Ukombozi wa mwanamke

Exaud J. Makyao

JF-Expert Member
Nov 30, 2008
1,518
22
DHANA YA UKOMBOZI WA MWANAMKE BADO NI TATA.

- ASASI NYINGI ZIMEANZISHWA KUWEKA MIKAKATI YA KUMKOMBOA
MWANAMKE.

- WANAWAKE WENGI WAMEINGIA MADARAKANI KWA KUWAAHIDI UKOMBOZI
WANAWAKE WENZIE.

- WANASIASA MAJUKWAANI WANASISITIZA UKOMBOZI WA MWANAMKE.

MIMI NAOMBA MNIELEWESHE,
- HIVI WANAWAKE WAKO UTUMWANI?

KAMA NI KWELI MWANAMKE YUKO UTUMWANI, ILI KUJIKOMBOA MWANAMKE ANAHITAJI KUMJUA ADUI YAKE.

BASI NIJULISHENI;
- NANI ADUI WA MWANAMKE ALIYEMTIA UTUMWANI?

Exaud J. Makyao
0784347001
 
DHANA YA UKOMBOZI WA MWANAMKE BADO NI TATA.

- ASASI NYINGI ZIMEANZISHWA KUWEKA MIKAKATI YA KUMKOMBOA
MWANAMKE.

- WANAWAKE WENGI WAMEINGIA MADARAKANI KWA KUWAAHIDI UKOMBOZI
WANAWAKE WENZIE.

- WANASIASA MAJUKWAANI WANASISITIZA UKOMBOZI WA MWANAMKE.

MIMI NAOMBA MNIELEWESHE,
- HIVI WANAWAKE WAKO UTUMWANI?

KAMA NI KWELI MWANAMKE YUKO UTUMWANI, ILI KUJIKOMBOA MWANAMKE ANAHITAJI KUMJUA ADUI YAKE.

BASI NIJULISHENI;
- NANI ADUI WA MWANAMKE ALIYEMTIA UTUMWANI?

Exaud J. Makyao
0784347001

Na kweli unahitaji kueleweshwa. Sijui unaishi ulimwengu gani. Binafsi, inanitia uchungu. Hivi, mfano, ulishawahi kusafiri kwa kutumia daladala na ukasikia hata kama wanaume wanagombana, lakini tusi litahusu "tabia fulani ya kike au sehemu zake za siri?" Nadhani uko familia na tusi kama: 'Ku****ko' na siyo 'm*** ya ****ko'

Imagine unasafiri na mama yako, dada yako, mke wako, mtoto wako wa kike au mwanamke yeyote, je kwako hayo hayahitaji ukombozi?

Baadhi ya dini zinamwona mwanamke kama "mtu mchafu" kwa vile wakati fulani anatokwa na damu sehemu zake za siri na siyo mwanamme anapotokwa na damu puani. Je, unasemaje kwa hilo?

Familia nyingi wanawake/watoto wa kike wanawekewa amri kali kuliko wanaume/watoto wa kiume ikiwa ni pamoja katika kula - mwanamke anamwandalia mwanamme chakula; mwanamme anakula chakula kizuri zaidi kuliko mwanamke; mwanamme anapewa kiti akalie na mwanamke anakaa chini; mwanamke anampigia magoti mwanamme; mwanamke anawekewa muda wa kurudi nyumbani na mwanamme hana muda maalum - akichelewa ana 'excuses' na mwanamke inabidi azikubali.

Lakini mwanamke akichelewa mwanamme siyo rahisi kukubali 'execuses'; mwanamme akifumaniwa anaweza kuomba msamaha na mwanamke akamkubali tena; mwanamke akifumaniwa mara nyingi anapigwa hadi kufa au anaachika.

Pia watoto wa kike wanauzwa. Kama kwenye familia fulani kuna watoto wa kike wengi mtu anaona atatajirika kwa mahari kuliko kuwa na watoto wa kiume tu. Pia baadhi ya familia kumsomesha mtoto wa kike ni hasara kuliko wa kiume.

Nafasi fulani hawapewi wanawake siyo kwa sababu ya uwezo wao ila kwa sababu ya 'prejudice' tu na wakati mwingine tunawaaminisha kuwa wao ni dhaifu na wanaume siyo.

