Ukweli kuhusu Benedict Mutungirehi na kundi la G211 pale UDSM mwaka 1994

Naomba mdau ukiweke hicho cha MZEE PUNCH bwana maana laaahh CHA MZEEE PANCHI mzee wa fuvu...kweli wewe noma

Mzee NYENJENKURU,

Ningetaka hata sasa kukiweka nitakiweka isipokuwa ninataka kwa kuwa-user tag wote mlioshiriki kwenye thread hii ya G211 na Mutungirehi maana nyinyi sitaki mkose uhondo huo. Hivyo, ndani ya masaa 24 nitakuwa nimeshakitoa.

Kwa kifupi ni kwamba kilitungwa na jamaa ambaye alikuwa anarekodi matukio yote ya ule mgomo wa mwaka 1990 hadi tarehe kilipofungwa Chuo yaani Saturday, May 12, 1990.

Mimi likipata mwaka 2003 alipokitoa lakini inaelekea kulifanyika njama ili kisijulikane mtaani. Kikapotea kama kilivyopotea kile cha Nyerere yaani (Uongozi wetu na Hatima ya Tanzania).

Nilipokipata hiki cha PUNCH na kile cha NYERERE nikaamua kuvi-scan vyote viwili na hadi leo vipo kwenye online database yangu, hata wakikamata computer zangu hawanipati labda waende kwenye servers za Yahoo au Google.

Sikuwahi kufikiri kuvitawanya mitandaoni kama hivi kwa sababu wakati ule 2003 internet haikuwa shida kwangu lakini online forum kama hizi kwa watanzania zilikuwa hazijazoeleka sana na hata Jamii Forum naamini ilikuwa haijazaliwa.

Forum zilipoenea siku moja nadhani miaka mitatu iliyopita nikaona humu JF wanauliza sana kuhusu kitabu cha NYERERE na ikaelekea watu wameshakata tamaa ya kukipata. Nilichofanya nikaamua kukisambaza humuhumu JF hadi kikakaa kwenye sticky kwa muda kama wa miezi mitatu na ushee.

Sasa kwa sababu mmetaka hiki cha PUNCH basi sina masaa zaidi ya 24 nitawashushia, lakini kwa masharti kwamba kinakuwa kwenye separate thread ili tuendelee kuchambuana huku kwa hili la G211 na Mutungirehi na kule kuwa na thread nyingine ya PUNCH.

Naamini watakuja members wengi maana kama walivyojitokeza kwenye hii na wengine hata kujiunga rasmi JF.

Keep in touch. Long live JF


Kusuhu cha g211 niwazo zuri tukagawana page kama ulivyosema ni wazo zuri sana. Anyway endelea kutupa uhondo wa enzi hizo

Ngoja kwanza tuendelee kupashana humuhumu kwanza, unajua watanzania wengi vitabu hawasomi. Ungeandika kitabu si ajabu ungechelewa sana kupata wasomaji kuhusu hii ya G211 na Mutungirehi ambapo kwa hizi siku mbili utaona kwamba imeshasomwa na watu 1,653 hadi natuma post hii. Ni watu wengi sana hao kusoma jambo moja, ukipata usomaji wa aina hii basi ni kweli meseji ime-spread.


.Anyway endelea kutupa uhondo wa enzi hizo...za FOE hivi Makoleo yupo jamani yule jamaa wa ME

Mkuu,

Nimemaliza Civil Engneering mwaka 1997 na hivyo Makoleo tuliachana naye first year kwenye Engineering Mechanics, hakuendelea kutufundisha. Atakuwa aliendelea kufundisha wenzake wa Mechanical Engineering.


asikia yule SUZY alikuwa anafundisha electronics workshop course kwa fist year ana Phd kwa sasa?

Aisee yule dada alikuwa mtulivu na smart. Walioendelea na Electrical Engineering watakuwa wanamjua zaidi. Si unajua tuliingia pale karibu wengi wetu ni ma-bachelor, aisee alikuwa anavutia wengi. Lakini hata tukiwa palepale alikuwa ameshaolewa na lecturere mmoja kule Electrical na hivyo wakawa naye Deprtment moja.

Prof. Mbwete nasikia ndiye Mkuu wa Open University hayuko tena pale. Prof. Materu wa kule Electrical tulimkuta akiwa Dean of Faculty alishaondoka zaidi ya miaka sita iliyopita, yuko either America au Europe kwenye international organisation. Hakutaka kusumbuana na serikali kugomagoma kama wanavyosumbuliwa madaktari ikibidi na wasomi wote.

