wao, daktari ataanzia kati ya shilingi 1,100,000/= na 1,200,000/= kutegemea kiwango kipi hatimaye kitaamuliwa. Madaktari wamekataa katakata na wameng'ang'ania shilingi 3,500,000/=.
 
madaktari wanaomba kuboreshwa huduma wao wanaongeza hela za kuchunguza maiti! Hii ni akili ya matope kabisa! Mtu anakaa hospital masaa 12 usiku unamlipa 20000 does it sound? Aafu kuipata utaandika barua mpaka pesa yote inaishia kwenye printing and typing costs. Wao kusinzia bungeni kwa masaa manne 150000! Wanalazimisha referal za kwenda nje ili walipwe wao na wake/vimada wao wanaowasindikiza,hivi mnajua kwamba wakienda kutibiwa india wanalipwa dola 450 per diem yeye na mkewe? Wengi wao wakija kulazimisha referal wanasema kabisa, na mimi nataka nivune hela za serikali!!... Khaaaaaa!!
 
Katibu wa Jumuiya hiyo, Dk Edwin Chitega alitaja madai yaliyowasilishwa katika kamati hiyo kuwa ni:-

1. Hali bora ya mazingira ya utoaji afya nchini,
2. Ongezeko la mishahara,
3. Posho za kufanya kazi katika mazingira magumu,
4. Posho za kufanya kazi katika mazingira hatarishi
5. Posho za kuitwa kazini.



Yaliyotekelezwa kwa mujibu wa PINDA Bungeni ni:-

1. Kuongeza malipo ya uchunguzi wa mwili wa marehemu kwa madakari ambapo wasaidizi sasa watalipwa Sh50,000 na madaktari Sh100,000.
2. Serikali ilikubali kuwaondoa mawaziri na
3. Watendaji wengine wa wizara hiyo,
4. Imeongeza malipo ya kuitwa kwa dharura
5. Mengine kadhaa.


Pima mwenyewe nani msanii hapo, kwani haya madai ni kwa muda wa miezi 3 sasa.

duh wasijedababisha idadi ya wagonjwa kufa kizembe kuongezeka watu wapate pesa ya kuchunguza maiti
 
madaktari wanaomba kuboreshwa huduma wao wanaongeza hela za kuchunguza maiti! Hii ni akili ya matope kabisa! Mtu anakaa hospital masaa 12 usiku unamlipa 20000 does it sound? Aafu kuipata utaandika barua mpaka pesa yote inaishia kwenye printing and typing costs. Wao kusinzia bungeni kwa masaa manne 150000! Wanalazimisha referal za kwenda nje ili walipwe wao na wake/vimada wao wanaowasindikiza,hivi mnajua kwamba wakienda kutibiwa india wanalipwa dola 450 per diem yeye na mkewe? Wengi wao wakija kulazimisha referal wanasema kabisa, na mimi nataka nivune hela za serikali!!... Khaaaaaa!!

Mkuu kama hili ni kweli inafaa mumwage data zaidi za hizi issue ili ichokonoe watu kujadili wazi wazi na kuanika huo uozo hadharani! Natamani tupate Rais asiye dhaifu aunde Mahakama maalum ya kushughulikia hizi kero za uhaini+uhujumu jamii!!
 
Doctors' strike threat: Who's telling the truth?
Friday, 22 June 2012 09:04
By The Citizen Reporters
Dodoma/Dar es Salaam.

The stage appears to be set for a doctors' strike starting tomorrow after negotiations with the government collapsed yesterday. The medics denied Prime Minister Mizengo Pinda's report to Parliament that they had reached an agreement on five of 10 demands.
Five hours after the PM's statement, the doctors denied that there was such an agreement and declared that they would go on a nation-wide strike beginning tomorrow.

Should the strike take off, medical services in public hospitals-including Muhimbili National Hospital-will be paralysed. Early this year, there were reports of patients dying after doctors in 13 public hospitals lay down their tools.

The doctors want a salary package of up to Sh3.5 million for a beginner along with housing allowance. Their last strike in January centred around eight issues.
Mr Pinda said during the PM's question-and-answer session that the two sides had agreed on allowances for post-mortem examinations, on-call allowances and removal of some senior officials in the ministry of Health and Social Welfare.