Hata tunatafsiri maandiko matakatifu vibaya kwa kusema: dhambi iliingia duniani kupitia mwanamke au barua za Paulo (out of context) tukisema... 'enyi wanawake watiini waume zenu' lakini hatusemi kile Paulo alichosema kwa wanaume: 'enyi wanaume wapendeni wake zenu.'

Kwangu mimi: ukimpenda mtu utamtii kwa mema; na kama utamtii kwa hayo mema, ina maana unampenda. Kwa hiyo, tafsiri nzuri: ni 'enyi wanandoa pendaneni na heshimianeni'.

Kuna pia misemo kama: unalia kama mwanamke; una'behave' kama mwanamke etc. Kuna mifano mingi sana. Inawezekana kwa hayo yote wewe unaona hamna shida kabisa lakini kama kweli unampenda mke wako, mama yako, dada yako au mwanamke yeyote usingependa adharirishwe kwa sababu ya maumbile yake au kwa vile yeye ni mwanamke. Au unasemaje?
 
Ukombozi wa Mwanamke ni kumpatia haki stahili katika yote. Adui mkubwa wa mwanamke ni Mfumo Dume uliotawala kwa karne nyingi huko nyuma ukapigiliwa misumari na dini zote kuu.

Idadi ya wanawake duniani ni theluthi mbili na wanaume ni theluthi moja. Hawa theluthi moja wanatawala kila rasilimali na kujitwalia fursa zote huku wanawake wakiachwa ama chombo cha uzalishaji mali.

Mwanamke anakuwa hana haki katika jambo lolote hata lilolohusu matumizi ya mwili wake mwenyewe labda aseme 'naumwa' tena Zanzibar ndio hatari zaidi maana hata akisena 'naumwa' anaambiwa 'uani'

Kufuatia hali hii, Barakuu la Umoja wa Mataifa likaitisha mkutano Mkuu wa Wanawake uliojilikana kwa jina maarufu la Mkutano wa Beijing. Mhe. Dr. Getrude Mongella toka Tanzania ndiye alichaguliwa Mwenyekiti wa mkotano huo.

Mkutano huo uliwakilisha wanawake toka kila sekta na kila jamii toka nchi zote duniani na ulipitisha maazimio yafuatayo...click google 'Beijing Declaration'.. Utekelezaji wa maazimio haya ndio ukombozi wa mwanamke.
Mpaka sasa ni nchi chache zimefanikiwa kutekeleza maazimio hayo. Tanzania inapiga hatua nzuri
 
Wanawake tunatakiwa kuachana na mawazo ya kwamba hatuwezi,bila buzi bila mume maisha hayaendi, kasema nani? wake up! Wale wa vijijini naweza kuwaelewa kidogo japo nao wanaamka coz wanafanya kazi zote wanaume wanashinda bar. Halafu sisi sisi ndio tunawalea hawa wanaume wakiwa watoto tunasaidia kupandikisha mbegu za mifumo dume vichwani mwao. Watoto wote wajue kupika, deki, change light bulbs, use a screw driver, pipe wrench, shika shoka and the like regardless of their sex.
 
Exaud hakuna swala la kuelimisha hapa.Naomba niwe "straight."Unachojua wewe ni kwamba mwanamke hayuko utumwani."Correct."Sasa swali ni kwamba nani alileta dhana hii ya kishenzi na ugombanishi kwamba mwanamke yuko utumwani?Ni Ibilisi akitumia "agents" wake ambao amewasambaza dunia nzima.Hawa ni watu walio muasi Mungu na wasio ijua kweli.Watu hawa wanasukumwa tu na tamaa zao za mwili na mali,vitu ambavyo shetani anawaahidi kuwapa kama watamtumikia kwa kuigeuza kweli ya Mungu kwamba mwanamume ndiye kichwa cha nyumba na mwanamke ni msaididizi wake.Kumbuka shetani siku zote nia yake ni kumpofusha mwanadamu ili amuasi Mungu.Kama wewe una imani yeyote ya dini, simama imara kwenye imani yako,usiyumbishwe na shetani,siku hizi ni za udanganyifu wa kutisha.
 