Wapo list ya wengi tu ninaowakumbuka na walishaondoka pale. Mfano Dr. Nsekela aliondoka mwaka 2000 akawa mbunge wa jimbo moja huko Tabora. Kisha baadaye akawa Mkuu wa Mkoa Mwanza, akahamishiwa Dodoma na hivi majuzi akachaguliwa kuwa Balozi nchini Italy.

Dr. Yonnah nasikia yuko inayohusika na Mawasiliano na ni mtu mkubwa huko. Ila sina uhakika na hilo.
 
Kazi ya watu usiuite uhuni rafiki yangu. Kwanza nashangaa ilikuwaje ukasoma Engineering wakati huwezi hata kujisimamia ktk maamuzi magumu km hayo. Wewe ungekuwa Doctor ungesema Ulimboka basi mimi naendelea na kazi,

Nilichaguliwa kusoma Engineering kwa sababu nili-pass qualifying subjects at A-level, na si kwa sababu nilikuwa nafanya mazoezi ya kutunisha misuli ili kuja kupigana na Mutungirehi au G72 au MANGWINI!

*******
Wewe ungekuwa Doctor ungesema Ulimboka basi mimi naendelea na kazi

Ulimboka na madaktari wenzake hawakuiga utoto wa kutunisha musuri kama nyinyi. Ulimboka na wenzake walitengeneza agenda wakazisambaza kwenye media na kila mmoja anawaunga mkono kwa agenda zao. Nyinyi mlijijua mlikuwa wafinyu wa ku-shape agenda na hamkuwa na hoja na ndiyo maana hata leo mnadhani ni fahari kusifia misuli yenu kama wabeba mkaa, au wabeba vyuma au wapigana mieleka.

Hakuna mafanikio yaliyokuja kwa kubeba mieleka. Migomo yote iliyofanikiwa duniani ilianza kwa kuweka agenda mbele, mnaweka altimatum, na altmatum ikipita bila agenda kuwa addressed basi dunia nzima itawa-support kwa mgomo wenu lakini hata hapo si kwa kurushiana viti kama kwa Mutungirehi au kuchanachana mitihani ya G72.
***********
Kazi ya watu usiuite uhuni rafiki yangu. Kwanza nashangaa ilikuwaje ukasoma Engineering wakati huwezi hata kujisimamia ktk maamuzi magumu km hayo. Wewe ungekuwa Doctor ungesema Ulimboka basi mimi naendelea na kazi, CEBE wa aina gani wewe hujaangusha majengo au madaraja kuvunjika?

Hii nchi kuna jambo gani linaenda bila watu kustrike kwanza?

Hii serikali inatufanyia mambo mangapi ya ajabu na wananchi wanalalamika umeona nini kinafanyika? Bila huo mgomo hiyo nafasi ya vote of no confidence nani angewapa? CoET oyeeeeee!!

*********
Bila huo mgomo hiyo nafasi ya vote of no confidence nani angewapa? CoET oyeeeeee!!

Ona sasa mnajichanganya na hata hukumbuki. hebu jijibu swali hili. Je, mlipompiga Mutungirehi mlikuwa mnafanya mgomo au mlikuwa mnafanya mapinduzi? Maana hamueleweki.

Mgomo, mlifanya baada ya kutangazwa kwamba mlichofanya pale Nkrumah Hall kilikuwa uhuni na Benedict Mutungirehi bado President wa DARUSO hadi atakapoondolewa na wengi kama alivyochaguliwa.

Wewe kama G211 jikite na ile test, ule mtihani na ile vurugu ya pale Nkrumah. Tuliporudi Chuo na nyinyi mko home tulianzisha referendum request kistaarabu bila nyinyi kuwepo.

Kwa maana hiyo waliomuondoa Mutungirehi ni sisi lakini baada ya kuhubiriwa makosa yake tukapiga kura ya kumkataa. Kwa maana hiyo sisi na wale mnaowaita MANGWNI ndiyo tulimuondoa Mutungirehi kwa ustaarabu, kwa sanduku la kura. Tulimuondoa kwa demokrasi na si ile demokrasi yenu na rafiki yenu yule NIPASHE ya kumtwanga na viti.

Tulithibitisha mabadiliko tunayaweza bila nyinyi. Na mliporudi mkawa mmejirekebisha na mkaaza kuheshimu maoni ya wengi. Ndipo mkajifunza kujenga hoja zinazoshawishi Chuo kizima na siyo misuli na mabuti yanayotisha Chuo kizima.
wakti nyinyi
 
Huyu anayejiita Subirijibu amenifanya nichangae hii mada japo nilikuwa napita tu. Kwanza Subirijibu ni TRAITOR tu na hii lable haitakaa ikutoke wewe na wenzako. Subirijibu anajaribu kupotosha baadhi ya mambo katika story yake hii. Wakati wa tukio la kumtoa "Mtungihela" , mimi nilikuwa First Year FOE naVurugu za kumtoa Muutngirehi hazikufanywa/kuanzishwa na G211, kwani kabla ya mkutano pale Nkrumah, tulishakubaliana kuwa G211 wakae floor ya juu wakiwa na Tshirt zao, na sisi 1st year, 3rd tukaeground floor. Sikumbuki vizuri tulikubaliana 4th year wakae wapi.