But, at a press conference in Dar es Salaam, the doctors denied that they had reached any agreement. The deputy chairman of the Interim Doctors' Association, Dr Godbless Charles, described the Prime Minister's statement as a "lie" and said they were disappointed by his statement. "We haven't agreed on any of the demands we have forwarded to the government," said Dr Charles.

The chairman of the Interim Doctors' Association, Dr Ulimboka Stephen, said that Mr Pinda's statement indicated that the government was not ready to deal with their grievances.
"We have, therefore, resolved to go on strike beginning tomorrow," he said at a news conference. "We will not go to the labour court as Mr Pinda has proposed.
"This matter will be handled by the doctors' association."

In Dodoma, Mr Pinda said the dispute between the doctors and the government would be decided by the labour court after the medics suspended negotiations.
Answering a question from the leader of the official opposition, Mr Freeman Mbowe, the PM said the talks stalled after the doctors refused to continue with dialogue on grounds that they had been negotiating with the government for over three months and nothing tangible had come out of it.

Mr Mbowe wanted to know the issues that had been agreed and what the government was doing to resolve those that were still outstanding.
He said the government was taking too long to resolve the problem. "Can the Prime Minister assure this House that the bureaucratic processes will help to resolve this issue before Saturday?" he asked.

But Mr Pinda responded that he was not aware that the doctors were planning to begin a strike on Saturday. If they did so, he added, they would be breaking the law as they had agreed that the matter should be handled by the labour court. The doctors' demands included removal of some of officials in the Health Ministry, according to the PM.

After discussions, the government reportedly gave in and removed the minister, his deputy, permanent secretary and the chief government medical officer.
But Mr Mbowe pointed out that the problem had not been resolved by the removal of the top officials and suggested that the problem may be about the structure rather than individuals.

Mr Pinda was adamant that since the matter had been forwarded to the labour court, it should be allowed to deal with it. He said the doctors had refused to continue their talks through the Commission for Mediation and Arbitration.
In another development, Mr Pinda said the government was determined to meet the demands of teachers, which are largely about payment of their arrears. "We have been seeing messages through our phones....I would like to urge teachers to disregard them as we are doing everything possible to pay them," he said.

Meanwhile, a Tanga-based organisation yesterday warned doctors against going on strike and said it had not halted proceedings to send them to the International Criminal Court (ICC) for crimes against humanity.
The Mwalimu Nyerere Ideology Conservation Society said last January's strike had affected health services and many innocent people had died for lack of medical care.

The chairman of the society, Dr. Muzammil Kalokola, said: "Our lawyers, inside and outside the country, are still investigating and collecting data that would enable us to send the doctors to the ICC in Switzerland."
"Their act has contravened human rights and the constitution Section 14 of the Tanzanian Constitution, which says that every Tanzanian has a right to live and get protection from the society for his life in accordance with the law," he said.

In Mwanza, doctors in the Lake Zone vowed to support whatever decision their colleagues countrywide reached. Dr Kiriti Richard said at their meeting that they were forced to reach this "harsh" decision after the government failed to respond to their grievances.
Reported by Peter Nyanje in Dodoma and Bernard Lugongo in Dar es Salaam.



 
Sasa ni wakati muafaka kuwafunglia kesi za mauaji kila daktari ataepangiwa kazi kama hakuwepo wakati huo na kimetokea kifo kwa daktari huyo kutokuwepo sehemu yake ya kazi na kaenda kwenye mgomo. Hakuna zaidi.

Mimi siwaungi hata kidole wacha mkono.
 
Sasa ni wakati muafaka kuwafunglia kesi za mauaji kila daktari ataepangiwa kazi kama hakuwepo wakati huo na kimetokea kifo kwa daktari huyo kutokuwepo sehemu yake ya kazi na kaenda kwenye mgomo. Hakuna zaidi.

Mimi siwaungi hata kidole wacha mkono.
Hivi kwa nini Pinda amelazimika kusema uwongo katika tamshi bungeni? Badala ya kuwalaumu madaktari lawama zielekezwe kwenye serikali dhaifu na viongozi wake walaghai.
 
Hivi kwa nini Pinda amelazimika kusema uwongo katika tamshi bungeni? Badala ya kuwalaumu madaktari lawama zielekezwe kwenye serikali dhaifu na viongozi wake walaghai.

Kwanini isiwe madaktari ndio waliosema uongo?
 