Wanawake wako chini ya wanaume katika anga zote ambayo ni natural hata kwa viumbe wengine! Hata kibayolojia- ukisema almost kila kitu inabidi utofautishe!
Mfano; normal HB (kiwango cha damu), men > women; normal waist circumference, men > women; daily energy requirements, men > women etc
Kujidai kujikomboa ni kwenda against nature na kuwafanya wasiwe na furaha!
Mwanamuziki mmoja wa Bongo anasema mwanamke hata akiwa na mapesa, asipokuwa na mume ni kazi bure, sugar ni sugar na chumvi ni chumvi!
 
Wa-Africa baadhi ya wakati huonekana watu wa ajabu kwa kuwa tunapenda kuchupia mambo.

Wanawake kwa kweli katika Jamii za Ki-Africa hugawana kazi na wanaume na huwa ni kinyume kwa mwanamume kufanya baadhi ya kazi na huwa kinyume kwa mwanamke kufanya baadhi ya kazi. Kuvua huwa kazi ya mwanamume kama kuteka maji ikawa ni ya mwanamke haya ni mambo ambayo yapo miaka na mikaka, sasa wazungu wao wanapotaka tuwe kama wao, hapo mashaka huanza na kututumilia na udhaifu tulionao na khasa kuwatumia wasomi wwetu na kuwajaza pampu kuja na hoja ya haki za wanawke.

Jamii zetu huwa na wakorofi ambao huwadhalilisha wanawake kama jamii nyengine zilivyo, M-Wafrica sio mwenye kumdhalilisha mwanamke , bali mwafrika ni mtu ampendaye mwanamke na utaposoma Historia utaona vipi Wa-Africa walipotoa roho zao katika kuwatetea wanawake.

Ahsante
Mzee Panganyile
 
Wanawake wako chini ya wanaume katika anga zote ambayo ni natural hata kwa viumbe wengine! Hata kibayolojia- ukisema almost kila kitu inabidi utofautishe!
Mfano; normal HB (kiwango cha damu), men > women; normal waist circumference, men > women; daily energy requirements, men > women etc
1.Kujidai kujikomboa ni kwenda against nature na kuwafanya wasiwe na furaha!
2.Mwanamuziki mmoja wa Bongo anasema mwanamke hata akiwa na mapesa, asipokuwa na mume ni kazi bure, sugar ni sugar na chumvi ni chumvi!
Mkuu,
Unachosema unaweza kuwa na point lakini pia you are missing a point.
1. Tunapozungumzia masuala ya haki na usawa haimaanishi kubadilishana mwanamke avae suruali na mwanaume avae sketi. mwanaume abebe mimba na mwanamke sijui afanye nini!Tunachozungumzia ni kuheshimiana na kukamilishana ( complimentarity), kuelewa tofauti zetu kijinsi [/U]na majukumu ya kijinsia na kuona ni jinsi gani kila mmoja awezeshwe kuyatimiza bila kumuumiza mwingine.
2. Suala la mwanamke kuishi bila mwanaume - huu ni mjadala mwingine.
 
Tunaposema kuwa wanawake wanaonewa au hawana usawa na wanaume tunachukulia vitu vinavyotokea katika jamii, kwa mfano kwenye miaka ya mwisho ya hamsini, na mpaka karibu na miaka ya sabini, wanawake Tanzania hawakuwa wengi katika masuala ya siasa, moja ya sababu ni kuwa haikuwa vizuri mtoto wa kike wa mtu au mke wa mtu kwenda hadharani na kuongea mambo ya siasa nk, pili hivi kwa nini wale vikongwe wanaowawa kwa shutuma za uchawi ( nadhani Shinyanga kama nimekosea naomba msamaha kwa ndugu zangu wa huo mkoa) wengi ni wanawake?
Sijui takwimu zikoje siku hizi lakini wakati nikienda shule wanaume walikuwa wengi kuliko wanawake kwenye mafunzo ya sekondari nadhani hata vyuo vikuu.

Wanawake wanafahamu kuwa katika masuala ya nyumba baba ni kiongozi, nadhani wanataka tu mila zinazowapunguzia ushiriki wao katika nyanja kuu za uchumi zikemewe.
 
