Ukweli: CCM haina hata Viongozi!

Deus F Mallya

JF-Expert Member
Jul 28, 2011
705
440
Ni wazi kuwa CCM ni chama kikongwe kulinganisha na Vyama vyote vya siasa hapa Nchini; Ukongwe huu wa CCM umedhihirika hasa miaka takriban saba iliyopita kwa baada ya wengi maelfu kukihama chama hicho.

Waliobaki ndani ya CCM kwa sasa hawana tena Credibillity ya kuitwa viongozi kwa sababu hawaaminiki,Hawajui miiko ya Taifa wala Mila na Desturi za Chama cha Mapinduzi. Tumeshuhudia Baraza la Mawaziri likivunjwa kama mara nne hivi kwa kipindi cha miaka Saba, Tumeshuhudia hata wale ambao ni wateule wa Chama cha Mapinduzi wakiwatusi wananchi kwenye majukwaa ya Kisiasa, Wengine walidiriki kuwachapa viboko waalimu, Wengine wakapigana ngumi kule Arusha (Muulize Ole Sendeka), Wengine wanadiriki kuwatukana waajiriwa (Proffesionals) Matusi ya nguoni hadharani kuwa usomi wake ni wa Degree ya Chupi, Wengine sasa wananyukana kwa kutoleana Bastola kugombea nafasi za 'Uongozi' na wengine kuamua kuwahonga wananchi vitumbua kwa ajili ya kuomba wachaguliwe!..Wengine wanalalamika kupewa nafasi wakiwa wadogo, Wengine kuua kwao si ajabu!.

Kwenye ulingo wa Siasa; Kiongozi yeyote makini akiona haya na mengineyo lukuki yasiyoandikika pengine kuukifu ukurasa huu yanatokea na kuendelea kuzidi angetafakari upya nafasi yake na uwezo wake wa kuongoza na kufanya maamuzi: Maamuzi hayo pekee ndiyo yangeweza kumtofautisha na hao wengine. Lakini ukimya huo wa kiongozi wake mkuu naye unampotezea Credibillity ya kuitwa kiongozi.
 
well said Deus.Kwa wapuuzi wanaona wateuliwa wa CCM ambao walikuwa wakiingia by deafault na kupewa coverage na magazeti kipindi hicho waandishi hawachambui kitu wala linganisha matukio,kuwa ni viongozi.hawa watu siku hizi nao wanajihesabu kuwa ni viongozi.CCM hata viongozi vijana kama akina Malima na Hussein Mwinyi hawajaonyesha kuwa na mawazo ya kisasa wala uwezo wa kufundishika kwa experience.Kwa ujumla chama kinakufa na kama ilivyo taifa stars haina tiimu ya vijana.
 
Mkuu Deus,
Mara chache sana ambapo ccm huwa wanakubali ukweli unaosemwa. Ccm wameshindwa kujirekebisha hasa kwa maandalizi ya huku uzeeni. Tayari kimepoteza na kinaendelea kupoteza wanachama makini ambao leo wangekuwa viongozi wazuri sana. Kwa mfano Mwaka 1995 waliondolewa wengi kwa hila za kifisadi akiwemo Mhe.Dr.Willibroad Slaa. Hebu jiulize leo Dr.Slaa angekuwa Rais wa nchi hii ingekuwa mbali kiasi gani? Watu wengine wengi ambao waliamua tu kukaa pembeni na kuiangalia ccm baada ya kuenguliwa kwa hila nao walishaonyesha juhudi zao kubwa kwa nafasi zao.

Kweli ccm Haina Viongozi.
 
well said Deus.Kwa wapuuzi wanaona wateuliwa wa CCM ambao walikuwa wakiingia by deafault na kupewa coverage na magazeti kipindi hicho waandishi hawachambui kitu wala linganisha matukio,kuwa ni viongozi.hawa watu siku hizi nao wanajihesabu kuwa ni viongozi.CCM hata viongozi vijana kama akina Malima na Hussein Mwinyi hawajaonyesha kuwa na mawazo ya kisasa wala uwezo wa kufundishika kwa experience.Kwa ujumla chama kinakufa na kama ilivyo taifa stars haina tiimu ya vijana.

