Membensamba
Senior Member
- Nov 4, 2010
- 157
- 10
Idadi ya wabunge wa bunge la jamhuri ya muungano, na ukubwa wa serikali binafsi unanipa shida kuoanisha faida yake kisiasa na gharama za kuviendesha hasa ninapofikiri umaskini mkubwa wa mwananchi wa kawaida. Sio tu kwamba tuna majimbo mengi mno ya uchaguzi, bali pia viti maalum vingi. Na kama hiyo haitoshi, kuna viti kumi zaidi vya mhe. raisi kujiwekea awapendao!
Huko Zanzibar nako kuna majimbo kila baada ya mtaa kama sio kata. Nchi ndogo, lakini makamu wawili wa raisi. Hebu wanaJF nipigieni hesabu hawa wote: Wabunge wa muungano na wa visiwani, na makamu wawili wa raisi wanagharimiwa sh ngapi kwa mwezi kama mishahara na marupurupu yao ya vikao?
Je gharama hii inalingana na umaskini wa nchi hii? Hivi nafasi yote hiyo (hatujataja ukubwa wa serikali ya muungano) kweli ni kwa maslahi ya taifa au ni njia ya kupeana kazi? Niambieni budget ya ku-run serikali ni sh ngapi kwa mwaka? Na inatoka ndani au ni msaada? Je gharama hiyo ikilinganishwa na budget ya elimu, afya, na kilimo tofauti ni justfiable kweli? Hebu wabunge zungumzeni maswala haya kama kweli mna maslahi ya taifa mioyoni mwenu tuwasikie.
Huko Zanzibar nako kuna majimbo kila baada ya mtaa kama sio kata. Nchi ndogo, lakini makamu wawili wa raisi. Hebu wanaJF nipigieni hesabu hawa wote: Wabunge wa muungano na wa visiwani, na makamu wawili wa raisi wanagharimiwa sh ngapi kwa mwezi kama mishahara na marupurupu yao ya vikao?
Je gharama hii inalingana na umaskini wa nchi hii? Hivi nafasi yote hiyo (hatujataja ukubwa wa serikali ya muungano) kweli ni kwa maslahi ya taifa au ni njia ya kupeana kazi? Niambieni budget ya ku-run serikali ni sh ngapi kwa mwaka? Na inatoka ndani au ni msaada? Je gharama hiyo ikilinganishwa na budget ya elimu, afya, na kilimo tofauti ni justfiable kweli? Hebu wabunge zungumzeni maswala haya kama kweli mna maslahi ya taifa mioyoni mwenu tuwasikie.