Wengi wa wanaume walikuwa na hadi sasa wanachukulia wanawake kama chombo cha starehe. Kuwaburudisha na kukata kiu ya matamanio yao ya kimwili. Hapa utasikia akisifiwa mwanamke mzuri ni yule anayemridhisha mumewe.....lakini mwanaume huyu hajiulizi kama huyu mwanamke anahitaji naye kuridhishwa na kujiuliza kama alishawahi kumridhisha hata siku moja.

Wengi wa wanaume wameshajiwekea mwanamke ni wa kukaa nyumbani, kupika chakula, kulea watoto, kutandika vitanda na kukirimu wageni. Inafikia kuwa mwanamke anafanywa mali ya mwanamume pale. Anzia kubadili jina na kutumia la mumeo...hakuna anayewaza kuwa mwanamke huyu anapoteza identity yake...ukifa sijui lazima ukazikwe kwa mumeo...... kama hamna mahali pa kuishi wakati mnaoana basi mwanamke yuko entitle kwenda kuishi kwa wakwe zake na sio reverse hata kama huko kwa mwanamke ana nyumba tayari na vitu kama hivyo.

Mwanamke hahitaji kukombolewa....atajikomboa mwenyewe na hivi sasa wengi wameshajikomboa...ndio wamekuwa viongozi wa familia zenye baba walevi, viruka njia.....na wasiopenda majukumu. Nazungumzia Tanzania.
 
Adui wa mwanamke ni mwanamke mwenyewe. Mfano mzuri ni wakati wa kampeni za awali za kugombea uteuzi wa mgombea uraisi wa chama cha Demokratik nchini Marekani. Nilishangazwa sana pale Mama Clinton (my choice) alipokuwa akiitwa majina ya ajabu ajabu na wanawake wenzake. Walikuwa wakimkosoa nguo avaazo, vipodozi anavyotumia, jinsi aongeavyo na mambo mengine. Nikashangaa sana na nikasema kweli hawa wanawake watabaki kuwa hivyo hivyo walivyo. Ukiangalia kisera Mama hakuwa tofauti sana na Obama lakini Obama alipata support ya wanawake wengi zaidi kuliko Fighter Hillary wangu. Yaani wanawake walikuwa wakizimia wakimwona Obama. Kulikuwa na Obama girl na wengine wengi kama huyo Obama girl. WTF!?!?!?

Asikudanganye mtu adui wa mwanamke ni mwanamke.
 
Wanawake wako chini ya wanaume katika anga zote ambayo ni natural hata kwa viumbe wengine! Hata kibayolojia- ukisema almost kila kitu inabidi utofautishe!
Mfano; normal HB (kiwango cha damu), men > women; normal waist circumference, men > women; daily energy requirements, men > women etc
Kujidai kujikomboa ni kwenda against nature na kuwafanya wasiwe na furaha!
Mwanamuziki mmoja wa Bongo anasema mwanamke hata akiwa na mapesa, asipokuwa na mume ni kazi bure, sugar ni sugar na chumvi ni chumvi!

Ni kweli, ila wanaume wameichukulia hii kama excuse ya kum-undermine mwanamke...na kwamba kila kitu anachofanya lazima kiwe na walakini...kwamba mwanamke hawezi kufikiri independently...kwamba mwanamke hawezi kuwa sehemu yeyote anayotaka kuwa bali ataambiwa kaenda kujiuza.

Hiyo ya mwanamke kutokuwa na mume ndio aheshimike nayo imepitwa na wakati. Ni wakati muafaka sasa kwa wanaume kubadili mitazamo yao juu ya mwanamke kama kiumbe duni na dhaifu, na kuwa kazi yake kubwa ni kumstarehesha mwanaume na kumzalia watoto.
 
Ni kweli, ila wanaume wameichukulia hii kama excuse ya kum-undermine mwanamke...na kwamba kila kitu anachofanya lazima kiwe na walakini...kwamba mwanamke hawezi kufikiri independently...kwamba mwanamke hawezi kuwa sehemu yeyote anayotaka kuwa bali ataambiwa kaenda kujiuza.