Kutihibitisha you are a number one TRAITOR ni kutaja watu wakati tulipoletewa barua baada ya kufukuzwa chuo na unajisifu kwa ubinafsi wako. Ninakwambia kitu kimoja kuwa hata kama hatukujui lakini "LABEL ya UTRAITOR ITAKUFUATA HADI SIKU UTAKAYOITWA NA MUUMBA"
 
neno traitor ni label sahihi kwenu na hata wewe leo inaonekana hujaacha usaliti ndiyo maana unataja wenzio wakati ukijihami kuficha jinalo halisi!YUDA ISKARIOT
 
Hii stori siijui kabisa, lakini nikiangalia tu kwa haraka haraka mabandiko ya wengi, mtoa mada anaonekana kushikwa na "guilty" ya kuwa labeled TRAITOR. Maelezo yake mwenyewe yako wazi kuwa alikuwa mmoja wa wasaliti waliowasaliti wenzao..... Mhhhh miaka mingi imepita, lakini madhara ya vitendo vyake bado yanamkaba mwenyewe.

Naona kitendo cha hao g211 kurudishwa na mahakama hatimaye wakamaliza chuo kilimkera sana. Pole. Vipi huko mtaani, huo mwaka walioupoteza umeleta matokeo gani? Muda ni mwalimu mzuri sana .....
 
Subirijibu; nimesoma post yako ya kwanza yote, na sasa hivi nina uhakika kuwa wewe ulikuwa ni sehemu iliyodhoofisha nguvu za wanafunzi wa engineering.

Wakati wa matukio hayo nilikuwa bado nafundisha hapo FoE na siwezi kuwajua majina ya wanafunzi waliohusika, ila ni kweli kuwa waalimu wa FoE walishaona kuwa elimu ya engineering Math iliyokuwa inatolewa kwa wanafunzi wetu haikuwa inakidhi tena malengo yake, wanafunzi walikuwa wanafundishwa zaidi abstract math kuliko applied math; na kukawa na uamuzi kuwa waalimu wa engineering washiriki katika ufundishaji wa somo hilo kwa kuendesha tutorials. Mimi binafsi nilishiriki katika ku-TA masomo hayo kwa mwaka wa 1995 na sehemu ya mwaka 1996 kabla sijaondoka.

Iwapo msimamo wenu ungekuwa ni mmoja kwa wanafunzi wote, kusingetokea tatizo la wanafunzi kufukuzwa kwa sababu watawala hupenda sana kugawanya wanafunzi katika makundi na kutumia mgawanayo huo kugandamiza kundi moja na kutishia wengine wote waliobaki. Inapokuwa hakuna mgawanyo utawala unakuwa hauna nguvu. Nyinyi ndio milikubali kutumiwa kugawanya wanafunzi, na hivyo kutumika kama chambo cha kuwavictimize wenzenu. Wakati huo Professor Materu hakuwa na interest sana na foE tena kwa vile term yake ilikuwa inafikia ukingoni na alikuwa anajaribu kujijenga kuchukua nafasi ya Director of Postgraduate Studies, kwa hiyo nyinyu mlifanya ushiriki wake katika kuwavictimize wanafunzi engineering akiwa sehemu ya utawala, iwe ni rahisi sana.
 
Muonamambo achana na huyu Traitor subirijibu. Jamaa ana uchungu wa ndani sana.

Ni kweli nilikuwa na usongo sana na nyinyi. Mngeachana na sisi mkajikita kwenye haki yenu mahakamani wala hakuna kati yetu angekuwa na habari na nyinyi.

Chuo hamkukijenga nyinyi, madarasa ya FOE hamkuyajenga nyinyi. Halafu eti kwa sababu mko wengi mkataze watu wasisomee kule. Kwa nini kila anayesoma thread hii asione kwamba huu ni uwendawazimu uliopitiliza.

BInafsi hizo harrasment ndizo ziliniudhi na ndizo zilikuwa msingi wa kuwataja. Na wa kwanza kumtaja ni yule mkurya aliyenifukuza darasani usiku nisijisomee, nimemsahau jina.