Ni kweli kabisa, Vijana waliotegemewa wangekuwa strong kuongoza chama na serikali wengi wameshindwa. Wamekuwa ni watu wa 'Kuingia na kutoka' tena kwa kashfa ndani ya serikali.. Wamekuwa ni watu wa majungu na majivuno!. Wamebweteka. Nasita kumtolea mfano Nape Nnauye alipokuwa nje ya 'System' ya serikalini alivyokuwa anaikosoa ccm na Serikali... Alipopata ukuu wa Wilaya akaacha kuikosoa Serikali akaanza kuikosoa CCM.. Alipopata ukatibu wenezi amesahau yote anakosoa vyama vya upinzani na kugusa nafsi za watu. Amesahau kuwa Taifa lina watu wengi sana ambao akianza kugusa nafsi zao mmoja mmoja hawezi kumaliza.

Bado ccm haina viongozi.
 
Mkuu Deus,
Mara chache sana ambapo ccm huwa wanakubali ukweli unaosemwa. Ccm wameshindwa kujirekebisha hasa kwa maandalizi ya huku uzeeni. Tayari kimepoteza na kinaendelea kupoteza wanachama makini ambao leo wangekuwa viongozi wazuri sana. Kwa mfano Mwaka 1995 waliondolewa wengi kwa hila za kifisadi akiwemo Mhe.Dr.Willibroad Slaa. Hebu jiulize leo Dr.Slaa angekuwa Rais wa nchi hii ingekuwa mbali kiasi gani? Watu wengine wengi ambao waliamua tu kukaa pembeni na kuiangalia ccm baada ya kuenguliwa kwa hila nao walishaonyesha juhudi zao kubwa kwa nafasi zao.

Kweli ccm Haina Viongozi.

Mapema mwaka jana kwenye gazeti la kiingereza la The East African nilipata wasaa wa kupenyeza makala zangu kadhaa ikiwemo iliyojaribu kuonyesha ilipojikwaa ccm. Makala ile ilieleza hata hiki ulichokiandika hapa.. Kuingia kwa 'Mafisadi' ndani ya System ya chama chochote cha siasa ndio huwa ugonjwa wa kudumu wa chama. Baada ya hapo chama huzidiwa na 'Wadudu' hao kwa kuwa huitana na kujengeana vibanda humo kwa wingi na hatimaye chama huzidiwa na ugonjwa huo na kufa. Kifo hicho hutokea pale ambapo waadilifu 'Wawili' ndani ya ccm hupaza sauti na kudhani kuwa bado wako salama. Hapo ndipo wanapohaha kukinusuru chama na wanapokimbilia kwa mfalme wanakuta maneno "Mene mene na tekeli"..
 
Mifano unayotumia haina ulinganishi. Mbona hutaji watu au mambo mazuri wanayofanya. Utaishia kupiga chabo vitu vidogodoga mpaka lini
 
Mifano unayotumia haina ulinganishi. Mbona hutaji watu au mambo mazuri wanayofanya. Utaishia kupiga chabo vitu vidogodoga mpaka lini

Mkuu nimekuachia nafasi na wewe utaje/uchagie kwa sehemu yako na pengine upongeze hayo 'Mazuri waliyofanya' na kukosoa hivyo vitu 'Vidogo vidogo nilivyopiga chabo' ...

Karibu.
 
Mapema mwaka jana kwenye gazeti la kiingereza la The East African nilipata wasaa wa kupenyeza makala zangu kadhaa ikiwemo iliyojaribu kuonyesha ilipojikwaa ccm. Makala ile ilieleza hata hiki ulichokiandika hapa.. Kuingia kwa 'Mafisadi' ndani ya System ya chama chochote cha siasa ndio huwa ugonjwa wa kudumu wa chama. Baada ya hapo chama huzidiwa na 'Wadudu' hao kwa kuwa huitana na kujengeana vibanda humo kwa wingi na hatimaye chama huzidiwa na ugonjwa huo na kufa. Kifo hicho hutokea pale ambapo waadilifu 'Wawili' ndani ya ccm hupaza sauti na kudhani kuwa bado wako salama. Hapo ndipo wanapohaha kukinusuru chama na wanapokimbilia kwa mfalme wanakuta maneno "Mene mene na tekeli"..