]Kwanini isiwe madaktari ndio waliosema uongo?[/QUOTE] unatakiwa ujiulize madaktari nchi nzima na pinda mtu mmoja nani rahisi kudanganya? ingekuwa ni dokta mmoja ndo kasema tungesema muongo. madaktari wan ahaki na serekali ndio ya kushitakiwa katika mahakama ya kazi kwa kusababisha vifo na sio madokta
 
]Kwanini isiwe madaktari ndio waliosema uongo?
unatakiwa ujiulize madaktari nchi nzima na pinda mtu mmoja nani rahisi kudanganya? ingekuwa ni dokta mmoja ndo kasema tungesema muongo. madaktari wan ahaki na serekali ndio ya kushitakiwa katika mahakama ya kazi kwa kusababisha vifo na sio madokta[/QUOTE]


Asante sana mkuu. JF ina vichwa!
 
Madaktari wamepiungukiwa akili na utu, haiwezekani kabisa muache watu wafe alafu nyie mje mlipwe mshahara bila kufanya kazi. Ningekuwa mimi ndiye Rais ningeamuru madaktari wote wafungwe jera kwa kusababisha vifo vya wasio na hatia. Sema tu mna bahati maana mkuu wa kaya wanadai ni dhaifu.
The unseen is illustrated by the seen.
 
Madakitari ndiyo wanaoishi kwenye mazingira magumu tu hapa Tz?

Au wao wanafanya kazi mahala pasipo watumishi wengineo?

Tuondeleeni u special wenu hapa ( U Mourihno) as mtu kama halidhiki ni juu yake kuchapa kazi au kusepa kunako malisho mazuri!
Ala hivi kama wao tu ndiyo watalipwa vizuri kila mzazi si atapeleka mwanae huko na mwisho tutakuwa na jamii ya madakitari, wewe mtu wa politic utakuwa wapi?
Au watapata faraja gani kuwatibu wagonjwa maskini wote?

Oongeleeni review ya mishahara ya watumishi wote na uwezo wa kajiinchi kenu kwa uhalisia.

Kama mgomo ni kwa ajiri ya kuonesha udhaifu wa serikali basi hao ma dr wote ni criminals wanafaa kuwa behind bars the mapema iwezekanayo.

too much jamani, nani aliwalazimisha kusoma fani wasizoridhika nazo?
 
Katibu wa Jumuiya hiyo, Dk Edwin Chitega alitaja madai yaliyowasilishwa katika kamati hiyo kuwa ni:-

1. Hali bora ya mazingira ya utoaji afya nchini,
2. Ongezeko la mishahara,
3. Posho za kufanya kazi katika mazingira magumu,
4. Posho za kufanya kazi katika mazingira hatarishi
5. Posho za kuitwa kazini.



Yaliyotekelezwa kwa mujibu wa PINDA Bungeni ni:-

1. Kuongeza malipo ya uchunguzi wa mwili wa marehemu kwa madakari ambapo wasaidizi sasa watalipwa Sh50,000 na madaktari Sh100,000.
2. Serikali ilikubali kuwaondoa mawaziri na
3. Watendaji wengine wa wizara hiyo,
4. Imeongeza malipo ya kuitwa kwa dharura
5. Mengine kadhaa.


Pima mwenyewe nani msanii hapo, kwani haya madai ni kwa muda wa miezi 3 sasa.

Kwanini tunaanza kusema Madaktari Watanganyika? Pale Muhimbili na Mnazi Mmoja

kuna Madaktari Wazanzibari Sasa Wao hawafai? Wajameni kama Adui wako

anakusengenya na kukubagua sio lazima uumtendee hivyo hivyo Mtendee Wema Mpaka

hapo Maamuzi yatakapotoka kama ni kuachana au Masuluhisho; Sio kurudia matendo

Maovu kwake... Hapo Utapata Baraka toka Kwa Mwenyezi Mungu.
 
Sasa ni wakati muafaka kuwafunglia kesi za mauaji kila daktari ataepangiwa kazi kama hakuwepo wakati huo na kimetokea kifo kwa daktari huyo kutokuwepo sehemu yake ya kazi na kaenda kwenye mgomo. Hakuna zaidi.

Mimi siwaungi hata kidole wacha mkono.