Narudia nisingewataja ndiyo hadi leo ningekuwa na uchungu, lakini tangu nilipowataja, na niliowataja wakaadhibiwa mwaka mzima kukaa home, na waliporudi wakawa wana adabu kuliko maelezo basi nikabaki na kumbukumbu tu lakini si uchungu.

Tena yule mkurya mwaka wake wa mwisho akawa mtu mstaarabu sana.
 
Hii stori siijui kabisa, lakini nikiangalia tu kwa haraka haraka mabandiko ya wengi, mtoa mada anaonekana kushikwa na "guilty" ya kuwa labeled TRAITOR. Maelezo yake mwenyewe yako wazi kuwa alikuwa mmoja wa wasaliti waliowasaliti wenzao..... Mhhhh miaka mingi imepita, lakini madhara ya vitendo vyake bado yanamkaba mwenyewe.

Naona kitendo cha hao g211 kurudishwa na mahakama hatimaye wakamaliza chuo kilimkera sana. Pole. Vipi huko mtaani, huo mwaka walioupoteza umeleta matokeo gani? Muda ni mwalimu mzuri sana .....

Ungesoma bila kukurupuka ungegundua shida kwangu na kwetu wote G72 haikuwa wao kushinda kesi. Shida kwangu ilikuwa ni harrasment zao kabla na baada ya kurudi.

Hata wangeishia kutuita TRAITOR bila kutughasi mimi binafsi isingenihangaisha. Lakini uhuni wa kutangaza tuistumie madarasa kujisomea usiku, hata leo ukijirudia nitataja tena hadharani zaidi maana ndiyo njia ya kujilinda.

Kama wewe unaita huo ni u-TRAITOR basi mimi naita uhuni ule ni UKICHAA.
 
neno traitor ni label sahihi kwenu na hata wewe leo inaonekana hujaacha usaliti ndiyo maana unataja wenzio wakati ukijihami kuficha jinalo halisi!YUDA ISKARIOT

Hivi ni shujaa gani anayeogopa kutajwa linaposimuliwa tendo la ushujaa wake? Mnajiita G211 kuwa mashujaa lakini wakati huohuo mnalaumu kutajwa humu JF!

Mnalaumu kwa sababu mnajua kuwa vitendo vya kihuni mlivyofanya enzi zile kwa matukio yale ni zaidi ya hivi nilivyotaja humu!

Nilitegemea kama kweli mlijisifia kuwa nyinyi G211 ni mashujaa na sisi G72 ni ma-TRAITOR basi mngesaidia kuweka list nzima ya G211 ili nchi nzima na walioko vyuoni wawaone mashujaa wa 1994 pale UDSM.
 
Msaliti ni Msaliti tu!!

Till now wewe bado traitor tu huna jipya !

Nyinyi ndiyo tuliwafanya walau muwe na discpline ya kuwa na jipya. Jipya ni kwamba baada ya zile varangati mkabuni mbinu ya kujenga hoja na si kuvaa mabuti na kuvamia madarasani maana huko tayari tuli-balance power iliyowashinda mwngini.

Mimi hata leo mngeniita MWOGA au hata mkitaka kuniita MWOGA ninaweza kuna walau mna akili kuliko akili zenu zilivyoganda kwenye neno TRAITOR.


MWOGA ni mtu ambaye mnapopanga mapinduzi anayaogopa na ikibidi anawaambia wazi kuwa hatayashiriki. Hana sababu lakini ni mwoga tu.

TRAITOR kamwe si mwoga. TRAITOR ni mshiriki mkubwa na TRAITOR mzuri ni yule anayeshiriki katika ngazi ya uongozi wa mapindui hayo lakini mwiho anawageuka na kuwaangamiza vizuri kwa sababu anawajua.

TRAITOR ni wachache sana. Hawafiki hata 3% kwenye organisation nyingi. Lakini waoga wanaweza kuwa wengi.

Katika G211 na G72 hatukuwahi kuwa na agenda tukabishana kisha tukakualiana tuisimamie. Nyinyi mlikuwa 75% na sisi 25%. Ikishakuwa hivyo huo ni mpasuko yaani DIVISION na wala huwezi kuita usaliti (TRAITOR).

Taabu yenu ya kushindwa kuchambua mambo kwa lugha rahisi ndiyi ilifanya tuone hamna lolote hadi mlipojifunza kujenga hoja miaka miwili iliyofuata baada ya nyinyi kukaa home mwaka mmoja.
 
Kwa nini umemtaja Mtatiro badala ya Daud Deo?