Kaka si wanasema wewe ni std seven?inakuweje sasa unachambua mambo yanayokuja thibitika kuwa sahihi?CCM ni kama mamba anayekaribia kufa ktk kidimbwi kidogo cha maji.Mzoga wake huaharibu maji yote.CCM ikicheleweshwa itaoza na nchi.
 
Ni wazi kuwa CCM ni chama kikongwe kulinganisha na Vyama vyote vya siasa hapa Nchini; Ukongwe huu wa CCM umedhihirika hasa miaka takriban saba iliyopita kwa baada ya wengi maelfu kukihama chama hicho.

Waliobaki ndani ya CCM kwa sasa hawana tena Credibillity ya kuitwa viongozi kwa sababu hawaaminiki,Hawajui miiko ya Taifa wala Mila na Desturi za Chama cha Mapinduzi. Tumeshuhudia Baraza la Mawaziri likivunjwa kama mara nne hivi kwa kipindi cha miaka Saba, Tumeshuhudia hata wale ambao ni wateule wa Chama cha Mapinduzi wakiwatusi wananchi kwenye majukwaa ya Kisiasa, Wengine walidiriki kuwachapa viboko waalimu, Wengine wakapigana ngumi kule Arusha (Muulize Ole Sendeka), Wengine wanadiriki kuwatukana waajiriwa (Proffesionals) Matusi ya nguoni hadharani kuwa usomi wake ni wa Degree ya Chupi, Wengine sasa wananyukana kwa kutoleana Bastola kugombea nafasi za 'Uongozi' na wengine kuamua kuwahonga wananchi vitumbua kwa ajili ya kuomba wachaguliwe!..Wengine wanalalamika kupewa nafasi wakiwa wadogo, Wengine kuua kwao si ajabu!.

Kwenye ulingo wa Siasa; Kiongozi yeyote makini akiona haya na mengineyo lukuki yasiyoandikika pengine kuukifu ukurasa huu yanatokea na kuendelea kuzidi angetafakari upya nafasi yake na uwezo wake wa kuongoza na kufanya maamuzi: Maamuzi hayo pekee ndiyo yangeweza kumtofautisha na hao wengine. Lakini ukimya huo wa kiongozi wake mkuu naye unampotezea Credibillity ya kuitwa kiongozi.
Akili yako ukiizoeza kuona mabaya tu ya nchi hii heri uhamie ughaibuni.

Ile bara bara uliyopata ajali si ilitoka kufanyiwa ukarabati mkubwa.
Na barabara za Singida -Arusha si mpya?
Leo injengwa barabara ya Dodoma -Arusha una habari?

Mkinywa mvinyo mnywe usioharibika!!
 
Kaka si wanasema wewe ni std seven?inakuweje sasa unachambua mambo yanayokuja thibitika kuwa sahihi?CCM ni kama mamba anayekaribia kufa ktk kidimbwi kidogo cha maji.Mzoga wake huaharibu maji yote.CCM ikicheleweshwa itaoza na nchi.

Aaaah... Mkuu unajua mtu anayekosa la kusema huwa anaropoka!.. Anaweza hata kukataa kuwa hukuzaliwa na binaadam ili mradi tu wakuudhi..

"Pengine ukisema sana watasema ulitangulia kutoka miguu badala ya kichwa; Yaani huna adabu" Mrisho Mpoto
 
Akili yako ukiizoeza kuona mabaya tu ya nchi hii heri uhamie ughaibuni.

Ile bara bara uliyopata ajali si ilitoka kufanyiwa ukarabati mkubwa.
Na barabara za Singida -Arusha si mpya?
Leo injengwa barabara ya Dodoma -Arusha una habari?