Dah! We chai sana you know nothing af una courage ya kukoment kichizi but pole Coz hujui kuwa hii ni nchi yetu sote
 
Kwanini tunaanza kusema Madaktari Watanganyika? Pale Muhimbili na Mnazi Mmoja

kuna Madaktari Wazanzibari Sasa Wao hawafai? Wajameni kama Adui wako

anakusengenya na kukubagua sio lazima uumtendee hivyo hivyo Mtendee Wema Mpaka

hapo Maamuzi yatakapotoka kama ni kuachana au Masuluhisho; Sio kurudia matendo

Maovu kwake... Hapo Utapata Baraka toka Kwa Mwenyezi Mungu.

Afya sio jambo la Muungano Mkuu Ndo maana.
 
Madakitari ndiyo wanaoishi kwenye mazingira magumu tu hapa Tz?

Au wao wanafanya kazi mahala pasipo watumishi wengineo?

Tuondeleeni u special wenu hapa ( U Mourihno) as mtu kama halidhiki ni juu yake kuchapa kazi au kusepa kunako malisho mazuri!
Ala hivi kama wao tu ndiyo watalipwa vizuri kila mzazi si atapeleka mwanae huko na mwisho tutakuwa na jamii ya madakitari, wewe mtu wa politic utakuwa wapi?
Au watapata faraja gani kuwatibu wagonjwa maskini wote?

Oongeleeni review ya mishahara ya watumishi wote na uwezo wa kajiinchi kenu kwa uhalisia.

Kama mgomo ni kwa ajiri ya kuonesha udhaifu wa serikali basi hao ma dr wote ni criminals wanafaa kuwa behind bars the mapema iwezekanayo.

too much jamani, nani aliwalazimisha kusoma fani wasizoridhika nazo?

Sijutii Kuzaliwa tz ila najutia kukutana na watanzania kama wewe, Najua unajua kuwa Kuna chama cha wafanyakazi wote na unajua udhaifu wake pi unajua kuwa kila mtu ana haki ya kuchagua kazi anayoipenda na anapaswa kulindwa katika kazi hiyo na hii ni nchi yetu sote sa daktari aende wapi wakati hii ndo nchi yake af Kama wafanyakazi wengine wana matatizo iweje wadaiwe haki zao na madaktari pekee yao wao wakiwa wamelala? Yaan nna maswali mengi ngoja niishie hapo.
 
Madakitari ndiyo wanaoishi kwenye mazingira magumu tu hapa Tz?

Au wao wanafanya kazi mahala pasipo watumishi wengineo?

Tuondeleeni u special wenu hapa ( U Mourihno) as mtu kama halidhiki ni juu yake kuchapa kazi au kusepa kunako malisho mazuri!
Ala hivi kama wao tu ndiyo watalipwa vizuri kila mzazi si atapeleka mwanae huko na mwisho tutakuwa na jamii ya madakitari, wewe mtu wa politic utakuwa wapi?
Au watapata faraja gani kuwatibu wagonjwa maskini wote?

Oongeleeni review ya mishahara ya watumishi wote na uwezo wa kajiinchi kenu kwa uhalisia.

Kama mgomo ni kwa ajiri ya kuonesha udhaifu wa serikali basi hao ma dr wote ni criminals wanafaa kuwa behind bars the mapema iwezekanayo.

too much jamani, nani aliwalazimisha kusoma fani wasizoridhika nazo?
Ndugu nakushauri utembelee hospitalini ushuhudie vifo ambavyo vingezuilika ktk mazingira ya vitendea kazi vinavyotosha na vya kisasa. Ktk swala la afya dr amesimama katikati ya selikali na mwananchi. mwananchi wa kawaida kama wewe ulivyo anapokosa huduma atamlaumu dr!, udhaifu wa selikali hii umewachonganisha ma dr. na waananchi. Prognosis ziko poor kwa kukosa vitendea kazi uzembe wa selikali upo sekta zote sema tu ya afya ni mtambuka kwani inagusa uhai wa mtu moja kwa moja. Wito: hebu selikali iwe serious kiutendaji na ipunguze anasa.
 
Afya sio jambo la Muungano Mkuu Ndo maana.

Hata kama sio jambo la Muungano haujui kuwa kuna Madaktari wa Kizanzibari Muhimbili, Mnazi Mmoja na hata kwingineko?

Sasa hata kama sio Jambo la Muungano ungependa waondoke waende Zanzibar hata kama wanatoa Huduma bora

kwa Wananchi wa Tanganyika? na Unajua Nchi ina Upungufu wa Madaktari...
 
Back
Top Bottom