Mkuu
Magwangala,
Daudi Deo alibebwa na Julius Mtatiro kupata Urais wa DARUSO. Utakumbuka kwamba kipindi kile Rais wa DARUSO ilipaswa awe Mtatiro bahati mbaya jina lake halikupitishwa na utawala. Sasa kwa vile Mtatiro hakuwa mgombea wanafunzi wengi walisema yeyote atakaenadiwa na Mtatiro watampa kura. Ushindi wa Deo Daudi ulitokana na kukampeniwa na Mtatiro. Sasa baada ya Deo Daudi kushinda Uraia na hatimae Mtatiro kupata Uwaziri Mkuu, Mtatiro alionekana yeye kama ndiye Rais wa ile Serikali.

Na hadi leo hii Jina la Mtatiro ndilo linakumbukwa katika ile serikali kuliko jina la Rais wake.

TUMBIRI (PhD, University of HULL - UK),

tumbiri@jamiiforums.com,
tumbiri@chadema.or.tz
 
Mugo"The Great";4172914 said:
Huyu anayejiita Subirijibu amenifanya nichangae hii mada japo nilikuwa napita tu

Njooni,

Tuiweke historia sawa maana ilipotoshwa vya kutosha au kama ilisimuliwa kiukweli basi ulikuwa na wa juujuu mno.

Kibaya ni kwamba mliowaita ma-TRAITOR waliogopa kuisimulia waziwazi. Na mimi binafsi nimefurahi imesomwa na wengi na sintachoka kujibu hoja zenu maana sina kazi ya kuumba uongo kwani ukweli ni mmoja tu na sichoki kuusimulia.

Mugo"The Great";4172914 said:
Huyu anayejiita Subirijibu anajaribu kupotosha baadhi ya mambo katika story yake hii. Wakati wa tukio la kumtoa "Mtungihela" , mimi nilikuwa First Year FOE naVurugu za kumtoa Muutngirehi hazikufanywa/kuanzishwa na G211, kwani kabla ya mkutano pale Nkrumah, tulishakubaliana kuwa G211 wakae floor ya juu wakiwa na Tshirt zao, na sisi 1st year, 3rd tukaeground floor. Sikumbuki vizuri tulikubaliana 4th year wakae wapi.



Sijakataa kuwa mlifanya vikao hata milioni moja kujiandaa kukaa vile pale Nkrumah kuhamasishana Mtungirehi apondwe na viti. Isingewezekana Nkrumah ikawa vile siku ile kama hakukuwa na vikao mara kadhaa. Hakika mlikuwa organised.

Nilichofurahia hapa ni kwamba unadhani umefanya vizuri kuongea habari ya vikao vyenu, lakini kumbe umetuthibitishia kwamba mapinduzi ya kihuni ya kumuondoa Mutungirehi mlihusika na kuyapanga mapema.

Tofauti na kaka zako humu G211 wanajitetea kwamba Discpilary Commitee iliwakuta not guilty kuhusu suala la Mutungirehi.

Kumbe Chuo kilifanya makosa kuwaita hao G211 peke yao kujitetea. Hearing Commitee ingekuita wewe kutoa ushuhuda basi ungetamka haya unayosema leo hao G211 au baadhi yao wangekutwa wako guilty na sasa wangefukuzwa rasmi na si kusimamishwa mwaka mmoja tu.

Ndiyo maana nasema ile mnayoita Spirit of FOE imewaharibu kwa sababu mlizoea kukaa kwenye vikao ndipo mje na msimamo mmoja kama FOE hata kama ni msimamo wa kupiga mateke na magumi Chuo kizima.

Leo hamko pamoja, mmesambaa kila pembe ya dunia JF yote inawashuhudia mnashindwa kujisimamia kwenye hoja hii hadi mnaiingia kichwakichwa mkizani mnateteana kumbe mnavurugiana.

Mkikutana uso kwa uso mnaochangia humu JF mnaweza kutandikana ngumi bure kwa kulaumiana kwamba "mbona wewe umeropoka na kuharibu mambo"




Mugo"The Great";4172914 said:
kwani kabla ya mkutano pale Nkrumah, tulishakubaliana kuwa G211 wakae floor ya juu wakiwa na Tshirt zao, na sisi 1st year, 3rd tukaeground floor. Sikumbuki vizuri tulikubaliana 4th year wakae wapi.

Unajua kwa nini nimekuwa nikichukia kile mnachoita Spirit of Engineering pale UDSM. Ni kwa sababu ya kujisifia mambo ya kijinga na kibabe kama haya unayosimulia.

Hao wote mliokubaliana vikaoni ni Engineering. Wala hamkuhusisha Chuo kizima kana kwamba huyo mnayeenda kumtwanga na viti ni Rais wa Engineering Student kumbe ni President wa Students of UDSM!

Halafu huo ndiyo mnataka niutetetee kwamba ndiyo Spirit ya FOE yaa Spiriti na Engineering. Hawa watoto wetu wa sasa si wataniita "baba mlikuwa vichaa mlipokuwa USDM"!