Mkinywa mvinyo mnywe usioharibika!!

mbona hujajibu waa kuchangia hoja.Unaandika vitu tofauti sana ukidhani unatete magamba.Barabara zingejengwa tuu hata kama tusingekuw ana serikali?somalia barabara zinajengwa hadi leo.....Leo mnashindana na nani aliyeshindwa?Mnakuwa kama konokono akijtamba kuwa sasa anatembea tofauti na kipindi cha nyuma alikuwa hatembei huku akishindwa jiona kuw anatembea kinyumenyume..hizo barabara tumekopa, na zitaaharibika kabla hatujamaliza lipa mikopo hiyo.Tutakauw akatikk ahali mabya sana.
 
Akili yako ukiizoeza kuona mabaya tu ya nchi hii heri uhamie ughaibuni.

Ile bara bara uliyopata ajali si ilitoka kufanyiwa ukarabati mkubwa.
Na barabara za Singida -Arusha si mpya?
Leo injengwa barabara ya Dodoma -Arusha una habari?

Mkinywa mvinyo mnywe usioharibika!!

Jicho la Jemedari wa Vita huona hatari iliyo mbele yake kwa ujasiri; Jicho la Askari mwoga huangalia sehemu yenye nyasi pevu na kujificha!.. Jicho la mjakazi jasiri huona yanayo mdhalilisha mfalme wake na kumuepusha na dhahama; bali Jicho la mwenye haya na aibu huinamisha kichwa na kuinama miguuni pa mfalme aliye uchi...

Huna mantiki ya kuniambia nisiangalie mabaya kwa mifano yako ya 2X2-4.. Huwezi. Unanijengea dhana ya Askari dhaifu au mjakazi mwenye woga. Unanijengea Udhaifu.. Mimi si DHAIFU. Loh!.
 
mbona hujajibu waa kuchangia hoja.Unaandika vitu tofauti sana ukidhani unatete magamba.Barabara zingejengwa tuu hata kama tusingekuw ana serikali?somalia barabara zinajengwa hadi leo.....Leo mnashindana na nani aliyeshindwa?Mnakuwa kama konokono akijtamba kuwa sasa anatembea tofauti na kipindi cha nyuma alikuwa hatembei huku akishindwa jiona kuw anatembea kinyumenyume..hizo barabara tumekopa, na zitaaharibika kabla hatujamaliza lipa mikopo hiyo.Tutakauw akatikk ahali mabya sana.

Wanataka tupongeze Kupanda kwa Deni la Taifa au kuporomoka kwa uchumi? Wanataka tupongeze kupanda kwa gharama za maisha ya Wananchi? Au kule kushuka kwa kiwango cha elimu? Wanataka tupongeze yale mabilioni ya JK yalivyofujwa au wanataka tupongeze zile zilizofanya sherehe za miaka 50? Wanataka tupongeze zipi na tumpongeze nani anayefanya nini kwa pesa za mikopo ambayo inariba kubwa kama hizo za china na WB? Wanataka tupongeze? Haya: na tuwapongeze.
 
Aaaah... Mkuu unajua mtu anayekosa la kusema huwa anaropoka!.. Anaweza hata kukataa kuwa hukuzaliwa na binaadam ili mradi tu wakuudhi..

"Pengine ukisema sana watasema ulitangulia kutoka miguu badala ya kichwa; Yaani huna adabu" Mrisho Mpoto

teh teh..nadhani una haki ya kuwadharau kwani umepata muda wa kuwasoma vyema kipindi chote waonapo michango yako na kuirukia kwa fujo.Kabla ya kujikuta wakiongea vitu hata babu ztu enzi za giza wasingeweza vifanya wakiwa na akili timamu.
 
teh teh..nadhani una haki ya kuwadharau kwani umepata muda wa kuwasoma vyema kipindi chote waonapo michango yako na kuirukia kwa fujo.Kabla ya kujikuta wakiongea vitu hata babu ztu enzi za giza wasingeweza vifanya wakiwa na akili timamu.