Hiyo ya mwanamke kutokuwa na mume ndio aheshimike nayo imepitwa na wakati. Ni wakati muafaka sasa kwa wanaume kubadili mitazamo yao juu ya mwanamke kama kiumbe duni na dhaifu, na kuwa kazi yake kubwa ni kumstarehesha mwanaume na kumzalia watoto.

Wanawake wanaji undermine wenyewe. Utawakuta wanampapatikia mtu mwenye jina na mwenye hela. Kila siku wako kwenye mivideo ya marepa na tena kwa hiari yao.

Sijawahi kuona hata siku moja ma cheerleaders wa kiume NBA au NFL...ni mademu tu walio robo au nusu uchi.

Wanawake watabaki kuwa hivyo hivyo walivyo. Men rule!!!!!!!!!!!!!
 
Wengi wa wanaume walikuwa na hadi sasa wanachukulia wanawake kama chombo cha starehe. Kuwaburudisha na kukata kiu ya matamanio yao ya kimwili. Hapa utasikia akisifiwa mwanamke mzuri ni yule anayemridhisha mumewe.....lakini mwanaume huyu hajiulizi kama huyu mwanamke anahitaji naye kuridhishwa na kujiuliza kama alishawahi kumridhisha hata siku moja.

Wengi wa wanaume wameshajiwekea mwanamke ni wa kukaa nyumbani, kupika chakula, kulea watoto, kutandika vitanda na kukirimu wageni. Inafikia kuwa mwanamke anafanywa mali ya mwanamume pale. Anzia kubadili jina na kutumia la mumeo...hakuna anayewaza kuwa mwanamke huyu anapoteza identity yake...ukifa sijui lazima ukazikwe kwa mumeo...... kama hamna mahali pa kuishi wakati mnaoana basi mwanamke yuko entitle kwenda kuishi kwa wakwe zake na sio reverse hata kama huko kwa mwanamke ana nyumba tayari na vitu kama hivyo.

Mwanamke hahitaji kukombolewa....atajikomboa mwenyewe na hivi sasa wengi wameshajikomboa...ndio wamekuwa viongozi wa familia zenye baba walevi, viruka njia.....na wasiopenda majukumu. Nazungumzia Tanzania.


Mama:

Kwa mtazamo wangu finyu. Naona evolution ime-play part. Na mfano mkubwa ni kuangalia jamii ambazo bado zinaishi ya kijadi bila kuingiliwa sana na mifumo ya kigeni kama vile Jamii za watindiga, wamasai, bushmen na nyingine.

Katika jamii hizi kuna mgawanyiko na matarajio ya kitu gani mwanamme au mwanamke afanye.

Na kwa sababu jamii zote duniani zilipitia muundo wa huu matatizo mengi ya wanawake ni legacy za evolution.

Katika familia yetu wote tulipewa nafasi sawa za kwenda shule. Lakini dada zangu walikuwa wakitoka shule, automatically walikuwa wanakwenda jikoni kufanya shughuli zingine na sisi watoto wa kiume tulikuwa huru kufanya shughuli zingine.

Katika mfano huu nataka kuonyesha kuwa overtime, professions zilizokuwa zinategemea nguvu zimebadilika. Miaka ya mwanzo mwanamme alitegemewa kuwa mlinzi wa nyumba, kwenda kuwinda kitoweo na n.k. Lakini kutokana na maendeleo ya jamii sio lazima mwanamme afanye tena. Na kama kungekuwa na ulazima, basi wakati natoka shule nilitakiwa kuchukua mkuki na kwenda kuwinda.

Kwa upande mwingine professions asilia za mwanamke azijabadilika. Mwanamke anatakiwa awe mama, mpishi na mambo mengine ambayo toka mwanzo wa dunia mwanamke anazifanya.

Hivyo kwa maoni yangu. Ukombozi wa mwanamke hauko mikononi mwa mwanamke mwenyewe. Jamii nayo inatakiwa kutambua umuhimu wa mchango wa mwanamke katika jamii.

Kuna wanawake Tanzania wanatumia zaidi ya masaa mawili kutafuta maji ya kutumia ndani. Resources walizonazo wanaume wa Tanzania zinaweza kuboresha maisha ya wanawake hawa katika kipindi kifupi. Na tusitegemea sana kuwa kutatokea mwanamke au kundi la wanawake wenye nguvu sana kuweza kuwasaidia wenzao.
 