Watoto hawa wanasoma JF na huwezi kuwazuia. Ni afadhali wasome wakaja kunieleza "Baba, kuna mtu mmoja kwenye JF anaitwa SubiriJibu nimeona anajibizana na classmates wenzako".

Ndiyo sababu tunaweka history sawa ili tusionekane wote tulikuwa wehu.
 
Subirijibu; nimesoma post yako ya kwanza yote, na sasa hivi nina uhakika kuwa wewe ulikuwa ni sehemu iliyodhoofisha nguvu za wanafunzi wa engineering.

Kichuguu,

Kwanza nikiri kwamba mimi ni msomaji wa post zako kwa miaka mingi. Na sikuwahi kufikiri kuwa ulikuwa lecturer pale FOE. Lakini kwenye hii nikuweke sawa kwamba umefanya makosa makubwa kutosoma post zote ili walau uchambue hata hoja za hawa mabwana waliojiita G211 na hoja zangu zilizofuata.

Wewe ukaishia kwenye ya kwanza na mimi sina budi nikujibu hata kama nimeshaeleza mara kadhaa na tuko page ya nne sasa. Nakujibu kama ifuatavyo:


hivi nina uhakika kuwa wewe ulikuwa ni sehemu iliyodhoofisha nguvu za wanafunzi wa engineering.

Kichuguu,

Na wewe kama wenzako mnataja sana hili neno NGUVU YA ENGINEERING ambayo wenzako wanaita SPIRIT OF ENGINEERING. Lakin wote wewe na wao hamfafanui hiyo SPIRIT au NGUVU ilikuwa imejikita kwenye mbinu zipi.

Je, mlikuwa mnajua kujenga hoja za kushwishi wanachuo wenzenu ambao mlizoea kuwaita MANGWNI? Tutaona paragraph zinazofuata.

Ndiyo maana nimesema sana humu kuwa, hata ningejikuta niko kwenye kundi la G211, basi leo hii ningeishi na majuto ya ajabu. Kwa sababu wanaosoma thread hii wamevutiwa na kuziita zileG211, G72 na MUTUNGIREHI kuwa ni harakati. Lakini ndani ya harakati hizo mwanaJF anasoma na kuona na kutaka kujua ni mbinu gani mliyokuwa mnatumia.

Bila hii thread, basi watu wangedhani kuwa Engineering walikuwa ni wataalamu wazuri wa kujenga hoja au point kiasi kwamba hoja zao zilikuwa hazipingiki yaani ziko researchful.

Lakini badala yake mwana-JF anasoma, sanasana anakuja kugundua kulikuweko ka-kikundi kanachapa watu makonde , kanazuia watu wasisome prep, kanamtwanga mtu na viti. Kumbuka haya mambo hayakuwa siri siku zile yaliandikwa sana magazetini.

Ilikuwa tukifika mtaani ndugu na jamaa wanauliza "Hallo, iweje eti Engineering mnaandikwa magazetini kuwa mmekuwa kama mabondia kutandika wenzenu makonde pale UDSM?"

Halafu wewe Kichuguu na wenzako, unataka nitetee hali hiyo eti tu kwa vile mmeibatiza jina SPIRIT OF ENGINEERING.
Ndiyo maana nasema ningeitetea hata kwa robo saa, basi ningepata shida sana maishani na dhamira ingenisuta miaka yote hadi kaburini.

Mna vichwa vya ajabu sana kutetea mambo ambayo yanastahili kufanywa na sokwe mtu aliyefunguliwa kule Gombe Reserve akaanza kutawanya watu mitaani kwa makonde!

ni kweli kuwa waalimu wa FoE walishaona kuwa elimu ya engineering Math iliyokuwa inatolewa kwa wanafunzi wetu haikuwa inakidhi tena malengo yake, wanafunzi walikuwa wanafundishwa zaidi abstract math kuliko applied math

Kichuguu,

Ndiyo maana nitarudia tena na tena kuwa hii thread imewachanganya maana hamkudhani iko siku mtaanikwa hivi. Sibishani na unachosema kuhusu ufundishaji wa Engineering Mathematics na unachosema kina ukweli fulani. Ukweli huo ndiyo maana ile test iliysababisha ikaitwa kuwa ngumu.

Thread hii imewaumbua kwa sababu wewe unaliona kama ni tatizo lakini mwenzako mmoja wa G211 kaja humu anajitetea kwamba ile test ilikuwa rahisi kama nyanya.

Ndiyo maana nasema mnazidi kunipa point kwamba tayari kulikuwa na tofauti kubwa mapema kwamba baadhi walishaona tayari wameshavuka First Year kama huyo G211 aliyeona test ni nyanya, na tayari wengine walishaona ile test ni ngumu na imewakamata na kuna hatari ya ku-DISCO.

