LENGIO
JF-Expert Member
- Apr 9, 2012
- 1,096
- 508
Eneo lilokuwa la wazi karibu na kilombero sokoni liliuzwa kwa kampuni lijulikanalo kwa jina EMOIL MARKET SOLUTION mwaka 2005 muda mfupi baada ya baraza la madiwani kuvunjwa na mkataba huo kusainiwa na aliyekuwa meya Lota Laizer.kwa kushauriwa na wataalamu na baadhi ya madiwani.Baadhi walioshiriki katika ufisadi huo ni aliyekuwa mwanasheria Andason msumba meya Lota laizer,diwani Karimu mushi na diwani wa viti maalum. Habari za uhakika walipewa hela inayozidi milioni 250.fedha hizo zigawanywa nyumbani kwa diwani karimu eneo la lemara,na ziliwasilishwa na mwanasheria Andason kwa kutumia gari aina pajero ambalo kwa sasa inamilikiwa na aliyekuwa meya lota laizer.Na kiunganishi kati ya halimashauri na kampuni husika ni aliyekuwa mtumishi idara ya ardhi anayejulikana kwa jina moja urassa ambaye inasadikika ni mmoja wa wamiliki wa kampuni hiyo akiwamo Basil pesambili mramba.kwa hiyo wa machinga wako sahihi kukomboa maeneo yetu ya wazi.bado kuna eneo lingine la wazi liko lovolosi pia wamejimilikisha hivohivo mramba na urassa.