Sasa hapo evolution inachukua nafasi gani Zakumi...kwa hiyo kuna gene inaplay hiyo part?

Sema ni matatizo ya kihistoria ya jamii husika.
 
Wengi wa wanaume walikuwa na hadi sasa wanachukulia wanawake kama chombo cha starehe. Kuwaburudisha na kukata kiu ya matamanio yao ya kimwili .
Ina maana Nyie hampati starehe? nyie ndio mnatuona sie kama chombo cha kustarehe an kuchuma si mnatuita ATM.......kuna msemo mmoja nimeupenda hapa JF sijui nani kauanzisha GENGE LENU LA TGNP

Wanawake wanaji undermine wenyewe. Utawakuta wanampapatikia mtu mwenye jina na mwenye hela. Kila siku wako kwenye mivideo ya marepa na tena kwa hiari yao.

Sijawahi kuona hata siku moja ma cheerleaders wa kiume NBA au NFL...ni mademu tu walio robo au nusu uchi.

Wanawake watabaki kuwa hivyo hivyo walivyo. Men rule!!!!!!!!!!!!!
Unaweza kuita vicheche......mimi nashangaa nyie wakina mama na genge lenu la TGNP si mna dini nyie na vitabu vyenu vinawaambiaje kuhusu mwanamke na mwanaume?....Kuna yule mama Helen Kijo Bisimba anawapoteza wakina mama wenzie.....

Hakuna ukombozi wala nini nyie mtaendelea kuwa chini ya wanaume daima yaani hata mfanyeje.....mkizidi ina maana mnapingana na maandshi ya vitabu mnavyoamini unless otherwise
 
Ukombozi wa Mwanamke ni kumpatia haki stahili katika yote. Adui mkubwa wa mwanamke ni Mfumo Dume uliotawala kwa karne nyingi huko nyuma ukapigiliwa misumari na dini zote kuu.

Idadi ya wanawake duniani ni theluthi mbili na wanaume ni theluthi moja. Hawa theluthi moja wanatawala kila rasilimali na kujitwalia fursa zote huku wanawake wakiachwa ama chombo cha uzalishaji mali.

Mwanamke anakuwa hana haki katika jambo lolote hata lilolohusu matumizi ya mwili wake mwenyewe labda aseme 'naumwa' tena Zanzibar ndio hatari zaidi maana hata akisena 'naumwa' anaambiwa 'uani'

Kufuatia hali hii, Barakuu la Umoja wa Mataifa likaitisha mkutano Mkuu wa Wanawake uliojilikana kwa jina maarufu la Mkutano wa Beijing. Mhe. Dr. Getrude Mongella toka Tanzania ndiye alichaguliwa Mwenyekiti wa mkotano huo.

Mkutano huo uliwakilisha wanawake toka kila sekta na kila jamii toka nchi zote duniani na ulipitisha maazimio yafuatayo...click google 'Beijing Declaration'.. Utekelezaji wa maazimio haya ndio ukombozi wa mwanamke.
Mpaka sasa ni nchi chache zimefanikiwa kutekeleza maazimio hayo. Tanzania inapiga hatua nzuri
Mkuu unless otherwise huamini dini....kama huamini dini zileee basi tujadili lakini hawa na genge lao la TGNP hawastahili haki wanastahili kuwa chini ya wanaume daima.Vitabu vinasema nyie mnaleta modernization kwenye vitabu vya kidini....acheni hizo
 
Haya masuala yenu ya mfumo dume ndio maana ndoa nyingi zinavunjika...yameanza huko ulaya mnaona kulivyo hali ngumu kindoa...Kijo Bisimba na yule Ananelia Nkya nawachukia na idea zao kutuvunjia ndoa zetu.

Mwanamke ni mwanamke tu na ataendelea kuwa chini ya mwanaume.
 
Yo yo nakubaliana na wewe japokuwa nami mwanamke na ukweli wauma...... huku kutokomeza mfumo dume kumesababisha mengi sasa ndoa zavunjika, watoto wanakosa malezi bora, heshima hakuna, cjui huko tuendako itakuwaje.
 
Back
Top Bottom