Kibaya ni kwamba tukakaa hivihivi bila kikao chochote au makubaliano yoyote na mtihani ukaja hatujawahi kukutana na kila mmoja akawa na uamuzi wake.

Ni upuuzi kuita watu TRAITOR wakati hamkuwahi hata kufikiria kuwa na jambo la pamoja la kujadili liwaweke wamoja.


Iwapo msimamo wenu ungekuwa ni mmoja kwa wanafunzi wote, kusingetokea tatizo la wanafunzi kufukuzwa kwa sababu watawala hupenda sana kugawanya wanafunzi katika makundi.

Unachosema ni kweli. Hata kama ungeishia post yangu ya kwanza nimeeleza kwamba mimi msimamo wangu dakika 20 za kwanza nilitamka kuwa tufanya moja kati ya mawili.

1: Tuwatoe waliomo kwenye vyumba vya mtihani ili tujadili kwanza hatima yetu huku hakuna hata mmoja akiwa darasani na hata tukifukuzwa basi tufukuzwe wote first year.

2: Tuingie tufanye mtihani maana haiwezekani wengine wafanye na wengine wasifanye.

Hakuna aliyesikiliza hili wazo langu, hadi dakika hiyo tension zilikuwa ni kubwa kila mmoja anatembea huku na kule na wala hatukuwa kama mkutano mmoja. Nikaona tunacheleweshana kijinga nikaisngia kuungana na waliokwisha anza mtihan dakia 25 kabla.

Nakumbuka kuna wakati Ladislaus Malima ilibidi akae pembeni analia machozi ingawa sijui ni kwa hasria au huruma. Ndivyo hali ilikuwa.


Wakati huo Professor Materu hakuwa na interest sana na foE tena kwa vile term yake ilikuwa inafikia ukingoni na alikuwa anajaribu kujijenga kuchukua nafasi ya Director of Postgraduate Studies, kwa hiyo nyinyu mlifanya ushiriki wake katika kuwavictimize wanafunzi engineering akiwa sehemu ya utawala, iwe ni rahisi sana.

Kichuguu, Huwa nakupa heshima zote lakini ninajisikia vibaya kukuaibisha mtu ninayekuheshimu kama wewe.

Ndiyo makosa yako ya kuishia post namba 1 ukaacha zingine. Ungesoma thread hii yote ungeona nimesema ni kweli Dean alikuwa Prof. Materu lakini suala lile siku ile na hata kabla lilishughulikuwa na Marehemu Dr. Nzali.

Kuhusu Prof. Materu kutokuwa na interest na FOE ninakushangaa, hata hawa G211 unaowatetea watakushangaa pia kwani Prof Materu aliwafundisha somo liitwalo Power Electronics wenzetu wa Electrical Engineer walipofika 3[SUP]rd[/SUP] year yaani Nov. 1995 hadi May 1996.

Kisha Prof. Materu huyohuyo ikabidi awachukue wa nyuma yao nao walipofika 3[SUP]rd[/SUP] Year yaani Nov. 1996 hadi May 1997. Kama ni kweli ulikuwa Tutorial Assistant tangu 1995 hadi 1996 maana yake ulimkuta Prof. Materu na ukaondoka bado yuko Faculty of Engineeing.

Ndiyo maana nasema najisikia vibaya sana kukuita MUONGO mkubwa lakini maadamu umedanganya sina jinsi nyingine ya kukuita ila kukuita MUONGO, na JF imeona leo kwamba Kichuguu ni MUONGO.

Inabidi G211 na nyinyi mnaowatetea, kama mnaweza basi tengenezeni email group mjipange huko, mtunge uongo wenu ndipo mvamie hapa JF kujibu post hizi.

Mkifanya hivyo, mtakuwa mmefanya kama mlivyokuwa mnafanya vile vikao vyenu vya siri na ile mikakati yenu ya kujipanga kutandika watu mabuti, kuwafukuza madarasani, kuliko sasa ambavyo mnakurupuka hapa JF kila mmoja na lwake halafu mnaishia kuletewa data za uhakika na mnaishia kuumbuka.
 