Wanaamua kukaa pembeni kujipanga kwa sababu inawezekana hawakujiandaa vya kutosha.. Zamu hii nimewaambia wakatafute ushauri kwa wataalam wa siasa pengine kwenye vyuo maarufu Duniani. Tatizo lao hawasomi huwa wanaangalia kumzuga mwalimu.
 
Jicho la Jemedari wa Vita huona hatari iliyo mbele yake kwa ujasiri; Jicho la Askari mwoga huangalia sehemu yenye nyasi pevu na kujificha!.. Jicho la mjakazi jasiri huona yanayo mdhalilisha mfalme wake na kumuepusha na dhahama; bali Jicho la mwenye haya na aibu huinamisha kichwa na kuinama miguuni pa mfalme aliye uchi...

Huna mantiki ya kuniambia nisiangalie mabaya kwa mifano yako ya 2X2-4.. Huwezi. Unanijengea dhana ya Askari dhaifu au mjakazi mwenye woga. Unanijengea Udhaifu.. Mimi si DHAIFU. Loh!.
Hii ipo ukurasa gani wa ilani ya chama chako?
Na ndio tatizo kubwa la kukopi na kupesti-hata wale wa darasa la saba wanajua hilo.wanasahau kuwa maji moto hayaunguzi nyumba!
 
mbona hujajibu waa kuchangia hoja.Unaandika vitu tofauti sana ukidhani unatete magamba.Barabara zingejengwa tuu hata kama tusingekuw ana serikali?somalia barabara zinajengwa hadi leo.....Leo mnashindana na nani aliyeshindwa?Mnakuwa kama konokono akijtamba kuwa sasa anatembea tofauti na kipindi cha nyuma alikuwa hatembei huku akishindwa jiona kuw anatembea kinyumenyume..hizo barabara tumekopa, na zitaaharibika kabla hatujamaliza lipa mikopo hiyo.Tutakauw akatikk ahali mabya sana.
Mkuu somo dogo la insha ya darasa la saba inakushinda?

Na huko Somalia unakozungumzia ni Arumeru au Somalia tunayoifahmu?
Ukiona fikra za uchambuzi zinakushinda ni vema ukatafuta pale panapo kutosha.
 
Nchi hii miaka kumi inaisha hatuna rais, hatuna mawaziri wala nini, viongozi wengi walioteuliwa na rais hawakustahili hata kuwa viongozi wa familia lakini wametwisha uongozi mkubwa kupindukia sasa matokeo yake ndo haya! Yaani ukimtazama kiongozi anavyoongea utazani hata darasa la chekechea hajakanyaga hana hekima wala busara jamani aliyewateua naye nadhani akili zilifanana matokeo yake nchi inaangamia kwa kukosa maarifa ya kiuongozi!
 
well said Deus.Kwa wapuuzi wanaona wateuliwa wa CCM ambao walikuwa wakiingia by deafault na kupewa coverage na magazeti kipindi hicho waandishi hawachambui kitu wala linganisha matukio,kuwa ni viongozi.hawa watu siku hizi nao wanajihesabu kuwa ni viongozi.CCM hata viongozi vijana kama akina Malima na Hussein Mwinyi hawajaonyesha kuwa na mawazo ya kisasa wala uwezo wa kufundishika kwa experience.Kwa ujumla chama kinakufa na kama ilivyo taifa stars haina tiimu ya vijana.

Kiongozi kama Hussein Mwinyi si mtu wa kumlinganisha katika uongozi unatakiwa kwanza uangalie nini kilichomfikisha hadi kuwa hapo alipi utagunduwa ni Mgongo wa baba yake hakuna jengine ni kule kupeyana bahashishi na hii imetokana na baba yake kucheza karata zake kwa umakini ndani ya chama na serekali pia katika jamii ikiwa katika pande za dini zote kuu mbili isitoshe muangalie jinsi alivyokuwa anakata mbuga sehemu hadi sehemu kugombania Ubunge ameanza mikowa ya bara hadi kumalizikia Zanzibar jiulize inakuwaje ?na kwa ujasiri gani utagunduwa serekali na chama ni vya Baba yake tukitaka tusitake kwa sasa hali ipo hivyo.
 
Back
Top Bottom