Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,884
- 6,885
CCM walivua gamba la unyerere na kuvaa lao ambalo linakitesa chama na kwa kweli halivuliki kirahisi. Ukiangalia historia ya familia ya Nyerere hakupenda kuwaingiza watoto wake kwenye siasa au serikalini kwa mgongo wake, na hivyo heshima yake ilisheheni na kupevuka.
CCM ya leo na viongozi wao ni tofauti na itikadi za mtazamo wa Nyerere, na ukiangalia safu ya uongozi utaona ni kile alichokisema Nape chama cha ukoo na viongozi wa ukoo kinyume na alivyoelekeza mashambulizi dhidi ya Chadema. Baba kabla hajang'atuka anamwandaa mwanawe kushika hatamu, na anapong'atuka ameshamtarisha na mwendelezo unakuwa wa mfumo wa kitemi. Haya yapo tunayaona kila siku lakini leo Nape anaelekeza kombora kwa Chadema wakati hakumbuki baba yake Moses Mnauye alikuwa kiongozi mwandamizi huko aliko.
Mwingine ambaye huna mkubwa katika serikali na chama cha CCM vigumu mno kupenya maana huko inategemea jina la mtangulizi wako katika siasa au chama, vinginevyo utaishia kuwa msindikizaji.
CCM ya leo na viongozi wao ni tofauti na itikadi za mtazamo wa Nyerere, na ukiangalia safu ya uongozi utaona ni kile alichokisema Nape chama cha ukoo na viongozi wa ukoo kinyume na alivyoelekeza mashambulizi dhidi ya Chadema. Baba kabla hajang'atuka anamwandaa mwanawe kushika hatamu, na anapong'atuka ameshamtarisha na mwendelezo unakuwa wa mfumo wa kitemi. Haya yapo tunayaona kila siku lakini leo Nape anaelekeza kombora kwa Chadema wakati hakumbuki baba yake Moses Mnauye alikuwa kiongozi mwandamizi huko aliko.
Mwingine ambaye huna mkubwa katika serikali na chama cha CCM vigumu mno kupenya maana huko inategemea jina la mtangulizi wako katika siasa au chama, vinginevyo utaishia kuwa msindikizaji.