Nimekuambia kuwa sijui mliohusika katika mgogoro ule, ile post yako ya kwanza inaonyesha kabisa kuwa mligawanyika, na mgawanyo huo ulisababsihwa na watu wa aina yako, kwani kama kweli ulikiri kuwa test ile ilikuwa ngumu sana, nafikri ilikuwa ni kwenye complex analysis, na ukasema kuwa mwalimu alifundisha bila kuelekwa na akatoa mtihani mgumu sana katika muda mfupi sana kiasi kuwa hadi dakika ya mwisho hakuna aliejua la kufanya, hiyo ilikuwa ni sababu tosha kabisa wanafunzi wote muwe na masimamo mmoja. Lakini nyinyi mligawanyika. Bila kujali iwapo mgawanyo ulitokea dakika ya mwisho au dakika ya kwanza, ukweli kuwa mligawanyika, na kundi ulilokuwamo wewe baada ya katika mgawanyiko huo ndilo lilikuwa kundi la uvurugaji. Mambo yaliyokuja kutokea mwishoni baada ya kesi ni matokeo ya mgawanyiko mliouanza akina nyie.

Mgogoro wenu ulikuja katika kipindi cha pili cha utawala wa Profesor Materu, na mimi ninajua namna alivyokuwa akifanya shughuli zake katika kipindi hicho. Iwapo mgogoro wenu ungetokea katika kipindi chacke cha kwanza huenda angeushughulikia tofauti kabisa na kipindi hicho cha pili.

Mikutano ya uimarishaji wa ufundishaji wa Eng Math iliandaliwa na Dr. Nzali (RIP) nadhani wakati huo akiwa First Year Convenor. Iwapo wanafunzi msingegawanyika, mngepata support ya namna fulani kutoka kwa waalimu wa engineering kuhusu madai yenu, lakini baada ya kugawanyika kukawa hakuna sababu ya waalimu kujiingiza. Dr Nyamwihula (RIP) a.k.a Bongi Benda, alikuwa ni mmoja wa waalimu waliojitolea kusaidia kufundisha Eng Math tutorials through mikutano ya Dr. Nzali. Kila idara ilitoa kama waalimu wawili au watatu ingawa electrical engineering ndiyo iliyopfunga kazi kwa kutoa waalimu wengi.

Sikufuatilia mjadala wote kwa sababu sijui kilichoendelea baada ya hapo na hasa kwa vile ilikuwa ni katika politics za wanafunzi, lakini mwanzo wake ndio nilioamua kuchangia kwa vila ulikuwa na institutional element.

------------------------
NB:

(a) Mkusanyo wa waalimu wa engineering kufundisha tutorials za eng math haukuhusu tutorial assitants na wala mimi sikuwa tutorial assiatant wakati huo kwani tayari nilishakuwa na masters muda mrefu. Waalimu wote ambao fani zao zilikuwa zinahusisha math waliombwa wajitolee kusaidia kuendesha tutorials hizo; ndiyo maana akina dr. Nyamwihula alikuwamo.

(b) Interest ya kiuongozi ni tofauti na interest za kitaaluma. Kiuongozi Materu alikuwa hana ambition yoyote ya kuendelea kuiongoza engineering, ila kama mwanataaluma bado alipenda kufundisha somo lake. Ambition za Materu kiuongozi wakati huo zilikuwa ni kubwa zaidi ya interest zenu wanafunzi wa wa mwaka pili wa engineering. Hata Professor Mwandosya alikuwa anakuja kufundisha Power Electronics wakati akiwa kamishna wa energy, ingawa hakuwa na inteterest yoyote ya kuongoza engineering. Professor Lwakabamba naye aliwahi kurudi kufundisha Thermodynamics alipotoka Nigeria ingawa hakuwa na interest ya kuongoza engineering mpaka alipoteuliwa kwenda kuongoza Rwanda. Professor Mawenya naye alikuwa anarudi kufundisha pale civil engineering huku akiwa anafanya kazi zake binafsi huko mjini. Dr. Mosha naye alikuwa anakuja kufundisha kule Mechanical engineering huku akiwa ni director wa kampuni fulani huko mjini. Hata professor Luhanga alikuwa anakuja kufundisha ingawa mara mwisho mwaka 1995 alisema nimechoka msinipe madarasa tena, kwa vile madarasa yake yakawa yanafundishwa na wengine tu. Nadhani unaelewa tofauti ya interest ninayoongelea na interest unayofikiria.

(c) Again, kuitana traitor au G112345 ni student politics ambazo mimi sitaweza kuzizungumzia kwa vile sijui undani wake; ninaloongelea ni ule mwanzo wa mgawanyiko wenu. Wewe ulikwenda upande mbaya wa mgawanyiko huo.
 
mimi wa kizazi hiki cha digital ingawa sijapitia chuo kukuu cha UDSM mpaka sasa naweza kujivunia mafanikio mawili matatu ya elimu yangu.haya nyie ma-G211 na ma-TRAITORS wa UDSM ya 1994 mnajivunia nini?i mean is there any positive impact alongside to what you have narrated before us?
 
Back
Top Bottom